Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, April 9, 2017

JE TUPO WENYEWE KWENYE ULIMWENGU? S02, Ep9 (Nyayo za Wageni Kutoka Sayari Ya Mbali - Usafiri, Dunia, na Anga)


Ni lini binadam wa zama za mawe alianza kuchimba chuma?
 Kulingana na Darwin, zana zake zilikuwa bado ni duni, na alitumia mawe butu siyo chuma.

Haiwezekani alichimba chuma katika zama za mawe, kulingana na Darwin na kulingana na historia wanayo tufundisha.


 Bado aliishi mapangoni kama wanyama wengine.

Lakini cha jabu kote duniani kumekuwa na mashimo makubwa ya kale mno, ya kale kuzidi historia ya ‘binadam wa leo’ mashimo hayo madini na vito mbalimbali vilikuwa vikichimbuliwa ikiwemo chuma.

Lion Cave, Swaziland, Afrika Kusini, moja ya mashimo ya kale mno, shimo hilo limekwenda chini zaidi ya futi 30, maelfu na maelfu ya tani za chuma zilichimbwa zama hizo. Wanahistoria wetu wanakuambia walitumia mawe na mifupa kuchimba chuma. Si kichekesho hicho, tani zote hizo walizifanyia nini? Maswali ni mengi yasiyo jibika.

Je binadam wa zama za mawe alikuwa akichimba chuma? Lakini si walichimba tu bali pia walisafirisha biadhaa hizo sehemu mbalimbali, maelfu ya mali kutoka eneo walilochimbia. Si kwamba walichimba, kusafirisha lakini pia waliweka kumbukumbu ya maandishi, na kimahesabu ya kazi yao hiyo. Kweli zama za mawe, au ... hivi ni kweli tulikuwa na zama za mawe? Darwin uko wapi mbona mambo magumu huku na vitu vingine hatuvielewi, au hukutufundisha vitu vyote?
Mathalani shimo hili lipo Marekani, Michigan, moja ya mashimo ya kale sana kuchimbwa chuma kabla ya zama za chuma. makabila ya Marekani ya kaskazini hayakuwa kuchimba chuma wala hakuna rikodi zozote zinazo onesha kuwa walikuwa na taaluma hiyo. Swali lile lile, nani alichimba na lini?
Kote duniani, Afrika, Ulaya, Amerika na mabara mengine, mashimo mengi ya chuma na madini mengine yalikuwa tayari yameshaanza kuchimbwa kabla ya sisi kuendelea nayo.

USAFIRI WA BAHARINI.
Kwenye miaka ya 1920, meli mbili za Kirumi zilipatikana chini kwenye ziwa Nemi, Italy. Kama kawaida meli hizo zikatajwa kuwa ni kazi ya moja ya viongozi wa dola ya Roma. Lakini kama yalivyo ma Pyramid ya Egypt na kwengineko, dai hilo halina mashiko.
Masalio ya moja ya meli hizo ilipo ibuliwa kutoka chini ya ziwa Nemi.

Meli hiyo ilionekana kuwa na uwezo wa kubeba watu 120. Inayo kebini 30, yenye bafu 4, eneo la wafanyakazi wa meli, sakafu ya marumaru (tiles), nguzo za chuma, maktaba, mgahawa, jiko n.k. Ni vigumu kuamini kuwa meli hiyo inaweza kuwa ni ya kale kuliko dola ya Roma, ingawa huduma zilizomo ni kama meli ya kitalii.

Muonekano wa meli hiyo endapo ingefanyiwa ukarabati. Ilifanyiwa lakini akaja kulipuliwa wakati wa WWII.


Ukienda Egypty unakutana na meli yanye urefu wa futi 350 na upana wa futi 60, yenye mgawanyo wa sehemu nne ya abiria kukaa juu ya wengine, kama vile first class, economy n.k. Lakini si ya kwenye milenia yatu, hapa bali maelfu ya miaka nyuma kabla ya Kristo.

Ukistaajabu ya Mussa utaona ya Firauni.
China, Ugiriki vimepatikana vyombo vya usafiri kwenye maji ambavyo vina urefu kati ya futi 250 mpaka 600 na vyenye uwezo wa kubeba karibu watu 600 kwa wakati mmoja, ambazo ni kubwa mno hata ukilinganisha na zile ambazo wazungu waliaanza kuzitumia baada ya kufanya uvumbuzi wa usafiri wa bahari.

Ukija Sumeria, kamusi ya watu wa Akkadia (Akkadian) inajumuisha sehemu maalum kwa ajili ya meli, ambapo imetaja majina mpaka 105 kwa ajili ya meli mbalimbali kulingana na ukubwa, kazi, kituo, safari inazofanya, mpaka nyambizi (submarine) n.k.
India nyaraka inayo kadiriwa kuwa ya miaka 3000 nyuma, inayo sura nane maalum zinazo zungumzia vyombo vya usafiri vinavyo safiri angani, juu ya maji na ndani ya maji. 
Mfano wa nyambizi katika zama zetu za leo.

Wakati kwenye historia wanatufundisha kuwa watu wa kale hawakuwa na maarifa, walianza kwa kuzigeuza meza zao na kuziweka kwenye maji wakaanza kusafiri nazo na taratibu ndiyo wakagundua majahazi, lakini historia nyingine inatuambia hapana, walikuwa na taaluma kubwa hata kutushinda kwa upande huo wa usafiri wa anga na maji.
Je tumekopi kutoka kwenye dunia isiyo fahamika?

Kwenye usafiri na mawasiliano vitu mbalimbali kutoka sehemu moja ya bara vilipatikana kwenye bara jingine. Mathalani maandishi, kazi za sanaa, bidhaa zinazo fahamika asili yake ni kona flani ya dunia, vimepatikana kwenye kona nyingine ya dunia vikiwa na kumbukumbu za maelfu ya miaka kabla ya Kristo. Lakini ni wazi kwa teknolojia tuliyo iyona na tutakayo endelea kuiyona ya viumbe hao, suala la usafiri kutoka kona moja ya dunia kwenda nyingine haliwezi kuwa na alama ya kuuliza.

Miji kama ya, TENNESSEE, GEORGIA, GUATEMALA, MEXICO, PERU, PANAMA, MEXICO, ECUADOR kutaja kwa uchache sana, kumepatikana vitu kutoka maelfu ya maili na vingine kutoka mabara mengine, vinavyo ashiria kuwepo kwa mawasiliano baina ya jamii hizo.

Lakini pia ukitazama ujenzi wa Pyramidi, ingawa nimetaja miji michache kuhusiana na hili, ila ukweli ni kuwa yalijengwa dunia nzima, kwenye mabara yote kwa muundo na utaratibu unao wiana, na hata maeneo ambayo yaliyo jengwa yalikuwa yanawiana kimazingira, au kinajimu, au kivipimo kwa maana ya latitude na longitude, na mengine unaweza kuchora mstari ulio nyooka kutoka jengo moja kwenda jingine kuzunguka dunia nzima.

Ngano za kale haziwezi kuwa za jabu zaidi ya hivi. Lakini hizi si ngano za kale, bali ukweli wa msingi, takwimu moja baada ya nyingine, kielelezo kimoja baada ya kingine, maisha ya watu maelfu ya miaka, kama siyo maelfu, elfu ya miaka kabla ya Kristo, hadithi zao, kazi zao, maisha yao na juu ya yote ushahidi wa hayo.

Wanahistoria, wanasayansi, wanajiografia, na wengine wabobezi katika fani zao wanazipokea habari na ushahidi huu kwa ukimya usio elezeka, hakuna katika nyuso zao ila macho ya kusalitiwa, moyo uliovunjika na ubongo uliofikia tamati. Kuukubali ushahidi huu ni kutoa kibali cha kuandika upya historia ya dunia, na hasa ya binadam ambayo kwa maelezo yao ni kuwa hauna zaidi ya miaka 4000 iliyopita.

Hatujafika bado, safari inaendelea, safari ya kukusanya ushaidi wa kutosha kabla ya kutoa hukumu.

Ni juzi tu wanasayansi wetu walikuwa wakisema dunia haiwezi kuwa tufe, sababu walio sehemu ya chini wangeanguka na kupotelea pasipo fahamika. 

Ni juzi walikuwa wakisema nyota za angani haziwezi kuzidi 1,500! Lakini uvumbuzi wetu wa leo unatuonesha kama ni watu wa nyuma mno kwa kila kitu ukilinganisha na maarifa na taaluma ya watu walio ishi miaka 15,000 KK au zaidi!

Wanajimu wa Babiloni, Egypt, Kaanani, Sumeria, Mesopotemia, India kutaja kwa uchache walimiliki zana bora na zali hali ya juu kwenye masuala ya anga, au kuwa wakweli zaidi kwenye hili, walirithi zana bora na za hali ya juu kwenye mambo mbalimbali kutoka kwa jamii isiyo fahamika.

Miji ambayo naitaja katika posti hizi ni kwasababu baada ya maelfu na maelfu ya miaka kupita ushahidi ulitufikia ni vipande vipande, ingawa kuna kila dalili kuwa maarifa na taaluma hiyo ilikuwa ulimwenguni kote zama hizo.
KUHUSU DUNIA

Maeneo kama EGYPT, CHINA, ENGLAND, GUATEMALA, TIAHUANACO, BOLIVIA, GREECE, INDIA, SUMERIA, BABILONI, SSYRIA, HITTITE, na SASIA MINOR; walikuwa na rikodi au walirithi rikodi zilizo kuwa zikionesha kuwa dunia ni duara, imezungukwa na mbingu. 

Wasumeria wao rikodi zao zilikuwa mpaka na majina ya nyota, na majina ya vikundi vya nyota vya anga la kusini na kaskazini. Wajenzi wa Pyramid kama tulivyoona hapo nyuma, wao walijua mpaka ukubwa wa kipenyo cha dunia, ukubwa wa duara la dunia, sehemu nyota zilipo, safari za nyota hizo zama hadi zama. Vipimo vyao vilikuwa sahihi kuliko vipomo tulivyo kuwa navyo karne ya 19!

Miji kama INDIA, CHINA, GREECE na ROME walikuwa wakifaham kuwa dunia ni duara na inaelea angani, inajizungusha kwenye mhimili wake kwa masaa 24, na inalizunguka jua, njia yaje ya kulizunguka jua imekaa kama yai. Wapi walirithi haya maarifa, kutoka kwa nani? Ghafla mbona yamepotea? Ghafla mbona tunakutana na binadam wa Darwin ambaye hajui chochote?

Ukija tena kwenye miji niliyo itaja yaani, unakuta vipimo vya dunia kwa maana ya uzito wa tufe la dunia lina uzito kiasi gani, hapo ni GUATEMALA. BABILONI NA EGYPTY  vipimo sahihi vya siku ngapi dunia inachukua kulizunguka jua, wameandika siku 365.2420, mahesabu yetu ya leo ni 365.2422!


 Ni kweli kulikuwa na binadam wa zama za mawe a.k.a binadam wa Darwin? Kwa taaluma hiyo katika zama hizo, binadam wa leo tungetegemea awe ameanzisha makazi kwenye Mars, sayari nyingine na hata kuvumbua ulimwengu (Universal) mwingine, ambayo kwenye sayansi ya leo bado ni nadharia.

KUHUSU MWEZI
INDIA wao walikuwa na vipimo kuhusu umbali wa kutoka kwenye mwezi kuwa ni maili 253,000. Vipimo vyetu vya leo vinatuambia ni 252,710. Watu wa mahesabu za makadirio na waachia mnipe jibu.  Vipi walijua hivyo vipimo za ambazo wanahistoria wetu wanatuambia ni zama za giza na ujinga?

CHINA, UGIRIKI, INDIA, CHALDEA, walikuwa na elimu kuwa mwanga wa mwezi si wakwake, kwamba mwezi hauzalishi mwanga, inaukopa mwanga huo mahali. Leo tunafaham kuwa mwezi unaakisi nuru yake kutoka kwenye jua!

Walifahamu njia inayopita mwezi kuizunguka dunia ipo kama yai, na kuna wakati mwezi unakuwa karibu na dunia, na wakati mwingine inakuwa mbali na dunia. Walikuwa na hesabu ya siku ambazo mwezi inazitumia kulizunguka jua. Mathalani watu wa MAYA walirikodi ni siku 29.53020, kwa mahesabu ya zama zetu ni siku 29.53059.

Naweza kuendelea zaidi na zaidi kwenye Jua na kila sayari unayoijua kwenye mfumo huo, hawa jamaa rikodi hizo walikuwa nazo, tena kwa usahihi wake.

NJE YA MILK WAY
Nje ya galaxy yetu inayo fahamika kama milk way. CHINA walikuwa na rikodi kuwa kile kinachonekana kama anga la buluu si chochote bali ni rangi inayo tengenezwa na ufinyu wa macho kuona. Leo tumejua kwamba buluu tunalo ona angani siyo mbingu ile, ni mtazamo wa mwenye kutazama kutokana na mchanganyiko wa gesi mbalimbali.

INDIA na UGIRIKI walikuwa wakitambua kwamba ulimwengu hauna mwisho, leo tumejua kwamba ulimwengu unatanuka na hauna mwisho.
Kabila la wa Dogoni walio ishi MALI, wao walikuwa wanajua kuwa nyota ziko mbali zaidi kuliko sayari. Leo huo ndiyo ukweli wa msingi kwenye sayansi yetu ya anga.

INDIA na UGIRIKI walikuwa na elimu kuwa nyota za angani hazihesabiki. Sisi tulikuwa tunasema hazi zidi 1,500. Lakini sasa inafahamika kuwa nyote zote kwenye ulimwengu (universal) huu hazihesabiki na idadi yake inazidi idadi ya michanga ya pwani zote za bahari zote za dunia hii. 

Yes sijakosea, idadi ya nyota zote kwenye ulimwengu (universal) zinazidi idadi ya michanga yote (kama utaweza kuhesabu kimchanga tu moja mpaka tu ngine) yote ya pwani zote za bahari zote kwenye dunia yote!
Ukifikia nukta hiyo kwanza mtukuze Mola wako mbora wa waumbaji.

SUMERIA na UGIRIKI walifahamu kuwa kila nyota ni mfumo kamili wa jua wenye sayari zake. Ni Juni 1984, American Astronomical Society walitangaza kuwa nyota 40 ambazo zipo karibu na sisi zimeonesha kutoa milipuko kama inayo tolea na nyota yetu kubwa inayo itwa JUA, na hivyo inaashiria kuwa nyota hizo zitakuwa zinayo vitu vigumu na hata sayari zinayo zizunguka.

Watu wa Dogoni walio ishi MALI, Africa walikuwa wakifahamu kuwa galaxy yetu, milk way ipo kwenye umbo mithili ya dawa ya mbu (dawa ya mbu ya zamani) umbo hilo kwenye lugha ya kigeni ni spiral, kwenye karne hii ndiyo sisi tumethibitisha hayo!

EGYPT, SUMERIA, WATU WA DOGONI walioishi MALI, watu wa fupi (mbilikimo) wa ITURI, walio ishi ZAIRE, leo Demokrasia ya watu wa Kongo; walikuwa na rikodi kuhusiana na Nyota ya SIRIUS A. 

Wameitaja nyota inayo izunguka Sirius A. Nyota hiyo ni nyeupe lakini haionekani, njia yake ni kama yai, umbali ilipo Sirius A na njia ya hiyo nyota inayoizunguka pia waliujua, inazunguka kuizunguka nyota inayo ng’ara sana ambayo ndiyo Sirius A kila baada ya miaka 50, pia nyota hiyo ni nyota nzito mno.

Kwa kutumia mashine ya telescope yenye nguvu na taaluma yetu ya leo tumeweza kuthibitisha kila taarifa iliyo tajwa na watu hao wa kale kuwa ni ya kweli na sahihi. Kale yenyewe si ya juzi, bali ya maelfu na maelfu ya miaka kabla ya Kristo, lakini leo sisi ndiyo tumekuwa na teknolojia ya kuthibitisha hayo.

Hatukuweza kuiyona kwenye teleskopi zetu mpaka mwaka 1862, na hatukuweza kipindi hicho kuipiga picha mpaka mwaka 1970. Nyota hiyo inayo izunguka Sirius A, uzito wake ni mkubwa kiasi kwamba mchanga au jiwe dogo unaloweza kuliweka kwenye kijiko kidogo cha chai kutoka kwenye sayari hiyo, kijiwe au mchanga huo ni sawa na tani 20,000 za mchanga au mawe kwenye sayari yetu! Nguvu zake za mvutano ni kubwa mara milioni 100 ukilinganisha na nguvu za mvutano za dunia yetu.

Jiulize ni wapi watu hawa katika zama hizo waliweza kufanya utafiti na gunduzi ambazo ndiyo kwanza tunazithibitisha leo? Walizirithi kutoka kwa nani? Mmiliki wa taaluma na teknolojia hiyo ni nani na alishi katika zama zipi?

Ndiyo kwanza kuna kucha, unajua kwamba watu hawa walikuwa na kompyuta? Unabaki mdomo wazi, vipi kuhusu ndege, vipi kuhusu njia chini ya bahari, vipi kuhusu barabara za mwendo kasi?
Upo?

afKama ni safari hata bado hatujaanza, tunaiandika upya historia ya binadam ...

Stay tune ushahidi bado haujatosha TUKUTANE NEXT TIME NA VIELELEZO VINGINE .... TCHAO.

25 comments:

  1. Makala hii imekata kiu ya wanafunzi,Walimu wa ngazi ya Elimu ya msingi ,sekondari na vyuo.Mungu ibariki blog hii,Mungu mbariki Salim Msangi.

    ReplyDelete
  2. A nice scholarly work

    ReplyDelete
  3. Hongera kaka kwa kutufumbua macho

    ReplyDelete
  4. Hongera kaka kwa kutufumbua macho

    ReplyDelete
  5. hongera bro kwa kazi nzr sana unayoifanya tupo tunajifunza mingi sana kupitia ww.

    ReplyDelete
  6. Ubarikiwe sana kaka Salim kwa Makala nzuri na ya aina yake.

    ReplyDelete
  7. Je suis ni kina nani? Ni kweli walihusika na kuzama kwa meli ya Titanic? Niko katika kujifunza ndugu yangu bwana Salim na ningeshukuru mno kupata ukweli na ufafanuzi juu ya hili. Ahsante!

    ReplyDelete
  8. Hii ya barabara chini ya bahari nayo kali wapo waliokuwepo kabla yetu

    ReplyDelete