Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, September 7, 2014

IKO WAPI NDEGE YA MALYSIA MH 370?


Mimi binafsi nililitilia shaka suala zima la ndege ya Malaysia kutoweka angani na isipatikane kokote kwenye uso wa dunia mpaka hivi leo, bado nalitia mashaka suala hilo kwamba halina ukweli wowote ndani yake, bali ni moja kati ya filamu zao nyingi wanazo ziigiza ilikuendelea kuulaghai umma, lakini zaidi mimi naona ni hayo ni MAANDALIZI YA KUMTAFUTA ADUI MPYA ATAKAYE CHUKUA NAFASI YA ‘VITA DHIDI YA UGAIDI’.

Kaa vizuri hapo ulipo ...


Kwa kuanzia tu, tuitazame moja ya nambari kuu zinazo pendelewa kutumiwa kishetani na Illuminanti, nambari 11, zaidi kuhusu nambari hii tazama posti hii salimmsangi.blogspot.com/2013/12/nambari-tisa-9-na-kumi-na-moja-11.html

Wakati ndege hiyo ya Malaysia ikipotea ndani yake kuliwa na abiria 227, nambari hiyo ni sawa na 2+2+7=11, ndege yenyewe ni Boeing 777 nambari inayogawika kwa 11.

Ndege hiyo ya Malaysia ilipatwa na ‘ugonjwa’ kama ule uliozipata ndege za 9/11 ambayo tunajua kuwa tukio lile lilifanywa na utawala wa Bush mwenyewe.

1.          Ndege hiyo ya Malaysia ilipoteza mawasiliano kama zilivyokuwa ndege za 9/11. Masaa mawili baada ya ndege hiyo kuondoka ilipoteza mawasiliano kabisa na kitengo cha anga ambacho ndicho kilicho kuwa na dhamana ya kuiongoza ndege hiyo.


2.        Ndege hiyo iliacha njia yake ya safari kama ilivyokuwa kwenye 9/11. Ndege hiyo ya Malaysia ikaendelea kusafiri maelfu ya maili nje ya njia yake iliyopaswa kupita bila hata ya kutuma taarifa za tahadhari na msaada kwenye kituo chochote cha kuongezea ndege na kisha ‘ikatoweka’ kama mazingaombwe vile.


3.        Ndege hiyo ikapotea kabisa na isionekane kama zilivyo potea ndege iliyo gonga Pentagon na ile ya Pennsylvania kwenye tukio hilo la 9/11.

4.        Kama ilivyokuwa kwenye 9/11, kwenye ndege ya Malaysia nako abiria simu zao zilikuwa hewani!!!!!
Kila mtu anajiuliza ni nini hicho? Ndugu na jamaa wa abiria kwenye ndege iliyo potea wamethibitisha kusikia milio ya simu walipojaribu kuwapigia wapendwa wao. Na pia baadhi ya kurasa za fecebook za abiria hao zimeonesha kuwa wapo ‘online.

Shirika hilo la ndege la Malaysia limethibitisha pia simu ya mhudumu aliyekuwepo kwenye ndege hiyo nayo iliita tu bila kupokelewa na mtu yeyote mpaka ikakata kama zilivyo fanya simu 19 za abiria walio kuwepo kwenye ndege hiyo baada ya kupigia na ndugu na jamaa. Hayo yalisemwa na msemaji wa shirika hilo bwana Hugh Dunleavy.
Lakini pia hadithi ya simu za abiria na ile ya muhudumu kuita inatupatia mwanga wa jambo moja, kwamba ndege hiyo haipo ndani wala chini ya bahari! Simu haiwezi kuita kama ipo ndani ya maji, lakini zaidi simu hiyo lazima iwepo karibu na mnara wa simu, ambao tunajua hauwezi ukawepo chini ya bahari isipokuwa aridhini.
5.        Kama ilivyokuwa kwenye 9/11 hapa napo kwenye ndege ya Malaysia mapema kabisa Illuminanti walianza kutoa dondoo za tukio zima takribani miaka minne kabla. Tizama picha hii inayofuata na linganisha na tukio lenyewe kisha kuna kichwa na kujiuliza ikiwa tangazo kwenye picha hiyo limetokea kwa bahati mbaya?



Tunapoendelea kulitolea macho suala hili, tunayo maswali ya msingi ya kujiuliza, kumbukua hapa tunazungumzia ndege kubwa aina ya Boeng, ndege ya kisasa kabisa, ndege hii haijalipuka, haijaanguka mahala kokote, si nchi kavu si baharini, imetoweka ghafla, narudia tena IMETOWEKA GHAFLA ikiwa angani, na haijapatikana mpaka hivi leo.

Vipi kama vile MUVI linajirudia ...?
Vipi wanataka kututengenezea Spetemba Ileveni nyingine au?

Swali # 1
Ndege zote aina ya Boeing 777 zimetengenezwa pamoja na ‘Black Box’ ambayo inaweza kuhimili mlipuko wa aina yeyote ule utakaoipata ndege hizo. Kisanduku hicho kinabeba taarifa zote muhimu yakiwemo mawasiliano ya hatua kwa hatua tangi ndege inapotokea mpaka inapo elekea.
Swali linakuja NI VIPI KIBOKSI HICHO KIMESHINDWA KUTUELEKEZA WAPI NDEGE ILIPO?

Swali # 2
Black Box zote zinayo uwezo wa kuendelea kusafirisha mawasiliano na kutambua wapo kilipo hata kwa muda wa siku 30 hata kama ndege ikiwa imezama baharini.
Swali linakuja ni kitu gani hicho kilicho zima ‘signal’ ya kisanduku hicho kiasi kwamba shughuli za kuipata ndege yetu zimekuwa ni ndoto. Tunajua ndege hiyo haijawaka moto wala kuzama baharini, sababu simu za abiri na wafanyakazi wa ndege zilikuwa zikiita kila zinapo pigwa. Sasa inakuwaje simu zinaweza kuendelea kuleta mawasiliano lakini kisanduku cheusi kipoteze mawasiliano kabisa?

Swali # 3
Ndege inapokuwa imepotelea baharini, mara zote kuna sehemu na mapande ya ndege hizo yataonekana yakielea baharini.
Kama ndege ya Malaysia ingekuwa imetungulia na kushushwa chini basi vipande lazima vingeonekana vikielea baharini, lakini viko wapi vipande hivyo? Ndege ya Boeing 777, imetoweka ghafla kwenye uso wa dunia, IMETOWEKA, ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni.

Swali # 4
Mahala ambapo ndege hiyo ‘imepotelea’  panafahamika. Waongozaji wa ndege wanakuwa taarifa zote za ndege husika, kumbuka wao ndiyo waongozaji, hivyo nukta ambayo ndege inakata mawasiliano na wao wanakuwa wanafahamu ilikuwa eneo gani, ilikuwa kwenye mwendo kasi wa aina gani, vyote hivyo vinaweza kutumika kuelekeza ni wapi mapande ya ndege hiyo yanaweza kuwa yameangukia. Lakini ni vipi ndege hii ya Malaysia imeshindwa kupatikana chochote pamoja na kwamba inafahamika ni wapi nukta ya mwisho ilionekana kwenye rada?


Swali #5

Tuseme Ndege 370 ya Malaysia imetekwa, lakini ndege haipotei kwenye rada hata kama ikitekwa. Sasa inakuwaje ipotee hata kwenye rada isionekane?

Ndege nambari 370 ya Malaysia aina ya Boing 777 HAIJALIPUKA, HAIJANGUKA KOKOTE, ILA IMETOWEKA?


HOW?

TUKUTANE TENA HAPA TO FIND THE HOW ...

6 comments:

  1. hahahaa c walisema mabaki yameonekana Australia

    ReplyDelete
    Replies
    1. Walisema yameonekana Australia lakini wamekuonesha hayo mabaki? Kama walivyo sema wanafahamu walipo wasichana wanao shikiliwa na Bokoharam lakini wamekuonesha hao wasichana? They Just think your fool to buy anything the y sell, no matter how crap it is ... so sad

      Delete
    2. Umesikia eti tena wanahisi mabaki ya ndege hiyo yanaweza kuwa haya yaliyoonekana Ktk kisiwa fulani huko Zanzibar!!

      Delete
  2. Hebu tujiulize,kama simu za abiria zilikua hewani kwanini wasiwasiliane na watu wa mitandao ili kujua simu hizo ziko wapi?halafu ulimwengu huu tulionao uko juu sana kwa sasa kiteknolojia,ni kweli kabisa teknolojia imeshindwa kabisa?

    ReplyDelete
  3. daaaahh hii ni vita na wanatamani malengo yao yakamilike kwa her au kwa shar,na wanapambana usiku na mchan kukamilishsha makusudio yao,hakika imani zetu za kwelii ndo mkomboz wetuuu

    ReplyDelete