Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Wednesday, August 24, 2016

MALKIA HILLARY, MRITHI WA MFALME OBAMA


Katika posti iliyo tangulia ya ‘MFALME OBAMA’ tumeona mchezo unao itwa ‘siasa’ na ‘demokrasi’ unavyo igizwa kwenye majukwaa na mawazo ya watu kurubuniwa ‘kuhalalisha’ mgombea kushinda kupitia kile kinacho itwa kura.


Nadhani utakuwa kwenye nafasi nzuri sasa kutambua kuwa, hakuna siasa, bali ni mchezo wa kuigiza wa kuwalaghai wanachi, na hakuna kinacho itwa demokrasia, ispokuwa mgombea alishashinda kabla ya wewe kumpigia kura, walihitaji kura yako ili kuhalalisha uteuzi wao.

Utakuwa na safari ndefu sana kama bado unafikiri au unayo mawazo ya kuwa mgombea anapitishwa na kushinda kwa kura za wananchi.

Kwa mara ya kwanza kabisa kwenye historia ya utawala na uongozi, kumekuwa na utaratibu tofauti na wa kipekee wa kuwaweka viongozi madarakani, mashirika makubwa na taasis zake duniani ndizo zinazo amua nani awe kiongozi wan chi gani, hii si Ulaya tu na Marekani, hapana; mfumo huu mpya unaimeza dunia yetu yote sasa.


Mashirika kama StarBuck, Nike, Adidad, Gap, Monsanto, Calvin Klein, General Motors, Ford, IMF, World Bank, McDonald, CIA, CFR, na mengine na mengine kutaja kwa uchache. Hichi ni kitu kipya katika siasa na utaratibu wa kuwapata viongozi, masharika hayo makubwa yana wateua viongozi hao, kuwalipia gharama za kampeni zao, na kusimama nyuma yao kuhakikisha wanashinda kwa gharama yeyote. Viongozi ahawachaguliwi na watu, bali na mashirikia hayo makubwa, kura yako inatumika kuhalalisha uchaguzi huo.

 Lakini sasa imefika mahali mashirka makubwa yanawaingiza wafanyakazi wao wakubwa na wenye wadhifa mkubwa kwenye nafasi mbalimbali za kiserikali ili waweze kutetea, kutunga na kupitisha sera ambazo zitalinda matakwa ya mashirika hayo.
Haijalishi wanasiasa watazungumza au kukuahidi kitu gani, hato kutumikia wewe, bali shirika au kampuni iliyo muweka kwenye nafasi hiyo.


Mwezi Aprili 2014 vyuo viwili vya Princeton na Northwestern vilivyo Marekani, vilkuja na hitimisho moja baada ya kufanya utafiti juu ya masuala ya kisiasa na utawala ndani ya Marekani, kuwa Marekani siyo nchi ya kidemokrasia, bali nchi inayo tawaliwa na watu wachache wenye nguvu za kiuchumi. 

Tafiti hiyo moja ya maeneo waliyo tazama ni kwenye sera 1,800 zilizopitishwa kutoka mwaka 1981 mapaka 2002, na kuhitimisha kuwa matajiri na wenye nguvu walipata kila kile walicho kitaka na kile ambacho walikitaka wamarekani wa kawaida hawakukipata.


Kila baada ya miaka miwili, mfumo wa vyama viwili wa siasa za Marekani unawapa wananchi wake ‘uhuru’ wa kuchagua mgombea mmoja kati ya wawili ambao tayari wapo kwenye ‘mifuko’ ya makampuni na mashirika makubwa duniani, yaani tayari wamesha teuliwa na mashirika hayo kuwakilisha mahitaji na matakwa yao.


Hivyo la kwanza na la msingi ni kuwa viongozi wa leo hawachaguliwi na wananchi, bali wanateuliwa na mashirika na taasisi, kazi ya wanachi ni kuhalalisha uteuzi huo.


Kwa muktadha huo tunapo utazama uchaguzi wa Marekani, kati ya Trump na Hillary unatizama ni nani mwenye ushawishi kwenye matakwa ya mashirika na makampuni hayo makubwa duniani? Huyo ndiye mwenye nafasi ya kuwa raisi.

Jingine ni Mshirika au sura zilizo nyuma ya mashirika na taasisi hizo zinataka kitu gani? Siyo wanachi wa Marekani wanataka nini, hapana, bali big brother wanataka nini na unatizama kati ya hawa wagombea wawili na nani anayo nafasi ya kutekeleza mahitaji hayo ya mabwana wakubwa.


Kuhusu Marekani inata nini kwa sasa, ambacho si lazima kiwe ni matakwa ya wamerekani, bali makampuni na mashirika yaliyo Marekani ila yanashikilia uchumi wa dunia kwa kiasi kikubwa, au sura zilizo nyuma ya makampuni mashirika na taasisi hizo je zinataka nini?

Mpaka mwaka 1990 Marekani haikuwa na mpinzani kwenye kiti cha enzi cha dunia, ilikuwa yenyewe ndiyo ‘Super Power’. USSR ilikuwa imevunjwa na ilikuwa dhaifu kiasi cha kuomba msaada kutoka kwa Marekani. 

Marekani ikawa na kazi moja tu, kuhakikisha wapinzani wake wa kale hawafufuki na kuwa na nguvu za kumletea ushindani yeye, wala wapinzani wapya hawazaliwi ambao watatishia mamlaka ya Marekani kwenye kiti hicho cha enzi. 

Marekani ikazidi kujizatiti kijeshi na kujiingiza kwenye maeneo muhimu kwenye uso wa dunia kama Mashariki ya kati, Asia na baadhi ya nchi za Afrika, lengo ni kujikusanyia malighafi na rasilimaliza kutosha kabla ya yeyote ilikujiongezea misuli ya kiuchumi na kijeshi dhidi ya yeyote anaye tishia kuwa, ‘Super Power’.


Kikaja kile kilicho fahamika kama Military Industrial Complex (MIC) kwenye sera za ndani na hasa sera za nje za Marekani, MIC ikawa na hitajio endelevu lisilo wezwa kukatishwa kila raisi mpya anapo ingia madarakani na sera zake mpya. MIC ikawa mwanzo wa mbio mpya za kujikusanyia silaha na kujitanua Zaidi na Zaidi.


Baada ya WWII Ulaya ilianguka kama Super Power. Kile kilicho fahamika kama ‘Pax Britannica’ kikaweka mazingira mazuri ya kunyanyuka kwa ‘Pax Amaericana’ na Washington ikapokea mikoba ya kutangaza demokrasia kote duniani kote kwa jamaa zake wa Ulaya. Marekani kwenye kiti hichi imeendelea kukikalia kwa msaada mkubwa kutoka kwa jamaa zake wa Ulaya.


Pax Americana haijapata kuwa kwenye changamoto kwenye historia ya muda wote ikiwa kwenye kiti cha enzi cha dunia kama ilivyo sasa. Imekuwa ni wazi zaidi kuwa nguvu ya dunia, maamuzi ya dunia, ushawishi wa dunia unaponyoka kwa kasi kutoka Pax Americana kuelekea kwenye nchi kama China, Urrusi, India, Brazil na mataifa mengine kutoka nchi za Asia. 

Sura hizi mpya zinakuja kuleta uwiano wa kimamlaka kwenye kiti cha enzi ambacho kwa miongo kadhaa kimekuwa kikaliwa na taifa moja tu, Marekani.

Vikao vya G7 vimekuwa vikifasiriwa kote duniani hasa na vyombo vya habari vya kimagharabi na vile vyenye maono ya namna hiyo kuwa ni vikao vinavyo husu nchi za viwanda zinazo kuwa kasi.


Lakini muelekeo huo nao umepata changamoto baada ya muungano wa nchi kama hizo kufanya kikao chenye maonokama hayo nchini Urusi kuashiria kuzaliwa kwa muungano mpya wa kiuchumi ambao unatishia muungano wa Ulaya na uwepo wa Marekani kama Super Power. 

Mkutano huo unazihusisha nchi vinara kama Brazil, India, China, Urussi, South Africa nan chi zingine kutoka kwenye muungano wa Shanghai Cooperation Organization. Vinara na washawishi wakubwa kwenye mkutano huo ni Beijing na Moscow ambao mahusiano yao yamekuwa imara Zaidi kila pale Marekani anapo onekana kukiuka sharia, kanuni na taratibu za kimataifa. 


Ni kama muungano wa nguvu hizi mbili upo dhidi ya kitisho cha Marekani.

China na Urrusi ni mataifa yenye nguvu sana kwenye maeneo yao, lakini kwa mmoja mmoja peke yake nguvu zao bado haziwezi kusimama dhidi ya Marekani ambayo bado unaushirika mkubwa na Umoja wa Ulaya na muungano wake wa majeshi ya NATO. Lakini nguvu hiyo inapo ungana pamoja, yaani Beijing na Moscow inakuwa ni ‘Super Power’ mpya imezaliwa dhidi ya Marekani. 

Ushirikiano wa nchi hizi China na Urrusi ambazo zote zina nguvu za kinyuklia, zote zina turufu ya VETO kwenye baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, zote zina nguvu kubwa ya kijeshi na kiuchumi na zote zimekuwa zikienda kinyume na sera za kimataifa za Marekani, ni wazi ‘Super Power’ inahama kutoka kwa nchi moja Marekani kwenda kwenye muungano wa China na Urusi.

Washington haikubaliani na ushawishi huu mpya hata kidogo. Kama tulivyoona kwenye Posti iliyopita ya ‘MFALME OBAMA’ icheki hapa
 http://salimmsangi.blogspot.com/2016/07/mfalme-obama.html ni kuwa moja kazi kubwa aliyo kuwa nayo Obama ni kuhakikisha ainaivuruga dunia kupitia ‘Proxy War’ ilikuondoa ushawishi wa China kwenye nchi ambazo nishati muhimu kama ya mafuta na rasilimali zingine zitakazo iwezesha China kukuza misuli yake zinapatikana.

 Tumeona moto ulio washwa Afrika na Arab Spring na hatimaye ugaidi kufanyiwa Franchise badala ya Al-qaeda na Talebani pekee tukapata vikundi visivyo hesabika vya kigaidi kama Isis, Boko Haram, Alshabab, Free Syria Army, n.k.

Vyote hivi vimefanya kwa gharama ya kumbana Mchina ambaye ushawishi wake maeneo hayo umezidi kutanuka kwa nguvu mno. Lakini Mfalme Obama hakuishia hapo, alitakiwa kumbana Mrusi pia. Nchi ambazo mwanzoni zilikuwa kwenye umoja wa USSR, zikapewa njia nyepesi ya kujiunga na Umoja wa nchi za Ulaya ilikuendelea kuidhoofisha Urusi na kusogeza majeshi ya NATO kwenye mipaka ya nchi hiyo na hivyo kulazimisha kuizunguka Urusi kijeshi. 

Mfalme Obama ilibidi aende mbali Zaidi hata kusaini mkataba na nchi ambayo utawala uliopita wa Bush uliitambua nchi hiyo kama ‘Mhimili wa Maovu’ duniani na moja ya nchi inayo wasaidia magaidi; Iran. Ilifika mahala Iran ikawekewa vikwanzo vya kiuchumi kwa kisingizio cha kumiliki viritubisho vya silaha za kinyuklia.


Lakini hayo yote Mfalem Obama ilibidi ayatupe kwenye ‘dustbin’ na kuingia makubaliano mapya kwamba Iran siyo muhimili wa maovu tena, Iran itaruhusiwa kuendelea kurutubisha mradi wake wa nyuklia kwa ‘manufaa’ ya raia wake, Irani haipo kwenye orodha ya nchi inazo fadhili magaidi, na Irani ipewe mabilioni ya dola ya aseti zake zilizokuwa zinashikiliwa na Marekani, yote haya mflame ilimbidi kuyafanya kwa gharama ya kuhakikisha mahusiano baina ya ‘Tehran’ na ‘Moscow’ yanakufa ili kuweza kumdhoofisha Mrusi na kumnyima mafuta kutoka Iran. 

Mflme Obama alisaini ‘New Deal’ na Iran lakini ushirikiano kati ya Tehran na Moscow bado ni kitisho kwa Mfalme, watoto wa mjini tunasema ‘Marekani ameingia choo cha kike.

Sasa mflame anaondoka na kazi aliyopewa haijaisha, na hii ikimaanisha hatari ya Marekani kuondolewa kwenye kiti cha enzi. Hivyo Mflame kabla hajaondoka  white house anayo kazi ya kuweka mazingira mazuri kwa mrithi wake kuhakikisha kuwa akiingia tu white house kazi yake kubwa na ya kwanza ni dhidi ya Urusi na China. 

Hivyo Mfalme akatengeneza mchezo wake Ukraine kama ule alio utengeneza Libya na kwengineko, utawala wa Ukraine ulio kuwa na mahusiano mazuri na Urusi ukaondolewa madarakani, na serikali mpya uvamizi mara moja ikaingia kwenye Umoja wa nchi za Ulaya na hivyo Ukraine kuwa na ushirika na NATO.


Ambacho mfalme na washirika wake wa Ulaya walicho kitegemea ni kuwa baada ya Ukraine kuhamia EU kibaraka wao mpya ataweza kuifukuza Urusi kutoka Crimea. Ukraine iliipokea Crimea kutoka kwenye umoja wa USSR mwaka 1954, lakini bado Urusi ilikuwa na makubalino na serikali iliyo pinduliwa dhidi ya kuitumia Crimea kama moja ya vituo vyake mahususi vya kijeshi, hivyo kuinyakua Crimea kutoka Moscow ni kuizorotesha Urusi kijeshi na hii ikimaanisha pia kuongezeka kwa majeshi ya NATO kwenye mpaka wa Crimea na Urusi kama wanavyo fanya kwa Ukraine.


Alichokifanya Putin hakuna aliye tarajia. Siyo Mfalme Obama wala washirika wa Ulaya walio ona ‘movie’ ya Putin kama ingechezwa, Putin akainyakuwa Crimea na kumuambia mfalme na washirika wake kwamba ‘Dubu anapo taka kitu chake haombi’. Sasa inabidi mfalme na washirika wake wawatumie vibaraka wake walio kuwepo Ukraine kuendelea kumchokonoa Putin kama walivyo watumia waasi wa Libya dhidi ya Ghadafi na sasa dhidi Bashir al Assad. 

Lakini huu ni mchezo hatari Zaidi ambao Mfalme ameamua kuucheza, lakini ni kama hana ‘option’ eidha akubali kwamba ‘Usuper Power’ unahama kutoka kwake kwenda kwenye muungano mpya, au akatae na apambane na huo muungano mpya kitu ambacho tunajua si Marekani wala huo muungano mpya watakao nufaika na vita hivyo, na hapo itakuwa ni WWIII.

 Wote wananyuklia, hivyo ni wazi mwisho wa vita hivyo si Washington, wala EU, wala China, wala Urusi watakao kuwa ni super power, wote hawa watakuwa taabani kama wata savaivu vita hivyo ila uwezekano wa kufutika kabisa kwenye ndoto za utawala wa dunia ndiyo mkubwa Zaidi. Lakini Mfalme yupo tayari kuingia gharama yote hiyo kuhakikisha ‘Washington’ inabaki kuwa kiranja wa dunia.

Usisahau mfalme bado anafanya mchezo huo dhidi ya China kwa kuyasogeza majeshi yake karibu Zaidi na maeneo ambayo China inayotumia kutanua ushawishi wake wa kiuchumi. Kumbuka majeshi ya Marekani ambayo hayajaweza kuwa na umiliki wa 100% kwenye nchi kama Vietnam, Afighanstan au Iraq nchi ambazo ni ndogo na kwa pamoja zina idadi ya watu takribani milioni 157 ukilinganisha na nchi kama China na Urusi ambazo kwa pamoja zinatengeneza idadi ya watu bilioni 1.5. Ni vipi mfalme anafikiria kuwa ataweza kupambana na nchi hizi ikiwa nchi yake imeshindwa kufanya hivyo kwenye nchi ambazo zilikuwa ni dhaifu eidha kiuchumi, kijeshi au kisiasa na hazikuwa na silaha za nyuklia. 

Ameshindwa kuwatawala watu milioni 157 kwa vipindi vitatu tofauti itawezekana kutawala watu bilioni 1.5 kwa wakati mmoja?

Mfalme anaendelea kujichimbia kaburi lake mwenyewe, na kama hajaridhika na urefu ambao kaburi lake limefikia inabidi mrithi wake aje aendelee kulichimba. 

Huyu hawezi kuwa Trump ambaye amesema anataka kurudisha mahusiano mazuri ya Marekani na Urusi, bali ni mwana mama, malkia Hillary Clinton aliyesema ‘China na Urusi lazima zilipe gharama za kuendelea kumkingia Assad kifua’. Utawala wake utakuwa mbaya zaidi kushinda ule wa Mume wake, Bush wawili, na Mfalme Obama zote kwa pamoja.


Lakini kama Marekani atakubali kuwa siku zake za kukalia kiti cha enzi zinahesabika, na kwa upole anatakiwa atengeneze mazingira ya kumuachia mrithi mpya au kushirikiana na muungano mpya wa Urusi na China, hapo dunia itatulia, Franchise ugaidi itatoweka, tutaanza kuzijenga nchi zetu na kubadilisha mitaala ya somo la siasa na historia na dunia mpya yenye amani kidogo na kamuelekeo kazuri itaanza kujitokeza. 

Lakini ni mpaka Mfalme na mrithi wake walikubali hilo, na vipi watalikubali ikiwa makampuni na mashirika makubwa yaliyo nyuma yao wanatengeneza faida kubwa kwenye biashara ya vita na vifo?

Kwa uapnde mwingine, siyo China wala Urussi iliyo onesha kutishika na nguvu za kiuchumi au kijeshi alizo nazo Marekani. Wakati majeshi ya Muungano wa NATO na Marekani yalipokuwa yanaikodolea macho Urussi dhidi ya Ukraine, hakuwa Putin bali mfalme Obama ndiye aliye pepesa jicho na kurudi nyuma. Putin amepeleka majeshi ya kutosha, vifaa vya kijeshi na washauri wa kutosha kwenda Syria na hakujali kama mfalme Obama atafurahishwa na hilo ama la.

Putin amekiri wazi wazi kuwa Ulaya na Marekani ndiyo waliyo itengeneza ISIS. Putin amekiri hadharani kuwa baada ya mapinduzi ya Ukraine alisimamia yeye mwenye binafsi kuhakikisha unaokoa maisha ya raisi aliyepinduliwa wa Ukraine, na alifanya hivyo, tizama Documentary inayo kwenda kwa jina la  


Crimea. The Way Home. Documentary by Andrey Kondrashev



Dunia inajua kuwa ni Putin ndiye aliyewarudisha Marekani na washirika wake nyuma kwenye proxy war dhidi ya Bashir Al Assad, na kwamba juhudi yake imekuwa ni sababu ya Assad kubakia pale ama vinginevyo yange mkuta yaliyo wakuta Saddam na Ghadafi. 

Lakini ni Putini huyu aliyebadilisha mawazo ya rais wa Uturuki, kuna hati hati Uturuki ikaondoka kwenye EU na kuingia kwenye nguvu mpya inayozaliwa Moscow na Beijing.

Tunakumbuka si muda mrefu nyuma Uturuki iliitungua ndege ya kivita ya Urusi na Erdogan akasema hawezi kuomba msamaha kwa jambo hilo, Putin hakuwa na papara, akambana kidogo kwenye mambo ya kiuchumi na mahusiano ya kidiplomasia baina ya Uturuki na Urussi yakiendelea kudorora.


Ghafla bin vuu yakaja mapinduzi yaliyoshindwa Uturuki, na ghafla bin vuu tena Erdogan akaanza juhudi za kurejesha mahusiano yake na Urussi. Akaomba msamaha kwa kuidungua ndege ya kivita ya Urussi kitu ambacho alisema hatofanya, lakini akafunga na safari mpaka Moscow akakutana na Putin na kufanya ‘press conference’. 

Erdogan alikwenda Moscow kipindi ambacho nchi yake ipo kwenye kipindi kigumu baada ya kushindwa kwa mapinduzi yaliyo taka kumtoa madarakani.  Hii ni kuonesha Imani aliyokuwa nayo juu ya Putin, kwamba ataendelea kuwa salama. 

Kumbuka Assad naye alifanya hivyo, wakati nchi yake inaendelea kupambana na ‘magaidi’ wanao fadhiliwa na Marekani na EU aliiacha nchi yake na kwenda Moscow akakutana na Putin na akarudi Damskasi bila wasiwasi.


Erdogan na Putin wakakubaliana kufufua mahusiano yao ya kibiashara tena. Kumbuka Marekani na EU wanasisitiza juu ya kuendelea kuwepo kwa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Urrusi, na juu ya kuendelea kuitenga Urussi kimataifa. Halafu hapa mwanachama wa EU na rafiki wa Marekani anazungumza juu ya kufufua mahusiano ya kibiashara na Urussi. 

Lakini si hivyo tu Erdogan akakubaliana na Putin juu ya kushirikiana kwenye masuala ya NISHATI; Kitu ambacho EU na Marekani wanapambana masaa 24 kuhakikisha Putin haendelei kupata vyanzo vingine vya nishati na vile alivyo navyo anyang’anywe, lakini hapa Uturuki, ambaye ni mwanachama wa EU anasaini makubaliano na Putini amabyo yatamuongezea Putin nafasi ya kupata nishati zaidi, nafasi ya kuwa na nguvu zaidi.


Erdogan alikuwa mdau muhimu wa kuhakikisha kuwa Assad anaondolewa madarakani, silaha za waasi zilipitia kwake, waasi walimuuzia mafuta waliyo yapora Syria. EU na Marekani walitumia aridhi na anga la Urussi kuishambulia Syria na ndege ya kivita ya Urussi ilipo pita kwenye anga la Uturuki kwenda kuwashambulia waasi wa ISIS ilidunguliwa. 



Lakini kwenye mkutano huo walikubalina namna mpya ya kumaliza tatizo la Syria, na hapa tunazungumzia njia ambayo anaipendekeza Putin na siyo Mflame Obama wala washirika wake wa Ulaya. Ni wazi mpaka hapo Uturiki ni mwanachama jina wa EU lakini kambi yake inaonekana kuhamia Moscow.

Erdogan akazungumza kuwa wamekubaliana na Putin juu ushirikiano kwenye mambo ya ulinzi na teknolojia yake ikiwemo silaha za nyuklia. Bado hujapata picha nini kinaendelea hapa.

Kifupi ni kuwa Erdogan amewapa mgongo EU na Marekani. Ambacho hakijasemwa waziwazi ni marasi wote wawili ni kwanini kumekuwa na mabadiliko ya haraka hivyo? Kwanini Uturiki imebadilisha kambi na kwenda kwenye kambi ya mtu ambaye miezi kadhaa nyuma alikuwa ni adui yake? Lakini ‘uki-read between the line’ kwenye mazungumzo yao na waandishi wa habari ingawa si moja kwa moja lakini ni kama kuna mkono wa Urussi kwenye kushindwa kwa mapinduzi yale.




Inasemekana kwamba shirika la ujasusi la Uturiki lilipokea simu juu ya kuwepo kwa mpango huo. Ndugu wa raisi Erdogan akampatia kaka yake taarifa hizo naye akamthibitishia kuwa ni za kweli. Erdogan akahama makazi yake, kitu ambacho kilimuokoa kutoka kuuwawa na waasi baada ya mapinduzi kufanyika. Simu hiyo iliyo sababisha mapinduzi kushindwa, na kuokoa kichwa cha Erdogan inasemekana ilitokea Moscow. Baada ya mapinduzi kushindwa na Erdogan kuokoka, mtu wa kwanza kupiga simu ya kumpongeza na kumpa moyo Erdogan alikuwa ni Vladimir Putin.


Game over! Erdogan akaona mtu pekee anayeweza kusimama naye siyo mflame Obama wala EU ambao inasemekana wana mikono yao kwenye mapinduzi hayo yaliyo shindwa. Uturuki kubadilisha kambi ni bishara njema kwa Assad na mbaya kwa mfalme Obama, na ambaye atakeye mrithi Obama kazi yake inazidi kuwa ngumu kuliko ilivyo tarajiwa, na hawezi kuwa mtu ambaye anataka kurejesha mahusiano ya Washington na Moscow, kwani kufanya hivyo ni kuhalallisha kuanguka kwa Marekani kutoka kwenye kiti cha enzi, bali yule ambaye ataendelea kuwahakikishia big brother kwamba Marekani itaendelea kukikalia kiti hicho hata kwa gharama ya kupigana vita vya nyuklia, huyo ndiye atakeye mrithi Mfalme Obama, naye si mwingine ila ni mwanamama Hillary Clinton, ambaye amesema yupo tayari kutumia silaha nyuklia ikibidi kufanya hivyo ili kuyalinda maslahi ya Marekani.

NDIYO KWANZA KUMEKUCHA MTANANGE UNAENDELEA HAPA HAPA ....

No comments:

Post a Comment