Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Friday, August 5, 2016

MFALME OBAMA: Ep 2


Mungu anapo wateuwa mitume wanakuwa wanatoka katika mkondo wa damu maalum, anakuwa chini ya uangalizi wa Muumba wake kuanzia maisha ya wazee wake, maisha yake akiwa tomboni, utoto wake, ujana wake mpaka anapo kabiziwa jukumu hilo zito na tukufu kwa ajili ya kuwaongoza watu wake. 



Hivyo mitume wote wa Mungu Mmoja ni ndugu kwa vile wote wanatoka katika mtiririko wa damu moja. 

Illuminati nao kwa maelfu ya miaka wamekuwa wakitumia utaratibu kama huu kuhakikisha wanamuweka mtu mwenye damu yao katika nafasi ya juu ya uongozi, mtu ambaye pande zake zote za maisha yake wamezimulika na zimekuwa kwenye uangalizi wao kwa muda flani, mfano mzuri ni Barack Obama.

Tumeona kwa ufupi sana namna gani pande zake zote za maisha yake zilivyokuwa zimezungukwa na CIA, kuanzia kwa babu na bibi mpaka kuja kwa mama na baba, lakini si huko tu, mtu yoyote ambaye aliyaathiri maisha yake utotoni na ukubwani kwa muda flani eitha kwenye elimu, mwalimu aliyemfundisha, chuo alicho somea kazi yake ya kwanza, watu alio fanya nao kazi, aina ya shirika alilofanyia kazi na mengina katika hali flani utakuta yalikuwa na mahusiano na CIA.

Vita vya mwisho baina ya mwanga na kiza vitapiganwa katika misingi ya damu, itakuwa ni vita baina ya damu tukufu ya mitume na damu chafu ya kishetani. Ndiyo maana kiongozi wa vita hivi kutoka upande wenye nuru atakuwa ni mtu anayeitwa Al Mahadi, mtu ambaye anayo nasaba ya moja kwa moja na vizazi vya mitume kupitia mtume wa mwisho Muhammad (Rehma na Amani Ziwe Juu Yake) Al Mahadi atasaidiana na mtume Issa (Rehma na Amani Ziwe Juu Yake) au kwa jina jingine Yesu. Al Mahadi huyu si yule anayetajwa kwenye dini ya Ushia.

 Kwa upande wa kiza vita hivi vitaongozwa na Dajjal maarufu kama Mpinga Kristo, Yesu ndiye atakaye muuwa  Mpinga Kristo ndani ya Jerusalem katika mahala panapoitwa Baabu Lud. Kisha baada ya hapo Yesu akishirikiana na ndugu yake Al Mahadi watasimamisha ufalme wa Mungu Mmoja katika jiji la Jerusalem, jiji ambalo Mpinga Kristo na watu wake watataka kulifanya kuwa ndiyo makao makuu ya New World Order kama tunavyoona harakati hizo zinavyo shika moto siku hadi siku.

Hilo halito fanikiwa, kitimbii chao hichi kitashindwa vibaya na dini ya Mungu Mmoja itasimamishwa kutokea hapo Jerusalem na kuondoa dhulama katika uso wote wa dunia. Hili pia litathibitisha kuwa Jerusalem siyo jiji la wafalme kama wanavyo dai Illuminati bali jiji la Mitume wa Mungu Mmoja.

Obama alipochapisha nsha yake inayohusu hamu na mpango wake kama kiongozi mtarajiwa wa Marekani alitumia jarida la Foreign Affair, jarida hili linachapishwa na asasi ya siri inayo julikana kama Counil on Foreign Relation, Obama pia ni freemason wa daraja la 32 katika hekalu la Prince Hall Freemason ambalo ni maalum kwa watu weusi[1]

Kijana huyu ni mtiifu kwenye muungano huu usio mtakatifu, mpaka kufikia daraja ya 32 na hatimaye kuruhusiwa kuikanyaga White House hapana shaka ameonesha kuwa anaweza kuibeba ajenda kutoka pale freemason mwenzake George W Bush alipoiachia mpaka pale ratiba ya ajenda itakapo muelekeza kuifikisha, hivyo sahau “changes” na tegemea hadithi ile ile uliyoipata kwa Bush na huenda mbaya zaidi itategemea ajenda inataka nini.

Mpakwa mafuta huyu wa nyumba ya Freemason amekuja na hadithi ya changes na hope, naam, tumaini, kuna matumaini tutaraji matumaini na mabadiliko. Maana ya tumaini peke yake imetegemea wakati ujao achilia mbali neno mabadiliko. Kwa maneno mengine tuko kwenye hali mbaya na kijana huyu ambaye safari hii nimeshuhudia dunia nzima ikimfanyia kampeni kama kiongozi wa dunia amekuja kutuambia tuendelee kuvumilia shida hizi walau kidogo kwani hapo mbele, hapo mbele kuna matumaini, upo na mimi mpaka hapo, kwa hiyo kama wanavyo ambiwa wale wenye Ukimwi waishi kwa matumaini ndivyo sasa tunambiwa sote tuwe na matumaini, tutumainie jambo, sawa?



Kwa maneno mengine tusubiri wakati ujao mambo yatakuwa mazuri, hii ndiyo maana hasa ya tumaini, haizungumzii wakati uliopo bali wakati unao kuja. Dunia nzima ilikuwa na bado iko kwenye matatizo, madhila, mashaka na uharibifu mkubwa, dunia nzima ilikuwa inahisia za tunataka mabadiliko sasa, msimamo ambao si mzuri kwa ajenda hivyo kampeni za tumaini zimekuja kufanya hayo mabadiliko, hali bado ni mbaya maradufu lakini walimwengu wanasema tumpe muda kijana, tuna mtumainia ataleta mabadiliko, hisia za mabadiliko sasa zimekufa na badala yake ni hisia za matumaini. Hakuna kilicho badilika lakini tuna tumaini hivi ndivyo mteule anavyo fanya kazi.

Watu wana tumaini la nini? Tumaini la mabadiliko, Bill Clinton na wengine pia wameshaitumia mbinu hii inayoitwa changes. Babylon Brotherhood wanajua kuwa watu hawaikubali hali waliyo nayo, na wanataka mabadiliko kwa hivyo njia nyepesi ni kuwaletea mabadiliko, kwa hiyo wanakuja na mavazi yale yale unayo taka wavae, na sura ile ile unayoipenda, lakini...

Je bwana Changes amepata kutuambia ana maanisha nini anapo zungumzia, tumaini, mabadiliko, na kuamini? Tumaini la nini, mabadiliko yepi, na tuamini nini? Mbinu hapa ni kumuacha mfuasi mwenyewe aamue ni mabadiliko na au ni tumaini gani analo taka na Obama anakuwa ndiyo jibu la matakwa yake. Tunacheza na akili za watu hapa, hatuwapi kile wanachotaka lakini tunawarubuni mpaka wanaona wamepata wanachotaka na wametukomoa, lakini kinyume chake ndiyo sahihi.

 Kwa hiyo Obama ana simama mbele ya watu hao kama ndiye kila kitu wanachotaka kuamini, kutumainia na badiliko. Vile ambavyo wapiga kura walivyo kuwa wanataka ndivyo Obama alivyo kuwa, chochote unachotaka kibadilike, chochote unacho kitumainia, chochote unacho kiamini kielekeze kwa Obama na hapo utamuona mtu aliye tayari kukuleta hayo, yeye ni kila kitu, yeye ni chochote unacho taka kiwe. Kwa hiyo Obama hakuwa na haja ya kupambanua alikuwa akimaanisha nini anapo sema changes, hope na belive

Hii ndiyo maana Obama alifananishwa na Messiah, Abraham Lincoln, John Kennedy na au Kennedy Mweusi na wakati mwingine alifananishwa na Buddha, vyovyote unavyotaka awe ndivyo anavyokuwa, chochote unacho kitaka mtizame yeye, na utapata tumaini la kukipata.



           Waambie watu kile wanachotaka kusikia, na nyamaza kimya juu ya kile wasichotaka kukusikia, utawateka vizuri sana, kwa mtu anaye onekana kuwa ni tofauti na Bush ndicho walimwengu walichokuwa wanataka. Lakini kuwa ambia peke yake haitoshi ila namna gani unawaambia, hii ndiyo inayoleta tofauti. Vipi unafanya unachokifanya hapa ndipo ilipo lala hatma ya mchezo mzima.

Akisimama kwenye jukwaa ni Obama, na anapo zungumza na kutabasamu ni Obama yule ambaye dunia ilikuwa ikimtumainia, lakini watu fulani nyuma ya mapazia wamemuandaa mteule wao na kumpa mafunzo ya namna gani ya kuzungumza na kuteka fikra za uma. 

Mazungumzo yake hayatoki moyoni bali kwenye ubao maalum ambao watazamaji hauwoni, aina hii ya teknolojia katika kuzungumza inajulikana kama autocue. Mafunzo maalum ya kudanganya macho ya uma kwa ‘kumaanisha kile unachosema’ ni kama mchezo wa kuigiza, Blair alifunzwa kutumia mbinu hii, na aliitumia vyema kama alivyo fanya Clinton,  Bush ndiye aliyeshindwa kuitumia njia hii ipasavyo ndiyo maana ilibidi kufanyika kazi ya ziada, ili kumfikisha White House. Kumbuka Bush hakushinda uchaguzi ule ila mpinzani wake ndiye aliyeshinda, na alipokuwa White House ilimbidi kutumia nguvu za kivita kutekeleza matakwa ya ajenda.

Wale waliotolea macho kampeni hizi, wakazitazama kwa jicho na fikra huru tangu kipindi cha Obama anapambana na Hillary mpaka Obama anasimama na John McCain watakubalina nami kuwa wakati huu ajenda ilikuwa inamuhitaji Obama, ni kwa sababu gani ajenda inamuhitaji mtu mweusi ndani ya white house ni swali litakalojibiwa na yeye mwenyewe katika kipindi cha utawala wake, hivyo kilichokuwa kikubwa kinafanyika ni kurubuni mtazamo na wawazo ya walimwengu hususani ya wapiga kura wa Marekani kumkubali kijana huyu mweusi.

Kazi hii ilikuwa ni nyepesi sana kwa sababu moja kuu, watu hawako huru, watu wamefungwa minyororo isiyo onekana, mawazo, mitazamo, maoni na maono ya watu wa vyombo vya habari, watu maarufu, na wale wenye ushawishi wa aina mbalimbali katika jamii ndiyo yaliyofanywa kuwa ni maono, mitazamo na misimamo ya walimwengu wote, kiuhakika opofu huo ndiyo uliwezesha kuchaguliwa kwa Obama na si hitajio la Wamarekani wala tumaini la walimwengu kama inavyonekana bali ni hitajio la Babilon Brotherhood na ndiye tumaini lao.

Wakati Obama na Hillary wanapambana niliona kasoro nyingi za makusudi katika kampeni za Hillary. Mwana mama huyo mwenye nafasi kubwa ndani ya mtandao wa Babilon hakuonesha ushindani wa dhati na wala hakuonesha juhudi zake za makusudi za kuwa anataka kuingia Ikulu, kwa wale waliofuatilia kampeni zake muda wote alionekana ameridhika na vile anavyoendesha mambo yake pamoja na kwamba mbinu zake zilikuwa hazimletei ushindi. 

Wakati kila nukta moja Obama aliyoipata kushawishi ulimwengu alitumia ipasavyo. Clinton hakuonekana kujutia kushindwa kwa mbinu na sera zake bali zaidi alionekana kama mtu anayejifurahisha kwenye majukwaa ya kampeni wakati Obama muda wote alionesha uso na moyo wa kazi.

Baada ya Obama kumshinda Hillary mambo yalizidi kuwa wazi zaidi kuwa ajenda inamuhitaji mtu mweusi. Kwa wale watumiaji wa internet na hasa wasomaji wa e-mail kwenye mtandao wa Yahoo na Hotmail kulikuwa na kampeni za kumpigia debe Obama. Kampeni hizo ziliendeshwa kupitia tangazo maarufu la Green Card ambalo mara nyingi utalipata unapofungua email zako kwenye hizo tovuti mbili.

Utakumbuka kipindi flani ambapo Marekani ilikuwa ikiandamwa na jinamizi la eitha au la wabadilishe katiba ya nchi hiyo ili iweze kumruhusu mzaliwa kutoka Austria na mcheza filamu maarufu Arnold Schwarznegger kugombea urais wa nchi hiyo, kipindi hicho kwenye tangazo la Greencard walikuwa wakiweka picha mbili tu, picha ya raisi aliyemaliza muda wake na picha ya Schwarznegger na wakikuambia yupi ni rais wa marekani kati ya hawa wawili?

 Katika kampeni za safari hii walianza na picha za Hillary, halafu baadae zikaja za Obama zote zikiuliza ni yupi rais wa Marekani, hawajapata kuweka ya John McCain na wala ya mgombea mwenza wake.

Wakati Obama akijizatiti na kuunga sera za chama chake, McCain kwa makusudi alikuja na sera mbovu zinazopingana na sera za chama chake na pia zinazopingana na sera za rais aliyekuwepo madarakani ambaye naye anatoka kwenye chama chake, kwa hiyo wakati Obama anasonga mbele na sera zilizoandaliwa vizuri McCain alikuwa na kazi ya kutatua migogoro ya kisera.

Kituko kingine ni mgombea mwenza wa McCain ambaye kwanza kubalina na mimi kuwa McCain hakupewa mwana mama huyo kwa bahati mbaya bali kwa makusudi mazima, wakati McCain anapingana na sera za Bush mgombea mwenza Sarah Palin alikuwa akipingana na sera za McCain, kama ni chombo basi kilikuwa kimeshapoteza dira yake hakifahamu ni wapi kinaelekea, narudia hayakufanywa haya kwa bahati mbaya. Sarah alizidi kuwachanganya na kuwakatisha tama wafuasi wa chama chake pale alipoanza kujitangazia kuwa yeye atashinda katika uchaguzi wa awamu nyinginena si huu anaofanyia kampeni, haya kuwa maneno ya kuwaambia wa fuasi wako, kwa maana nyingine ni kuwa uchaguzi huu yeye na McCain wameshashindwa, alisema maneno haya wiki kadhaa hata kabla ya kura kuanza kupigwa, kwa mtu yoyote mwenye akili hawezi akawapa kura watu ambao tayari wameshaonesha kuwa hawako tayari kufanya kazi wanayoiomba. 

Wakati Republic wakiwa katika makanganyiko huo kwa Democrat kila siku mpya iliashiria ushindi kwao.
Wakati wa kile walichokiita US Presidential Debate McCain alizidi kuonekana kituko kwa kutengeneza mazingira ambayo Obama aliyatumia kujitangaza vyema, wakati Obama anazipambanua sera zake McCain alifanya kazi ndogo sana kuhusu hilo bali zaidi aliuliza maswali ambayo yalihitaji ufafanuzi zaidi kutoka kwenye sera za Obama ambapo kijana huyo mweusi akazidi kuzichanganua sera zake kwa watazamaji. 

Baada ya mjadala huo waendeshaji wa mjadala huo kupitia televisheni ya VOA bwana Jim Malone mwandishi wa habari yeye alimponda McCain waziwazi na wakati huo huo akimpamba Obama, bwana Barry Wood ambaye anasimamia habari za kiuchumi katika kituo hicho cha televisheni na yeye aliungana na Obama, hivyo maoni ya watu hawa wawili yanakuwa maoni ya mamilinioni ya watazamaji na hivyo ndivyo Obama alivyoikanyaga White House.

Kwa picha halisi Kennedy Mweusi ni kibaraka wa matajiri wakubwa wanaomiliki Wall Street na benki nyingine kubwa ndani ya Marekani na kimataifa, anawakilisha kazi za asasi nyingine za siri kama Trilateral Commission, Bilderberger Group, Council on Foreign Relations, Skull and Bones Society na Ford Foundation. Mama yake Obama ambaye amepata kufanya kazi katika mashirika mbalimbali yakiwemo World Bank,US Agency for international development na Ford Foundation amemuachia Obama uongozi wa biashara za familia ambazo nazo zinamuelekeo ule ule wa Ford Foundation na ambapo mashirikia hayo daima yamekuwa yakipata dira na muongozo wake kutoka kwa Ford Foundation na alipo toka hapo akaingia kwenye asasi ya siri mama wa Umoja wa mataifa Trilateral Commission.

Matakwa na baraka nyingi kutoka kwa asasi za siri kama, the Trilateral Commission, the Bilderberger group, the Ford Foundation, Skull and Bones, the Chicago School, the Council on
Foreign Relations, na kutoka kwenye vitengo vingine vinavyoshikilia sehemu muhimu ya utawala wa Marekani wakiwemo vinara wa Wall Street ndicho kilicho mfanya Obama kuonekana ni Kenndedy mweusi mbele ya mwanamama mweupe Senator Clinton. Obama si tumaini la wa Marekani na au walimwengu kama wanavyo sema watu wengine bali ni tumaini la Babylon Brotherhood.

Kasi ya Obama aliyo kuja nayo haina tofauti na ile ya Hitler wa Ujerumani, Wajerumani walikuwa katika hali ngumu kiuchumi na kijamii, wakiwa katika hali mbaya kama ile akatokeza mtu aliyeitwa Hitler ambaye kwa sera zake alionekana kama Messiah kama ambavyo anavyo onekana Obama. Alingia katika madaraka kwa namna ambayo Obama kaingia nayo White House, sisemi Obama ni Hitler wa Marekani ila nakuonesha namna gani mbinu moja ianavyotumiwa zaidi ya mara moja na mabilioni hawana hata wazo la kung’amua hilo. Hitler naye aliahidi mabadiliko (changes), matumaini (hope) na kuamini juu ya kitu fulani (belive), watu waliibuka na kumuunga mkono Hitlar wakiwa na tumaini. Walichokipata ni serikali ya kifashisti.


No comments:

Post a Comment