THREE ... TWO ... ONE ... ACTION!!! YES CIA WAKIPROJUZI MUVI ZA BIN LADEN.
Hadithi ya Osama ni moja ya hadithi zilizofanywa ni za kusisimua kwelikweli
na vyombo vya magharibi, nami kuielezea kwa kina chake itahitaji makala
nyingine kama na ninahofia muda haupo upande wangu. Isipokuwa Osama alishakufa
tangu 2001, lakini kwa takribani miaka 10, CIA wamekuwa wakirusha kaseti ‘mpya’
za audio na vidio za Osama Bin Laden, na kila CIA ‘walipozindua’ kaseti hizo
zilipata mauzo ya kutosha kwenye vyombo vya habari vya magharibi na muuzaji wa
‘jumla’ wa kaseti hizo walikuwa ni Al-jazeera. Tizama posti hii salimmsangi.blogspot.com/2013/07/obama-alazimika-kumfufua-osama-bin-laden.html
Kwa muda wote huo hakuna
kiongozi wowote wa Talibani au wa Al-Qaeedah aliyejitokeza hadharani na kusema
kaseti hizo ni uzushi na urongo, walikaa kimya kama ambavyo Washington walivyo
taka wawe kimya.
MWAKA 2004 OSAMA ALIKUWA MZEE, NA MWAKA 2007 OSAMA KARUDI KUWA KIJANA ZAIDI, MAAJABU, KADIRI UMRI UNAVYOKWENDA YEYE ANAKUWA NI KIJANA TU.
Obama alipokuja kutangaza kifo cha ‘kutengeneza’ cha Osama bin
Laden, na ambacho mpaka sasa kinapigiwa zumari watu wacheze kwa namna
mbalimbali, ikiwemo kuandika kitabu cha uzushi kuhusiana na namna Osama alivyo
uliwa na kikosi maalum, filamu na taarifa mbalimbali, Al-Qaeedah wakaibuka huko
walipotoka na kusema watalipiza kifo hicho cha kiongozi
wao?!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
NEXT TIME CIA WANIPE MIMI KAZI YA KUCHANGANYA PICHA, HUYU JAMAA ALIYECHANGANYA HIZI AMEKULA PESA YAO BURE, HII HATA MTOTO ANAISHTUKIA KUWA NI FEKI, NADHANI WANAHITAJI MTU MWENYE MASTER YA PHOTOSHOP KUTUDANGANYA VIZURI.
UMEIYONA NA HII, KAMA VILE IMEPIGWA KWENYE MAKAMERA YAO YALE YA KIVITA NA NINI ... KUMBE URONGO MTUPU, TIZAMA PICHA INAYO FUATA.....
PICHA INAYO ONEKANA NI MAITI YA OSAMA HAPO JUU IME-EDITIWA KUTOKA KWENYE PICHA HII HAPA, MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA. TIZAMA PICHA INAYOFUATA ...
MCHANGANYA PICHA WETU AMETUMIA PICHA HII NA HIYO YA PILI KUTUPATIA 'UTHIBITISHO' WA KIFO CHA OSAMA, LAKINI PICHA HII TUNAIPATA KATIKA MOJA YA MUVI ZA HOLLYWOOD. KAMA KWELI WALIMUUWA KWA 'KIKOSI MAALUM' MBONA PICHA WANAZO TUPATIA NI FEKI?
Inashangaza, mbona mtu huyu alishakufa kifo cha kawaida tangu 2001, ni kifo
kipi mnacho kwenda kulipiza? Au kwa vile mnacheza nyimbo za Washington basi
mnataka kila mtu acheze? You can fool
some people sometimes, but you cant fool all the people all the time.
Al-Qaeedah, makundi ya waasi, Al-shabab, Boko Haram na makundi mengine
yanayoitwa ya kigaidi, lao, na Washington, lao na Ulimwengu wa kimataifa wa
kimasonia, lao na Illuminanti ni moja! Wewe ndiye adui, wanapigana vita, na ni
vita dhidi yako na familia yako, Watch out!!!!!!!!!!!
TUTUMIE AKILI ZETU NA SIYO ZILE ZA KUSHIKIWA NA VYOMBO VYA HABARI NA WANASIASA ...
Mpango wa Brzezinski kupitia kwa Obama ni kutengeneza
mitandao ya kisiasa ambayo itaweza kuiporomosha Urusi, utakumbuka mpango wake
huu ulianza tangu wakati wa Jimmy Carter ambapo yeye alikuwa ni msimamizi wa
siasa za mambo ya nje za Marekani ambapo akapelekea kuundwa kwa Taliban ambao
waliifanya kazi hii vizuri sana nyuma ya kile kilichoitwa ‘Holy War’, lakini
safari hii mpango huu hautailenga Urusi peke yake bali pia China nayo
itaingizwa ndani ya nyumba.
Brzezinki amekuwa makini akisambaza propaganda
zinazo lenga kuchora msitari wa kutokuelewana baina ya Umoja wa Ulaya na Urusi
kupitia Kosovo ambayo mustakabali wake wa kisiasa unaonekana kuachwa katika
hali ya utata kwa makusudi ili Moscow iweze kunyooshewa vidole kwa aina yoyote
ya uwozo unaotokea hapo. Sasa hivi ni Cremea na unaona hali ya mambo inavyo kwenda.
Lakini kwanza Obama anatakiwa kuwatoa wa China nje ya
Afrika kwa namna yeyote inayo wezekana. Hata hivyo Brzezinki ana picha kubwa
zaidi juu ya hili la kuwafukuza wa China nje ya Afrika. Kupitia kwa Obama,
almaaruf, Kennedy Mweusi kama alivyoitwa wakati wa uchaguzi, Brzezinki anao
mpango wa kuwapora Wachina kila aina ya rasilimali wanayonunua kutoka Afrika,
ikiwemo mafuta, gesi za asili, madini na kila kile ambacho kimebakia kama
makombo baada ya vile walivyo pora wakati wa ukoloni, baada ya ukoloni na
kwenye ukoloni mambo leo. Tizama posti hii kwa uhondo kamili juu ya vita vya Obama na wachina ndani ya Afrika, http://salimmsangi.blogspot.com/2014/05/boko-haram-mshirika-wa-marekani-nigeria.html
Mpango ulio chaguliwa juu ya hili ni njia ile, ile
iliyopendekezwa na mababu wa Freemasons, Priory of Sion kwenye kile
walichokiita Protocal of Sion, njia hiyo ni kuzivunja vunja nchi za ki Afrika
kupitia vita vya wenyewe kwa wenyewe kitu kitakacho wakimbiza wa China nje ya
Afrika. Na hili litasimamiwa vilivyo na kile kinachoitwa Africom ambayo
imeundwa na Marekani na mawakala wao wengine.
AFRIKA MOTO
Kupitia mpango wa Brzezinki Afrika itakuwa ni uwanja wa
mapambano baina ya Marekani na China, na maanisha mapambano ya kiuchumi na
siasa, lakini mapambano ya bunduki itakuwa ni baina ya wa Afrika sisi kwa sisi.
Afrika itawaka moto, mauaji ya watu chini ya jangwa la Sahara yatakuwa ya
kutisha. CIA wataingilia kati na hata kuingilia siasa za nchi za ndani za
Afrika kwa uwazi kabisa nyuma ya kile kitakachoitwa vita vya ugaidi ambavyo
wakala wake ni Al-Qaeda ambao kwa sasa kutokana na taarifa za vyombo vya habari
za kimagharibi na hata vya hapa Afrka Al-Qaeda tayari wako ndani ya nyumba,
wako Afrka, Algeria na Tunisia na kazi zao chafu zimeshaanza kuonekana, kumbuka
Algeria ni moja wapo ya nchi zinazo zalisha mafuta kwa wingi Afrika.
Utakumbuka Al-Qaeda ilikuwa ikidhaminiwa na CIA kupitia
hela za dawa za kulevyea wakati Taliban wakidhaminiwa na Brzezinki na mtandao
wake wa Trilateral Commission. Hakuna Holy War wala Jihadi kama alivyo Kennedy Mweusi
vikundi hivi ni sawa na mwanasesere anayechezeshwa kwa kamba zilizoshikiliwa na
bwana wakubwa hawa. Moto umeshawaka Nigeria moja ya wazalishaji wakubwa wa
Mafuta Afrika, Boko Haram wananguruma na wanao kufa ni wa Afrika.
(sehemu hiyo hapo juu niliandika muda kabla
moto haujawaka Afrika, lakini yametokea, moto umewaka, serikali zimepinduliwa,
Wachina wamekimbia, Illuminati wanabeba chao na Waafrika bado tunapigana risasi
kwa faida yao)
Uingereza na Israeli kwa pamoja kwa miongo kadhaa
wamekuwa wakiivunja vunja Sudan, lakini leo picha iliyoko Darfur inatumiwa na
Marekani pamoja na Uingereza kama kisingizio cha kuitawalia nchi hiyo mambo
yake nyuma ya kile wanacho tuambia kuwa
kuna uvunjaji mkubwa wa haki za binaadam katika eneo hilo.
Kusema Sudan inakiuka haki za binaadam hakuhusiani kabisa
na mpango wa kuondoa zahama hilo kama vyombo vya habari vya kimagharibi na
mawakala wao wanavyo dai lakini zaidi inahusiana na mpango wa kukata 7% ya
mafuta ya China ambayo yanatoka Sudan. Habari zinasambazwa kwa kasi kuwa
shughuli za kiuchumi za China nchini Sudan zinazorotesha kwa kiasi kikubwa
utaratibu wa kuondoa baa la njaa na tatizo la mafuta duniani. ( Tarpley, Webster Griffin Barack H. Obama: the
unauthorized biography / Webster Griffin Tarpley ISBN-13: 978-0-930852-91-7
(Digital), 978-0-930852-81-8 (Offset edition) Uk 376)
Aina hii ya
propaganda muda si mrefu inapokelewa na vikundi vinavyojiita vinasimamia haki
za binaadam ambavyo ni vikundi vya watu wale, wale katika sura tofauti lakini
nyuma ya ajenda ileile.
.jpg)
Nchi yoyote duniani ambayo kwa namna moja ama nyingine
inanufaika kiuchumi na au kiviwanda kutokana na ushirika wake na China na kwa
maneno mengine China nayo inajijenga misuli yake ya kiuchumi na viwanda
kutokana na miradi yake mbalimbali iliyomo nchini humo, nchi hiyo haiwezi
kuepuka mpango huo wa Brzezinki. Mfano ni Burma na Venezuela ambazo historia ya
maendeleo yao kiuchumi haijakamilika bila kuitaja China. Shughuli inayo endelea
Pakistan ambapo Kennedy mweusi amekiri yuko tayari kuipiga bomu la nyuklia
Pakistan endapo itaonekana kushindwa kupambana na Taliban na Al-Qaeda, shughuli
hiyo haina lolote kwenye kile kinachosemwa vita dhidi ya ugaidi bali zaidi, ni
vita vya kuizorotesha nchi hiyo ambaye muda mrefu imekuwa mshirika wa China,
vurugu hizo ni za kuwakimbiza wa China kutoka humo. Tunaona siasa za vuta ni
kuvute baina ya Pakistan na Marekani sasa.
China itakapo tengwa na kupokonywa washiriki wake wote wa
kiuchumi, na kunyimwa uwezekano wowote wa kupata mafuta na malighafi zozote
kutoka nje ya China, hatua itakayo fuata ni kuizorotesha serikali ya China na
wakati huo, huo kuipambanisha na Urusi, suala la kuizorotesha serikali hiyo
tumeliona linavyoshika kasi kupitia Tibet kwa kiongozi wao wa kiroho Dalai
Lama. Lakini kwa vile Urusi na China zote
zinafahamu kuhusu njama hizi za Brzezinki mchezo unakuwa mgumu ,na hasa pale utakapo jenga
mazingira ya kuanganisha mahusiano yenye chuki ya Urusi na China dhidi ya
Marekani na washirika wake wapya. Upande mwingine wa shilingi mwanasesere huyu
atakuwa na kazi ya kuiunganisha Iran na Syria na kwa pamoja zisimame kuwapinga
wa China na wa Rusi. Kinachotakiwa ni Bashir Al Assad atoke pale na paweke
kibaraka mwingine, ambaye moja kwa moja atakuwa ni adui wa Urusi na China, kama
tunavyo ona, anayempa kiburi Assad ni Mchina na Urusi, sasa hali hiyo inabidi
ibadilike, halikadhalika kwa Iran, soon
she is next baada ya Syria.
.jpg)
HAIJALISHI NI SHIDA NA MADHARA KIASI GANI YATAPATIKA KWA UMMA, KINACHO JALISHA NI MALENGO YA MILENIA NYINGI KUTIMIA, THE END JUSTFY THE MEANS ... NOTHIN MORE
Mwandishi wa kitabu cha Barack H. Obama: anajaribu kutupa
taswira ya mchezo mzima kuhusu Iran na Marekani kuanzisha ushirikiano wa kiuchumi
na kisiasa dhidi ya Urusi na China namna utakavyo kwenda, haya ndiyo maoni
yake,
Iran itashawishiwa wawe rafiki na
Marekani kwa ahadi ya kupewa nguvu sawa na Marekani ndani ya Mashariki ya kati,
si m China wala m Rusi, si m Pakistan wala Egypt atakaye kuwa na sauti ila Iran
mshirika wake mpya, Marekani. Rasilimali ngapi za Iran zinazozuiliwa na
Marekani kwa muda wote huo sasa zinafikia thamani ya dola bilioni mia na zaidi,
vipi unaonaje Iran akipewa na ahadi hii ya kupata rasilimali zake hizo. Unaonaje
ahadi ya kutolewa kwenye orodha ya nchi zinazo dhamini ugaidi na vikundi vyake
(hatua hii
imeshaanza kufanyiwa kazi). Bila
kuwasahau washirika wakubwa wa Iran Hezbollah kuwa na wao watapata chochote.
Lakini hayo ni mambo madogo tu, unaonaje ishu ya nuklia kama alivyo fanya Bush
Baba alimkabidhi Saddam silaha nyuma ya mapazia halafu Bush mwana akaja kuzidai
mbele ya hadhara, unaonaje Iran akapewa ruhusa ya kuendeleza mradi wake huo
nyuma ya mapazia (Hili nalo limeshapatiwa baraka na Washington). Tunaweza kukupatia teknolojia bora
kushinda hii uliyonayo, silaha bora na mabomu ambayo unaweza kuyarusha kokote
pale duniani na yakafika Moscow, sema tu kama ndiyo hilo unalo taka, sasa hivi
tutakupatia. Ujue tu kwamba adui yako mbaya kuliko wote hajawahi kuwa Marekani
bali Urusi. Si unakumbuka namna walivyo kufanya walipo chukua baadhi ya maeneo
yako wakati wa WWII, ule ulikuwa ni uharibifu mkubwa. Sisi hatujawahi kufanya
kitu kama hicho na wala hututa jaribu kufanya hivyo. Tunachotaka sisi ni kuwa
marafiki na kukusaidia kuwa na nguvu za
kutosha kupambana na adui yako wa kweli, Moscow... kama unavyo fahamu
mheshimiwa rais wananchi wako wanaichukia Urusi kuliko wanavyoichukia Marekani
na Uingereza na wakati wowote utakapo wachukia wa Rusi ujue unawaridhisha watu
wako na sisi tutakusaidia... sema tu unataka nini... unaonaje kuhusu manuwari,
tukakupatia manuwari inayokwenda mpaka bandari za kusini ya Urusi zikiwa na
mizinga ya kinuklia ,hapo utawazuia Urusi wasiendelee kukuibia mafuta yako
kutoka kwenye bahari ya Caspian, na kama wakijaribu kujibu mapigo usiwe na hofu
tutakuwepo kukupa sapoti. Fikiri mwenyewe kuhusu hili. Halafu kuna hawa wa
China, kwa nini unapenda kufanya nao biashara sana, muda si mrefu watakuweka
kwenye mfuko wao wa suruali yao kutokana na jinsi unavyo wauzia, halafu tunajua
hulipendi hilo... bora ufanye biashara na sisi hata kama ni kwa dola.
Tunachotaka ni kuwa ufahamu kwamba sisi ni wa kweli vibaya mno. (Ibid)
.jpg)
UNADHANI NI KWELI OBAMA ALIKUJA KUCHEZA MPIRA NA KIKWETE KWENYE ILE MITAMBO YETU YA UMEME ISIYO ISHIWA NA KASHFA?
Jamaa huyu hayuko mbali sana na ukweli kwa sababu ni
mchezo huu, huu aliufanya Brzezinki kwa wa Afghanistan kupitia Mujaheedina
ambao ni zao la mpango wake, akawa pambanisha na Urusi na kilichobakia hapo ni
historia, alifanya hivyo kupitia kwa Jimmy Carter, leo mchezo uleule wa mtu
yule, yule utafanyika kupitia kwa Obama. Halafu wa Syria nao watafuatwa, (tayari
Syria kumesha waka moto) watashikwa kama walivyo shikwa kwenye Gulf War ya
mwaka 1991. Lengo si kuwapambanisha wa Iran na Syria bali kuwa unganisha dhidi
ya China na Urusi. Usisahau Khomeini kufanya mapinduzi yale ulikuwa ni mpango
wa Freemasons nyuma ya asasi zake za siri.
Kinacho endelea Afrika na duniani leo ni kazi mahususi ya
kuandaa pande za mahasimu kwa ajili ya WWIII, Pakistani tunajua anazo nyuklia,
Iran nyuma ya mapazia kama ilivyo kuwa kwa Iraq keshapatiwa ‘green light’ kuendelea na mradi wake,
zinazojiita nchi za kiislamu, na zile ambazo tunaona zinapinduliwa na waasi
kama Egypti, Libya, Syria, Iraq, Pakistani, Iran na wengine watakao pitiwa na
upepo huu, wanaandaliwa kuunda upande mmoja au muungano mmoja dhidi ya maadui
wa Uislamu na Waislam. Utasikia vikundi hivi vikija na dai la Khilafa kote
duniani, hivyo hawataishia, Syria au Libya au Somalia, hapana wataingia kila
pale watakapo ruhusiwa na mabwana zao wakubwa kuingia, kumbuka upande mmoja wa
vita unaandaliwa, dhidi ya Ulaya, Marekani, Israeli na washirika wao.

Kipindi hichi siyo Marekani wala Uingereza atakaye
anzisha vita hivyo, chokochoko baina ya Israel na Iran ndiyo cheche zitakazo
washa moto huo ambapo baadaye kila mmoja ataita washirika wake, Israel
washirika wake wapo tayari na tunawafahamu, lakini washirika wa Iran ndiyo
kwanza wanaanza kupanga safu, kitakacho fuata ni WWIII.
Malengo ya makuu ya vita hivyo ni kuisimamisha Israel
kama ‘New Super Power’, hii ni muhimu kwa vile ni kutokea hapo Jerusalem ndipo
Dajjal anatakiwa atawale, na tunajua Illuminanti kwa zaidi ya miaka 2000
wamekuwa wakiandaa zulia ambalo Dajjal atatembea juu yake, na mahala ambapo
dola ya Dajjal itakapo anzia ni Israel, na kama yeye atataka kuwa kiongozi wa
dunia na hatimaye kujiita mungu, hili haliwezekani kama atasimama nyuma ya dola
dhaifu, lazima asimame nyuma ya dola yenye nguvu na iliyoundwa kwa na
kuandaliwa kwa muda mrefu kwa ajili hiyo, dola hiyo si nyingine ila ni Israel,
na hapo ndipo patakapo kuwa makao makuu ya serikali ya dunia. Hivyo basi Issa
(as) atakapo kuja kazi ya kwanza ni kumuondoa Dajjal ndani ya Israel, hichi
ndicho kipindi ambacho miji mitakatifu itaachwa na waumini wa kweli kwa ajili ya kwenda
kuungana na jeshi la Issa (as) dhidi ya Dajjal. Mpinga Kristo huyu atauwawa
sehemu inayo itwa Baablud, leo hii panaitwa Telaviv, na hapo itakuwa ndiyo
mwisho wa kitimbi hichi cha Babylon Brotherhood kilichofanyiwa kazi kwa zaidi
ya miaka 2000 na vizazi kadha wa kadha vya Illuminanti. Kazi ambayo imekuwa ndiyo mzizi na chemchem ya
kila dhila, mateso, shida, chuki matatizo na kila baya unaloliona leo kwenye
uso wa dunia. Kazi hiyo mbaya iliyofanywa kwa milenia nyingi itakwisha pale
Baablud. Freemason, Illuminanti, Babilon Brotherhood, asasi zao nyingine nyingi
za siri na kazi yao ya milenia nyingi itazikwa hapo.
“Wanapo kujia wanaafiki husema:
Tunashuhudia ya kuwa wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu anajua
kuwa wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu anashuhudia ya kuwa
hakika wanaafiki ni waongo.”
“Wamevifanya viapo vyao ni kinga, na
wao wakajizuia kuifuata Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika ni mabaya kabisa waliyo
kuwa wakiyafanya.”
“Hayo ni kwa sababu ya kuwa
waliamini, kisha wakakufuru; kwa hivyo umepigwa muhuri juu ya nyoyo zao. Kwa
hivyo hawafahamu lolote.”
“Na unapo waona, miili yao
inakupendeza, na wakisema, unasikiliza usemi wao. Lakini wao ni kama magogo
yaliyo egemezwa. Wao hudhania kila ukelele unao pigwa ni kwa ajili yao. Hao ni
maadui; tahadhari nao. Mwenyezi Mungu awaangamizilie mbali! Vipi wanapotoka na haki?”- Quran 63:1-4
KAA MKAO WA KULA KWA AJILI YA ZILE POSTI NILIZO AHIRISHA ....
naomba niwe napost hizi habari kwa blog yangu kaka yangu! nimezipenda xana na nimekua nikitafuta sehem ya kuzipata.
ReplyDeletewww.robhinsontz.blogspot.com
0756 891212.
Ur fans from Utegi Rorya Tz.
Unakaribishwa mdau na wazo lako ni zuri sana, unaweza kunirushia email kwenye anuani hii, kitabuchetu@yahoo.com, halafu tutajadiliana namna ya kulifanikisha hilo.
Delete