Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, March 27, 2016

NAMTAFUTA MUNGU Ep: 3


Leo tunaendelea na safari yetu ya kumtafuta MUNGU, lakini kwanza tumetizama asili yetu ambayo mapak sasa bado hatujafahamu ni wapi, hivyo inakuwa vigumu hata kufahamu ni nani aliye nyuma ya vyote tunavyoviona ikiwemo sisi wenyewe. Sayansi imekosa lugha ya pamoja ya asili yetu ni wapi?

Leo tunaitazam roho, kitu kingine ambacho sayansi haikitambui, lakini tunaona athari ya uwepo wake katika maisha yetu ya kila siku, huenda huku kwenye roho tunaweza kutambua asili yetu na hatimaye kumtambua MUUMBA wetu ... tuendelee.

Sunday, March 13, 2016

NAMTAFUTA MUNGU Ep: 2


Leo kwenye safari yetu tunatizama, 'new age' ambayo ni dini lakini pia ni sayansi au ni mtazamo wa ulimwengu na binaadam ambao unakubalika na wanasayansi wengi ... ni sayansi kwa maana mtazamo wake unaathiriwa na Darwin, lakini pia unahusisha nyanja mbalimbali za sayansi ... na waumini wake wanaegemea kwenye sayansi kuthibitisha misimamo ya dini hii ...

Hatuja kata tamaa bado tunamtafuta Muumba wa haki, tuachane na Darwin, ingawa nitarudi tena kwake wakati nitakapo kuwa nahangaika kutafuta asili ya binadamu hasa ni wapi lakini kwanza tutizame wana New Age wanatusaidiaje katika kumtafuta Muumba.

Monday, March 7, 2016

NAMTAFUTA MUNGU

“Mwenyezi Mungu, na Malaika, na wenye ilimu, wameshuhudia kuwa hakika hapana mungu ila Yeye, ndiye Mwenye kusimamisha uadilifu; hapana mungu ila Yeye Mwenye nguvu na Mwenye hikima.”

“Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Na walio pewa Kitabu hawakuhitilafiana ila baada ya kuwajia ujuzi, kwa sababu ya uhasidi ulio kuwa baina yao. Na anaye zikataa Ishara za Mwenyezi Mungu basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.” (Quran 3:18-19)

Leo nataka tuzungumzie mada moja tata kidogo, pana lakini iliyofanywa ndogo na akili zetu ... nataka tumtafute Mungu



     Je ni kweli kuna ‘Mungu’ yaani yule mbaye aliyeumba vyote tuvionavyo na tusivyo viona, tunavyo fahamu na tusivyo fahamu. Au ni ‘ulevi’ wa imani za kidini unao tufanye tuamini kuwa Mungu yupo.