Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Monday, March 7, 2016

NAMTAFUTA MUNGU

“Mwenyezi Mungu, na Malaika, na wenye ilimu, wameshuhudia kuwa hakika hapana mungu ila Yeye, ndiye Mwenye kusimamisha uadilifu; hapana mungu ila Yeye Mwenye nguvu na Mwenye hikima.”

“Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Na walio pewa Kitabu hawakuhitilafiana ila baada ya kuwajia ujuzi, kwa sababu ya uhasidi ulio kuwa baina yao. Na anaye zikataa Ishara za Mwenyezi Mungu basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.” (Quran 3:18-19)

Leo nataka tuzungumzie mada moja tata kidogo, pana lakini iliyofanywa ndogo na akili zetu ... nataka tumtafute Mungu



     Je ni kweli kuna ‘Mungu’ yaani yule mbaye aliyeumba vyote tuvionavyo na tusivyo viona, tunavyo fahamu na tusivyo fahamu. Au ni ‘ulevi’ wa imani za kidini unao tufanye tuamini kuwa Mungu yupo.


Ni kweli kuna haja ya kuwa na ‘Mungu’ katika maisha yetu ya kila siku au ni ufinyu wa fikra za kibubusa zinazo tufanya tuamini kuwa hatuwezi kuishi bila ‘Mungu.’ Je huyo ‘Mungu’ alitokea wapi, asili yake ni ipi? Je anao wazazi, watoto je? Haya ni mengine mengi ni moja ya maswali mazito yanayo izunguka nadharia au imani ya kuwepo kwa ‘Mungu.’



Maswali haya yamebeba uzito mkubwa sana katika fikra za viumbe huru hawa wawili, binadamu na majini.

Lakini ugumu wa majibu katika maswali haya na uhakika wa majibu hayo unakwazwa na nyenzo duni za ‘mtafiti’ wa maswali hayo na pili ‘mtafiti’ mwenyewe hajitambui kuwa yeye ni nani, ni nini hasa makusudio ya yeye kuwepo kwenye eneo hili linalo itwa dunia. 

Hivyo ikiwa ‘mtafiti mwenyewe atashindwa kujitambua, kutambua asili yake, imekuwaje akawepo hapa ni wazi pia hatoweza kutambua nini hasa makusudio ya kuumbwa kwake na zaidi hata asili ya kila kinacho mzunguka na aliyeviweka hapo hatoweza kumtambua.

Hivyo utaona hata majibu ya maswali magumu juu ya kuwepo kwa MUNGU hayatokuwa na mashiko bali dhana na nadharia ambazo zitakubaliwa katika kipindi fulani cha historia na kukatiliwa katika kipindi kitakacho fuata.


 Kwakuwa ‘mtafiti’ huyu ameanguka katika hatua za awali na zilizo za msingi katika ‘utafiti’ wake, majibu yake ya mwisho katika suala analo lifanyia utafiti yatakuwa na msururu wa makosa ya msingi na udhaifu mkubwa katika kujibu dhana nzima ya kuwepo au kutokuwepo kwa Mungu.
SEARCH FOR THE GOD?

Binadamu na Majini kama mashine au viumbe ambao mpaka sasa kwa mnasaba wa post hii hatujafahamu asili yao ni wapi, basi hawawezi hata kidogo kujibu swali la kwa nini wapo hapa. Mathalani mashine yoyote ile haiwezi kujiamulia sababu ya kutengenezwa kwake, bali ni yule aliye itengeneza ndiye anaye fahamu ni nini makusudio ya kutengeneza mashine hiyo. 

Halikadhalika majini na wanaadam mpaka watakapo weza kufahamu ni ipi asili yao, hawatoweza kujibu swali la ni yapi madhumuni ya wao kuwepo hapo na hivyohivyo hawato weza kujibu swali la ni nani aliye nyuma ya vyote wanavyo viona na wasivyo viona.
MASHINE ITAWEZA KUMTAMBUA MTENGENEZAJI WAKE?

Lakini kupatikana kwa ‘mtafiti’ mwenyewe katika mazingira haya inatosha kumfanya ‘mtafiti’ akiri kuwepo kwa nguvu inayo simamia maisha ya ‘mtafiti’ ambaye endapo ataikana nguvu hiyo basi moja kwa moja atafanya kosa la kimsingi kabisa kwa kuipatia nguvu hiyo jina jingine au kumpatia mwingine asiye stahiki nguvu hizo.



Historia kwa zama zote imethibitisha kuwepo kwa kosa hilo. Hivyo swali la msingi juu ya kuwepo kwa MUNGU haliwezi kujibiwa na kuthibitishwa na yeyote isipokuwa MUNGU mwenyewe. 

Kama ambavyo mashine haiwezi kujibu swali la ni nini kazi yake ndivyo ilivyo kwa binadamu na majini hawawezi wao binafsi kwa kutumia uduni wa ufahamu wao,na uduni wa zana atakazo zitengeneza kutokana na ufahamu huo kuweza kujibu swali tete na lililo na msingi wa mustakabali wa maisha yake na vyote vinavyo mzunguka juu ya kuwepo au kutokuwepo kwa MUNGU.

Charles Darwin, mwana materilist ni miongoni mwa walio fanya kosa hilo katika nadharia yake ya evolution.’ Kwa vile Darwin alikataa juu ya kuwepo kwa yule ambaye anaweza kufanyiza uhai katika ulimwengu wote, mazingira ya ulimwengu yakawa ni magumu kuachwa bila kutafutiwa ‘yule’ ambaye anaweza kuwa ndiyo sababu ya ulimwengu kutokea. 

Hivyo Darwin ‘uwazi’ au nafasi hiyo akaijaza kwa kutumia, ‘uwezekano wa kinasibu’ au kibahati ndiyo uliyo weza kuleta maisha katika ulimwengu na vyote vinavyo tuzunguka.

Lakini kibaya zaidi ni kuwa nadharia hii ya Darwin haikuweza hata mahala pamoja katika sayansi ya utafiti kuthibitisha ukweli wake.
MTAZAMO WA UMMA JUU YA NADHARIA YA EVOLUTION

Kutokana na nadhari ya bwana Darwin ni kuwa vitu kadhaa visivyo na uhai vilikuja pamoja kwa nasibu na kutengeneza ‘seli hai’ ya kwanza.

Kosa la kwanza kabisa kwenye hili ni Darwin kuacha kuelezea kitu kimoja ambacho ni kidogo mno, lakini chenye maana kubwa mno kwenye darasa zima la uumbaji nacho ni asili ya vitu hivyo vilivyo jikusanya kwa nasibu na kutengeneza seli hai ya kwanza.


Kwenye ulimwengu wa Darwin ni kama vitu ‘visivyo hai’ vilisha kuwepo kabla, lakini asili ya hivyo ‘vitu visivyo hai’ ni wapi? Kiuhakika kabisa madai haya ya Darwin yalikuwa na makosa ya msingi kabisa kwenye ulimwengu wa tafiti za kisayansi. Kisha Darwin akaendelea na makosa yake ‘kibubusa’ kama ifuatavyo; 
NADHARIA YA EVOLUTION KATIKA PICHA

Seli hai hiyo moja iliyo patikana kwa nasibu, ikageuka kwa nasibu tena na kuwa kiumbe hai cha kwanza kama mnyoo, kisha kosa likaendelea tena kuwa mnyoo huyo mmoja kwa nasibu tena akageuka na kuwa kiumbe hai kingine, na kingine, na kingine mpaka dunia yetu hii ikajaa viumbe wote unao waona ukiwemo wewe mwenyewe unayesoma posti hii.
BUT HIMSELF HE LOOK LIKE MONKEY PERHAPS WHY HE CAME WITH THE THEORY

Ingawa nadharia hii ni kichekesho, haikuweza kuoneka hivyo kipindi ambacho inaanzishwa, na kupewa ushirikiano na wale ambao wanaitwa ni ‘wanasayansi’ ingawa nadharia hiyo haijafuata sharia yoyote ya kisayansi kukazidi kuipa nguvu na kuisambaza kote duniani.
NDIYO WATOTO WETU WASIFUNDISHWE UDARUWIN NA EVOLUTION.

Ikafundishwa kwenye mitaala mbalimbali, kibubusa au hata kwa makusudi. Mpaka leo bado nadharia hii inafundishwa pamoja yakuwa nuru kali ya sayansi ya leo inathibitisha makosa ya msingi ya nadharia hii, lakini watu fulani wenye ajenda ya ‘kumfuta’ au ‘kuzima’ nuru ya muhusika katika sanaa hiyo ya uumbaji wanaendelea kwa uduni na udhalili wa mbinu zao kuipigia debe nadharia hii na kuendelea kuifundisha.

KAZI INAENDELEA YA KUPOTOSHA VIZAZI NA VIZAZI

Kama walivyo materilist, Freemasons nao wanamkana Mungu, ingawa materialisim wao wanakana kabisa dhana ya uumbaji, Freemasons wao wanaikubali lakini hawampi Mungu Mmoja sifa hiyo bali miungu wengine wanao wakubali wao, akiwemo shetani. 
MMOJA WA MIUNGU YA KIFREEMASON ANAYEFAHAMIKA KAMA JAHBULON

Hivyo nadhari hii ya Darwin ilikubaliwa kote kwa materilist na Freemasons, ingawa kila mmoja aliikubali kwa sababu tofauti na mwingine. Materilist wao waliikubali na bado wako na nadharia hii ya Darwin kwa vile ndiyo njia nyepesi ya kukidhi mahitaji yao ya kuonesha kuwa hakuna Muumba, kwa wao nadharia ya Darwin inakubalika si kibubusa tu, bali kisayansi.
FREEMASON NA EVOLUTION NI TOTO YA DUGU BOJA.

Kwa Freemasons kwa vile wao wana lengo la kuwaongoza walimwengu wote kwenye shimo la kiza, kukataa kuwepo kwa Muumba ni njia nyepesi kwao katika kuwasaidia kuwapotosha walimwengu na lengo lao mahususi la kuumbwa na kuwapatia malengo mengine kama tulivyoona, hivyo nadharia hii Freemasons wanaikubali si kwasababu wanakataa uumbaji, lakini kwa vile wanamkataa Muumbaji mwenyewe.
NADHARIA YA UUMBAJI KWA FREEMASON IMEEGEMEA KWA WAUNGU WA KIPAGANI.

Hivyo nguvu kubwa ya fedha, wanasayansi, wanahistoria, watafiti na utafiti vilitumika katika ‘kuibariki’ nadharia hii ya evolution. Mazingira yasiyo halisi yakatengenezwa, masalio yasiyo halisi nayo ‘yakavumbuliwa,’ na yote yakija na hadithi nzuri za kuipa nguvu, kuipamba na kuikamilisha nadharia hii ya evolution. 
USANII MWANZO MWISHO

Lakini yote waliyo kuwa wakiyafanya kwa ajili ya kuuhadaa ulimwengu na walimwengu yalianguka patupu, kama wasemavyo waungwana; njia ya muongo ni fupi

Hakuna nyanja yeyote ya sayansi inayo husiana na suala zima la viumbe na uhai iliyo weza kuthibitisha madai ya Darwin, siyo microbiology, wala biomathematics, wala cell biology, wala biochemistry, wala genetics, au anatomy, au physiology, au anthropology na wala hata paleontology, isipokuwa nyanja zote hizo zimefanikiwa kuweka mezani ushahidi usio na shaka na usio hesabika kwa wingi ambao unaivunja vunja nadhari ya evolution.

Lakini huo haukuwa mwisho wa ‘tafiti’ hizo au nadharia hiyo, kwa vile the end justifying the means, kuitupilia mbali nadharia hii inaonekana ni gharama mno kwa Freemasons na wana materilist, kuitupa nadharia hii kutahalalisha kufunguliwa kwa makufuli mazito na minyororo mizito ya kifikra waliyo fungwa walimwengu tangu kuja kwa nadharia hii, mabuku rejea ya chomwe, kazi mbalimbali za ‘kitafiti’ na urongo zichomwe, ‘wanahistoria,’ na ‘wanasayansi’ wapoteze kazi na fedha, msumari wa mwisho ugongwe kwenye jeneza la wanamaterilist na kifo cha wanamasonia kitangazwe.


hakuna ambaye kajiandaa kwa hili, hivyo kwa gharama yeyote ile nadharia ya Darwin lazima iendelee kupewa hadhi ya kisayansi na sifa zisizo zake, utafiti uzidi ‘kutengenezwa,’ na ‘kuvumbuliwa’ ili kunusuru uso wa sayansi ya leo.
Masalio halisi ya historia katika udongo (fossil) yamekuwa ndiyo kikwazo kikubwa kwa nadharia hii ya Darwin. Masalio hayo yanathibitisha kuwa maisha ya viumbe wote duani hayakupitia mabadiliko yanayo elezewa na Darwin. Utafiti wenye mashiko unakubali kuwa viumbe hai wako vilevile kama walivyo kuwa mamilioni ya miaka kabla ya leo, yaani hawakupitia kitu kinacho itwa ‘evolution.’
AINA HII YA MASALIO NI KIKWAZO KWENYE NADHARIA HII YA DARWIN, SABABU HAYA NI MASALIO YA ZAIDI YA MIAKA MILIONI MIAMOJA NA ... HAYAONESHI KIUMBE HICHI KUPITIA MABADILIKO YEYOTE YALE.

Masalio ya historia katika udongo ni kama maandishi yasiyo futika. Masalio hayo ni sehemu ya kiumbe kilicho pata kuwepo eneo hilo. Kutokana katika kona mbalimbali za dunia, masalio hayo yame patikana na kuweza kueleza ni kiumbe chanamna gani kilichopata kuwepo eneo hilo. 

Masalio hayo yanathibitisha kuwa viumbe walipatikana wakiwa wako kamili, wala hakuna masalio yanayo onesha kiumbe kikibadilika kutoka kiumbe fulani kwenda kingine. Hii ni kuthibitisha kuwa uhai kwenye ulimwengu huu umeumbwa kutoka kusiko na chochote. Lakini pia masalio ambayo tunakutana nayo kwenye mabuku rejea, majarida, makala na vyombo vingine vya habari; ambayo yanaonesha kuwa uhai umetokea kwa nasibu, na viumbe wamekuwa wakibadilika hatua kwa hatua si masalio ya kweli bali ni yakutengeneza na kughushi.
MIAKA MILIONI MIA MOJA, YUPO VILE VILE KAMA HAWA TUNAO WAONA SASA.

Kwenye masalio hayo kutoka kwenye kona mbalimbali za dunia na yaliyo kusanywa kwa muda mrefu yameendelea kuthibitisha kuwa, samaki tunaye mwona leo ndiye samaki aliyekuwepo mamilioni ya miaka kabla, wadudu wa leo ndiyo wadudu wa mamilioni ya miaka kabla, hali kadhalika kwa ndege, reptilia na wewe mwenyewe, hakuna aliye badilika kutoka umbile la kiumbe fulani na kuelekea kwenye umbile lingine lililo bora zaidi, bali vyote vimekuwa na maumbile yake kamilifu tangu enzi na enzi.
MIAKA MILIONI 300, LAKINI MPAKA LEO ANAONEKANA VILEVILE, HAKUNA MABADILIKO

Kiumbe hai kinapo kufa tishu laini ambazo zinapatikana kwenye misuli ya kiumbe hicho na viungo vingine havichukui muda kuanza kuoza. Katika mazingira ya baridi kali au sehemu ambazo barafu inapatikana ikiwa imegandamana, tishu hizo zinakuwa haziozi, hivyo kiumbe hupatikana akiwa mkamilifu. Sehemu zilizo ngumu kwa kiumbe husika ndizo zinazo stahimili muda mrefu sana na kuweza kutengeneza masalio yake. Kwenye mimea mara nyingi huwa ni sehemu ngumu ya mmea kama vile shina lake na hata wakati mwingine majani yake kutegemeana na mazingira ya eneo husika.



Darwin anasema kuwa uwezo wa sokwe kuweza kuigiza tabia za binadamu inatosha kabisa kusema sokwe ameweza kubadilika na kufikia binadamu wa leo. Sokwe anapo fundishwa kufanya vitu mbalimbali vinavyo fanywa na binadamu, huvifanya vizuri vitu hivyo, anawezwa kufundishwa kutofautisha rangi na maumbo ya vitu mbalimbali, lakini dai hili ni duni mno kulinasibisha na kulifanya ndiyo moja ya misingi ya dai la kubadilika kwa viumbe hasa sokwe kutoka hatua hiyo na kuwa binadamu; kwa sababu kuna viumbe wengine wengi ambao wana utambuzi na ufanisi mkubwa katika vitu mbalimbali wanavyo weza kufundishwa, kama vile mbwa, paka, farasi, ndege na wengineo. Lakini kwa nini kubadilika na kuwa binadamu kiumbe aliye huru kutokee kwa sokwe peke yake na siyo hao viumbe wengine, au kwa nini evolution imruhusu sokwe na manyani kuwa binadamu na iwazuie hao wengine.

Mathalani ndege aina ya kasuku anapo fundishwa, anaweza kutofautisha kati ya umbo la duara na mraba, rangi nyekundu na bluu, na anaweza kupanga vitu katika uwiano ulio sawasawa, lakini zaidi Kasuku anaweza kuongea kwa kuigiza sauti ya binadamu, kitu ambacho sokwe hawezi kufanya; kutokana na nadharia ya kibubusa hapana shaka kasuku alikuwa na nafasi kubwa kabisa ya kuwa binadamu kuliko sokwe[1], lakini Darwin mwenyewe kasha mchagua sokwe wake.

Wanakaa kwenye meza makubwa ya duara, wamevaa miwani zao, wanataja mabuku makubwa ya rejea, wanataja maneno ya Kilatini, kwa kujua au bila kujua na kukuambia sokwe amevuka daraja na kuwa binadamu, lakini nyani alikuwa, bado yuko, na ataendelea kuwa nyani na hivyo ndivyo ilivyo kwa viumbe wengine wote. 

Huu ni ukweli wa msingi kabisa ambao tafiti zinazo fuata sharia ya sayansi ya utafiti zinavyo tueleza, hivyo ndivyo tunavyo ona kwenye maisha yetu ya kila siku, na hivyo ndivyo ile sauti yetu ya ndani kabisa inavyo sema, kwamba nyuma yetu yupo ambaye ameyafanya haya na wala hayajatokea kibubusa kama Freemasons nyuma ya ajenda zao wanavyo tueleza.
HOW CAN DARWIN EQUATION FIT HERE???

Inakadiriwa kupatikana kuwepo kwa aina 6,000 za sokwe kote duniani katika zama zote za historia, na wengi kati ya aina hizo za sokwe wamekwisha futika. Leo hii kuna aina 120 tu za sokwe walio bakia. Rasilimali kubwa ya wana evolution ipo kwenye aina hizi 6,000 za sokwe walio pata kuishi kwenye mgongo wa aridhi.

Wanatengeneza mazingira ya mabadiliko ambayo wanadai binamu alipitia mpaka kufikia binadamu kamili kwa kupanga mafuvu ya sokwe walio toweka pamoja na ya binadamu na kisha kuyatolea maelezo yao yakibubusa. Kwa njia hii hata msomi aliye shikwa akili anaingia ‘line.’ Lakini hata hivyo wakati umefika wa kuchora mstari mwekundu kwenye mbinu hizo, wapo watafiti huru na wasomi ambao, maslahi ya uma yanakuja kwanza na tafiti hizi zinatuthibitishia kuwa yote hayo yanayo fanywa na wana evolution si kingine bali kughushi kukubwa mno.


Ikiwa nadharia yao ni ya kweli kwa nini basi wanaghushi, masalio, maelezo na hata mazingira lakini zaidi mpaka hongo za aina kwa aina zinatolewa ili makosa ya msingi kwenye nadharia hiyo yafumbiwe macho. Kwa nini?


FUVU LA PILTDOWN MAN

Piltdown man, masalio haya yanasemwa yaligunduliwa mwaka 1912 na Charles Dawson, wakasema masalio hayo yana muda wa miaka 500,000, nayo yalichukuliwa kama ushahidi tosha wa maendeleo katika mabadiliko ya kutoka kwenye sokwe kuwa binadamu. 
PAMOJA NA KUGUNDUA UGHUSHI HUO LAKINI BADO WANAENDELEA KUTUFUNDISHA KUWA EVOLUTION ILITOKEA.

Lakini miaka arobaini baadaye na baada ya ‘masalio’ hayo kupatikana wanasayansi wakaamua kuyachunguza tena na wakakuta kuna ughushi wa hali ya juu mno.


Fuvu la Piltdown Man liligundulika kuwa ni fuvu la binadamu hasa aliye ishi miaka 500 iliyo pita. Mfupa wa taya la chini ni taya la sokwe aliyekufa karibuni, meno yake yalibadilishwa na kuongezwa ili yaweze kufanana na binadamu, Kisha mifupa yote ikapakwa potassium dichromate ili iweze kuwa na mwonekano wa kale.[2]
THEY CAN LIE AT WHATEVER COST AND TIME, JUST

TO MAKE SURE YOU REMAINS IN CHAIN AND FOOL.

Mwaka 1922, Henry Fairfield Osborn, mkurugenzi wa American Museum of Natural History, alitangaza kuwa amefanikiwa kupata jino la gego la zama za Pliocene.,


KWA KUTUMIA JINO HILO MOJA UKWELI FAMILIA NZIMA IKAJENGWA, HII NDIYO SAYANSI YETU.

Jino hilo lilikuwa na sifa za sokwe na binadamu na likasemwa kuwa linatokana na ‘Nebraska Man’ eneo ambalo jino hilo ‘liligunduliwa.’ 

Kwa kutumia jino hilo moja mifupa ya ‘Nebraska Man’ ilipatikana na mtu kamili akatengenezwa, na hata familia nzima ya Nebraska Man ikapatikana. 
HOW FAR CAN THEY GO TO MAKE US BELIEVE IN THEIR THEORY ...?

Lakini mwaka 1927, mifupa mingine inayo husiana na jino hilo ilipatikana, na ushahidi huo mpya ukathibitisha kuwa jino hilo la gego siyo la sokwe wala binadamu bali ni la nguruwe pori anaye patikana Marekani anayefahamika kama Prosthennops.[3]
YES, HALIKUWA JINO LA BINADAM, BALI LA NGURUWE, LAKINI CHA AJABU JINA LA NGURUWE LILIWEZA KUUNDA MIFUPA SI YA BINADAM MMOJA, BALI WA FAMILIA YAKE YOTE. MAAJABU YA DARWIN HAYO NA EVOLUTION YAKE.


Mwaka 1932 kiroja kingine kilipatika India, ‘masalio’ ya kile kilicho itwa Ramapithecus yaligundulika. Masalio hayo yalidai kuthibitisha ule mstari ambao sokwe alibadilika na kuwa binadamu, tukio ambalo wana evolution wanadai kutokea miaka milioni 14 iliyo pita. ‘Masalio’ haya ya Ramapithecus yalitumika kwa miaka 50 kama ushahidi wa msingi kabisa kuthibitisha nukta hiyo ya mabadiliko kutoka sokwe kwenda binadamu. 

Lakini tafiti zilipo kuja kuchukua nafasi yake, tafiti za kweli ilibainika kuwa meno ya Ramapithecus yanazo sifa zilezile walizo nazo sokwe. Mwaka 1982 Aprili, jarida la Sayansi likiwa na makala ya “Humans lose an early ancestor” lilitangaza kuwa Ramapithecus ni sokwe wa aina ya orangutan  ambao wamesha futika.[4]

Tunaweza kwenda zaidi na zaidi katika kuonesha mapungufu kwenye ‘masalio’ ya Darwin na evolution yake, hata hivyo kuna kazi mbalimbali zilizo fanywa kwenye hili somo, ningeshauri kwa wakati wako binafsi uzipitie mwenyewe uliuweze kuona, na mmoja kati ya wasomi na watafiti walio weza kufanikisha hili ni Harun Yahya, unaweza kutembelea wavuti wake na utajionea kazi hizo kwa kina kirefu, na ikiwa hutaweza kutosheka na hilo kunayo mabuku rejea aliyo yataja kwenye kazi hizo, majarida ya kisayansi na vyanzo vingine, basi unaweza kuvipitia ili kuweza kujikinaisha mwenyewe.. Utamu wa ngoma ni uingie ucheze.

Kama ulivyo kwisha kuona hakuna utafiti wa kisayansi, ila ule wa kughushi unao thibitisha juu ya nadharia hii ya evolutiona na hadithi za Darwin. Wapo wanasayansi ambao wanaamini nadharia hii eidha kibubusa au wanayo ajenda tofauti na nadharia hiyo, na haswa tunakuwa na shaka kama kweli ni kibubusa hasa pale wanapo amua kughushi tafiti zao ili kuwapotosha walimwengu, swali la msingi ni kwa nini basi wanaghushi?

Wakati Darwin alipo amua kuivalisha nadharia yake nguo, au kuelezea mazingira yaliyo pelekea kupatikana kwa evolution, Darwin alikuja na survive for the fittest.’ Yaani aliyekuwa na nguvu ndiye aliyeishi, aliyeweza kuhimili misukosuko mbalimbali ndiye aliyeweza kubadilika kutokana na mazingira hayo na kuhama kutoka kiumbe kimoja kwenda kingine.

Hivyo maendeleo ya viumbe hao yalitegemeana na uwezo wa kiumbe husika kupambana na mazingira yake. Mwenye nguvu ndiye aliyeshinda. Mdhaifu alifutika kabisa. Hivi ndivyo Darwin anavyo beba nadharia yake.

Darwin anadai kuwa mpambano huo wa kuishi haupo tu kwenye mazingira bali ndani kabisa kwenye moyo wa viumbe wote, ‘survive for the fittest’ ni moyo wa shughuli za viumbe wote, ni dira na mwelekeo kwa viumbe hao, ndiyo kitu pekee kinacho chochea maendeleo kwa viumbe hao zama hadi zama. Kwenye kitabu chake kilicho kwenda kwa jina la The Origin of Species, "The Origin of Species by Means of Natural Selection or the Preservation of Favoured Races in the Struggle for Life", anaelezea kwamba ‘fight for survival,’ si kwamba inapatikana kwa hayawani tu lakini pia kwa makundi ya rangi mbalimbali ya binadamu. Hivyo watu wa rangi fulani ni bora juu ya watu wa rangi nyingine kutokana na uwezo wao wa kuhimili mpambano wa ‘fight for survival.’
NADHARIA HII INAFUNDISHA KWAMBA MATAIFA YAMENDELEA HATUA MBALIMBALI ZA EVOLUTION, ISPOKUWA KWA WATU WEUSI NA BARA LAO, WAO BADO WAKO KWENYE KUNDI LA SOKWE, YAANI KUWA MWEUPE NDIYO KUWA BINADAM MKAMILIFU.

Darwin akasema kuwa watu wa rangi nyeupe, (Wazungu) ndiyo kundi ambalo linaonekana kuwa na uwezo mkubwa wa kupambana kushinda kwenye ‘fight for survival,’ wakati watu kutoka bara la Afrika na Asia wakiwa wameachwa nyuma katika mpambano huo na hivyo kuashiria kuwa muda si muda watu weusi na watu wa Asia watafutika kabisa kutokana na kushindwa kwao na watu weupe hasa kutoka bara la Ulaya ndiyo watakao bakia, au survive.
NOT ME SAID THAT! ITS DARWINISIM

Utaona kuwa nadharia ya Darwin ilizaa ugonjwa mwingine mbaya sana, ugonjwa wa ubaguzi wa rangi, kwani watu wa bara la Ulaya kutokana na nadharia hii ni kuwa wao tayari wamesha fanikiwa na kuendelea katika hali ya ubinadamu kamili, wakati watu wa Afrika na Asia wao wameachwa nyuma na wapo kwenye hatari ya kufutika kama walivyo futika viumbe wengine.

Hivyo mtu yeyote asiyekuwa mweupe wa Ulaya yeye bado yupo kwenye hatua ya mabadiliko ya kuelekea kwenye ubinadamu kamili, wakati mtu mweupe wa Ulaya tayari yeye ni binadamu mkamilifu. Uwazi huu baina ya hawa binadamu wawili wa Darwin utapelekea binadamu wa Asia na Afrika kufutika kabisa kwani mwenzao wa Ulaya tayari keshakamilika na tayari anafahamu mbinu na njia za ‘fight for survival,’ zaidi kuwashinda wenzake na hivyo yeye pamoja na masokwe wengine wote watatoweka.

Mwana anthropologist wa India Lalita Vidyarthi anaelezea ni namna gani nadharia ya Darwini ilivyo leta ubaguzi wa rangi kwenye fani ya sayansi ya jamii;
Nadharia yake (Darwin) ya survive of the fittest ilikaribishwa na kukumbatiwa na wana sayansi ya jamii wa kipindi hicho, na waliamini kuwa binadamu amefanikiwa katika hatua mbalimbali za evolution, mafanikio ambayo yana onekana kwa watu weupe wa Ulaya (Wazungu). Katika nusu ya pili ya karne ya kumi na tisa ubaguzi wa rangi ulikubaliwa kama ukweli wa msingi na sehemu kubwa ya wanasayansi wa Ulaya[5]
BLACK MAN CONSIDERED TO A PROPERTY OF WHOMEVER MAY HOLD ON 'IT' FIRST AND HE CAN SALE 'IT' TO WHOMEVER HE WANT TO WHATEVER PRICE HE WANT AND ME MAY USE 'IT' IN WHATEVER MANNER HE DESIRE. AND IF THE MASTER CHOSE TO KILL 'IT' NO PROBLEM IT IS YOUR PROPERTY, SO DO AS YOU PLEASE.

Kwenye sayansi ya leo nadharia ya Darwin si kwamba imeshindwa kuthibitisha madai yake, lakini zaidi ni kwamba imepitwa na wakati, mbele ya uso wa kweli wa masalio ya kihistoria nadharia hiyo inayeyuka kabisa. Hivyo madai ya msingi ya nadharia hiyo ambayo ni kukataa kuwepo kwa Muumba nayo yanakuwa yameruka patupu.

Hayana ushahidi wowote ule. Hadaa na uongo wa aina kwa aina unatumika kuibeba nadharia hii, eidha kwa kughushi hayo yanayo itwa masalio ya kihistoria au kwa kupika taarifa mpya ambazo zinaonekana zitaibeba nadharia hiyo lakini bado, penye ukweli uwongo hujitenga, na penye nuru kiza hutoweka, kila wanalo kuja nalo bado linakuwa na soni kwenye uso wa sayansi ya leo, soni ya kushindwa na kudhalilishwa kwa kila ‘uvumbuzi’ wanao kuja nao.

Hakuna kote duniani, kokote kule, ambako yame patikana masalio yanayo thibitisha kuwa viumbe uhai wa wanyama, wadudu au mimea umepitia katika hatua mbalimbali za mabadiliko mpaka ukakamilika na kuwa kamilifu. Bali masalio hayo yanaelezea hadithi tofauti na ile ya Darwin, kuwa mdudu alikuwa ni mdudu mamilioni ya miaka nyuma na bado ni mdudu leo, mende alikuwa ni mende zama hizo na ni mende leo, samaki alikuwa ni samaki mamilioni ya miaka huko nyuma na bado ni samaki leo, n.k.

Hivyo viumbe wote walitokea wakiwa na ukamilifu na kila kile ambacho tunacho waona navyo leo ndivyo walivyo kuwa navyo mamilioni ya miaka nyuma, huu ni ushahidi ambao umeandikwa chini, kwenye matabaka mbalimbali ya aridhi kote duniani kutoka kwenye masalio ya viumbe, wanyama, wadudu, ndege, samaki n.k.; lakini endapo unao mtazamo tofauti au umeweza kunaswa kwenye nadharia ya kibubusa ya Darwin, tuletee ushahidi wako na uweke hadharani kila mtu aone ili tuweze kukubaliana na hayo unayo tuambia, lakini usipige kelele kwa maneno matupu yasiyo na ushahidi.

Bado tunamtafuta Muumba, katika yote tunayo yapitia kwenye ulimwengu wa sasa na yanayo tokea kote ulimwenguni, na tunayo yasoma kwenye mfulululizo wa posti hizi na yale ambayo tunadhani yanaweza kutokea endapo uma utaendelea kulala kwenye usingizi wake wa pono, swali moja la msingi ambalo msomaji hatosita kujiuliza ni ‘Je Mungu Yupo?’ au nililishwa ulevi wa kidini niweze kutawalika vyema, na kama yupo iko wapi nafasi yake juu ya haya yote yanayo jitokeza kwenye uso wa dunia leo hii?

Kujibu maswali hayo hatuna budi kwanza kumtafuta huyo ‘Mungu,’ na kwenye hilo tumeanzia kwa Darwin mwenyewe ambaye yeye si kwamba tu alimkataa Muumba lakini kitendo cha nadharia hii kukubalika kufundishwa kwenye mitaala mbalimbali kote duniani ni kusema kuwa ‘kiserikali’ Muumba hayupo na hivyo ndivyo serikali mbalimbali duniani zimewafundisha wananchi wake kumkataa Muumba. 

Hivyo utaona nadharia hii kwa gharama zozote zile wananchi wanalazimishwa kukubali kuwa uhai kwenye uso wa dunia ulitokea kwa nasibu na hakuna yeyote anaye paswa kujinasibisha na chanzo cha uhai kwenye ulimwengu. Serikali haina dini, lakini si sawa kusema hivyo kwa sababu neno dini kati ya tafsiri zake nyingi ni ‘mfumo wa maisha’ hivyo serikali kama serikali haiwezi kujiongoza bila kuwa na ‘mfumo’ wake au ‘utaratibu’ wake wa kiutendaji ambao nao utakuwa na mipaka yake ambao ndiyo ‘dini’ ya serikali.

Hivyo serikali inapo sema haina dini haimaanishi kuwa haina mfumo, inayo, na msahafu wa mfumo huo au dini hiyo, au biblia ya mfumo huo ni katiba ya nchi. Dini ambayo serikali haina ni dini ya kukubali kuwa kuna Muumba. Ingawa utashangazwa kuwa pamoja na kwamba serikali haziko tayari kufuata muongozo wa huyo Muumba kwa vile kivitendo na kinadharia zinamkataa na kukataa kazi zake na kuwalazimisha wananchi wake kumkataa kwa kuwafundisha nadharia ya Darwin kama ukweli wa msingi juu ya chanzo cha uhai kwenye ulimwengu huu, serikali bado zinamuomba Muumba katika shughuli zao za kila siku, nami najiuliza ni Muumba yupi ambaye zina mwomba na Muumba yupi ambaye zinamkataa?

Leo hii hata ukikutana na profesa wa historia, au daktari, mwandishi, mwanasayansi ambaye anakubaliana na nadharia hii ya Darwin kuna vitu kadhaa ambavyo atakueleza kuthibitisha uhalali wa madai yake, tutavitizama vitu hivyo na makosa yake ya msingi kabla ya kuachana na nadharia hii na kutafuta ukweli mwingine wa msingi juu ya kuwepo kwa Muumba wa ulimwen
HOW CAN CHANCE STAND THAT?


Moja: Magwiji kwenye nadharia hii wanasema kuwa ushahidi wa kisayansi umethibitisha kuwa uhai umekuja kwa nasibu kutokana na mgongano wa kinasibu wa kikemikali. Ukweli ni kuwa hakuna ushahidi wowote wa kisayansi au utafiti wowote ule au majaribio yoyote yale kwenye sayansi ya miamba, mimea au tawi lolote kwenye sayansi ya historia linalo thibitisha madai hayo, na zaidi ya yote hata kinadharia tu, nadharia hiyo imethibitika haiwezekani.

Pili: Wanadhani kuwa masalio ya historia yamethibitisha kuwa uhai wa viumbe kwenye dunia hii ulianza hivyo, na kwamba umekuwa ukipitia mabadiliko mbalimbali. Huu ni uwongo hakuna masalio yoyote yale, kokote pale yaliyo kuja kupatikana na yakathibitisha hivyo, isipokuwa yote ni masalio ya kughushi yanayo kubaliana na uwongo wao huo. Masalio yote yanathibitisha kuwa viumbe wote wamekutikana wakiwa ni wakamilifu wa maumbile yao tangu awali na kuwa hawajapitia hatua yoyote ile katika zama zozote zile.

Tatu: Masalio ya ndege wa Archaeopteryx, ambaye alihesabiwa kama ushindi mkubwa kwenye nadharia hii kwamba ndege huyo hapo kabla alikuwa ni reptiliani. Lakini imegundulika kuwa Archaeopteryx alikuwa ni ndege kamili mwenye uwezo wa kuruka, na hakuna reptiliani mbaye ameweza kupatikana kuwa yeye ndiye asili wa ndege huyo. Times do tell the tales.

Nne: Katika mchakato wa kuwathibitishia walimwengu juu ya ukweli wa nadharia ya evolution, kulipatikana kile kilicho itwa ‘horse series,’ ambapo wana evolution walichukua ‘masalio’ ya farasi walio ishi katika zama tofauti sehemu tofauti duniani na kuyapanga, hasa kufuatana na maumbile yao. Kutoka dogo kwenda kubwa, kuthibitisha kuwa kiumbe hicho kimepitia mabadiliko ya evolution katika zama mbalimbali mpaka alivyo leo. Hili lilichukuliwa na wana evolution kama ushahidi wao wa msingi sana juu ya nadharia yao kuwa ni ya ukweli. Lakini imekuja kuthibitika kuwa farasi hao hawana mahusiano yoyote baina ya mmoja na mwingine, kwamba farasi aliyetangulia katika ‘series’ hiyo si kweli wa nyuma yake ndiye baba au babu yake bali katika mpangilio wao huo wa kuangalia maumbile, walifanya kosa kwani aliyedhaniwa kutangulia ndiye alikuwa wa mwisho na wajamii tofauti kabisa ya farasi tofauti na ile waliyo mpanganayo.

Tano: Wana evolution walimchukulia kipepeo aina ya moth katika wakati wa mapinduzi ya viwanda England kama moja ya ushahidi wao mkubwa wa kipepeo huyo kupita njia ya mabadiliko inayo tambuliwa na Darwin kama evolution. Walicho kuwa wakidhani ni kwamba kipepeo huyo ameweza kubadilika rangi yake na kuwa yenye kukolea zaidi kutoka kwenye ile iliyo fifia. Lakini kama zilivyo shahidi zao nyingine, hii nayo ilikumbwa na vikwazo, kwamba moth hakubadilika rangi bali wakati wa mapinduzi hayo ya viwanda kulikuwa na moth wa aina mbili, mmoja ni yule aliyekuwa na rangi iliyo kolewa, wakati mwingine ni yule ambaye alikuwa na rangi iliyofifia, moth wenye rangi iliyofifia walianza kutoweka na wakati huohuo wale wenye rangi iliyo kolea wakiongezeka kwa kasi kubwa. Hivyo dhana kuwa walibadilisha rangi yao kwa kutumia kile kinacho itwa na wana evolution kama ‘naturalselection’ hakikutokea kabisa, na utafiti wao ulikuwa ni wakughushi kama walivyo zoea, na hivyo ushahidi wao mwingine ukaanguka patupu.
YANI CHOCHOTE WAKIONA KINAYO NAFASI YA KUPIGIA DEBE UWONGO WAO, BASI WANAKURUPUKA NACHO.

Sita: Wanasema kuna mafuvu ambayo ni ‘masalio’ ya historia yanayo thibitisha kuwa mwanzo binadamu alikuwa ni sokwe na kuna ambayo yanaonesha namna alivyo piga hatua moja mpaka nyingine kutoka sokwe mpaka binadamu kamili. Lakini kama tulivyo ona hakuna aina hiyo ya masalio hata kidogo popote pale ulimwenguni, na yale wanayo yaita ni ‘masalio’ si chochote bali ni ya kughushi. Hivyo hawana ushahidi wa kushikika zaidi ya maneno marefu, marefu ya Kilatini kutoka kwa wataalamu wao.
URONGO MWINGI, LAKINI SASA TUMEJUA NI TAARIFA ZA KUPIKWA.

Saba: Wanasema wanaevolution kuwa binadamu anapo kuwa kwenye tumbo la uzazi au yai anapitia hatua za mabadiliko ya ki-evolution kama wanavyo pitia viumbe wengine. Wamefikia kusema binadamu katika hatua zake za awali akiwa tumboni alikuwa na matezi kama yale ya samaki, ambayo kutona na mabadiliko ya evolution yamekuja kutoweka. Mwana baiolojia wa evolution Ernst Haeckel alipo kuja na hoja hiyo mwanzoni aliibadilisha hata michoro yake na kwa makusudi kabisa ili kuthibitisha madai yake hayo, lakini baadaye hata wanasayansi wenzake wa evolution walikiri kuwa namna yake ya kughushi ilikuwa hata si yakisayansi. Kwa maneno mengine ni kweli wanaghushi, lakini huyu mwenzao hakughushi kisayansi.
UHUNI MTUPU, WANACHORA VIMICHORO VYAO, SABABU WATU  HAWANA MUDA WA KUTAFITI AU NYENZO BASI WANAJUA WATU HATUTAGUNDUA UHUNI WAO.

Nane: Wanasema wana evolution kuwa binadamu na viumbe wengine wanavyo viungo ambavyo vimetoweka kutokana na kwamba waliacha kuvitumia viungo hivyo kwasababu mbalimbali za mabadiliko ya ‘natural selection,’ wako wanao amini kuwa binadamu pia alikuwa na mkia lakini umetoweka kutokana na kwamba hautumii. Kulipa nguvu dai lao hilo wana evolution wanaipinga DNA, kwani kama tunavyo jua maumbile ya kiumbe chochote kile, tabia, shughuli, sifa n.k. vyote vimeandikwa kwenye DNA yake. Dai hili nalo ni sawa na msemo usemao ‘mfa maji haachi kutapatapa,’ viungo vyote walivyo navyo viumbe wote akiwemo binadamu vinafanya kazi, hakuna kiungo kulicho patikana kuwa kimeacha kufanya kazi kwa sababu ya mabadiliko ya kimazingira, ni kama aliye viweka hapo anajua ni kwasababu gani viko hapo na havijatokea kwa nasibu au kwa utaratibu wa ‘natural selection’ na hapa tupo kwenye juhudi ya kumtafuta huyo mbunifu aliye anzisha haya yote kwani mjomba wetu Darwin tunaona hana jipya zaidi ya kufoji ili kutupotesha kwenye ukweli wa msingi juu ya kuwepo kwa mbunifu mwenyewe.

Hizi ni kati ya zile tu ambazo ukikutana na waumini wa evolution utakuta wamejikita huko kama ushahidi wao wa kuthibitisha ukweli wa madai yao ya kutokea kwa evolution. Sababu ambazo kama tulivyo ona hazina mashiko yeyote kwenye jicho la sayansi ya leo na kwenye fikra za watu huru.

Watu wengi hudhani kuwa nadharia hii ya eveolution muasisi wake ni Darwin, lakini kama nilivyo kwisha kutaja huko mwanzo, nadharia hii ni kazi ya wanafalsafa wa materilist ambao waliona kwao nadharia hii inayo tija kwa mipango yao, nao kwao siyo kwamba inayo ukweli au kanuni za msingi za kisayansi lakini kwa vile juhudi ni kumkataa Muumba na hata kuikataa roho, kwa wanamaterilist nadharia hii kwao inabaki kama ukweli wa msingi pamoja na kuwa kila tofali lake moja limejengwa kwa kanuni za uwongo na kughushi na bila kanuni za sayansi ya utafiti.

Kama utamkataa Muumba kwenye kazi ambazo zinathibitisha zenyewe, au zinasimama zenyewe kama ushahidi wa kazi za Muumba, hapana shaka kazi hizo lazima uzitafutie mbadala, na kwa Darwin na materilist wenzake ‘mbadala’ huo umekuwa ni ‘survive for the fittest,’ kama kanuni ya msingi ya maendeleo ya uhai kwenye sayari hii na nukta ya msingi ya kuendelea kuwepo kwa uhai na viumbe katika uso wa dunia. Hivyo mwanadamu ametokea kwa nasibu na ameendelea kuwepo achilia mbali kutoweka kwa viumbe wengine na kuyashinda majanga mbalimbali kutokana na kanuni hii ya ‘survive for the fittest.’ Hivyo mwanadamu ni ‘lijinyama’ lisilo na maadili wala muongozo wowote kwani kuwepo kwake hapa hakutegemei yeyote wala chochote zaidi ya uwezo wake wa ‘survive for the fittest, matokeo ya nadharia hii kumfuta Muumba kwenye kazi anazozifanya na kazi hizo kuzipatia jina jingine au kumpatia mwingine mbali na Muumba mwenyewe, moja kwa moja kuna mwondolea binadamu msingi wa utashi wake kwamba hawajibiki kwa lolote analo fanya liwe baya au zuri kama wanavyo sema wamasonia kuwa ‘the end justfy the means’ na ‘the end’ yenyewe ni ku-survive for the fittest’ haijalishi ni lipi kiumbe huyu atafanya kulifikia lengo hilo la ku-survive hatowajibika kwa yeyote kwa vile yeye mwenyewe katokea kwa nasibu na siyo kazi ya yeyote katika kutokea kwake, na kuendelea kuwepo kwake hakutegemeani na yeyote bali uwezo wake wa kuwashinda walio wadhaifu kwa namna yeyote ile ili aweze ku-survive.
MTOTO HUYU ANATAMBAA KUELEKEA KUNAKO KAMBI YA CHAKULA YA UN, AMBAYO KUTOKA HAPO NI UMBALI WA KILOMETA MOJA, NDEGE ANAMSUBIRIA MTOTO HUYU ASHIWE NA NGUVU KABISA AANZE KUMLA, BINADAM MWINGINE ALISIMAMA AKAPIGA PICHA HII NA KUONDOKA, HAKUMSAIDIA MTOTO HUYU KWENYE UBAYA UNAOMSUBIRI MGONGONI KWAKWE SABABU ALIHOFIA ATAPATA MARADHI YA KUAMBUKIZA, HIVYO ALIONDOKA NA HAKUNA ALIYEJUA NINI ILIKUWA HATMA YA MTOTO HUYU. HAPO NDIPO TULIPOFIKA, LAKINI MATANI NA MATANI YA VYAKULA YANAMWAGA KILA MWAKA KOTE DUNIANI, LAKINI BAJETI YA ULINZI YA MAREKANI YA MWAKA MMOJA INATOSHA KUONDOA UMASIKINI WOTE DUNIANI, NA HAKUNA ATAKAYE KUFA KWA NJAA, BAJETI YA KUANDAA MASHINDANO YA KOMBE LA DUNIA INAWEZA KUONDOA NJAA KWA KIASI KIKUBWA KWA NCHI MASIKINI. 
BUT WHO IS CARE?
IS SURVIVAL FOR THE FITTEST.

Matoke ya mafunzo hayo ni uharibifu usiyo kuwa na macho, unyama ushenzi na ufedhuli ambao hauwezi kufikirika achilia mbali kutamkika. Nguvu ya utashi na akili huru ya kutafakari na kutambua mambo itakuwa imefunikwa na matakwa ya nafsi ya mwanadamu, Matakwa ambayo hayatoweza kuwa na kikomo ya nafsi iliyo haribika, hakuna sheria wala mipaka ambayo nafsi hiyo itaweza kuitambua, siyo sheria za nchi wala za Muumba. Nafsi hiyo imefisidika kupita kikomo kwa vile kanuni inayo iyongoza imemnyang’anya jukumu lake kama kiumbe kilicho umbwa na kujiita kiumbe kilicho jiumba. Hii ndiyo hasa maana ya kutokea kwa nasibu, kwamba hujaumbwa bali umejiumba, na ukiwa umejiumba ni nani atakaye kuwa na mamlaka na wewe, inamaana wewe ndiyo muumba mwenyewe. Kila kinacho kuzunguka kimejiumba chenyewe tofauti yako wewe na viumbe wengine siyo utashi wa akili huru, bali uwezo wako wa ku-survive for the fittest. Kwa msingi huu haijalishi nini utakacho kifanya, hakuna wakuuliza.

Haya ndiyo maradhi ya makubwa ya jamii yetu ya leo. Lakini baya zaidi ni kuwa wapo ambao bado hatuja kubaliana na nadharia hii ya Darwin na wenzake hivyo tuko kwenye juhudi ya kumtafuta Muumba; hivyo basi Freemasons na wenzao wametangaza vita dhidi yetu, vita hiyo ipo katika sehemu mbili, kutumaliza kabisa sisi na sehemu ya pili kuvibadilisha vizazi vyetu kukubaliana na nadharia hii. Kama tutakavyoona katika posti zitakazo fuata kuwa hivi sasa kuna vita vikubwa dhidi ya afya yako na wewe mwenyewe binafsi na kuna vita dhidi ya familia yako katika mbinu njia na namna mbalimbali.

Zingine unazitambua na zingine huzitambui kabisa. Suala la watoto kupigania haki zao, kinamama kupigania haki zao, hizi ni moja ya mbinu zao,jamii hizi mbili yaani kina mama na watoto tunajua fika kuwa wanazo haki zao za msingi na zinazo tambulika na kuheshimika katika kila jamii, lakini kwa kutumia jina hilohilo kama vile ni watu ambao mafunzo mengine hasa ya kidini na kijamii zingine yamewanyima haki zao, ili kuingiza ‘haki’ ambazo unajua wakipewa haki hizo moja kwa moja itapelekea katika kufanikisha mpango wako wa kumfuta Muumba katika maisha yao na kuwafanya ni wanyama wanao -survive for the fittest- basi wewe moja kwa moja hukuja kuwapa haki zao bali kuwanyang’anya haki yao ya msingi kabisa ambayo ni haki ya uhuru, haki ya kutokuwa mnyama bali kuwa kiongozi ambaye atathibitisha kuwa kazi zinazo fanywa na Muumba hazifanywi kwa bahati mbaya au kimchezo mchezo bali kwa sababu, msingi na madhumuni maalum.


Kwa wao hakuna ‘nyeupe’ wala ‘nyeusi’ wanasema hivyo wakimaanisha yaani hakuna jema wala baya. Hivyo hata ikibidi kuuwa watu bilioni tano kama wanavyo tekeleza mpango huu kwa njia mbalimbali hilo kwao halionekani kama ni kitu, ‘kibaya’ bali njia ya wao ku-survive. Mamilioni ya watoto wanakatishwa uhai wao kwa njia ya utoaji mimba, mamilioni wengine wanaachwa kwa makusudi wafe kwa njaa, mamilioni wengine wanauwawa kwa kuchomwa sindano yenye magonjwa mbalimbali, mamilioni wengine wanapatiwa chanjo ambazo baadaye zitazalisha madhara ya kukatisha uhai wa watu hao, mamilioni wanakufa kwa vita wanavyo vidhamini wao, haya yote hayana tafsiri ya ‘ubaya,’ ‘uovu,’ ‘unyama,’ na mengineyo ambayo ungeyaita kwao hakuna ‘nyeusi,’ wala ‘nyeupe,’ kwao kuna matokeo tu, na matokeo yenyewe ni ku-survive, ni njia gani utatumia uweze ku-survive, haijalishi; na kwa nini ijalishe chochote ikiwa kwao hakuna Muumba?

Kitabu cha mwanauchumi wa Uingereza Thomas Malthus alicho kiita An Essay on the Principle of Population, kinatajwa kuwa ndiyo chachu ya kazi ya Darwin, mwanauchumi huyo kutokana na mahesabu yake aliona kuwa kasi ya ongezeko la watu duniani inakuwa mno, kwa sababu kwa materialisim kila mtu ni mungu mwanauchumi huyo akijivisha viatu visivyo vyake aliona hilo ni tatizo kwa kasi ya watu kuongezeka kuwa kubwa na akapendekeza vitu kadhaa vifanyike ili kupunguza kasi hiyo ya ukuaji wa watu duniani. Machafuko, majanga, vita, njaa na magonjwa ndizo nyenzo aliziona kuwa zingefaa katika kukamilisha zoezi la kupunguza kasi ya ukuaji na idadi ya watu kwenye sayari hii kwa ujumla. Kuna watu ambao wanapaswa kufa ili wengine waishi, si unawajua ni akina nani wakwenda na akina nani wa kubaki, ambao wamesha survive for the fittest yaaniWazungu wa Ulaya hao wanayo haki ya kuishi, watu wa Asia, Afrika, Amerika ya kusini na wakazi wa asili wa Amerika ya Kaskazini, Australia, hao bado wanajivuta vuta, wanapaswa kufa.

 Hii ni survive for the fittest hivyo machafuko, vurugu, vita, magonjwa, ukame na mengine hapa ni nyumbani kwao, sababu hizi ni zana ambazo lazima ziendelee kutumika ilimradi anayetakiwa kufa bado tupo hai, bado tunazaliana.

Wakati naanza kupata pata akili nilikuwa nikijiuliza kwa nini vita haviishi, ni kweli hakuna namna ambayo vita hivi, njaa na magonjwa kwenye bara letu vinaweza kutoweka na dunia kuwa sehemu ya amani, sikuwa na elewa kuwa kikwazo ni nini, kumbe hata mimi niliyekuwa nikijiuliza swali hili sina haki ya kuishi, kumbe nimekuja kwa bahati mbaya sikutakiwa kabisa niwepo, sasa ndiyo naelewa kwa nini waasi wanaweza kupewa silaha nzitonzito lakini hawana hata ndala, nguo zao chakavu na wamedhoofu kiafya. Kumbe sisi tunapaswa kuendelea kuuwana ili weupe waishi.[6]
HII SIYO NADHARIA, BALI NDICHO WANACHO KIFANYA HASWA USIKU NA MCHANA.

Kwenye nusu ya kwanza ya karne ya kumi na tisa kote Ulaya, viongozi na wakubwa wengine walikuwa wakikutana kuangalia ni namna gani wataweza kupambana na tatizo jipya wanalo liona, nalo ni ongezeko la watu duniani. Njia gani zitumike ili kuweza kufuata muongozo wa Malthus katika kupongeza idadi ya watu, hasa masikini, si kwa kuwaondolea umasikini wao, bali kuwaua au kuwatengenezea mazingira ya vifo vyao, na kuwafunga vizazi vyao. Ikafahamika kuwa ili kuwamaliza watu masikini lazima nchi za Ulaya zihakikishe kuwa badala ya kuwasisitizia watu masikini katika masuala ya usafi, wawahimize wawe na tabia ya uchafu, ambayo itapelekea kuwepo kwa maradhi aina kwa aina. Miji yao ifanywe kuwa na mitaa yenye njia nyembamba, tuwajaze watu wengi kwenye nyumba ndogo, miji ijengwe karibu na mabwawa machafu, tuwalazimishe watu wakaishi kwenye mazingira magumu, maeneo ambayo hayafai watu kuishi.[7]

Mbadala huo ukitumika wale madhaifu ambao wameshashindwa kwenye vita hivi vya survive for the fittest watatokomea, na idadi ya ukuaji ya watu itapungua na kuwa kwa idadi ile tunayo taka. Darwin naye akaibeba muongozo huu wa Malthus na kuanisha kuwa unapatika kwa kila kiumbe, akawataka watu wamkane Muumba wao na akawatengenezea njia ya mapambano baina ya madhaifu na wale wanao jiona kuwa ni fittest.
Nadharia hii ya Darwin ikamzaa mtoto aliyeitwa ‘ubaguzi’ kwenye karne ya 19 ambaye naye kwenye karne ya ishirini akamzaa mjukuu wa Darwin kupitia ‘ubaguzi’ aliyeitwa ‘fashisti.’ Adolf Hitler kwenye kitabu chake cha Mei Kampf, anakubali kuwa ni maono ya Darwin ndiyo yaliyo muongoza mpaka kufikia hatua ya kupambana vita vya kibaguzi kati yake na ‘rangi’ nyingine zote zilizo salia.

Abiria mwingine aliyekata tiketi ya first class kwenye ndege ya Darwin ni mkomunisti. Abiria huyu ndege hii anaipenda sana. Mahusiano baina ya ‘abiria’ huyu anayeitwa komunisti na ‘ndege’ inayo itwa Darwin ni kuwa wazazi wa abiria huyu Marx na Engels wote walikuwa ni washangiliaji wa ‘huduma’ zinazo tolewa na ‘ndege’ ya Darwin. Marx na Engels wamezisoma kazi za Darwin ikiwemo the Origin of Species na walipendezwa sana na kazi hiyo hasa kwenye upande wao wa ki-materialism. Kwenye kitabu chake alicho kiita The Dialectics of Nature, Engels ambacho amekiandika kwa kufuata maoni ya Darwin, amejaribu kuongezea ‘utamu’ kwenye nadharia ya evolution kwenye sura aliyoiita ‘The Part Played by Labour in the Transition from Ape to Man,’ wakomunisti wa Urusi ambao walifuata nyayo za Marx na Engels, kama vile Plekhanov, Lenin, Trotsky na Stalin wote wanakubaliana na nadharia ya evolution ya Darwin. Mao ambao alisimamisha ukomunisti China na kuuwa mamilioni ya Wachina kufanikisha lengo hilo alisema;
Ujamaa wa China umejengwa chini ya misingi ya nadharia ya Darwin ya evolution.”.[8]
 Kwenye kitabu alicho kiita China and Charles Darwin, mwanahistoria wa Harvard University, Janes Reeve Pusey ameelezea kwa kina madhara ya Darwin kwenye ukomunisti wa Mao nchini China.[9] Mahusiano baiana ya nadharia zote mbili, ukomunisti na evolution hayana upenyo, kwa vile evolution inaipa nafasi ukomunisti kutekeleza ajenda, sera, mipango na maono yake kupitia tafsiri ya evolution. Ukomunisti umeuwa takribani watu milioni 120 katika harakati zake za kujipenyeza kwenye maisha ya ulimwengu huu, lakini halionekani hilo ni ovu kwa vile wana-survive for the fittest.

Darwin na nadharia yake inayo tumiwa kama msingi wa kukataa kuwepo kwa Muumba, mpaka leo haijaweza kuthibitisha madai yake hayo, zaidi ni matatizo makubwa katika karne hii na zilizo pita katika nyanja mbalimbali za maisha yetu ya kila siku, vurugu, umwagaji wa damu, umasikini, mauwaji na mengine na mengine na mengine ambayo kwenye dunia ya leo yana onekana kuwa ni mambo ya kawaida kutokana na ‘baraka’ za Darwin kupitia nadhari ya evolution kwenye misingi ya survive for the fittest.

Tulikuwa tunamtafuta Muumba wa ulimwengu, lakini cha kwanza tulicho kiangalia ni sayansi ya leo iliyo jengwa kwenye misingi ya Darwin ambayo inafanya kila inalo weza nyuma ya watu fulani, kuthibitisha kuwa hakuna Muumba, hata hivyo tumekutana na mapungufu ya kutosha juu ya madai yao hayo, na zaidi ya yote tumeona kuwa nadharia hiyo imejengwa katika misingi ya maelezo ya uwongo na ushahidi wa kughushi. Watu makini wenye mipango makini katika kufikia jambo lao, katu hawawezi wakajenga misingi, kuweka maelekeo na njia ya kufikia malengo hayo kwa kutumia maelezo ya uwongo na takwimu za kughushi, na hakuna jambo lenye uzito na majibu elfu moja yenye kuridhisha kwetu sisi wanadamu kama kutambua asili yetu ni wapi, na ramani ya Darwin inatupeleka kwenye shimo la nyoka na nge na katu haitaweza kujibu maswali yetu magumu juu ya nini madhumuni yetu ya kuwepo hapa, ikiwa imeshindwa kuthibitisha asili yetu ni nini ni wazi haiwezi kutuhakikishia hatma yetu ya maisha ni ipi, hivyo marafiki, maadui, wapendwa, ndugu, wasomi, vijana wenzangu, wanavyuo, wahadhiri, wanafunzi na kila binadamu kokote alipo hatuna budi kuachana na nadharia ya Darwin katika kila nyanja ya maisha yetu tuliyo ruhusu nadharia hii ikaingia na hasa kwenye suala la muhimu na zito kuliko yote, suala la kumtafuta Muumba wa ulimwengu huu.

Nadhari ya Charles Darwin na kokote alikoitoa imeshindwa kututhibitishia ikiwa ni kweli hakuna Muumba, na sisi tunamtafuta Muumba, na ukweli ndiyo utakao tuweka huru na Darwin siyo mkweli.

TUKUTANE HAPA HAPA NEXT TIME, BADO TUKO KWENYE SAFARI YA KUMTAFUTA MUNGU ... WAPI TUTAINGIA TUTAJUA HAPA HAPA....







[1] Atlas of Creation, Harun Yahya
[3]Gregory, W.K. (1927). "Hesperopithecus apparently not an ape nor a man
[4]Atlas of Creation na Harun Yahya

[5]Ibid
[6]Si weupe wote wenye nadharia hii, kiuhakika hapa naugusa mfumo mzima wa Illuminati wala sina dhana ya ubaguzi wa rangi, kwangu mimi binadamu wote ni sawa mbele ya Muumba na m’bora wetu ni yule anaye tuzidi kwa matendo mema ambayo kayaelekeza Muumba kupitia kwa mitume wake wapatao laki moja na ishirini na nne elfu, na Muhammad (s.a.w) akiwa ni wa mwisho kwenye mlolongo huo wa mitume
[7]Michael J. Behe, Darwin's Black Box, New York: Free Press.
[8]H. S. Lipson, "A Physicist's View of Darwin's Theory", Evolution Trends in Plants.
[9]Benjamin Farrington, What Darwin Really Said, New York: Schocken Books.

3 comments:

  1. Salaam brother Salim,
    Nichukue fursa hii kukupongeza sana kwa moyo wako na jitihada zako kutuletea elimu hizi za hali ya juu sisi ndugu zako (waislam) na wengineo pia (wasio amini)
    Binafsi nimepata faida sana kupitia blog yako, na pengine labda nimezidi kupata faraja kuwa kile nilichokuwa nakiamini (na kuendelea kukiamini) mpaka leo hii kumbe kuna ndugu yangu mwengine (wewe) yungali katika upande wangu.
    Mara zote nimekuwa nikiwaza mengi kuanzia dunia na mambo ya aakher na kila mara nimekuwa nikitamani walau apatikane mtu japo mmoja nitakayeweza ku-share nae haya mengi niliyonayo akilini mwangu.
    Naamini ni Mungu ameniongoza (alhamdulillah) kupata fursa ya kuifikia blog yako na kuhakiki niwazacho na nikiaminicho juu ya mambo lukuki yanayoendelea katika ulimwengu huu ambayo binafsi nayaangalia katika jicho hasi (-) sana tangu nilipoanza kupata akili na kujitambua.
    Dunia imekuwa nyeusi na inayotisha mno (kwa wenye akili na uelewa kama Mimi, wewe na wengineo wachache) 'nitaendelea'....

    ReplyDelete
  2. Makala zako hakika ni za thamani ya hali ya juu kaka. Niendelee kukupongeza kwa kazi hii ngumu na ya kujitolea kutuelimisha. Naamini elimu kama hizi no ngumu kuzipata mahali kokote hasa kwa sisi tulio katika 'dunia ya tatu' na ambao tulishaathiriwa na mambo ya kidunia.
    Tumekuwa wagumu kuamini kuwa tunapotea, ama tulishapotea na hatimaye hata pale ambapo anatokea mtu mwenye ufahamu/ujuzi kama wewe na kujaribu kutufahamisha nyeusi ni ipi na nyeupe ni ipi... basi mtu huyo ataonekana kutuko, kikwazo au aso-maana kwao na labda kuishia kuchekwa pia kisa hujaandika habari za kileo zinazoendana na matakwa yao. Huku ndiko kupotea kaka.
    Nina mengi sana ya kuzungumza kabla ya kuanza kuchangia nilonayo kwenye mada zako. Inshaallah nitaendelea kufuatilia mfululizo wa kila makala yako na kuielewa vizuri. Ila kwanza wacha tu nikupongeze kwa hiki ulichoamua kukifanya na inshaallah Mungu atakulipa. Mimi nitakuwa balozi wako mzuri kufikisha haya kwa wengine.
    Asante sana kaka Salim. Una akili sana wewe!

    ReplyDelete
  3. Salim msangi kwanza napenda kukupa pongezi maana mimi mwenyewe nilikuwa najiuliza hivi kama kweli nilifundishwa darasani kuwa Binadamu katokana na nyani mbona mpaka leo nyani wanazaliana na hawabadiliki kutoka stage moja kwenda nyingine!!!!!? Na kibaya zaidi wapo wanao wafuga nyani sasa mbona abadiliki japokuwa karahisishiwa kuservive??? Hakika ALLAH ndio kila kitu maana kwa neno "kuwa" uwa linakuwa vile atakavyo.

    ReplyDelete