Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Monday, August 15, 2016

MFALME OBAMA: Ep 4 finito



Siasa kama ulivyo mchezo wowote kuna wachezaji, kuna wachezeshaji na bila kusahau wachezeshwaji, mara nyingi wachezeshaji katika mchezo huu ndiyo wachezaji, na wale ambao tunadhani ni wachezaji ndiyo wachezeshwaji. 



Brzezinski na timu yake nyuma ya mapazia ya vyombo vya habari ndiyo walikuwa wachezaji na Obama mbele ya kamera za vyombo vya habari alionekana kama mchezaji lakini kwa hakika alikuwa mchezeshwaji kama mwana sesere aliyefungwa kamba kichwani, mikononi na miguuni na alivichezesha viungo hivyo kila kamba hizo zilipovutwa, Brzezinkis ndiye mkono ulioshikilia kamba hizo.

Mpango wa Brzezinski kupitia kwa Obama ni kutengeneza mitandao ya kisiasa ambayo itaweza kuiporomosha Urusi, utakumbuka mpango wake huu ulianza tangu wakati wa Jimmy Carter ambapo yeye alikuwa ni msimamizi wa siasa za mambo ya nje za Marekani ambapo akapelekea kuundwa kwa Taliban ambao waliifanya kazi hii vizuri sana nyuma ya kile kilichoitwa ‘Holy War’, lakini safari hii mpango huu hauta ilenga Urusi peke yake bali pia China nayo itaingizwa ndani ya nyumba. 

Ukiitizama Urusi Brzezinki amekuwa makini akisambaza propaganda zinazo lenga kuchora msatari wa kuto kuelewana baina ya Umoja wa Ulaya na Urusi kupitia Kosovo ambayo mustakabali wake wa kisiasa unaonekana kuachwa katika hali ya utata kwa makusudi ili Moscow iweze kunyoeshewa vidole kwa aina yoyote ya uwozo unaotokea hapo.

Lakini kwanza Obama anatakiwa kuwatoa wa China nje ya Afrika. Wachina ambao wanachukuliwa kama taifa linalo jitahidi kulisaidia bara hili kiviwanda na kulipatia nafasi za kusimamisha uchumi wake kwa njia mbalimbali ikiwemo mgawanyo sawa wa kimapato katika miradi mbalimbali hali hii ni kikwazo kikubwa kwa mawakala wa fremasonry yaani International Monetary Fund na World Bank ambao wao nia yao ni kutonyonya mpaka tone la mwisho la damu yetu.

 Hata hivyo Brzezinki ana picha kubwa zaidi juu ya hili la kuwafukuza wa China nje ya Afrika. Kupitia kwa Kennedy Mweusi Brzezinki anampango wa kuwapora wachina kila aina ya rasilimali wanayonunua kutoka Afrika, ikiwemo mafuta, gesi za asili, madini na kila kile ambacho kimebakia kama makombo baada ya vile walivyo pora wakati wa ukoloni, baada ya ukoloni na kwenye ukoloni mambo leo. 

Mpango ulio chaguliwa juu ya hili ni njia ile ile iliyopendekezwa na mababu wa fremason, Priory of Sion kwenye kile walichokiita protocal of sion, njia hiyo ni kuzivunja vunja nchi za ki Afrika kupitia vita vya wenyewe kwa wenyewe kitu kitakacho wakimbiza wa China nje ya Afrika. Na hili litasimamiwa vilivyo na kile kinachoitwa Africom ambayo imeundwa na Marekani.

Kupitia mpango wa Brzezinki Afrika itakuwa ni uwanja wa mapambano baina ya Marekani na China, na maanisha mapambano ya kiuchumi na siasa, lakini mapambano ya bunduki itakuwa ni baina ya wa Afrika sisi kwa sisi. Afrika itawaka moto, mauwaji ya watu chini ya jangwa la sahara yatakuwa ya kutisha. CIA wataingilia kati na hata kuingilia siasa za nchi za ndani za Afrika kwa uwazi kabisa nyuma ya kile kitakachoitwa vita vya ugaidi ambavyo wakala wake ni Al-Qaeda ambao kwa sasa kutokana na taarifa za vyombo vya habari za kimagharibi na hata vya hapa Afrka Al-Qaeda tayari wako ndani ya nyumba, wako Afrka, Algeria na Tunisia na kazi zao chafu zimeshaanza kuonekana, kumbuka Algeria ni moja wapo ya nchi zinazo zalisha mafuta kwa wingi Afrika. 


Utakumbuka Al-Qaedah ilikuwa ikidhaminiwa na CIA kupitia hela za dawa za kulevyia wakati Taleban wakidhaminiwa na Brzezinki na mtandao wake wa Trilateral Commission. Hakuna Holy War wala Jihadi; kama alivyo Kennedy Mweusi vikundi hivyi, ni sawa na mwanasesere anayechezeshwa kwa kamba zilizoshikiliwa na bwana wakubwa hawa. Moto umeshawaka Nigeria moja ya wazalishaji wakubwa wa Mafuta Afrika.

 (sehemu hiyo hapo juu niliandika muda kabla moto haujawaka Afrika, lakini yametokea, moto umewaka, serikali zimepinduliwa, wachina wamekimbia, illuminati wanabeba chao na waafrika bado tunapigana risasi kwa faida yao)

Uingereza na Israeli kwa pamoja kwa miongo kadhaa wamekuwa wakiivunja vunja Sudan, lakini leo picha iliyoko Darfur inatumiwa na Marekani pamoja na Uingereza kama kisingizio cha kuitawalia nchi hiyo mambo yake nyuma ya kile wanacho tuambia  kuwa kuna uvunjaji mkubwa wa haki za binaadam katika eneo hilo.

Kusema Sudan inakiuka haki za binaadam hakuhusiani kabisa na mpango wa kuondo zahama hilo kama vyombo vya habari vya kimagharibi na mawakala wao wanavyo dai lakini zadi inahusiana na mpango wa kukata 7% ya mafuta ya China ambayo yanatoka Sudan. Habari zinasambazwa kwa kasi kuwa shughuli za kiuchumi za China nchini Sudan zinazorotesha kwa kiasi kikubwa utaratibu wa kuondoa baa la njaa na tatizo la mafuta duniani.[1] 


Aina hii ya propaganda muda si mrefu inapokelewa na vikundi vinavyo jiita vinasimamia haki za binaadam ambavyo ni vikundi vya watu wale wale katika sura tofauti lakini nyuma ya ajenda ileile.
Nchi yoyote duniani ambayo kwa namna moja ama nyingine inanufaika kiuchumi na au kiviwanda kutokana na ushirika wake na China na kwa maneno mengine China nayo inajijenga misuli yake ya kiuchumi na viwanda kutokana na miradi yake mbalimbali iliyomo nchini humo, nchi hiyo haiwezi kuepuka mpango huo wa Brzezinki.


 Mfano ni Burma na Venezuela ambazo historia ya maendeleo yao kiuchumi haijakamilika bila kuitaja China. Shughuli inayo endelea Pakistan ambapo Kennedy mweusi amekiri yuko tayari kuipiga bomu la nyuklia Pakistani endapo itaonekana kushindwa kupambana na Taliban na Al-Qaedah, shughuli hiyo haina lolote kwenye kile kinachosemwa vita dhidi ya ugaidi bali zaidi, ni vita vya kuizorotesha nchi hiyo ambay muda mrefu imekuwa mshirika wa China,vurugu hizo ni za kuwakimbiza wa China kutoka humo. 

Tunaona siasa za vuta ni kuvute baina ya Pakistani na Marekani sasa.

China itakapo tengwa na kupokonywa washiriki wake wote wa kiuchumi, na kunyimwa uwezekano wowote wa kupata mafuta na malighafi zozote kutoka nje ya China, hatua itakayo fuata ni kuizorotesha serikali ya China na wakati huo huo kuipambanisha na Urusi, suala la kuizorotesha serikali hiyo tumelioa linavyoshika kasi kupitia Tibet kwa kiongozi wao wa kiroho Dalai Lama.  

Lakini kwa vile Urusi na China zote zinafahamu kuhusu njama hizi za Brzezinki mchezo  unakuwa mgumu,na hasa pale utakapo jenga mazingira ya kuonganisha mahusiano yenye chuki ya Urisi na China dhidi ya Marekani na washirika wake wapya. Upande mwingine wa shilingi mwana sesere huyu atakuwa na kazi ya kuiunganisha Iran na Syria na kwa pamoja zisimame kuwapinga wa China na wa Rusi.[2]

(Mpango huo wa kuionganisha Iran na Syria dhidi ya Urusi umekwama baada ya Assad kushindikana kutolewa madarakani, ingawa kwa upande wa Iran Kibaraka amefanikiwa hata kuwaruhusu waendelee na mradi wa nyuklia wenye manufaa kwa binadam, na kuziruhusu asset zilizokuwa zimezuiliwa na Marekani zirudi Iran, lakini bado ni pagumu sababu Muiran na Mrusi wanaujua mchezo mzima mwisho wake ni wapi)

Muandishi wa kitabu cha Barack H. Obama:The Unauthorised Biography anajaribu kutupa taswira ya mchezo mzima kuhusu Iran na Marekani kuanzisha ushirikiano wa kiuchumi na kisiasa dhidi ya Urusi na China namna utakavyo kwenda, haya ndiyo maoni yake,

Iran itashawishiwa wawe rafiki na Marekani kwa ahadi ya kupewa nguvu sawa na Marekani ndani ya Mashariki ya kati, si-m-China wala m Rusi, si m Pakistani wala mu Egypt atakaye kuwa na sauti ila Iran mshirika wake mpya, Marekani. Rasilimali ngapi za Iran zinazozuiliwa na Marekani kwa muda wote huo sasa zinafikia thamani ya dola bilioni mia na zaidi, vipi unaonaje Iran akipewa na ahadi hii ya kupata aseti zake hizo. 

Unaonaje ahadi ya kutolewa kwenye listi ya nchi zinazo dhamini ugaidi na vikundi vyake. Bila kuwasahau washirika wakubwa wa Iran Hezbollah kuwa na wao watapata chochote. Lakini hayo ni mambo madogo tu, unaonaje ishu ya nuklia kama alivyo fanya Bush Baba alimkabidhi Saddam silaha nyuma ya mapazia halafu Bush mwana akaja kuzidai mbele ya hadhara, unaonaje Iran akapewa ruhusa ya kuendeleza mradi wake huo nyuma ya mapazia.


Tunaweza kukupatia teknolojia bora kushinda hii uliyonayo, silaha bora na mabomu ambayo unaweza kuyarusha kokote pale duniani na yakafika Moscow, sema tu kama ndiyo hilo unalo taka, sasa hivi tutakupatia. Ujue tu kwamba adui yako mbaya kuliko wote hajawahi kuwa Marekani bali Urusi.

(I STILL WONDER HOW DOES THIS GUY COME TO KNOW THIS,NI KAMA ALIKUWA ANAANDIKA SCRIPT YA MOVIE YA OBAMA, SABABU KAICHEZA HIVYO HIVYO)

 Si unakumbuka namna walivyo kufanya walipo chukua baadhi ya maaeneo yako wakati wa WWII, ule ulikuwa ni uharibifu mkubwa. Sisi hatujawahi kufanya kitu kama hicho na wala hatuta jaribu kufanya hivyo. 

Tunachotaka sisi ni kuwa marafiki  na kukusaidia kuwa na nguvu za kutosha kupambana na adui yako wa kweli, Moscow... kama unavyo fahamu muheshimiwa rais wanachi wako wanaichukia Urusi kuliko wanavyo ichukia Marekani na Uingereza na wakati wowote utakapo wachukia warusi ujue unawaridhisha watu wako na sisi tutakusaidia... sema tu unataka nini... unaonaje kuhusu manuari, tukakupatia manuari inayokwenda mpaka bandari za kusini ya Urusi zikiwa na mizinga ya kinuklia, hapo utawazuia Urusi wasiendelee kukuibia mafuta yako kutoka kwenye bahari ya Caspian, na kama wakijaribu kujibu mapigo usiwe na hofu tutakuwepo kukupa sapoti. 

Fikiri mwenyewe kuhusu hili. Halafu kuna hawa wa China, kwa nini unapenda kufanya nao biashara sana, muda si mrefu watakuweka kwenye mfuko wao wa suruali yao kutokana na jinsi unavyo wauzia, halafu tunajua hulipendi hilo... bora ufanye biashara na sisi hata kama ni kwa dola. Tunachotaka ni kuwa ufahamu kwamba sisi ni wakweli vibaya mno. [3]

Jamaa huyu hayuko mbali sana na ukweli kwa sababu ni mchezo huu huu aliufanya Brzezinki kwa wa Afighanistan kupitia mujaheedina ambao ni zao la mpango wake, akawa pambanisha na Urusi na kilichobakia hapo ni historia, alifanya hivyo kupitia kwa Jimmy Carter, leo mchezo uleule wa mtu yule yule utafanyika kupitia kwa Obama. Halafu wa Syria nao watafatwa, watashikwa kama walivyo shikwa kwenye Gulf War ya mwaka 1991. Lengo si kuwapambanisha wa Iran na Syria bali kuwa unganisha dhidi ya China na Urusi. 


Viongozi wote wa nchi za viwanda kama vile wanachama wa G8, vibaraka wao wanao patikana katika ngazi tofauti za uongozi kwenye nchi mbalimbali duniani, vikundi vya waasi na vikundi vya kigaidi, wote kwa pamoja wanashirikiana juu ya kufanikisha ajenda yao ya kishetani, wanafanya kazi kama watu tofauti wenye mitazamo na maono yanayo pingana kwenye majukwaa ya kisiasa, lakini juu kabisa kileleni wanaongoza na ajenda moja, ajenda ya New World Order. Ambalo walimwengu tunaweza kujiuliza ni; wachache wangapi katika viongozi wetu hawako kwenye mfuko wa Illuminati?

Mkono wa Illuminat umekuwa mrefu kiasi cha kuweza kuichagulia nchi yoyote duniani kiongozi na kuwapangia sera za kiutawala. Haijalishi kama angeshinda McCain badala ya Obama jibu lingekuwa lile lile kwani anaye tawala si Obama bali asasi za siri, mashirika na makampuni makubwa nyuma ya mapazia. Kama unataka kujifanya kuwa wewe ni mchezaji badala ya mchezeshwaji unaondolewa kwenye systeam, kama wakina Kennedy, Ali Bhuto wa Pakistan, Aldo Moro wa Italy na wengine wengi.

Fahamu kuwa kila vita vikubwa vinavyotokea, vilivyotokea, mapinduzi ya kisiasa, anguko la kiuchumi, magonjwa ambayo hayahusiani chochote na maumbile asilia kama vile Ukimwi, Ebola, Swine Flu na mengine yatakayo kuja, ni kazi iliyo pangwa vizuri na kuetekelezwa na watu wale wale ambao wako mstari wa mbele kujifanya wanataka kufanya tofauti na hivyo.
Unajua ni kwa nini unavutika na makala za namna hii?

Unavutika nazo kwa sababu unatafuta jibu la swali ambalo unadhania hakuna aliyetayari kukupatia jibu lake. Huna maelezo yakutosha juu ya unacho taka ispokuwa unahisi kipo. Unahisi kuna kitu ambacho hakipo  sawa hapa duniani. Kama ugonjwa hisia hizo zinakunyima utulivu. Hisia hizo ndizo zinazo kufanya uvutike na makala za namna hii, kuna kitu ambacho hakiko sawa.

Kila mahala, kila kona nguvu hizi za muungano usio mtakatifu zimetapakaa. Hata sasa mahali ulipo zipo. Unaziona unapo tizama kupitia dirishani, ukitembea, ukiwasha luninga yako. Unazihisi nguvu hizo za kimasonia unapokwenda kazini, unapokwenda kwenye nyumba ya ibada, na hata unapolipa kodi yako kwa serikali ambao mara zote ni vibaraka na wanaseserere wa big brother, nguvu hizo ni dunia iliyo vutwa mbele ya macho yako na kuyapofua kiasi cha kutoona ukweli.

Kutoona ukweli? Ukweli ni upi?

Ukweli ni kuwa wewe ni mtumwa wa ulimwengu wa kimasonia. Kama walivyo watu wengine, umezaliwa kwenye gereza hili lenye uzio usio onekana, harakati za kila siku za kile kinachoitwa kutafuta maisha zimeyapofua macho yako usione minyororo na kuta nene zinazokufunga kifikra, kimaumbile na kiroho, u mtumwa wewe. Bahati mbaya hakuna wa kukuonesha nguvu hizo za kishetani zimejikita kiasi gani, unapaswa uwone mwenyewe, ni nacho jaribu kufanya ni kukuonesha njia ya kwenda kujikomboa na kuwa huru, na kuonesha mlango na wewe ndiye unayepaswa kupita kwenye mlango huo.
Jiandae na posti ya 'MALKIA' atakaye mrithi 'MFLAME' Obama ... tchao



[1] Tarpley, Webster Griffin Barack H. Obama: the unauthorized biography / Webster Griffin Tarpley ISBN-13: 978-0-930852-91-7 (Digital), 978-0-930852-81-8 (Offset edition) Uk 376
[2] Ibid
[3] Ibid

1 comment: