Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Saturday, April 1, 2017

JE TUPO WENYEWE KWENYE ULIMWENGU? S02, Ep8 (Nyayo za Wageni Kutoka Sayari Ya Mbali - Ujenzi wa Maajabu)

Ili tuweze kuwa na hitimisho lenye vigezo vya kitaaluma na kisomi hapana budi kuchambua kila aina ya ushahidi tunao upata, hivyo bado tunaendelea kuvipitia hivi vielelezo, ingawa unacho kiona hapa kwenye hizi posti ni kama 'karanga kwenye dafu la nazi' hivyo ni wajibu wako msomaji kuzama kwenye bahari pana ya vyanzo mbalimbali uweze kujiridhisha.


TIAHUANACO, BOLIVIA

Yale ambayo hayawezi kutokea, yametokea hapa. Ni eneo ambalo mkandamizo wa hewa ni mkubwa mno, kiasi kufanya hewa ya oksijeni kuwa ndogo sana. Lakini tofali lenye uzito wa tani 200 limekokotwa kwa umbali unao kadiriwa kufikia maili 90, kwenye eneo ambalo hewa ya oksejeni ni ndogo mno ni vipi kazi hii ilifanyika.

Jengo lililobaki kama masalia limejengwa kwa utaalam ambao hauwezwi kulinganishwa na teknolojia yetu, mbele ya ujenzi huo utaalam wetu wa ujenzi unasimama kama kituko.
Maheka na maheka maumbo ya jabu yamesimama, mapyramid, vyumba chini ya aridhi, mageti makubwa mno ambayo vyote hivyo vinathibitisha kutumika kwa taaluma ya hali ya juu mno kwenye Sanaa ya ujenzi, na si ya hali ya juu tu, lakini pia ambayo katika zama zetu leo, bado sana kuifikia.

Mageti mengi hapa utayaona yamejengwa kwa jiwe moja tu. Mathalani ‘Gate of the Sun’ ni jiwe kubwa mno kupata kuchongwa duniani na kusimamishwa kama geti. Futi 10 kwenda juu na upana wa futi 6.

Ukubwa wa majengo mengine hapa ni maajabu ndani ya maajabu. Hekalu la Jua limejengwa kwa mawe ambayo kila moja uzito wake ni baina ya tani 100 mpaka 200. Kuta za hekalu hilo zimejengwa kwa mawe yenye uzito wa tani 60 kila moja, ngazi zake zimetandazwa kwa mawe yenye ujazo wa tani 50 kila moja.

Mawe yamechongwa kwa ustadi mkubwa kiasi huwezi kuona ni wapi ynaungana na yakapigwa polishi.

 SACSAYHUAMAN, PERU


Inatamkwa ‘sexy woman’ ingawa haimaanishi hivyo. Ni kama ngome, juu kileleni kwenye mlima utaona mji wa zamani wa Cuzco. Mawe yenye ujazo ule ule wa tani 50 mpaka 200 unayakuta hapa. Hayapo chini, bali juu kusimamisha majengo yenye mvuto wa kipekee. 

Mawe hayo yameonganishwa moja juu ya jingine au pembeni kwa ustadi ambao huwezi kupitisha kisu au wembe baina yake. 

Jiwe moja unakuta limechongwa sawa sawa ili kuwezesha mawe mengine kumi na zaidi kuunganishwa na hilo ili kwa pamoja yatengeneze ukuta. 

Tizama picha hiyo hapo chini na uone jinsi gani kila jiwe limeweza kufiti na mwenzake sawia kwa kila upande na kwa ndani pia! Hi si kazi ya asili, yupo aliye nyuma ya kazi hii, yupo ambaye aliifanya kazi hii. 

Ni nani huyo, na katika zama zipi?

Kwa umbali wa kama yadi 100 kwenye eneo hilo pamelala pande linguine la jiwe lenye ukubwa sawa na jingo la ghorofa 5, lenye uzito unao fika tani 20,000! 

Halionekani kuwa ni kazi ya asili kwenye mazingira yake, bali kazi iliyofanywa kwa makusudio maalum, nani mfanyaji wake? Hata sasa hatuna mashine ya kusogeza uzito wa namna hiyo.

BAALBEK, LEBANON

Mahekalu mawili ya warumi yamejengwa juu ya msingi wa kale mno ulio kuwepo hapo kabla ya mahekalu hayo kujengwa. Mahekalu hayo makubwa kupata kuwepo kwenye dola ya warumi hata kidogo hayawiani na msingi unayo yabeba.
Msingi huu unadhihirisha taaluma ya hali ya juu kwenye fani ya ujenzi, ujuzi ambao mpaka leo historia haijatengeneza kopi yake.

Jiwe moja kwenye msingi huo linaukubwa sawa na basi, urefu wa futi 82 na kimo cha futi 15, likikadiriwa kuwa na zito baina ya tani 1,200 mpaka 1,500.

Mapande hayo ya mawe uliyatizama utaona yame nyanyuliwa kutoka aridhini kwa futi 20. Hata kwa kutumia zana za sasa, na teknolojia yetu ni kichekesho, hatuwezi kusogeza mapande hayo ya mawe. Lakini yalinyanyuliwa na yakawekwa kwa vipimo sahihi, mahala sahihi yaliyopaswa kuwekwa, na kuunganisha moja na lingine kiasi baina yake huwezi kupenyeza makali ya kisu kilicho nolewa.

Ni akina nani hao waliyo fanya kazi hii iliyo lenga kubakizwa hapo milele?


Ni vigumu mno kumuweka binadam wa sasa kwenye picha hii, wala si binadam wa Darwin anayefit hapo. Inahitaji watu 40,0000 kulisogeza jabali hilo, hata kama watapatikana na walisogeze ni vipi wau 40,0000 wanaweza kutosha kwenye eneo hilo la ujenzi na kuweza kulinyanyua jabali hilo?



Haiwezekani, kifupi inakuambia si binadam walio fanya kazi hiyo, wala hakuna mashine yeyote, kokote duniani kwenye majengo haya ambayo imeachwa kama alama ya namna gani walifanyiza kazi hizo. Fumbo juu ya fumbo. 

Ni viumbe gani hao, katika zama zipi? Mbona teknolojia yao na yetu ni kama nazi na karanga unapolinganisha na yetu.


EASTER ISLAND


Mbali kwenye kisiwa kilicho tengwa.
Mamia ya mawe ya ajabu yenye sura zinazo lingana na binadam, kila moja lina uzito baina ya tani 35 mpaka 50. Sura hizo zingine zimevalishwa kofia nyekundu. Kofia peke yake zinafikia uzito wa tani 10 kwa kofia moja. Kipenyo cha duara kwenye kofia hizo ni futi 25 na kimo cha futi 7. Kofia hizo ‘zilivalishwa’ baada ya masanamu hayo kusimamishwa.

Masanamu hayo yalichongwa karibu na mlima, kisha yakabebwa kutoka hapo umbali wa maili 5 mpaka mahala yalipo sasa bila kuacha alama yeyote. Masanamu mengine ni makubwa mno kukaribia jengo la kisasa la ghorofa saba.

Swali ni vipi waliweza kuchonga masanamu hayo, na vipi waliyabeba kutoka yalipochongewa mpaka yalipo sasa bila kuvunjika, na vipi waliweza kuyachomeka aridhini mithili ya vijiti?


Lakini swali la muhimu na msingi zaidi ni AKINA NANI HAO WALIO FANYA KAZI HIYO?
WALIIFANYA KATIKA ZAMA ZIPI?
 YU WAPI MWALIMU WA SOMO LA HISTORIA ATUSAIDIE KUTUPA MAJIBU?

YU WAPI DARWIN ATUAMBIE BINADAM HUYO ALIISHI ZAMA GANI?

Guys we are stilling build our case ...but worry not, at the end Inshallah we will find WHO is behind these, and if possible WHEN ... so stay tune till next time....

18 comments:

  1. Ahsante kaka kwa kutuelimisha ila utata juu ya utata

    ReplyDelete
  2. Endy chande amefarika je unaweza kutupa info kidogo

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kuhusu Endy Chande unaweza kutizama posti za awali kabisa kwenye blogi hii, sikumzungumzia yeye mahususi, lakini nilizungumzia freemason wa aina yake, ambao ni maarufu kama blue degree freemason, au freemason ambao hawavuki daraja la 3. Hawa wanatumika kama mauwa kwenye ukuta, hawa ni kinga ya kile ambacho freemason wa daraja la juu wanacho fanya, na hawa huwa hawafaham ubaya wowote wa freemason, sababu hawa ndiyo kazi yao kutoa misaada mbalimbali ya kijamii. Zaidi unaweza ukazitazama hizo posti.

      Delete
  3. Jee hawa viumbe wapo duniani tayari au wanaandaliwa mazingira ya kuja?
    Jee kuna ushahidi wa picha za ukweli na sio za kuchora,kwamba hawa viumbe wanapatika sayari flani?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Endelea kufuatilia posti hizi mpaka mwisho maswali yako yote yatakuwa yamejibiwa.

      Delete
  4. Inavyoonyesha hivo viumbe ni vikubwa (GIANTS) kuliko binaadamu wa kawaida kwa kujenga majengo hayo yenye matufali ya uzito wa tani,Jee hao viumbe waliishi mwaka gani?

    ReplyDelete
  5. Inavyoonyesha hivo viumbe ni vikubwa (GIANTS) kuliko binaadamu wa kawaida kwa kujenga majengo hayo yenye matufali ya uzito wa tani,Jee hao viumbe waliishi mwaka gani?

    ReplyDelete
    Replies
    1. soon we will have the answer, keep on visit our blog.

      Delete
  6. Assalaaam alaykum warahmatu llaaaah wabarakaaatuh,mbona sijauona mwisho wa maswali haya? Nani aliejenga piramidi,mchora ramani na elimu ya sayari na hao Kizazi cha Nyoka

    ReplyDelete
  7. Mbona haiendelei Post hii tukapata majibu ya waliofanya kazi hii

    ReplyDelete
  8. Mbona Post hii haiendelei tukawajua wahusika wa Kazi hii

    ReplyDelete