Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, January 14, 2018

JE TUPO WENYEWE KWENYE ULIMWENGU? S02, Ep11 (Nyayo za Wageni Kutoka Sayari Ya Mbali - Time Travelling na Hisabati)



Time Traveling ni moja ya nyanja zenye kusisimua kwenye sayansi ya kosmolojia. Tafiti zinaonesha ‘time traveling’ ipo, lakini inafanyikaje kwa zana gani, bado teknolojia yetu haijaweza kulijibu swali hilo.


Lakini kwenye nakala za kale mno, ambazo bado waandishi wake bado hatuwajui kuwa ni viumbe gani na wazama zipi, zinaelezea matukio yanayo husiana na ‘time traveling’.

Wanasayansi wa Marekani kwa wiki mbili walisafiri angani kuizunguka dunia wakiwa na madege yao aina ya Jets, moja ya ndege zinazo kwenda kwa kasi mno kwenye teknolojia yetu ya leo ya usafiri wa anga. Walibeba katika ndege hizo saa za atomiki. Lengo likiwa ni moja tu, kuthibitisha nadharia ya Einstein ya ‘time relativity’.


ambayo inasema kuwa, saa/muda/wakati unakwenda taratibu, unapokuwa kwenye chombo kinacho safiri kwa kasi, kadiri chombo hicho kinavyo kuwa na kasi kubwa ndivyo muda unavyo zidi kwenda taratibu. Walithibitisha hilo ni kweli baada ya wiki mbili kuizunguka dunia wakiwa na jeti na saa za atomiki.


Wanaanga ambao watasafiri kwenye chombo ambacho kina kasi inayo karibia kasi ya umeme, umri wao utaenda taratibu kulinganisha na wale ambao wamewaacha kwenye uso wa dunia.

Kwenye chombo kinacho kwenda kwa kasi inayo karibiana na umeme, wakiwa huko angani wataona kuwa muda unakwenda sawa na walio kuwa duniani, lakini ndani ya miaka michache watakuwa wamezikaribia nyota za mbali mno.

Aliporudi kutoka angani, alimkuta ndugu yake kazeeka, yeye bado ni kijana vilevile.

 Baada ya miaka ishirini na moja ndani ya chombo chao hicho watakuwa wapo katikati ya galaxy yetu inayo fahamika kama milk way, lakini hapa duniani itakuwa imepita miaka 75,000!

Lakini nadharia hii, tunayoiita ya Einstein ya ‘Time Relativity’ ilithibitishwa kuwa ni kweli, ilifahamika huko nyuma katika zama ambazo kulingana na Darwin binadam bado alikuwa ni kiumbe duni anayetumia zana duni.

Kwenye ngano za wa Japan, wanayo hadithi ya mtoto ambaye alisafiri kwenda angani miaka 3, aliporudi duniani alikuta miaka 300 imeshapita.

Mtume Isaya  anazungumzia safari ya mbinguni, alipo ambiwa anarudi duniani, akauliza mbona imekuwa haraka hivyo nimekuwepo hapa kwa masaa mawili tu, malaika akamuambia, siyo masaa mawili bali miaka 32, Isaya akawa anahofia akirudi duniani atazeeka haraka na kifo, akaambiwa asiwe na wasiwasi akirudi duniani atabaki kama alivyo. (Tomas Endrew- We are not the First)


INDIA, walikuwa na taaluma ya ‘law of gravity’. Maarifa haya ndiyo msingi wa safari za anga na kasi ya usafiri wenyewe. Law of Atraction, pia ilifahamika India, sasa hivi inahubiriwa sana kwa namna mbali mbali na hasa kutoka nchi za Mashariki ya mbali, ambapo watu wa Magharibi wamechukua mafunzo hayo na kufanya moja ya biashara kubwa, na sasa watu wa New Ages na makanisa yao wamefanya kama moja ya misingi ya mafunzo ya dini yao, lakini kinacho fundishwa ni kama mchicha, kulinganisha na mbuyu.

Greece, Britain, Egyty, Guatemala kutaja kwa uchache walikuwa na maarifa juu ya ‘anti gravity, vacuum, na mahesabu ambayo yana vipimo vya kasi ya umeme!

Guatemala walitumia neno ‘kinchiltun’ kumaanisha miaka 57,600,000. Ni kitu gani walikuwa wakikipima kwa miaka hiyo? Walitumia neno ‘alautun’ wakimaanisha siku 23,040,000,000 au miaka 63,123,000! ‘Kalpa’ ikimaanisha kipindi cha miaka bilioni 4.32. Aina hii ya vipimo ndiyo inayo tumiwa na wanasayansi wetu wa anga kupima umbali wa baina ya nyota, galaksi na sayari mbalimbali. Mathalani umbali baina ya nyota tunatumia neno ‘light years’ ambayo ni mamilioni ya miaka, umbali baina ya galaksi tunatumia neno ‘parsecs’, ambalo ni kipimo kinacho unganisha 3.26 light years.

Unaweza kufanya nini ndani ya sekunde moja? Unaweza ukakonyeza jicho lako mara sita, kusogea urefu wa nchi sabini. Unaona ni kitu kidogo sana unaweza kufanya ndani ya sekunde moja. Lakini unaweza kufikiri ni nini kinaweza kufanyika kwenye ‘tatu ya mamilioni ya sekunde’, soma vizuri siyo sekunde milioni tatu, hapana, ‘TATU YA MILIONI YA SEKUNDE’ Yaani muda utakao utumia kukonyeza jicho lako mara moja, kabla hujaanza kulifunga jicho, tayari 1/300,000,000 ya sekunde imeshapita! Ni kitu cha namna gani unacho weza kukipima kwenye muda huo, na kwa nini utake kukupima kitu hapo, unatumia nini kukipima? Maswali ni mengi na siyoni wa kuyajibu. India walifanya kipimo hicho, na wakakirikodi, lakini ni zamani hasa, makumi elfu ya miaka nyuma! Walikiita ‘Kashta’ kipimo hicho.

HISABATI
Wagiriki walipokuwa wakirikodi tarakimu, hawakuweza kuzidi ’10,000’ kilichozidi hapo kwa wagiriki kilirikodiwa sawa na ‘infinity’, yaani kisicho na mwisho. 

Ajabu ni kuwa watu walio ishi Syria ya kale, milenia kadhaa kabla ya Wagiriki walirikodi nambari zenye tarakimu kumi na tano! Hata kompyuta haiwezi kurikodi tarakimu kumi na tano! Hawa watu si walikuwa mbali kushinda wagiriki, lakini mbali kutushinda sisi kwenye zama za sayansi na teknolojia? Who are they?

Peru walifahamu matumizi ya ‘sifuri’, 0 ni tarakimu muhimu katika mahesabu yoyote yale, bila hiyo hakuna haesabu inayofanyika, kompyuta na program zake zinajengwa kwenye msingi wa 0 na 1. Siyo Peru peke yake, India, Mexico, Babiloni, China kutaja kwa uchache.
Ni kweli Darwin alikuwa najua anacho kisema?
Pythagoras alikuwa ni mwanachama wa secrete society, hii ni mada nyingine, lakini kwenye sanamu hilo hapo kuna alama mahususi inayo mtambulisha kama mwanafunzi wa secrete society, umeiyona alama hiyo?


Hesabu za maumbo, hesabu za desimali, zilikuwa zinafahamika maelfu ya miaka hata kabla ya wale walio itwa ‘wavumbuzi’ wa hesabu hizo kuzaliwa! Mara nyingi wanao itwa ‘wavumbuzi’ unakuta ni watu walio tafsiri kazi hizo kutoka kwenye vyanzo vingine na hasa vya kale mno na kuleta kwenye lugha inayofahamika wakati huo, lakini hawasemi ni wapi wametolea kazi hizo.

 Hakuna jipya chini ya Jua. Hesabu hizo zilifahamika Mexico, Egypty, Peru, Babilon, Ur, Chaldea.
Kipenyo cha ‘Great Pyramid’ la Gaza, Kairo, Misri na kipenyo cha ‘King Cahmber’ kilichomo ndani ya Piramidi vinahusisha pembe tatu ya ‘3 by 4 by 5 na 2 by 3. Aina hii ya pembe tatu ndiyo ile iliyotumiwa na mwana mahesabu wa Kigiriki Pythagoras ambaye kwa kufuata historia ya kiserikali aliishi miaka 2000 baada ya Pyramid kujengwa, na yeye eti anaitwa ‘muasisi’ wa hesabu hizo za pai. Lakini tukifuata historia ‘mpya’ isiyo na ukakasi ni kuwa mwana mahesabu huyo aliishi miaka 15,000 baada ya Piramidi hizo kujengwa. Niambie ni wapi Pythagoras ‘alivumbua’ hesabu hizo?

Ukija kwenye hesabu za ‘phi’, aljebra, trigonometry, squre roots, cube root, na Logarithims tunakuta jamii za kale mno kushinda hata hao wanao itwa ‘wavumbuzi’ wa hesabu hizo walikuwa wanazijua. Egypty, Mesopotamia, Ur, Babilon, India, Peru, China kutaja kwa uchache. Ni kama hizi kazi tunazikopi kutoka mahala fulani, ni kama kuna wateule fulani wanao teuliwa kupitia miiko na taratibu fulani ambao wanakwenda kujifundisha maarifa haya kwa siri ikisha baadae wanakuja kutuambia kuwa fulani, ‘kavumbua’ kitu fulani.

Egypty ya kale walikuwa na alama fulani ya kimahesabu waliyo itumia kuonesha ‘mamilioni’ yaani badala ya kila wakati kuandika tarakimu yenye masufuri mengi, walibuni alama ya kimahesabu ya kuonesha kitu hicho. Hilo linaweza kufanyika endapo kitu hicho kinayo matumizi ya mara kwa mara na hivyo kumrahisishia mtumiaji wake asipate tabu, kama vile ambavyo leo tunatumia, MB, GB, TB n.k.

 Lakini cha ajabu ni kuwa dhana ya mamilioni sisi tumeanza kuitumia kwenye karne ya 17, yaani juzi tu; sasa ni akina nani hao ambao walikuwa Egypty na katika zama zipi ambazo mamilioni kilikuwa kitu cha kawaida mno kiasi kuwekewa alama mahususi kumrahisishia mtumiaji?
Niendelee kukuchosha na ugonjwa wa taifa, a.k.a ‘Hisabati’?

Twende kwingine usije ukakimbia blogi yangu bure kwa kudhania nafundisha hisabati hapa.

ROBOTIKA
Ni majuzi tu hapa robotika linalo itwa Sophia limepewa uraia katika nchi za Kiarabu. Yeah, kabla ya hapo tulizoea kuyaona kwenye viwanja vya Hollywood marobotika kama Cyborg, Terminator, Iron Man, Transformer, i, Robot, Robo Cop, A.I Artificial, Star Wars ... niendelee? Kuna vitabu vya kutosha na cartoon na vitabu vya komiki, lakini yote hayo tulidhani ni ‘fiction’, ngano au hekeya ... tulikuwa tumekosea.

Hawa jamaa ni kama walikuwa wanajua juu ya teknolojia hiyo, halafu wanatengeneza filamu na vitabu kuziandaa akili zetu juu ya hicho wanacho kificha, akili zetu zikisha kubaliana nao, kisha sasa wanakileta kitu chenyewe. Ni nani ambaye mwaka 1953 alikuwa anaitazama filamu ya Robot Monster ambaye angefikiri kuwa mwaka 2017, robotika anaye itwa Sophia angepewa uraia na kualikwa kwenye mahujiano na vituo mbalimbali vikubwa vya luninga ulimwenguni? Nani?

Labda huko mbali, ni nani ambaye mwaka 1999 alikuwa anatizama filam ya Matrix, ulidhani kweli 2012 tungekuwa na ‘smartphone’, lakini kwenye Matrix walionesha ‘Touch Computer’, teknolojia ambayo inaonekana kuja baada ya ‘smart phone’, hivyo 1999, sehemu fulani kwenye pembe nne za dunia palikuwa na teknolojia hii ambayo mpaka 2012 ndiyo ikafanywa ‘biashara.’

Sijui tunaelewana, nataka tupate picha kwamba kila unacho kiona, kwenye vitabu au filamu kama ‘science fiction’ kitazame vizuri kwa jicho la tatu, huenda ni bidhaa itakayo ingizwa sokoni miaka kumi ijayo. Lakini kwanini SIRI?

Hatukuwa na hatujawahi kuwa wa kwanza kutengeneza Robotika.

Whaaaaaaatsss?!
Yes, you read it correct, we were never the first? Somebody else already beat us on that too.

Unataka kujua kuhusiana na Robotika za kale?, luninga je?, Kompyuta? Ndege kama bombadia je? ...

Hey lets catchup soon for another episode ...Tchaaaooooo....

3 comments:

  1. Enter your comment...dah tunakukubali sana naomba utupe ukweli wa taifa la israil na Donald trump

    ReplyDelete
  2. Sasa ndugu Hawa jamaa kumbe hawana discovery yeyote mpya zaid ya kutuzingua2

    ReplyDelete