Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, September 4, 2016

MALKIA HILLARY, MRITHI WA MFALME OBAMA Ep: 2


Tangu taifa la Marekani lilipoanzishwa, ni bidhaa mbili tu ndiyo limekuwa likiuza kote duniani, na hakuna yeyote aliye faida na bidhaa hiz Zaidi ya Marekani yenyewe. Bidhaa mbili tu ndiyo zimeifanya Marekani kuwa Super Power.


Marekani imekuwa na inaendelea kuuza makaratasi yanayo itwa ‘Dollar’ na kila nchi kwa usalama wake lazima iwe na makaratasi haya kwenye hazina yake ama ‘UCHUMI’  wa nch hiyo uonje joto ya jiwe.

Bidhaa ya pili inayouzwa na Marekani kwa faida kubwa sana inatwa ‘Demokrasia’ nchi lazima inunue biadhaa hiyo itake isitake. Bidhaa hii ‘definition’ yake ya ukweli anaijua ‘Washington’ mwenyewe, sababu unaweza kuwa ‘umeinunua’ bidhaa hii na unaitumia vizuri lakini Washington akasema ‘Hiri rijamaa harina Demokrasia’ akaja akakung’oa au unaweza hata usiwe na hiyo bidhaa lakini wala Washington hakufati, pia unaweza ukawa nayo na ukawa unaikanyaga kanyaga tu wala Washington asihangaike na wewe, lakini siku unataka kitu hapo ndani kwako, hiyo bidhaa inayo itwa ‘demokrasia’ lazima utaitafuta definition yake na hautaipata, maana ataingia kwa mlango huo huo.

Kwa kuiuza na kuifanyia ‘masoko’ biadhaa hiyo Marekani imezivama kijeshi nchi Zaidi ya 70 kote duniani, Marekani imejaribu kupindua nchi zisizo pungua 34 ambazo zilichaguliwa kihalali kupita hiyo bidhaa inayo itwa ‘demokrasia’, si hivyo tu kwa ajili ya kuuza bidhaa hiyo Marekani imejaribu kupindua bila mafanikio nchi zisizo pungua 19 ambazo nazo pia ni wateja wa hiyo bidhaa ya ‘demokrasia’, lakini kama nilivyo sema ni Marekani tu ndiyo inayo jua maana hasa ya ‘demokrasia’ kama ambavyo ni Marekani tu ndiyo inayo jua tafsiri ya ‘ugaidi’.


Yote haya ni lazima yafanyike ili kuhakikisha kuwa Marekani inabakia kuwa ‘the only super power’, lakini kama tulivyo ona kwenye post iliyo tanguliwa, wimbo huo unaweza ukashuka ‘chati’ soon, na Marekani iko tayari kuihatarisha Amani ya dunia, ikibidi kupigana vita vya kinyuklia na mataifa yenye silaha za nyuklia, kwa sababu tu, ‘wimbo’ huo usishuke chati. Huo wimbo unao itwa America the Only Super Power’ aka ‘Still No 1.’ Aka ‘Shoot first think later’ aka …, You got to love da song, it never got old!

Huo wimbo huo, ndiyo unao amua ni nani atakuwa mirithi wa Mflame Obama. Lazima awe ni mtu ambaye si tu anajua kuyaimba vizuri mashiri ya wimbo huo, lakini pia kucheza kwenye ‘beat’ yeyote ile utakayo pigwa …, unafikiri kati ya Hillary na Trump nani nazo sifa za kuimba na kucheza wimbo huo kwa wakati mmoja?


Tangu Marekani akae kwenye kiti hicho juhudi kubwa iliyo fanya ni kuhakikisha kuwa inabakia hapo basi. Marekani ndiyo nchi pekee yanye vituo vya kijeshi kote ulimwenguni kuliko nchi nyingine yeyote, na lengo la vya vituo hivyo ni kuhakikisha Marekani inabakia, Still No 1. Wakati Uingereza ilipokuwa Super Power na ikiitawala dunia, mbali na kufanya wizi kwenye makoloni yake na unyonyaji, lakini kidogo walitengeneza miundo mbinu ya kuyafanya makoloni yake yajitutumue kwenye Nyanja mbalimbali, tuliliona hili pia wakati Mjerumani ni mtawala wa Afrika Mashariki. 

Lakini Uncle Sam, yuko tofauti kabisa, yeye anabomoa na kuvunja vunja hata vile vichache na duni vilivyo achwa na wenzake, na kuiacha nchi hoi, dhoofu, taabani inayo hesabu siku za kuishi. Lakini ikiwa lengo ni kuhakikisha anabaki kwenye hicho kiti milele, basi njia na utaratibu anao utumia Marekani hauwezi kuepukika, sababu taifa lolote litakalo achiwa listawi, au litakalo kuwa ni uchochoro wa taifa jingine kustawi, taifa hilo lazima lipigishwe magoti na kuomba msamaha, sababu ni tishio kwa Marekani.


Barack Obama aliahidi ‘Change’ kwenye kampeni zake. Alipo pewa usukani, jiulize nani alipewa nafasi muhimu kwa ajili ya hiyo, ‘Change’? Alikuwa ni Hillary Rodham Clinton, Secretary of State (SS), mara tu baada ya Hillary kupata shavu hilo, binafsi nilijiambia, hapa rais siyo Obama, rais ni Hillary Clinton, na habari ya ‘change’ ikawa ni kitabu kilicho fungwa na kutupwa kapuni, kitabu cha zamani tulicho kuwa tunasomewa na Bush II, kikarudishwa mezani na mwana mama akaanza kutiririka mistari. Unaijua kazi yake ya kwanza aliyo ifanya kama SS?


Marekani ni siasa za mambo ya nje, zingine ni blah blah tu. Unataka kuwa rais wa Marekani tuambie utaifanyia nini Marekani kwenye siasa za mambo ya nje; full stop. Siasa za mambo ya ndani zitafanywa na raia wa Marekani wenyewe, kama alivyo sema Kennedy, ‘ … ask what YOU can do for your country.’ Hillary Clinton inaonekana wimbo wa ‘still no 1’ anaumudu kuimba na kuucheza.


Ilikuwa Juni 28, 2009 jeshi lenye silaha lilimpindua raisi aliyeingia madarakani kwa kupigiwa kura, raisi wa Honduras, Manuel Zelaya. Japo nchi ya Hondoras imeinunua ile bidhaa ‘adimu’ inayo itwa ‘demokrasia’, lakini nabii na muuzaji wa bidhaa hiyo, mfalme wa dunia, na serikali yake, waliuchuna kama vile hakuna kilicho tokea, mteja wao kapata matatizo baada ya kutumia bidhaa yao, lakini ‘service line’ zao hazikuwa zikipatikana katika kumsaidia bwana Manuel Zelaya. Hondurus ni moja ya nchi ambazo serikali ya mfalme imeweka majeshi yake yenye nguvu hapo, ingetumia tu jeshi lake na kuwaondoa waliofanya mapinduzi na kumrudisha Zelaya madarakani, lakini haikufanya hivyo.


Ispokuwa mapinduzi hayo Bi. Hillary aliyaita ‘Smart Power’. Lakini ni mapema mwezi huo kabla ya mapinduzi Bi. Hillary alikuwa kwenye ndege na kutua kwenye nchi ya Honduras na kuhudhuria kikao cha mwaka cha Oraganization of American State (OAS) kikiwa na ajenda kuu; ‘Namna ya kuzuia Cuba isiondolewe vikwanzo’ vilivyofikisha umri wa miaka 47 tangu kuwekwa. Vikwanzao ambavyo wengi wa wanachma wa OAS vinaviona vikwanzo hivyo kama ni kumbukumbu iliyo pitwa na wakati ya Cold War. Nchi kama Venezuela, Bolivia, na Ecudor wanaviona vikwanzo hivyo kama mfano wa wazi wazi juu ya sera za kibabe za Marekani.

Katika kusaidia nchi yake Manuel Zelaya ilivuka mstari mwekundu uliowekwa na Washington. Alikuja na utaratibu wenye tija juu ya kulimaliza  tatizo la dawa za kulevyia nchini mwake, mwaka 2007 Zelaya alikuwa ni raisi wa kwanza kwenda Cuba baada ya miaka 46 na akakutana na Raul Castro na kuweka mipango ya kidiplomasia na kuiendeleza nchi yake, mbaya zaidi akajiunga na kile kinacho fahamika Alternativa Bolivariana para los Pueblos de Nuestra América

 (ALBA),  ambayo ilundwa 2004 na Cuba ikishirikiana na Venezuela kupitia maono ya Hugo Chavez. Washington hawakupendezwa na haya yote, na Hillary alipokuwepo hapo wakati wa mkutano wa OAS hakuwa amemtizama mwenyeji wake huyo kwa jicho zuri, na mara baada ya Hillary kuondoka, haikuchukua muda na serikali hiyo ya Zelaya ikaondolewa, na Hillary akaita mapinduzi hayo ‘Smart Power.’

Utakutana na Hillary kwenye kesi ya Libya akiimba na kucheza wimbo wa ‘Still No 1.’ Inajulikana sasa kote ulimwenguni kuwa walioipindua serikali ya Ghadaffi walikuwa ni mamluki walio pigana vita kwa niaba ya Marekani, lakini Zaidi imefahamika kuwa Hillary kama SS na ofisi ilishughulika vilivyo kufanikisha hilo. 

NATO waliruhusu silaha za aina kwa aina zikishushwa kwenye ndege kuelekea kwa waasi. Kama nilivyo sema awali, baada ya Hillary kupewa nafasi ya SS, nilihisi Obama hatakuwa na sauti kumshinda malkia huyu wa vita, na ndivyo ilivyo kuwa, mamuzi mazito ya kuendelea kuwapa waasi silaha, fedha, hifadhi na taarifa za kiitelejinsia dhidi ya serikali ya Ghadaffi yaliamuliwa na Hillary Clinton. (http://www.newsmax.com/World/GlobalTalk/Moammar-Gadhafi-Mohammed-Ismael-Hillary-Clinton-qaida/2015/02/26/id/626958/ )

Itaendelea Inshallah ....

No comments:

Post a Comment