Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Monday, January 1, 2018

JE TUPO WENYEWE KWENYE ULIMWENGU? S02, Ep10 (Nyayo za Wageni Kutoka Sayari Ya Mbali - Barabara chini ya Aridhi)


Wakati wa harakati nyingi katikati ya mji, baadhi ya mitaa inabadilishwa na kufanywa njia moja (One way street), alama za barabarani, alama za mitaa, ‘service road’, mji wa kisasa kabisa, unaweza fikiri ni New York au Madrid kama siyo Kuala lumpur, lakini unaonaje nikikuambia kuwa hiyo inaweza kuwa ni ni Babiloni ya kale, Nineveh, au Aztec Mexico?

Yees, here we go like this ...


TOLTECS, MEXICO mpango mji wa miaka 400 mbele. Hata leo hatuna mpango mji wa miaka 50, pengine hata wa miaka 10 hatuna. Lakini Mexico maelfu ya miaka nyuma mipango mji ulilenga kukidhi mahitaji ya miaka 400 mbele!

PAKISTANI, GUATEMALA, BABILON walijenga miji na mitaa yenye barabara pana kama miji na barabara za nchi tunazoita ‘zilizoendelea.’
Mpango mji wa jiji la kale la Roma, POMPEII, ambao kimakosa 'unadhaniwa' kuwa ulijengwa na waroma.


ANTIOCH, SYRIA walikuwa na taa za barabarani. INDUS VALLEY, PAKISTAN, MEXICO walikuwa na mfumo imara wa maji taka, mitaro mikubwa na mambomba katika kila mtu. Miji mikubwa ya kisasa kwenye ‘nchi zinazo endelea’ hakuna mifumo imara ya maji taka ukilinganisha na zama hizo.
Masalio ya mji wa kale Pompeii, nyuma yake ni Mlima wa Volcano wa Vesuvius, ambao mlipuko wake umeuzika sehem kubwa ya mji huo.

Dalili ya mvua ni mawingu, panapo fuka moshi pana moto chini. Kinukta kiduchu cha mpango miji nilicho kigusa, ni kama ‘tip of iceberg’ kwenye hili linalofuata, are you ready ...
Barabara zao zilikuwa pana, na imara, masalio ya barabara katika eneo la Leptis Magna, Libya. Aina hii ya ujenzi wa barabara hizi unaweza ukaikuta Cairo, Lebanon na hata kwenye baadhi ya mitaa ya Zanzibar.


BARABARA
COLOMBIA, ECUADOR, PERU, CHILE,BOLIVIA NA ARGENTINA.

Ustaarabu na miji ya Amerika ya kusini, mpaka leo kwenye somo rasmi la ‘historia’ inafundishwa kuwa ulianzishwa na watu wa INCA, kama ambavyo wanavyo fundisha ustaarabu wa Egypty na Mafarao. 
Luxor Temple, Egypty. Mpaka sasa wanahistoria hawajaja na maelezo yenye kuridhisha juu ya ujenzi wa majengo ya namna hii katika Egypt ya kale ambayo ni kama 'yalishuka kutoka mbinguni.'

Lakini ushahidi wa kutosha unaeleza kuwa Inca kama walivyo mafarao miji hiyo waliikuta, hawakuijenga wao. Barabara za ‘highway’ zilikuwepo Peru kabla ya watu wa Inca kufika. Barabara hizo ndizo tunazo zijenga sasa katika miji yetu mikubwa ili kuweza kukidhi mahitaji ya vyombo vya usafiri, wingi wa watu, kupunguza ajali, na kusafiri kwa kasi na salama.


Kwenye ramani hii, unachoona kama mstari mwekundu ni barabara za Inca, ambapo urefu wake unakadiriwa kufika zaidi ya kilometa 40,000!

 Miaka mingi kabla hajazaliwa Kristo barabara hizo zilikuwepo Peru, Colombia, Chile na kwengineko. Baadhi ya barabara hizo zinatumika mpaka sasa kuendeshea magari yetu.
Hiyo siyo mito, ni barabara za Inca, ambazo wamezirithi kutoka kusiko julikana ... lakini haikuwa kazi ya Inca wala mababu zao, ni kazi ya nani?

Mh! Kulikuwa na magari kabla ya kuja Kristo?
Tulia bado tunakusanya ushahidi ...

Barabara hizo katika maeneo niliyo yataja, zinaungana na mtandao wa barabara nyingine ndogo na kutengeneza mtandao mpana wa barabara za kuingia na kutoka ndani ya mji. Barabara hizo zinafika mpaka kando ya mto Amazoni, halafu zinanyanyuka kuelekea kwenye vilele vya milima na kuteremkia pwani. Hazijatokea kwa nasibu, zimejengwa.
Urithi wa barabara kutoka kwa kizazi kisichojulikana, mpaka kwa watu wa Inca walizitumia kuendeshea magari ya farasi na farasi, mpaka kwenye zama zetu ambapo tunazitumia kuendeshea magari!

Wajenzi wa barabara hizo walipokuta mlima, hawaku uzunguka, bali walitoboa katikati na barabara ikapitishwa! Zipo tunazitumia leo, tunajiuliza ni nani walifanya haya, yakuwapi magari yao, au walifanya kazi hiyo kwa ajili ya kuendeshea magari ya punda na farasi?
Machu Picchu, huwezi kwenda Peru halafu usifike Machu Picchu.

Si barabara tu, na madaraja yake, madaraja imara ambayo bado tunayatumia mpaka leo hii.
Miji mingine yenye barabara za kisasa kama za karne 21, lakini zikiwa zimejengwa maelfu ya miaka kabla hatujaanza kuetengeneza kalenda ni EGYPT, ROMA, MEXICOSANTA CRUZ,



 GREECE, ENGLAND, kutaja kwa uchache sana. Barabara pana, zimenyooka, sehemu nyingine ni pana zaidi sawa na ‘highway’ zetu za sasa zinazo ruhusu magari manne kupita kwa wakati mmoja.
Majumba yao tumeona ni makubwa, barabara zao nazo ni pana, huwezi sema zilijengwa kwa waenda kwa miguu au njia ya farasi.


MIFEREJI YA MAJI.
NORTH COAST, PERU. Mfereji wenye urefu wa maili 70, ujengwa katika ubora ambao mpaka leo bado unatumika.

YUCATAN, MEXICO, kunayo mtandao wa mifereji 30, ambapo mingine inayo upana wa mpaka futi 160, mifreji hiyo inatoa maji kwenye vyanzo vikubwa kama mito, maziwa na bahari kisha inakwenda kuyamwaga maji hayo kwenye mabwawa makubwa, kabla ya kuyasambaza katika mji! Hii ni taaluma ya Hydraulic Engineering, lakini hapa tunazungumzia kipindi ambacho hata binadam wa leo tunamashaka kama alikuwepo.

GUATEMALA.
Picha ya karibuni iliyo pigwa na satelite kwenye misitu ya eneo hilo imenasa na kuonesha mifereji iliyo jengwa kwa ustadi na utaalam wa hali ya juu. Mifereji hiyo imechukua eneo la squre maili 11,185, kwa kilimo cha umwagiliaji, mifereji hiyo inaweza kuwatosheleza mamilioni ya watu!

CARTHAGE, TUNISIA. Mfereji wenye urefu wa maili 87.6 na uwezo wa kubeba galoni 7,000,000 kwa siku moja.
Muundo wa mifereji ya chini ya aridhi wa Qanat uliopo Iran, asilimia 75 ya maji ya Iran yanatoka humu, lakini nani mjenzi wa mifereji hii ya chini ya aridhi, siyo wa Persia wala binadam wa Darwin.


PERSIA. Mifereji iliyo enda chini ya airdhi maili 170,000 kwa ajili ya kukusanya maji kutoka milimani na kuyaleta tambarare jangwani! Pamoja na teknolojia na maendeleo, na rasilimali walizo nazo Iran ya sasa, lakini asilimia 75 ya maji yao yote wanayo yatumia sasa, wanayategemea kutoka kwenye mifereji hiyo ambayo hatujajua mpaka sasa mjenzi wake ni nani. Yes mifereji hiyo iko safi na inafanya kazi yake tangu maelfu ya miaka huko nyuma, mpaka sasa. Hatumjui huyo injinia bado.
Kulingana na muandishi huyu, Qanat na mifereji mingine ya chini ya aridhi kwenye jangwa hilo ni kama mishipa ya damu kwenye mwili. Lakini nani mjenzi wa kazi hii?


MOROCCO. Mtandao wa njia za chini ya aridhi, kwa umbali wa futi 250 kwenda chini, na hapa ni chini ya jwangwa, ulitengenezwa kwa ajili ya kukusanya maji kutoka chini ya aridhi. Njia hizo kila baada ya maili 100 kumewekwa mabomba kwa ajili ya kuingiza na kutoa hewa.


Morocco, kama Iran.

Hata sasa, na maarifa, elimu, teknolojia na rasilimali tulizo nazo kufanya mradi kama huu chini ya jangwa ni vigumu mno kuliko kuufanya sehemu zisizo na jangwa. Lakini ulifanyika na uko hapo.


Ukiwa juu ya aridhi, mifereji hiyo imejengewa ukuta kama kisima, lakini hicho siyo kisima ni shimo la kuingiza na kutolea hewa.

EGYPT. Maandishi haya, yananifanya nikifikirie tena ikiwa mfereji wa Suez maarafu (Suez Canal) kama kweli ulijengwa na mafarao! Utakumbuka kwenye posti za nyuma tumezungumzia kupatika meli za kale mno hapo Egypt kushinda kipindi cha utawala wa mafarao.


Ukiwa ndani ya mifereji hiyo, chini ya aridhi hichi ndicho unacho kiona, ni kama upo kwenye mji mwingine kabisa, lakini hapa ni chini ya aridhi yenye jangwa kubwa barani Afrika.


MAPANGO, MAHANDAKI NA NJIA ZA CHINI YA ARIDHI

DOMINICA. Shimo la dhahabu, lina kina cha urefu wa futi 16,000 kwenda chini na upana wa mile 6. Tuliligundua shimo hili kwenye karne ya 15, kipindi hicho habari za hili shimo ndiyo ilikuwa ‘story’ ya mjini.

Lakini kwenye mabara yote saba, kumekuwa na taarifa na ushahidi pia wa kuwepo kwa mapango makubwa, mahandaki na njia pana za chini ya aridhi na chini ya bahari pia, zinazo kwenda maelfu ya maili kwa urefu. Njia hizo za chini ya aridhi na chini ya bahari zipo zinazo unganisha bara moja na jingine!
Ramani hii inaonesha namna dunia nzima inavyo weza kuonganishwa kwa kutumia mahandaki na njia za chini ya aridhi


Haya si kwamba ni moja ya maajabu makubwa, lakini ni moja ya habari zinazo fichwa kwa kila hila na mbinu ilimradi tu watu tusifahamu.

Utawaambia nini watu? Kwamba watu wa kale tunao ambiwa walitumia zana duni za mawe na vijitu waliweza kutengeneza si tu majumba makubwa, ambayo bado yapo mpaka leo, barabara pana na imara tunazo zitumia mpaka leo, mifereji na mabwawa makubwa yanayotumika mpaka leo, lakini eti kwamba walijenga barabara chini ya aridhi, na si chini ya aridhi tu, na chini ya bahari pia, na si chini ya bahari tu, lakini refu kiasi cha kuonganisha mabara mawili au zaidi?
Njia 'mpya' za chini ya aridhi na chini ya bahari zinazo pendekezwa kwenye mchoro huu, karibu asilimia 80, zinafuata njia za kale mno, ambazo mpaka sasa hatuja fahamu wachimbaji wake ni akina nani, na kwa vile 'serikali' zote na taasisi zao elimu zeme linyamazia hilo, inaonekana kuwa wao ndiyo wavumbuzi au teknolojia imekuwa kubwa kiasi wameweza kutengeneza njia za chini ya aridhi, lakini si kweli, ni njia ambazo wamaezikuta na kwa makusudi hawasemi kuwa zilichimbwa na nani.

Whaaaaaaaat! Are you talking about?
Yeah! The truth is stranger than fiction dear!

Habari ya barabara na njia za chini ya aridhi na chini ya bahari tumekuwa tukizisikia kwenye hadithi za kufikirika na ngano za kale, na sote tukidhani ni hadithi za kufikirika, lakini kuna ukweli zaidi ya ngano na hekaya.
Mtambo wa kisasa kwenye teknolojia yetu, unao tumika kuchimbia njia za chini ya aridhi. Mtambo huu haujafikia ubora wa zana zilizotumika makumi elfu ya miaka huko nyuma katika kufanya kazi hiyo. Ni zana gani walitumia.

AFRIKA.
Tuanzie nyumbani, mcheza kwao hutuzwa. Utakumbuka kwenye posti iliyopita tulizungumzia watu wa Mali na mbilikimo wa Zaire, ambao walikuwa na ujuzi na taaluma ya nyota na sayari mbalimbali ambazo ni majuzi tu ndiyo tumekuja kuzigundua na kuthibitisha. Kwenye hili la njia za chini ya aridhi Afrika hatupo nyuma, na siyo Afrika tu, hata hapa kwetu Tanzania hatupo nyuma.



MOROCCO mpaka SPAIN. Ipo njia kubwa chini ya bahari siyo chini ya aridhi, narudia tena, chini ya bahari, ambayo inaiunganisha Morocco na Spain, au kwa uwazi zaidi Afrika na Ulaya. Yaani unapo tembea kwenye njia hiyo unaanzia chini ya aridhi, kwenye handaki halafu unakwenda mpaka unaifikia bahari, lakini hapa bahari inakuwa juu, wewe unakuwa chini, moja kwa moja mpaka Ulaya.


Kama unavyoona, bahsri ipo juu, njia ipo chini ya bahari.

Serikali ya Spain na Morroco wanaangalia uwezekano wa kuonganisha tena Ulaya na Afrika kupitia eneo hilo. Lakini wataalam walio pewa kazi hiyo ya utafiti na kuja na suluhisho, wanaitilia mashaka njia ya chini ya bahari, si kwamba si salama, lakini wanasema ‘Hatuna teknolojia ya kuweza kuitoboa miamba hiyo ambayo ni migumu sana.’ 
Morocco na Spain wana pendekeza njia ya namna hii, ambapo itapita ndani ya maji, na siyo chini ya maji, sababu hatuna teknolojia ya kuchimba chini ya maji! Je waliochimba chini ya maji ni akina nani, wa zama gani, kwa teknolojia ipi?

Hivyo wanapendekeza pajengwe mfano wa bomba kubwa ndani ya bahari, lakini siyo chini ya bahari, hapana, ndani ya maji ya bahari ambalo ndilo liwe njia ya treni kutoka Morocco mpaka Spain.

Swali la kujiuliza ni wakina nani waliichimba hiyo njia ya chini ya bahari ya kutoka Morocco mpaka Spain, waliichimba kwa teknolojia gani, ya zama gani, kiasi kwamba leo sisi kwenye zama tunazo ita za teknolojia tunashindawa kufanya kitu kama hicho?

Mwandishi wa kitabu cha The Lost World of Agharti, anasema kunazo taarifa za wasafiri wa kiafrika juu ya kuwepo kwa uwanda mkubwa wa njia, mahandaki na mapango chini ya aridhi ya bara hilo, ambazo msafiri anaweza kwenda mamia ya maili. Anasema mathalani upande wa Malawi, kusini mwa ziwa Tanganyika, chini ya mto Kaoma, kuna handaki na njia za chini ya mto huo ambazo msafiri anaweza kwenda kuanzia alfajiri mpaka jua la utosi ndiyo anaweza kutokea upande wa pili.
Amboni

Tanga, kunako mapango ya Amboni, mengi yameandikwa, hasa kuhusu vinyago na baadhi ya michoro na kipindi fulani makazi ya wahalifu, mashujaa n.k. Lakini kimoja ambacho hakijaandikwa sana ni kuhusu mahandaki na njia zinazo anzia kwenye mapango hayo na kukupeleka mpaka chini ya Mlima Kilimanjaro!



Ni maneno ya wakazi wa maeneo hayo, na baadhi ya ‘tour guider’. Wanasema kuna ambazo zitakupeleka mpaka Kilimanjaro na zitakazo kupeleka mpaka Mombasa. Hakuna taarifa rasmi ya kiserikali juu ya njia hizo, lakini ni juu ya watafiti na wanahistoria kujitupa kwenye hilo na kulifanyia kazi.

AFRIKA YA KASKAZINI.
Mmisionari, David Livingstone anaandika, “Makabila yanaishi chini ya aridhi, kwenye mahandaki na wamejenga nyumba humo chini ya aridhi.” (The Lost World of Agharti,)

NIGERIA
Kwenye wilaya ya Wama, kume patikana mapango ya kale na mahandaki yenye njia za chini ya aridhi, ambazo wakazi walitumia pia kama sehemu za kujifichia, njia zingine zinakwenda mamia ya maili mpaka kwenye bahari ya Atlantik, karibu na nchi ya Guinea.

EGYPT
Handaki ambalo mlango wake umefungwa, chini ya moja ya Pirami la Geza. Handaki hilo inasemekana linakwenda mpaka Tibet, kunako milima ya Himalaya.



ULAYA
GREAT BRTITAIN. Kuna mahandaki makubwa na ya kutosha kwenye eneo la Yorkshire. Kumekuwa na ngano na hadithi za kale mno kwa wakazi wa hapo juu ya jamii inayo ishi chini ya mahandaki hayo.

FRANCE
Mwaka 1834 kanisa la Gapennes katika eneo la Picardy lilipo dondoka ikafahamika kuwa kanisa hilo lilikuwa limejengwa juu ya mtandao mpana wa mahandaki na njia za chini ya aridhi, utafiti ulipofanyika zaidi ya mahandaki 100 yalipatikana eneo hilo.
Moja ya mahandaki yanayo patikana Ufaransa, hili limejengwa upya na kutiwa nakshi, lakini asili yake ni la kale mno. Bado tunawatafuta wajenzi wa asili wa kazi hizi.


UJERUMANI
Ushahidi wa kutosha unathibitisha uwepo wa mahandaki na njia za chini ya aridhi ambazo katika vipindi mbalimbali vya vita yalitumika na wakazi kwa ajili ya kujifichia. Wakazi wa maeneo husika wanayafahamu mahandaki hayo kwa jina la ‘Southern Siberia’ sababu mtu anaweza kutembea kwenye mahandaki hayo kutoka Ujerumani mpaka mpaka Siberia, hayo ni maelfu kama siyo malaki ya kilometer, chini ya aridhi, kutoka Ulaya mpaka Asia.
Handaki hili Ufaransa walilibadilisha na kufanya ni kama kaburi, wakajaza mifupa na mafuvu ya watu, na sasa limegeuka kuwa kivutio cha utalii. Lakini ukilitazama unaona kabisa ni njia inayo elekea mahala fulani.

SOUTH AMERICA
Juu kabisa kwenye vilele vya milima ya Andes, mahandaki yana iunganisha milima hiyo na Machu Picchu, na maeneo mengine, ambapo kuta za mahandaki hayo zimechongwa vizuri kwa ustadi mkubwa, huwezi kuiita ni kazi ya mazingira yake, bali ni kazi ya kizazi fulani cha zama za kale, lakini ni kizazi gani?, Kwenye zama zipi? Handaki jingine linapita chini ya mto Urubamba.

ECUADOR
Yamepatikana mahandaki na mtandao mpana wa mahandaki kwa urefu wa maelfu ya maili, kutoka Ecudor mpaka Peru. Na pia inaunganisha Lima mpaka Cuzco na inaendelea mpaka Bolivia au hata mpaka baharini.

PERU
Baada ya tetemeko la ardhi la mwaka 1972 kwenye mji wa Lima, wataalam wa uwokozi waligundua kuwa sehemu kubwa ya jiji hilo, chini ya aridhi kuna mahandaki na njia za chini ya aridhi zenye mtandao mpana za kuonganisha handaki moja na jingine na zote zikiwa zinaelekea milimani.

Hadithi na ushahidi wa kushikika kuhusiana na barabara, njia, mahandaki ya chini ya aridhi, chini ya bahari na chini ya mito mikubwa na midogo; ni nyingi na za kale mno, kiasi watu wakizipuuza na kudhani ni ngano za kale za kufikirika, lakini; HAPANA, nenda Peru, Brazil, South America yote, Ulaya, Asia, Afrika.
Mchoro huu ukionesha baadhi ya mji ulio patikana chini ya aridhi Uturuki, huu ni mji chini ya aridhi.

Lakini wakati unafikiri juu ya mahandaki hayo ya chini ya aridhi. Nikuongezee tu kuwa kwa maeneo kama Amerika ya Kusini,Afrika, Amerika ya Kaskazini, Ulaya, Asia kifupi kwenye mabara yote, mpaka kwenye bahari ya Pasifiki na visiwa vyake kumepatikana pia mahandaki na njia chini ya aridhi, na miji mikubwa chini ya aridhi ... Tunaiandika tena historia ya binadam ...
Kama huwezi kuamini mpaka uguse, kama Thomas, basi andaa mabegi nafunga safari mpaka Uturuki, Jiji chini ya aridhi. Kwa Teknolojia yetu sasa hivi tunajenga ghorofa mbili mpaka tano au kumi chini ya aridhi, lakini siyo jiji. Jiji kamilifu lenye njia nyumba za wakazi, maduka, sehemu ya mifugo mifumo ya hewa na maji taka, chini ya aridhi. Najiuliza ikiwa binadam tuna 'evolve' kwenda mbele kama alivyo tuambia Darwin au tuna 'evolve' kurudi nyuma?


Naweza kuendelea na kuendelea, lakini kwanini nikuchoshe, bahari ya maarifa imejaa na kumwagika mpaka kwenye pwani, upatikanaji wa taarifa tangu binadam wa ‘Darwin’ aanze kutumia zana za mawe haujawahi kuwa mpana hivi, fanya utafiti wako binafsi, kisha ulete hapa kuthibitisha haya au kuyapinga, uhuru ni wako.

Guys till next ... still there is so much to cover on subject and I am working on it ... our goals is to found who was behind all these and if possible to rewrite the history of a man on earth ... Tchaoooo

2 comments:

  1. Enter your comment...kaka umetutupa xana xx ni watu wakalibu tunafatilia unachokiandika

    ReplyDelete