Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Monday, August 8, 2016

MFALME OBAMA: Ep 3



The First Gay President, ndiyo habari iliyo kuwa imebeba jaridal la Newsweek, muandishi alijikita zaidi kwenye mtazamo wa Obama juu ya ndoa za jinsia moja, hata hivyo  habari zenyewe zilikuwa ni kama moshi kwenye moto unao waka chini. 



Ni kweli Obama ni shoga au amepata kujihusisha na vitendo hivyo? Kiukweli kabisa hayo ni maisha binafsi ya Obama na hayana umuhimu au haja ya kuyaandika kwenye posti hii, hata hivyo hilo lingekuwa sawa endapo Obama angekuwa ni mtu wa kawaida katika jamii, lakini jukumu lililopo kwenye mabega yake kama raisi wa taifa la Marekani, taifa  ambalo sina haja ya kukuelezea nguvu za ushawishi wake katika kitu au  jambo lolote lile dhidi ya mataifa mengine. 

Hapana shaka maisha binafsi ya mtu yoyote atakaye kalia kiti cha juu cha serikali hiyo kama binadam yatakuwa na ushawishi juu ya namna gani serikali yake iwe, na hapo ndipo tunapoona ipo haja ya kuandika japo kwa uchache kukupa mwanga juu ya kile kinacho wezwa kufanywa na mtu huyu, yatakapo tokea usishangae.

Larry Sinclair amekuja na kitabu alicho kiita , “ BARACK OBAMA & LARRY SINCLAIR: Cocaine, Sex, Lies & Murder?”, Je inawezekana Sinclair alikiandika kitabu hicho kwa ajili ya kumkashifu Obama kisiasa na kumuondolea uwezekano wa kushinda kiti cha uraisi kwa Marekani?

Larry mwenyewe anasema ni kitu gani kilicho msukuma yeye kuandika kitabu hicho,

“Kilicho nishawishi mimi kuliweka hadharani jambo hili ni hamu yangu ya kupenda kumuona mgombea uraisi (Obama) akiwa mkweli na muwazi. Sikutaka jambo la ngono liwe hadharani. Lakini ni muhimu kwa mgombea kuwa mkweli juu ya utumiaji wake wa dawa za kulevyia mwishoni mwa miaka ya 1999.”[1]



Obama mwenyewe alikiri juu ya kutumia kwake kwa bangi na dawa za kulevyia wakati akiwa high school lakini si baada ya hapo. Kilicho msukuma  Sinclair kutokana na maelezo yake ni kwanini mgombea huyu aseme alitumia vitu hivyo wakati akiwa High School wakati kumbe mwishoni mwa mwaka 1999 alikuwa bado anatumia? Kwenye kitabu chake alicho kiita Dreams From My Father, Obama amekiri kuvuta bangi akiwa High School lakini hajasema ni lini aliacha, na mpaka sasa anajulikana kama mvutaji sigara.

Wayne Madsen mchunguzi na muandishi alikuja na taarifa nzito kuwa Obama ni mwanachama wa kikundi cha mashoga. Madsen akaripoti pia kuhusu vitendo vya kishoga baina ya  Obama na wanaume wengine, akiwemo Doanald Young, muongozaji wa kwaya kwenye kanisa  la Chicago ambalo Obama ni mwanachama kwa miaka 20.[2]

Mahusiano yanayo ambatana na vitendo vya kishoga baina ya Obama na Young yalithibitishwa na Larry Sinclair, ambaye naye alikiri kufanya vitendo hivyo vya kishoga na Obama ikiwemo pia kutumia dawa za kulevyia aina za kokeni.
Pia kulikuwa na mashoga wengine wawili kwenye kanisa la Jeremy Wright linalo fahamika kama Trinity United Church of Christ ambalo Obama ni mwanachama kwa miaka 20. Mashoga hao ni Larry Bland na Nate Spencer. 

Mwishoni mwa mwaka 2007 wakati Obama anaanza mchakamchaka wa kugombea uraisi kwa tiketi ya chama cha Democrat, ndani ya wiki 6 tu, mashoga hawa wote watatu walipatikana wamekufa. Bland alipigwa risasi Novemba 17, 2007, Young naye alipigwa risasi Disemba 24, 2007. Spencer alitangazwa amekufa kwa Nimonia na HIV Disemba 26, 2007.[3]

Inasemekana watu hawa ilibidi wauwawe ili kuficha uchafu wa Obama ambao ungemuhatarishia nafasi yake ya kuwa raisi wa taifa hilo kubwa duniani.

Wayne Madsen anasema kuwa Barack Obama na Rahm Emanuel wote hawa wawili walikuwa watembeleaji wakubwa wa ‘The Down Low Club’ na ‘Man’s Country’ pamoja na ‘purple Hotel’ sehemu zote hizi hutumika kwa vitendo vya kishoga pamoja na utumiaji wa dawa za kulevyia. Kuna mashoga wanao jiuza sehemu hizo, kuna vyumba maalum kwa ajili ya kufanyia starehe na mashoga. 

Lakini Obama na Emanuel walizitembelea sehemu hizi kila mtu kwa wakati wake na siyo pamoja.

Sinclair amedai kufanya vitendo vya kishoga na Obama mara mbili, na wakati mwingine wakishirikiana naye kwenye utumiaji wa dawa za kulevyia ambazo Obama alilipa dola 250 kwa Sinclair kwenda kuleta dawa hizo, hapo ni mwishoni mwa miaka ya 1999. Maelezo haya ya Sinlcair yanachukuliwa kuwa ni ya ukweli na si yakutunga kutokana na kile kinacho fahamika kama Reverse Speech.

Hii Reverse Speech ni aina ya utaratibu unao tumiwa na mtu kutoa taarifa zilizo hifadhiwa kwenye ubongo wake kipindi cha nyuma. Kwenye ubongo kuna sehemu ya Conscious na Subconscious. Kwenye Conscious level vitu hotokea na kurikodiwa kwa idhini ya muhusika mwenyewe, lakini si kwenye Subconscious Level, hapa kitu hakikatizi, ni kama black hole, uwe macho au umelala, unajitambua au hujitambui chochote kitakacho katiza kupitia mifumo yako ya fahamu kitarikodiwa kwenye  Subconscious Level na hakito futika milele.

 David John Oates mtu kutoka Australia aliyekuja na utaratibu huu, mgunduzi wa njia hii ya Reverse Speech ni mtu aliye bobea kwenye fani ya  Hypnotherapist. Na njia yake hii imekuwa ikitumiwa hata na wasimamiaji wa sharia katika kumpata mhalifu na anasema kwa miaka 24 tangu njia hii ya Reverse Speech ianze kutumika haijapata hata mara moja kwa mtu kurikodiwa uwongo kwenye Reverse Speech.

 ‘Haiwezekani kurikodi uwongo,’ anasema Oates ambaye amerikodi makumi elfu ya watu kwa kutumia njia hii. Kama Sinclair angekuwa ana danganya basi uwongo huo ungeonekana kwani Reverse Speech ni kama kuirudisha siku nyuma, ni kama kurudi na kuiyona jana, utasema kila kitu kilicho katiza kwenye Subconscious Level.

Hadithi hii yenye kiza kuhusu maisha ya Obama ni vigumu kufutika. Mama yake na Young alifanya mahojiano na ‘The Globe’, alisema mtu aliye muuwa mtoto wake ni yule ambaye anaye jaribu kumlinda Obama na aibu ya ushoga kutokana na kuwa Doanald Young alikuwa na mahusiano ya kingono na Obama. Mwili wa Young ulipatikana ukiwa na mashimo ya risasi katika namna ambayo inawezwa kuitwa ni assassination-style

Mama huyo Norma Jean Young aliliambia ‘The Globe’ kuwa mwanaye huyo alikuwa ni shoga wa wazi wazi na alikuwa hafichi hilo na Obama alikuwa ni rafiki yake wa karibu. Mama huyo anasema kuwa Chicago Police Department hawaja weka uzito katika kumtafuta muuwaji wa mwanae. Naye mke wa marehemu ambaye naye alikuwa ni polisi kwenye kituo hicho cha Chicago anasema kuwa , “kuna la zaidi kwenye hii hadithi, naamini kuwa wanamkinga mtu flani au wanamlinda mtu flani.”[4]

Zaidi kuhusiana na hadithi hii kajitafutie mwenyewe kitabu hicho cha Larry Sinclair na mwisho wa siku huenda utakawa pamoja kwenye mstari wa mapambano.

Mbali na kampeni yake ya hope, change na believe nini tunachoweza kukitarajia kwenye mfumo wake wa uongozi. Watu wengi wanakiona kile ambacho wanachotaka kukiona kuhusu Obama, wanayaona matumaini na mabadiliko, picha ya Obama ni vile unavyo taka yeye awe na au afanye. 

Matumaini ya wengi ni kuwa Obama si mpenda vita, hakubaliani na uvamizi wa Iraq uliofanywa na freemason mwenzake. Lakini ndani ya White House hatofautiani na Bush kiutendaji, anahitaji wanajeshi zaidi wakiwemo wale kutoka European Union wapelekwe Afighanistan. 

Amesema atatumia nguvu za kijeshi kuizuia Iran kuendeleza mradi wake wa kinyuklia. Amemchagua Hilary Clinton kuwa katibu mkuu wa nchi ambaye ni mwanachama wa asasi za siri vilivyo ndani ya mtandao wa Babylon Brotherhood, vikundi hivyo ni Bilderberg Group, Trilateral Commission, na Council on Foreign Relation. Katibu wake wa ulinzi ni Robert Gate ambaye naye ni mwanachama wa asasi za siri vya Bilderberg Group na Council on Foreign Relation.

Tunapozidi kulikodolea macho jopo lake la utendaji tunazidi kupata mashaka na mteule huyu. Kwenye timu yake hiyo kuna mtu anaye itwa Zbigniew Brzezinski ambaye alikuwa ni mshauri wa taifa hilo katika uongozi wa Jimmy Carter na ambaye pia ni miongoni mwa waanzilishi wa asasi ya siri kinachoitwa Trilateral Commission kwa ushirikiano na David Rockefeller. 

Jamaa huyu, Brzezinski alikiri hadharani kuwa alidhamini na kutoa mafunzo kwa watu ambao leo wanajulikana kama ‘magaidi’ nchini Afighanistani ili kupinga uatawala wa Kisovieti uliokuwa ukiishikilia Kabul kwenye miaka ya mwishoni mwa 1970. Wapigania uhuru hao wa Brzezinski walikuja kujulikana kama ‘Mujahideen’ na baadae wakaunda Taliban na kisha kile kinacho julikana kama Al-Qaeda.

 Huyu ndiye mtu aliye nyuma ya kijana anayesema hapendi vita. Lakini juu ya yote Obama alikuwa ni mwanafunzi wa Brzezinski katika chuo cha Culombia wakati huo Zbigniew Brzezinski a.k.a ‘Zbig’ akiwa ni profesa kwenye chuo hicho akifundisha somo lihusianalo na Soviet na pia anadhaniwa kama hakuwa CIA basi alikuwa ni mtu wa karibu mno na CIA kuliko kitu chochote kile[5]

Akiwa mshauri wa Carter ‘Zbig’ alihusika vilivyo kuidondosha USSR, leo yupo nyumba moja na mwanafunzi wake kwa ajili ya kumalizia kazi aliyoianza wakati wa uongozi wa Carter.

Hata hivyo si kweli wanavyo tuambia kuwa kijana huyu mweusi si mpenda vita, hatuja sahau alipokuwa anafanya kampeni kuwania nafasi ya useneta kwenye jimbo la Illinois mwaka 2003 na 2004 Obama alimpinga Bush kwenye mpango wa kuivamia Iraq. Lakini mwaka 2005 na 2006 Obama alikuwa ni tumaini la Bush kwenye vita hivyo. 

Baada ya kuchukua ofisi hiyo Januari 2005 alipigia kura mapendekezo manne tofauti ya kivita yanayo gharimu dola bilioni 300. June mwaka 2006, Obama alipiga kura ya NO kwa John F. Kerry kupinga pendekezo lake la kutaka majeshi ya Marekani ya punguzwe kutoka Iraq.[6]

Leo anadai wanajeshi zaidi wapelekwe Afighanistan kupambana na watu ambao Brzezinski kawatengeneza na kuwaandaa. Hotuba za Obama zimeonekana pia kwa kiasi kikubwa kuegemea na kutegemea maandishi kutoka kwenye vitabu vya Zbigniwe Brzezinski, vitabu ambavyo vinaelezea namna watakavyo iwezesha New World Order kutokea. Mfano wa vitabu hivyo ni kile alicho kiandika mwaka 1970, kilicho kwenda kwa jina la Between Two Ages: America's Role in the Technetronic Era.[7]

Aliyekuwa mshauri wa kampeni wa bwana Obama ni mtoto wa Brzezinski, bwana Mark, wakati mtoto wake mwingine bwana Ian alikuwa mashauri wa siasa za nje kwa bwana McCain na wakati huo huo mtoto wake wa kike ambaye alikuwa anamuunga Obama mkono Mika Brzezinski akiripoti kampeni hizi kupitia televisheni ya MSNBC. Kwa hiyo bwana Brzezinskin alikuwa ameutawala mchezo mzima na hivyo ilikuwa rahisi sana kuamu nani ashinde na nani ashindwe.[8]

Tangu miaka ya 1981na 83 Obama alikuwa ni lulu kwa Zbigniew Brzezinki na Trilateral Commission, na hao pamoja na asasi zingine za siri ndiyo waliokuwa wasimamizi wakubwa wa kampeni zake. Mara ya mwisho Trilateral Commission kumuweka kwenye madaraka kibaraka wao alikuwa ni Jimmy Carter, ambaye mambo ya nje ya serikali yake aliyakabidhi kwa Brzezinski na shughuli za kiuchumi akamkabidhi ajenti wa Trilateral Commission Paul Adolph Volcker. Tumeuona uongozi wa Kennedy Mweusi namna ambavyo umebeba picha ya kibaraka aliyepita wa Trilateral Commission.[9]



Ni kweli kijana huyu aliyeibuka kwa ghafla na kuwa Messiah wa uma, katoka kusiko julikana na kuingia ndani ya White House kana kwamba mtu yoyote anaweza kuikanyaga himaya hiyo ambayo kwenye ramani ya siri ya nchi hiyo White House inawakilisha kichwa cha Lucifer. 

Hapana lazima anamahusiano na wanao unga mkono sera za Lucifer, nabii hawezi kufanya kazi moja na Lucifer ila lazima na yeye awe na maono ya kishetani. Obama amaenza kufahamiana na Brzezinski tangu miaka ya 1980, na muda mrefu alkuwa ameshachaguliwa kupakwa mafuta kuingia White House na tangu zama hizi alikuwa akidhaminiwa na Trilateral Commission pamoja na Ford Foundation ambayo ndipo mama yake alipo kuwa akifanya kazi, wadhamini wengine ni Citigroup,UBS, Morgan Chase, Morgan Stanley na wengine wengi.

Wadhamini wake wakubwa ni wale ambao wanataka kuwatia watu katika gereza ambalo Obama anasema anataka kulivunja. Hii ni moja ya sababu iliyomuwezesha kuendesha kampeni ya nguvu katika historia ya Marekani. Ni kweli atafanya kazi ya kulivunja gereza la wadhamini wake au kuliboresha?[10]

Mshauri wake wa mambo ya kiuchumi ni bwana Paul Adolph Volker, mwanachama wa Trilateral Commission, Council on Foreign Relations, na Bilderberg Group na ambaye pia alikuwa kiongozi wa Federal Reserve kutoka mwaka 1979 mpaka 1987. 

Mtu mwingine ndani ya timu hiyo ya washauri wa mambo ya uchumi kwenye kitengo cha kufufa uchumi ni Austan Goolsbee ambaye ni mwanachama wa Skull and Bones. Katibu mkuu wake wa mambo ya fedha ni mwanachama wa kizayuni bwana Timothy Geithner ambaye pia ni mwanachama wa Trilateral Commission, Council on Foreign Relations, Bilderberg Group. 

Kwenye timu hiyo ya mambo ya fedha tunakutana na mtu mwingine ambaye naye anafuata siasa za kizayuni bwana Robert Rubin, kiongozi mwanadamizi wa Citigroup, mwenyekiti mshiriki wa Council on Foreign Relations. Rubini pia ni mwanachama wa Bilderberg Group.  Rubin pia alikuwa katibu wa fedha kwenye utawala wa Clinton, halafu baadae nafasi hiyo akapewa Larry Summers ambaye naye ni mwanachama wa Trilateral Commission, Council on Foreign Relations, Bilderberg Group, safari hii Obama amemchagua Summers kuongoza baraza la mambo ya uchumi, jamaa huyu ni mshabiki wa kile kinachoitwa Free trade, kwa maneno mengine unyonyaji huru. 

Mwaka 1991 alipokuwa kiongozi wa mambo ya uchumi kwenye World Bank aliandika ujumbe unao dai kuwa “... uchafu wa bidhaa mbovu na zenye sumu zinapaswa kutupwa katika nchi zinazoendelea ...”[11]
Ujumbe huu uliposomwa hadharani aliyekuwa katibu wa mazingira kipindi hicho bwana Jose Lutzenburger akapingana na Summers na kuyaita mapendekezo yake ya kiuwendawazimu, baadae Lutzenburger akafukuzwa kazi kwa kauli yake hiyo na Summers akateuliwa kuwa Treasury Secretary na Bill Clinton na sasa ‘Kennedy Mweusi’ kamteua kuwa kiongozi wa National Economic Council. 

Watu wale wale walio sababisha mtikisiko wa kiuchumi, financial Crisi,s ndiyo walio chaguliwa na Obama kuamua mustakbali wa dunia kuhusiana na zahama hilo.
Kama ambavyo wa Khazair (wewe unawaita wayahudi) walivyokuwa wamemshikilia Bush ndivyo ambavyo walivyo katika timu ya Obama. Kijana huyu kesha weka wazi msimamo wake wa kuitetea Israeli. Makamu wake wa rais ambaye ni Joe Biden mwanachama wa Council on Foreign Relations na Bilderberg Group anaunga sera za kizayuni na yuko pamoja na Obama kuisaidia Israeli kwa hali yoyote ile. 

Obama amemteua mfuasi mwingine wa kizayuni Rahm Emanueli kuwa Chief of staff, na mfuasi mwingine wa kizayuni Dennis Ross kama mshauri wa mambo yahusiyo Mashariki ya Kati. Jamaa huyu alikuwepo pia katikau wongozi wa Bush baba na Clinton.[12] Bado unaniambia kuna mabadiliko? Bado unaimba nyimbo za matumaini?




[1] ellowshipofminds.wordpress.com/2010/05/31/larry-sinclairs-gay-sex-with-obama/
[2] http://fellowshipofminds.wordpress.com/2010/07/25/mom-of-murdered-obama-gay-lover-speaks-up/
[3] Ibid
[4] Ibid
[5] Wayne Madsen , Special Report:The Story of Obama: All in The Company (Part II), AUGUST 16, 2010, From Washington D.C. (USA) 
[6] Tarpley, Webster Griffin Barack H. Obama: the unauthorized biography / Webster Griffin Tarpley ISBN-13: 978-0-930852-91-7 (Digital), 978-0-930852-81-8 (Offset edition) Uk 254
[7] http://www.davidicke.com/articles/political-manipulation-mainmenu-72/18281-barack-obama-the-naked-emperor
[8] Ibid
[9] Ibid
[10] Ibid
[11] Ibid
[12] Ibid

2 comments:

  1. I cant stop reading these articles day after day....Keep going depp brow..Lets the world know what is hidden behind the Devil KIngdom. Ubarikiwe

    ReplyDelete
  2. Numekuelewa Sana mtu wangu

    ReplyDelete