Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, March 13, 2016

NAMTAFUTA MUNGU Ep: 2


Leo kwenye safari yetu tunatizama, 'new age' ambayo ni dini lakini pia ni sayansi au ni mtazamo wa ulimwengu na binaadam ambao unakubalika na wanasayansi wengi ... ni sayansi kwa maana mtazamo wake unaathiriwa na Darwin, lakini pia unahusisha nyanja mbalimbali za sayansi ... na waumini wake wanaegemea kwenye sayansi kuthibitisha misimamo ya dini hii ...

Hatuja kata tamaa bado tunamtafuta Muumba wa haki, tuachane na Darwin, ingawa nitarudi tena kwake wakati nitakapo kuwa nahangaika kutafuta asili ya binadamu hasa ni wapi lakini kwanza tutizame wana New Age wanatusaidiaje katika kumtafuta Muumba.



Ninapo zungumzia ‘NewAge’ msisitizo wangu upo kwenye majibu mazito au mepesi yanayo tolewa na watu wa sasa kutokana na msukumo na ushawishi wa maendeleo ya sayansi kwa ujumla, lakini hasa sayansi ya anga na sayansi ya saikolojia. 

Sayansi ya nafsi au saikolojia ilikuwepo tangu na tangu, lakini zaidi katika zama zetu hizi kumekuwa na taarifa nyingi zaidi, maandishi mengi zaidi, makala nyingi zaidi na wataalamu wengi zaidi kuhusiana na elimu hii, halikadhalika kwenye sayansi ya anga. 

Sayansi hizi mbili zimekuwa na msukumo mkubwa katika kulielezea suala tete na kujibu maswali magumu juu ya kuwepo kwa MUUMBA. Lakini pia katika sayansi hizi mbili na hasa ile ya anga tutakuta kwa kiasi kikubwa imekopa mawazo, mitizamo na maono kutoka kwa mjomba wetu, mjomba Darwin.


Ingawa Sayansi inathibitisha juu ya kuwepo kwa MUUMBA kwa namna mbalimbali, na baadhi ya wanasayansi wakibadili misimamo yao na hata kuanza kufuata mafundisho ya baadhi ya dini, kama kukubali kwao juu ya kuwepo kwa MUUMBA, lakini bado sayansi hiyo kwa namna mbalimbali inatumika kama silaha ya kumkataa MUUMBA, na baadhi ya wanasayansi wakisimama kama uthibitisho kuwa hakuna MUUMBA.

Sayansi ya leo na watafiti wake wanatumia zaidi majukwaa ya sinema na tamthilia na vitabu vya hadithi za kufikirika kama darasa la kuwaelekeza walimwengu kuwa ni namna gani ulimwengu umetokea kwa nasibu na wakati mwingine ukiwaonesha walimwengu muumba mwingine wanao mfahamu wao wanasayansi na wakifanya juhudi kuwashawishi walimwengu kupitia vyombo mbalimbali vya habari, makala na majarida kumkubali mungu wao.
HOOLYWOOD WANAPENDA NADHARIA YA WAUNGU KUTOKA SAYARI YA MBALI

Ingawa si rasmi sana lakini katika nchi nyingi za Ulaya na zile zinazoitwa za ‘dunia ya kwanza’ kwa muda mrefu kumekuwa na ‘tetesi’ kuwa aliens au viumbe kutoka sayari nyingine ndiyo miungu wa ulimwengu huu. Dai hili limekuwa likiletwa kwenye akili za watu na hasa vizazi vya sasa kwa kupitia kazi za filamu, tamthilia, majarida na vitabu. Kazi zenye gharama za mabilioni ya dola zinatengenezwa kutoka kwenye katuni mpaka tamthilia zenye maudhi na fikra pandikizi kuwa muumba wa ulimwengu huu ni Aliens.

Mkufunzi kwenye masuala ya Mashariki ya Kati na Biblia bwana Zacharia Sitchin alikuja na vitabu kadhaa akielezea kuwa ‘Anunnaki’ walio tajwa kwenye masalio ya kale ya wa Sumeri, kama watu walio kuja kutoka mbinguni na kutua duniani. 

Sitchin akawalinganisha Anunnaki na ‘Nephılım’ walio tajwa kwenye agano la kale kama walio kuja duniani kutoka mbinguni. Baada ya miaka mingi ya utafiti na kutafsiri kazi hizo za kale na lugha yake kuja kwenye lugha ya watu wa sasa Sitchin akahitimisha kuwa dhana ya ‘Anunnaki’ kutoka kwenye kumbukumbu na masalio ya historia ya kale ya wasumeri na ile dhana ya ‘Nephilim’ kutoka kwenye agano lake kuwa zote zinaelezea kitu kimoja, au zote msingi wake ni mmoja. 

Dhana hiyo au msingi wa dhana hiyo ni kuwa hapo zamani sana, zama za kale kabisa kabla binadamu hajafika kwenye uso wa dunia, jamii ya viumbe fulani kutoka sayari au ulimwengu mwingine walifika kwenye sayari hii ya tatu kutoka kwenye jua na kutokana na maendeleo yao ya sayansi waliweza kuanzisha uhai katika sayari hii, hasa uhai wa kiumbe kinacho itwa mwanadamu.

Dhana hii ndiyo inayo tiririka kwenye mishipa ya uhai wa asasi zote za siri za Illuminati wakiwemo Freemasons. Kama nilivyo tangulia kusema Freemasons hawamkatai MUUMBA, bali haki hiyo wanawapatia viumbe wengine.

Dhana ya Sitchin na wenzake si kwamba uhai umetokea kibubusa, hapana, uhai umetengenezwa, au uhai umeumbwa, lakini ni nani huyo aliye umba uhai? Hapa ndipo tunapo chora mstari wa mgawanyiko baina ya waumini wa MUNGU MMOJA na wafuasi wa ndani kutoka kwenye asasi mbalimbali za siri na zile za kishetani. 
WAUNGU KUTOKA SAYARI YA MBALI

Darwin tulisha mkataa mapema kwa vile yeye anadai uhai umeibuka kibubusa madai ambayo ameshindwa kuyathibitisha. Lakini sisi tulio bakia baada ya kumkana Darwin tulidhani kuwa tunaimba wimbo mmoja na wenzetu ambao nao wanadai kuwa uhai, umefanyizwa na haukuja kinasibu, lakini tumeona wao wanayo muumba wao tofauti na yule tunaye mfahamu.
HOOLYWOOD WAKIWA KAZINI

Lakini swali ambalo ningependa sote tujiulize ni kuwa; ni nani huyo aliyeiumba sayari hii ya tatu kutoka kwenye jua ambayo viumbe hao waliikuta ipo tayari na wao wakafanyiza uhai? 

Kutoka kwa wana New Age ambao wanaamini kuwa Aliens ndiyo mungu muumba wa ulimwengu, hakuna uthibitisho au maelezo yeyote kwa njia ya maandishi au matamshi waliyo yatoa kwenye hadhara kujibu swali hilo hapo juu, kuwa ni nani aliyeumba dunia. Ukiwabana wana New Age kuhsiana na uumbaji maelezo na vielelezo vyao vinaangukia kwenye mikono ya Darwin. Hivyo weka akilini mwako hilo kuwa asubuhi kabisa ya nadharia hii ya Aliens tunakutana na kizingiti, na swali lisilo weza kujibika.
UFO, AINA YA CHOMBO KINACHO TAJWA KUTUMIWA NA MIUNGU HAYO.

Tukiegemea kwenye kazi ya ‘mtume’ huyu wa NewAge bwana Sitchin na wenzake kama Alan F. Alford, R. A. Boulay, Neil Freer, Dr. Arthur David Horn, Dr. Joe Lewels, C. L. Turnage, Lloyd Pye, Laurence Gardner, na William Bramley wanasema hivi; 

Takribani miaka 450,000, kundi la viumbe wenye maumbile yanayo karibiana sawa na haya ya binadamu wa leo lakini wao wakiwa ni bora zaidi kimaumbile, walifika kwenye dunia hii wakitumia vyombo maalum vya usafiri wa angani. ‘Mitume’ hawa wanatuambia kuwa viumbe hao walitoka kwenye sayari ambayo ukubwa wake ni mara tatu kulinganisha na dunia yetu. Sayari waliyo tokea wasumeri waliita Nibiru ambayo inasemekana kuwa watu wa kale waliifahamu na kuichora sayari hiyo.
NIBIRU KWENYE SOLAR SYSTEAM

Wasumeri kupitia kwa ‘mitume’ hawa wanasema kuwa sayari hiyo ni ya 12 kwenye mfumo wetu wa jua wa ‘Milkway’ lakini wanasayansi wa sasa bado hawajaweza kuing’amua sayari hiyo au kuinasa kwenye mitambo yao kwa vile inasafiri kupitia kwenye orbiti iliyo na umbo kama la yai na hupita karibu na dunia yetu kila baada ya miaka 3,600. Viumbe hao walifika hapa duniani wakati sayari ya Nibiru ilipo kuwa karibu sana na ile ya dunia, nao walitua juu ya maji.
MICHORO UNAO ELEZEA SAYARI YA NIBIRU

Viumbe hao walihitaji kuweka kambi sehemu ambayo wangeweza kupata maji, hali ya hewa nzuri na mali ghafi zingine za kuwawezesha kuishi na kuendelea na safari yao, sehemu hiyo haikuwa nyingine bali kwenye aridhi yenye rutuba ya Mesopotamia, leo inafahamika kama Iraq.

Lingine ambalo tunaweza kuliona hapa ni kuwa viumbe hawa kutoka sayari ya mbali nao walikuwa ni wahitaji wa malighafi zilizomo hapa duniani kwa ajili ya wao kuweza kuendelea kuishi. Swali ni je MUUMBA anaweza kuwa muhitaji wa alivyo viumba? 
MICHORO YA KALE INAYO ELEZEA KUHUSU WAGENI HAO

Muumba anaweza kutegemea mazingira fulani tu ndiyo afanikishe jambo lake kama wao walivyo tegemea sayari yao ikurubiane na dunia yetu ndiyo watue kwenye maji? Majibu ya maswali yote haya ni hapana, MUUMBA yupo huru na juu ya vile alivyo viumba na wala haitaji chochote kutoka kwa viumbe wake na ameepukana na mapungufu yote hayo. Hivyo tena hapa tunaingia na walakini mwingine juu ya mungu huyu wa New Age.
MAFUVU HAYA SI YALE YA SOKWE WA DARWIN, UHAKIKA WAKE KWAMBA SI YA KUGHUSHI BINAFSI SIJAUPATA, LAKINI SI AINA YA HISTORIA INAYOFUNDISHWA KWENYE MITAALA YETU YOTE KOTE DUNIANI, SWALI KWANINI HAYAFUNDISHWI AU HAPASEMWI CHOCHOTE KUHUSIANA NAYO, SIJUI, LAKINI KUNAYO NADHARIA NYINGI NYUMA YA MAFUVU HAYA, NA MOJA WAPO NI MAFUVU YA BINADAM WALIO ZALIWA BAINA YA BINADAM NA WAGENI KUTOKA SAYARI YA MBALI.

Wageni hao wakaanza kuitawala dunia wakiongozwa na mfalme Anu, au El au An kutegemeana na tafsiri na mapokezi. Watawala hawa wapya walihitaji madini katika sayari hii kwenda kuitumia kwenye sayari yao, na walihitaji nguvu kazi ya kuweza kuwasaidia kuchimba malighafi hizo. Ndipo ‘miungu’ hao walipo amua kumuumba binadamu ambaye ataweza kufanya kazi hizo, katika lugha ya Kisumeria binadamu huyo alitajwa kama LU.LU jina ambalo kutokana na ‘tafsiri’ za ‘mitume’ hao Kiyahudi lilitamkwa kama Adama, yaani lenye maana ya kilichotengenezwa kwa udongo.


Lakini miungu hao si kwamba ndiyo walianzisha maisha ya binadamu, bali kutokea kwenye nadharia ya Darwin tayari alikuwepo kiumbe ambacho bado hajawa binadamu kamili, na miungu hao wakamchukua kiumbe huyo na kuchanganya DNA yake na ile ya miungu na kumtengeneza Adama ambaye atafanya kazi za machimbo Afrika.

Hivyo basi kwanadharia hii, Aliens hawawezi kuwa ndiyo MUNGU kwa vile wao wenyewe walikuja na kuikuta dunia ipo tayari, lakini pili walikuwa ni wahitaji wa hichi walicho kikuta hapa kwa maana nyingine wanayo mapungufu ya kuweza kutengeneza malighafi hizo. Tatu ni uzoefu wao wa kuweza kuwa na maarifa makubwa kwenye ‘baiolojia’ na ‘DNA’  na kwa kuunganisha seli hai za binadamu ambaye alikuwa bado hajakamilika, bado alikuwa ana-evolve- kuelekea kwenye ubinadamu kamili, kutokana na nadharia ya Darwin na kuchanganya na ile seli hai au ‘DNA’ ya Anunnaki na kumpata binamu mwenye sifa za kuweza kufanya kazi wanazo zitaka.

Lakini mpaka leo utaratibu wa kisayansi wa kunakili DNA ya kiumbe kimoja na kuchangana na ile ya kiumbe kingine haujaleta tija yeyote na wala haujaweza kutoa kiumbe tofauti na vile ambavyo DNA zao zimechanganywa na zaidi, madhara na mapungufu kwa viumbe hao imekuwa ni kubwa zaidi. Lakini hata hivyo hadithi ya ‘mitume’ hawa wa New Age kuhusishwa na ile ya mjomba Darwin ambayo kama tulivyo iona haina mashiko yoyote kunatufanya moja kwa moja kuona nadharia hii ya New Age inayo fundishwa kwenye kumbi za filamu haina jipya zaidi ya mwendelezo wa kazi za mjomba Darwin.
MOJA YA VITABU VINAVYO ELEZEA MISINGI YA NEW AGE, KUNAYO NA FILAM YAKE PIA, NA MSURURU WA VITABU SASA VINAVYO KWENDA NA MAUDHUI HAYO HAYO.

Mbali na ‘mitume’ hawa wa New Age kuwapa Anunnaki sifa ya uumbaji, hakuna kitabu chochote kinacho daiwa au kuthibitishwa kuwa kimeandikwa na Anunnaki kinacho thibitisha dai hilo, au ambacho Anunnaki wenyewe wanadai kuwa wamehusika na kazi ya uumbaji.

Tukiacha Aliens ambayo nayo misingi yake ni ile yakumkataa MUUMBA, lakini ikiwa haijitoshelezi na yenye mapungufu yanayo zusha maswali katika kila mstari wake mmoja wa maandishi; tunayo New Age Movement, ambayo hasa ndiyo wamejaribu kuipika iwe mfano wa dini kwa watu wote.

New Age Movement tofauti na zilivyo dini zingine haina kitabu chochote,haina kiongozi wa kiroho, haina makao makuu,haina muongozo rasmi, haina imani rasmi. New Age Movement ni uhuru wa kiroho unahusisha mahusiano baina ya wanachama na waumini ambao muungano wao, au mahusiano yao yanajengwa na wao kuwa na aina moja, mtizamo mmoja, ufahamu mmoja au uelewa mmoja kama msingi na muongozo kwenye kitu wanacho fahamu. 


Si lazima waumini wakubaliane katika kila jambo, likiwemo moja tu la kuwaunganisha hilo linatosha.
    
New Age Movement ni juhudi za watu mbalimbali kote duniani za kutafuta utulivu wa roho, akili, na mwili nje ya mfumo wa dini zenye kuamini juu ya kuwepo kwa MUUMBA. Katika New Age Movement muumini anaweza kuendelea kujiita ni Mwislamu, Mkristo au Myahudi kwa jina na kwa maneno lakini kivitendo si mfuasi wa dini hizo, kivitendo anakana juu ya kuwepo kwa MUUMBA. 
KWAO DINI ZOTE ZINATAKIWA ZIUNGANE NA KUWA MOJA.

Katika New Age Movement MUUMBA, anahusishwa na nafsi ya mtu binafsi, kuwa MUUMBA ni kuweza kujitambua wewe mwenyewe na kufikia daraja la juu sana katika uwezo na ufahamu wa kajitambua wewe binafsi. Mafunzo yao yanafundisha kuwa wewe ni sehemu ya nguvu kubwa na muhimu iliyo anzisha ulimwengu huu, wewe na nguvu hiyo ni kitu kimoja, unachotakiwa kufanya ni kuitambua nguvu hiyo, ukiitambua nguvu hiyo, utajitambua wewe, na ukijitambua wewe, utamtambua MUUMBA, na wewe na MUUMBA ni kitu kimoja, na hicho ndicho unacho takiwa kukitambua, kuwa wewe ni MUUMBA, wewe ni MUNGU.



New Age Movement wanaamini kuwa kila mmoja wetu ni mungu isipokuwa watu hawafahamu, kwa vile bado hawajajitambua.

Kwa nchi za Ulaya New Age Movement ni moja kati ya dini zinazo kuwa kwa kasi mno. Hii ni kwasababu dini yenye mizizi mirefu ndani ya Ulaya, yaani Ukristo umeshindwa kwa kiasi kikubwa kukidhi mahitaji ya kiroho, na kiakili kwa waumini wake ambao sasa wameamua kutafuta mbadala wa hitajio hilo la kiroho na kiakili.

Imani ya kwanza na iliyo ya msingi kwa New Age Movement ni kwamba, Kila kitu unachokiona ni mungu, kila kitu unacho kiona, ukiwemo wewe mwenyewe ni sehemu ya kitu kimoja ambacho kimesababisha kuwepo kwa uhai kwenye ulimwengu huu. Kwa kutojitambua kwetu ndiyo sababu tumejiweka katika hali ya chini kama ‘kiumbe’ lakini sisi ni miungu ambao bado hatuja jitambua. 

MUNGU kwa NEW Age Movement haina tafsiri ambayo sisi tunaitumia katika dini zetu kama vile kwenye Uislamu ambapo MUNGU ni MMOJA TU, HANA MSHIRIKA, HAJA ZAA WALA HAJAZALIWA, WALA HAKUNA MFANO KWAKWE YEYE KITU CHOCHOTE.


Kwa New Age Movement tafsiri ya MUNGU ni tofauti na hiyo ya Uislamu, New Age Movement wanatambua jina MUNGU kwenye misingi hii; Ni nguvu iliyo leta uhai, siyo nguvu ya kimaumbile bali ya kiroho, ambayo ipo ndani ya kila kitu, kila mtu, kila ‘kiumbe’ndani ya kila nyota, sayari na galaxy. Mungu ni kila kitu unacho kiona, na kila kitu ni Mungu, huu ndiyo ufahamu, ukweli wapekee na ulio wa msingi kwenye imani ya New Age Movement.

Msingi wa pili wa imani ya New Age Movement ni kuwa hakuna wa kuabudiwa. Kutokana na kuwa kwenye imani hii kila kitu na kila chenye uhai ni Mungu, basi hakuna wa kumuabudu mwenzake, bali kilichopo kila anaye jitambua au atakaye jitambua kuwa yeye ni ‘mungu’ basi afanye vile ambavyo ufahamu wake wa hali ya juu unavyo muongoza, au afuate maelekezo ya juu kabisa kutoka kwa, ‘mwalimu,’ mkufunzi ambaye anaamini hivyo.

Msingi wa tatu wa imani hii ni kuwa , Ulimwengu, uhai, na vitu vyote vya asili havikuumbwa na Mungu, bali vyenyewe ndiyo miungu. Kwamba ulimwengu na uhai vimetokea kwenye ‘nguvu ya uumbaji’ iliyo ndani ya ulimwengu, ndani ya kila kitu na kila kiumbe.

Msingi wa nne ni kuhusiana na maisha baada ya kifo. New Age Movement wanaamini kuwa hakuna kifo, kuna wanao sema kuwa roho inahama na kwenda kwenye kitu au kiumbe kingine, kuna wanao sema kuwa roho inapumzika kidogo kabla ya kuamua kuwa ni mwili gani tena iuchukue na kuendelea na maisha. Hakuna pepo wala moto wala siku ya mwisho, hizo ni imani za kibubusa walizo nazo watu kutokana na ufinyu na ufahamu wa nini hasa maana ya mungu.

Msingi wa tano ni kuwa hakuna shetani, hakuna uovu. Kinacho itwa wema au matendo mema ni nguvu ya uungu watu waliyo nayo ambayo hawaifahamu na ‘kimakosa’ wanadhani wameamrishwa kufanya hivyo na mafundisho fulani, lakini kumbe hiyo ni asili yao wao kama miungu kufanya mambo mazuri bila kutegemea malipo ya pepo au moto, kwanza hivyo vitu havipo, na wanacho kifanya kama wema ni nguvu ya uungu waliyo nayo. Na wanacho kifanya kama ubaya ni kutokana na kushindwakajitambua kuwa nafasi yao ipo kwenye duara la uungu.

Msingi wa Sita, uokovu kama unavyo tafsiriwa kwenye mafunzo ya dini ya Ukristo; hakuna kwenye New Age Movement. Tafsiri ya uokovu kwao inakuja hivi;Mtu anapofikia hatua ya kuitambua nguvu za ‘maumbile’ zilizo sababisha kuwepo kwa uhai kwenye ulimwengu huu, na akatambua kuwa yeye ni sehemu ya nguvu hizo, basi mtu huyo anakuwa ameupata uokovu. 

Zipo njia mbalimbali zinazo tumika kwa mtu kuweza kufikia hali hiyo ambazo zinahusisha na ‘kucheza’ au kuubadilisha hali ya ufahamu wa ubongo kwa kutumia vitu kama vile hyponosis, meditation,aina fulani ya muziki, aina fulani ya dawa,lakini pia hali hiyo inaweza kufikia kwa kutumia aina mbalimbali ya ‘vifaa’ vya kiroho kama vile aina ya madini ya Crystals,aina maalum ya karata, uchawi, kupokea taarifa maalum kutoka kwa viumbe wasio kuwa binadamu maarufu kama channeling


Wanaamini kuwa uokovu kwa watu wote utafikiwa pale ambapo sehemu kubwa ya watu watatambua kuwa wao wote ni wa moja, wao na mungu ni wamoja, ni kitu kimoja, hali hiyo ndiyo itakayo leta New World Order, kwa vile ulimwengu mzima utatambua kuwa binadamu wote ni wa moja, ustaarabu wao ni mmoja, na kutakuwa na serikali moja ya dunia kuhakikisha kuwa kuna furaha na amani.

Msingi wa Saba, mateso ambayo binadamu inayashuhudia kote duniani ni matokeo ya uchu, ulafi, chuki, ujinga wa kutofahamu nafasi yetu hapa duniani kama miungu. Pia wakati mwingine wanaamini kuwa mateso yanatokea kwa sababu maalum kama vile kusaidia ukuaji wa kiroho na kujifunza somo maalum la maisha haya na mateso yanayo tokea yanaweza kutafsiriwa kama ni aina ya somo ambalo tunalipitia kama waungu.

Msingi wa Nane, utoaji mimba si suala linalo katazwa, kwa vile hakuna mafunzo rasmi yanayo ainisha hilo, na hata hivyo New Age Movement ni wapiganiaji wa kubwa wa haki za wanawake ikiwemo hii ya kuwaruhusu kutoa mimba. Utaona haki hii ya utoaji mimba inawiyana sawia na mipango na mbinu za kupunguza idadi ya watu duniani, mbinu inayotumiwa sana na maadui zetu.

Misingi hiyo nane niliyo itaja ya New Age Movement siyo rasmi, kwa vile dini hii haina kitabu maalum kama muongozo wake, lakini hizo nane ni za msingi na utazikuta katika kila muongozo na mwalimu wa New Age Movement. Unaweza usizipate katika mpangilio nilio ueleza, zinaweza zikaongezeka au kupunguzwa lakini utazikuta zimesimamia katika mazingira na nadharia hizo kuwa sisi binadamu na kila kinacho tuzunguka ni miungu.

Ingawa jina lake ni ‘New Age’ Movement, mafunzo yake siyo ‘New’ katika historia ya mwanadamu katika kumkana MUUMBA. Nadharia ya ‘umoja’ (oneness) imeelezwa vyema katika kitabu cha kimila cha Kiyahudi ambacho ni lini hasa kimeandikwa mpaka leo hakijulikani, lakini kilicho wazi kwenye kitabu hicho ni kwanza si kazi ya Wayahudi, bali ni ‘urithi’ walioupata wakati wanatoka Babyloni, ni kazi ya mashetani Wababyloni ambao Wayahudi walipokea kwa njia ya mdomo.

Kutoka karne ya kumi na nane mpaka karne ya ishirini, ulimwengu umeshuhudia kufufuliwa kwa kazi za kale mno na waandishi mbalimbali zilizo beba maudhui ya New Age Movement. Alikuwepo Paracelsus kwenye zama za kati ambaye kazi zake zilibeba maudhui ya ki-hermatik. Ingawa mafunzo ya hermetic yanatajwa kama ni falsafa ya Ulaya, mapokeo au mafunzo au dini ya Ulaya lakini kiuhakika kabisa asili yake ni mashariki ya kati, nayo ni mafunzo yenye asili ya uchawi na inayo husiana na miungu wa kale wa Egyptna elimu ya kishetani iliyo pokelewa Babylon na Waisraeli wakati wakiwa utumwani hapo.
MOJA YA MISINGI NA MAFUNZO YA KIHERMATIC, 'AS ABOVE SO BELOW'

Karne ya kumi na nane ilimshuhudia Emanuel Swedenborg, huyu alikuwa ni mwana sayansi, mwana falsafa na theolojia wa Kisweden. Mwenyewe alijiita kupitia kwenye kazi yake aliyo ichapisha mwenyewe kama ni mtumishi wa bwana Yesu Kristo, kazi hiyo ilikwenda kwa jina la True Christian Religion. 

Lakini zaidi alifahamika kwa kazi yake maarufu iliyo kwenda kwa jina la Heaven and Hell. Alipo fikisha mika 53 aliingia kwenye maisha ya kiroho rasmi na hapo akaanza kuona ndoto na maono yanayo muongoza na anayo poswa kuyatumia kuiongoza jamii. Anasema alipokea maono kutoka kwa bwana yanayo mwelekeza kuandika upya kuhusiana na maisha ya mbinguni kwa ajili ya kuujenga upya Ukristo.

Kutokana na imani ya ‘kanisa jipya’ au imani ya Wakristo ambao wanafuata mafunzo ya New Age Movement, ni kuwa  Emanuel Swedenborg, amefunguliwa macho ya kiroho ambayo yana muwezesha kuanzia kipindi hicho na kuendelea, kuweza kutembelea, peponi, motoni, kukutana na malaika, mashetani na viumbe wengine wa kiroho na kwamba siku ya hukumu ya mwisho imeshatokea mwaka 1757, katika maelezo yake ni kuwa hilo limetokea  katika ulimwengu wa roho na yeye akishuhudia.

Aina hii ya mafunzo iliporuhusiwa kuingia kwenye milango ya kanisa ikawa ni chumbuko la mafunzo ya New Age ndani ya makanisa. Maajabu na mazingambwe kufanywa ni sehemu ya ibada. Mstari baina ya uchawi, ushirikina na ibada umekuwa mwembamba kiasi wakati mwingine unashindwa kutofautisha kipi ni kipi.


Kutoka karne ya kumi na tisa mpaka ile ya ishirini, mizizi na mbegu za New Age Movement ilizidi kuota kupitia kwa watu kama Godfrey Higgins,Eliphas Levi, Helena Blavatsky, na George Gurdjieff . Kazi ya mwana mama Alice Bailey na asasi ya Theosophical Society zilipulizia roho ya uhai kwenye dini hii ‘mpya.’

Kwa jina ni New Age Movement, lakini kimafunzo ni moja kati ya dini za kale za kipagani. Ndani ya New Age Movement kuna mafunzo ya  yanahusiana na imani ya Mungu mmoja, miungu zaidi ya mmoja, imani za kale za kishetani, imani ya inayo nadi kuwa dunia nayo ni mungu mama, sayansi, elimu ya nyota, elimu ya mazingira, saikolojia na fizikia. Wakati mwingine mafunzo yake yana beba jumbe au yanaathiriwa na mafunzo ya dini za Mungu mmoja na zile za kishetani. Utakuta huko kuna baadhi ya mafunzo ya Kiislam, Kikristo, Kiyahudi, Kibuddha, Taoism, Usufi, upagani mambo leo,mafunzo na nadhari za kimagharibi, ilimradi ni vurugu na mchanganyiko wa kila namna.
MALENGO NI KUZIUNGANISHA DINI ZOTE KUWA MOJA. KUMEKUWA NA JUHUDI ZISIZO RASMI ZA KUONGANISHA MITAALA YA KIDINI SHULE ZOTE KUTOKA MSINGI MPAKA VYUO, MAMBO HAYO YANAKWENDA KIMYA KIMYA

Hapa kwetu baadhi ya watu hawa walipata kuhojiwa na Redio ya Clouds kwenye kipindi chao maarufu cha ‘Leo Tena,’ mwanzo walijinadi kuwa wao ni Freemasons, lakini katika maelezo yao hawakuthibitisha ni namna gani wao ni Freemasons, maelezo yao yalikuwa ni ya kujikanganya, mmoja akafahamika kuwa ni mshirikina au mganga wa kienyeji, wakati mwenzake akijaribu kujitutumua kuwa ni Freemasons lakini maelezo yake yakimtaja kama mwana ‘New Age Movement.’ 


Alijitahidi kadiri alivyo weza kuonesha mfanano na uwiano baina ya dini kubwa duniani, maelezo yake yalikuwa yakilenga kuziunganisha dini mbalimbali duniani na hasa hizi dini kubwa, kitu ambacho ndiyo roho ya New Age Movement.

Lakini pia New Age Movement moto wake unakolezwa na kile kinacho fahamika kama ‘Age of Aquarius’ ambacho tutakutana nacho kwenye post zingine nikizungumzia mambo yanayo randana na haya..

Binadamu wa leo amesimama kwenye kona, kwenye daraja linalo elekea kwenye zama mpya, maarufu kama Age of Aquarius.  Tunapo likaribia geti la zama hizo mpya, matumaini mapya, mipango, ndoto, mitazamo, nadharia, imani na mwelekeo mpya nao inafunguka. Hali hii ya ‘New Age; sauti yake ilianza kupazwa tangu miaka ya 1960 kupitia vyombo mbalimbali vya habari, majarida na aina nyingine za mawasiliano, lakini bado si watu wote wanafahamu nini hasa maana ya ‘New Age.’

Wimbi la nchi za Magharibi kwenye miaka 1960 kuhusiana na New Age kuliwafanya watu wengi kuamini kuwa tumeingia kwenye New Age. Kuna wanao dai kuwa tumeingia kwenye zama za Aquarius tangu mwaka 1781, wapo wanao dai hatutaingia mpaka miaka 50- 100 ijayo, na mengine na mengine. Lakini ni vigumu sana kusema ikiwa tayari tumeshaingia au la katika zama hizo au ni lini kiuhakika tutaingia, kwa vile tukio zima linategemeana na safari ya kutoka ‘nyumba’ moja ya Zoadic kwenda nyingine, na kwa vile ukubwa wa nyumba moja na nyingine ni tofauti na nafasi baina ya nyumba hizo hali kadhalika, inakuwa ni vigumu mno hasa ikichukuliwa kuwa kwenye hesabu zetu mzunguko huo umewekwa kwa kipindi maalum, bila kuzingatia tofauti ya umbali na ukubwa baina ya vikundi hivyo vya nyota.

Kwenye miaka hiyo ya 60 mpaka 70, idadi kubwa ya wasomi wasio makini, waliwashawishi wanafunzi pamoja na watu wengi kuondoka katika nchi zao za kimagharibi kuelekea nchi za mashariki, hasa India, kwa ajili ya kutafuta ‘hekima, elimu,ukweli, ufunuo , nuru na karma njema.

Ni wachache kati yao ndiyo walio elewa kuwa, wanaifuata njia ileile, iliyopitwa na mwana mama miaka mia kabla, mwana mama huyo kupitia safari kama hiyo akaweka misingi ya ‘NewAge Movement’, ambayo leo hii tunaiona duniani kote, kama ni inayo fufuka.
WAKINA MAMA VINARA WA NEW AGE, SI BURU VUGUVUGU HILI LINALISIMAMIA KWA NGUVU ZOTE HAKI ZA AKINA MAMA.

Mwanamke huyo hakuwa mwingine ila ni Helena P. Blavatsky, ambaye anafahamika kama mtume wa dini hii ya New Age. Mwaka 1875 mwana mama huyu alianzisha asasi iliyo fahamika kama Theosophical Society.

Mwana mama huyu alifundisha upagani, udugu wa kidunia, na muungano wa dini zote duniani, isipokuwa dini za Mungu mmoja, hizo alisema haziwezi zikaungana na kile alicho kiita ukombozi kwa mwanadamu.

Alimlaumu na kumkashifu Mungu mmoja, kuwa hakuwa akitenda haki, na alisema huyo alikuwa ni Mungu tu wa wana wa Israeli na siyo zaidi ya hapo, anasema kuwa vitabu vitakatifu vimekosewa, kwani ni shetani ambaye ndiye aliyekuwa Mungu mzuri na wa haki.

Alisema kuwa alikuwa na uwezo wa kuwasiliana na viumbe wenye roho tu, kama vile majini na malaika. Vitabu vyake kama vile ‘Isis Unveiled’ na ‘Secret Doctrine’ aliweza kuvinadika kupitia taarifa ambazo zilikuja kutoka kusiko julikana na kumiminika kichwani mwake naye akaanza kuyaandika,  wakati mwingine hutokea mkono huanza kuandika wenyewe bila mamlaka yako, na wakati huo unakuwa upo kwenye hyponetic au kwa hapa kwetu tunaweza kusema umepandisha shetani, njia hizi pia hufahamika kama channeled.

Kwenye kitabu chake alicho kiita ‘The Secret Doctrine’ Blavatsky ameandika hivi;

“Lucifer anawakilisha uhai, mawazo, maendeleo, ustaarabu .”

Kwenye kitabu chake, 'The Secret Doctrine' Blavatsky ameandika, 
“Haki na uhuru kwa Lucifer ni alama kuu, ni Nyoka, ni Mwokozi na ni Lucifer ndiyo Mungu wa sayari yetu na Mungu wa pekee,” 
halafu akaendelea kuandika, 
“Na bikira wa Virgo (kikundi cha nyota ya virgo) ambaye amekuja kuwa Mama wa Mungu na Mama wa Shetani kwa wakati mmoja, kwani ni mama mwenye Baraka siku zote, lakini kwenye historia uhalisia, Lucifer au Luciferius ndiyo jina. Lucifer ndiye mtakatifu na nuru ya mbinguni, ni roho mtakatifu na shetani kwa wakati mmoja.”

Blavatsky alipo kufa mwaka 1891, Annie Besant, mwanamama mwanajeshi, masonia na mwanachama wa asasi ya Fabian Socialist Society ya England alichukua nafasi ya Blavatsky. Mwana mama huyu alikuwa ni rafiki wa George Bernard Shaw, H.G Wells na viongozi wengine wa asasi hii ya Fabian, hivyo alikuwa kwenye nafasi nzuri mno ya kupenyeza mawazo ya mwenzake aliye mtaangulia kwa watu muhimu mno. Unakumbuka nembo ya asasi hii ni Mbwa Mwitu aliye vishwa ngozi ya kondoo.

Alishiriki katika maandamano mbalimbali kwenye kupaza sauti yake isikike juu ya kile anacho kitaka walimwengu wakifahamu, aliandika vitabu mbalimbali kuongezea nguvu kwenye kazi zilizo tangulia za Blavatsky.

Baada yake huyu akaja mwanamama mwingine aliyekwenda kwa jina la Alice Bailey. Utamkumbuka mwana mama huyu nimemtaja kwenye posti zinazo zungumzia ndoa za jinsia moja, namna alivyo weka mapendokezo ya kufikia lengo la wanaume kuowana wao kwa wao na wanawake wao kwa wao, leo tena tunakutana naye kwenye New Age Movement, na dini hii haipingani na mambo ya kishoga, kama tulivyoona kwenye dini hii hakuna jema wala ovu. 

Bailey naye akishirikiana na mume wake Foster Bailey, ambaye alikuwa ni mwana masonia wa daraja la 32, wakiwa wameshikilia jukumu la asasi ya  Theosophical, walifanikiwa kuweka misingi imara juu ya kile ambacho leo tunakiita ‘New Age Movement.’ Katika hili waziwazi waliweka hadharani mguso wao wa kiushetani, na wakatengeneza kampuni ya uchapishaji iliyo kwenda kwa jina la Lucifer Publishing Company na jarida waliloita jina la Lucifer. Kwa vile dunia ya kipindi hicho ilikuwa ‘bado’ haijawa tayari na maono hayo ya kishetani na kuona kwamba wangeonekana ni kichekesho, walibadilisha jina la kampuni hiyo na kuita ‘Lucis Publishing Company’ lakini mguso wa kiushetani bado uko palepale, kwani walicho fanya ni kufupisha jina la bwana mkubwa wao, kutoka ‘Lucifer’ kuja kwenye ‘Lucis.’

Mwaka 1922 wakaanisha ‘Lucis Trust’ ambayo mpaka leo bado ipo na inafanya kazi kwa mwavuli unao zibeba asasi zingine zilizo za kishetani au zenye maono na malengo ya New World Order ikiwemo dini mpya kwa watu wote, ambayo wafuasi wake kwa sasa ni ‘wana NewAge.’ Baadhi ya mashirika na asasi zilizo chini au zinazo dhaminiwa na ‘Lucis Trust’ ni United Nations, Arcane School, World Goodwill, Triangles, Lucis Publishing, Lucis Productions, Lucis Trust Libraries na New Group of World Servers.

Alice Bailey naye alipokea ‘ufunuo’ wake kupitia kwa Djwhal Khul ambaye kupitia kwake aliandika vitabu ishirini. Lengo kuu ni kutengeneza kile kinacho fahamika kama ‘Harmonic Convergence,’ pia unafahamika kama muungano wa kiroho, au nukta ya mageuzi ambayo itafikiwa au kutokea pale ambapo mataifa yataweka kando kasoro na tofauti zao, katika sura mpya itakayo fahamika kama ‘New World Order’ na muungano mpya wa kidunia, wakati ambao serikali ya dunia, na dini moja ya dunia itapatikana, zama mpya au zama za Aqurius zitakuwa zimeanza. 

Ni kutoka hapo tu. Ndipo mmoja anaye ngojewa atakapo tokea, kama ni Yesu, Mahdi, Krishna, Maitrayaa au yoyote yule katika dini au mafundisho yoyote yale anaye tajwa kuwa atarudi, basi wakati huo ndipo atakapo onekana, kama nilivyo kwisha tangulia kueleza katika posti zilizo pita, maadui zetu wanayo hiyo teknolojia ya kufanya watu hao waonekane kuwa ‘wamerudi,’ lakini zaidi watu hao hawato waita watu katika mafundisho ya dini waliopata kuifundisha hapo kabla, lakini watawaita watu katika ‘muungano wa kidunia,’ ‘katika dini mpya ya muungano wa kidunia,’ katika dini ya wana NewAgers’. 

Kama kawaida viongozi wako wa kidini watakuwa mstari wa mbele kuwaunga mkono jamaa hawa na kukushawishi wewe muumini  wao kwa vifungu vilevile kutoka kwenye kitabu chako kitakatifu uwaunge mkono ‘wateule’ hawa wa kale lakini wakiwa na dini mpya kabisa.

Kwenye kazi zake Bailey ameweka wazi kabisa kuwa, patakuwepo na dini mpya;

“Mafunzo ya kiroho yamehama kutoka kwenye imani za zamani na kuja kwenye nuru mpya ya kiroho ambayo itaiangaza na kutapakaa duniani kote kama dini mpya kwa dunia yote. … Uyahudi ni wakale mno, na zaidi umejitenga na hauna ujumbe wa kweli wa kiroho na kiakili kushinda ule unao tolewa na imani mpya … imani ya Kikristo nao imeshatekeleza malengo yake. Waanzilishi wake wanatafuta kuleta agano jingine  jipya ambalo litawamulika watu kila kona. (Uislamu nao hauna lolote zaidi ya vurugu tunazo ziona)


Mwandishi wa kazi moja matata, bwana David Livingstone, alipoandika ‘Terrorism and Illuminati’ kwenye utafiti wa kazi hiyo alifichua kuwa Lucis Trust inafanya kazi zake kupitia wana bodi wateule wa kimataifa kama vile, John D. Rockefeller, Norman Cousins, Robert S. McNamara, Thomas Watson, Jr. wa IBM na kinara wa New World Order na Freemasons wa daraja la 33 na mwenye mikono iliyo jaa damu za walimwengu bwana Henry Kissinger.

Oganaizesheni hii ya Bailey pia inafanya kazi kwa mashirikiano na asasi zingine ambazo nazo ni washiriki na wachezaji wazuri wa nyimbo za New World Order kama vile; CFR, Bilderberger group na Trilateral Commission.

Aprili 25, mwaka 1982, mamilioni ya watu kote duniani, walisoma vichwa vya habari vya magazeti mbalimbali, kote duniani, vikisema, ‘KRISTO SASA YUPO HAPA.’ Habari hizo zilikuwa na maudhui kwamba, katika historia ya ukuaji na maendeleo ya mwanaadamu, kiumbe huyu mwana wa Adam amekuwa akiongozwa na watu wenye nuru, viongozi wa hekima, viongozi wa daraja la juu kiroho, ambao viongozi hao nao wanaongozwa na mwalimu wa dunia, ambaye anafahamika kama Lord Maitreya. 

Taarifa hiyo ilidai kuwa kwa wakati huo  ‘Kristo’ alikuwa anaishi duniani, na ndani ya miezi miwili tu, atajidhihirisha kwa kila mtu amuone. Wakati huohuo Mwingereza Mkristo anaye fuata ‘agano’ jingine jipya, au mfuasi wa ‘Ukristo wa kisasa’ na mfuasi wa imani ya Theosophical, bwana Benjamin Crème, alianza kuizunguka dunia na akitangaza kuwa yeye anazungumza kwa niaba ya ‘Kristo.’

Katika mahojiano yake na mazungumzo yake mbele ya hadhara, alielezea kuwa, si kwamba anasimama badala ya Yesu Kristo, bali ni kwa niaba ya ‘Mwalimu wa Hekima,’ ambaye kutoka kwake Yesu Kristo, Buddha, Krishna, Muhammad na wengine ni wanafunzi wake. Kwa maneno mengine Crema alikuwa anatuambia kuwa na yeye sasa ameingia kwenye orodha hiyo ya kina Muhammad, Yesu Kristo, Krishana na wengine, kwani na yeye sasa Crème anazungumza na ‘Mwalimu’ yuleyule aliye wafundisha wakina Yesu na wenzake, yaani Crème ni mtume, mtume wa ‘New World Religion.’ Haswa ndivyo alivyo kuwa na ndivyo alivyo mpaka hivi sasa.

Kampeni hii ya kimasoni ya Crème, iliyo fanywa nyuma ya jina la Ukristo, ilidhaminiwa na oganaizesheni ya New Age Religion inayo fahamika kama Tara Center, kutoka makao yake makuu ya London, Los Angeles na New York. Lakini mwalimu huyu wa Crème au Lord Maitreya hakuweza kujitokeza kama ilivyo elezwa, nadhani wimbi hili la New Age na dini yao lingekuwa limejitundika kitanzi chake yenyewe, ingekuwa limejichimbia kaburi lake, propaganda na vipindi vyao mbalimbali kote kwenye redio na luninga vingeanguka patupu.


Lakini haikuwa hivyo, uwezo wa binadamu kuchanganua mambo umekwisha kabisa, uwezo wa kufikiri umefunikwa na kiza cha majibu mepesi ya wanasiasa na vipindi vya luninga, Crème bado anatambulika kama mtume wa New Age, na mtandao mpana wa New Age unaingia na kupenya kwenye kila kona ya dunia, kupitia mitandao ya kitaifa na kimataifa, kupitia vikundi vya wanaharakati mbalimbali, watizame kwa makini wale wanao jiita ni ‘ma-activist’ au ‘wanaharakati’ tizama vifungu vya ‘biblia’ yao, tizama msukumo ulio nyuma ya kazi zao, utaona vidoti vinavyo chora picha ya New Age, picha ya New Age Religion, picha ya Crème.

Mitume hao wa New Age utawakuta katika kila taasisi za kitaifa na zisizo za kitaifa, mmoja mmoja au kikundi na hata makundi, wanaojijua na wasiojijua, miongozo yake utaikuta kwenye mikutano ya Umoja wa mataifa, kumbuka moja ya wafadhili wa kazi za Umoja wa Mataifa ni Lucis Trust. Utaikuta miongozo hiyo kwenye sera za mashirika yenye nguvu na ushawishi kwenye dunia ya leo kama vile; Club of Rome, Aspen Institute, Council on Foreign Relations, World Federalists, World Bank, na mengine na mengine.

Wafuasi wa dini hii mpya utawakuta kwenye sura mbalimbali kama vile, wanajimu wanao amini juu ya nguvu za nyota na kuvipa viumbe hivyo sifa zisizo zake, utawakuta kwenye vikundi vinavyo dai kupigania haki za wanawake, haki za watoto, haki za binadamu, haki za mashoga. Utawakuta kwenye wanaharakati wa mazingira, utawakuta kwenye wafuasi wa Kabbala, utawakuta kwenye viongozi wa kidini na wafuasi wa dini kuu tatu kama vile Uislamu, Ukristo na Uyahudi lakini wakipaza sauti vifungu katika baadhi ya mafundisho kwenye vitabu vyao vibadilishwe ili kuendana na ‘hali’ ya sasa. 

Utawakuta kwenye duara la wanasayansi, wana diplomasia, viongozi wa taasisi mbalimbali duniani, viongozi wa nchi, utawakuta kwenye maduara ya watu maarufu na matajiri wa dunia hii leo. Hawana chochote zaidi ya biashara. Lakini wao kuwa wafanya biashara siyo shida, shida ipo kwenye madai yao na ushuhuda wao. 

Hapa kwetu Tanzania tunao wengi, na kila leo wanaibuka, lakini tabia na sifa zao zimevaa vazi la wana-newagers. Mfano msafi kabisa kwenye aina hii ya dini na mitume wake ni Babu wa Loliondo. Sina haja ya kuandika hapa ni nini kilitokea yalishaandikwa na kusemwa na bado familia zilizo athirika na kitimbi cha Babu wa Loliondo, zimelipa gharama kubwa ikiwemo uhai kwa wapendwa wanafamilia wenzao, kutokana na madhara ya New Age Movement. 

Si maanishi kuwa Babu wa Loliondo ametumwa na akina Creme moja kwa moja, hapana, namaanisha kile alichosema na alichokifanya kwa watu waliomsikia na kumuamini na kumfuata kinayo sifa, sura na tabia za akina New Age Movement.

Leo hii tunao mitume na manabii mbalimbali, ambao wanadai kupokea maono kutoka kwa MUUMBA mwenyewe, lakini kila tunapo watizama mitume hawa wa leo, kila tunapo sikiliza maneno yao, nafsi zetu zinakiri kuwa kuna shida katika shuhuda zao, katika kazi zao, katika maneno yao na alama zao, lakini kwa vile dunia ya leo imezama kwenye kuutengeneza mwili kuliko roho, kasoro hizo tunazifunika, ile tupate kile jicho letu ilicho tupatia, moyo wetu ulicho tamani bila kuwa na wasiwasi wowote juu ya matendo yetu.

Hayo ni madhara yanayo tokana na mafundisho ya Darwin kwa walimwengu. Ingawa Darwin alikataa juu ya kuwepo kwa roho, wakati New Age wao wakisisitiza kuwa roho ipo, na hiyo ni moja ya misingi yao mikubwa kwenye dini hii; lakini wengi wa wafuasi wa dini hii utawaona waapo kwenye kwa ajili ya kupata manufaa ya kiwiliwili kuliko roho.

Hiyo ndiyo athari ya mafunzo ya Darwin, kwamba watu wamesahau kuwa wanayo asili mbili, asili ya roho na asili ya mwili, watu wamebaki na asili moja tu na ndiyo inayofanyiwa kazi usiku na mchana, asili ya mwili. Hii ni kwasababu tangu tupo chekechea mpaka tunastaafu ajira, tunacho fundishwa, tunachokiona, tunacho aminishwa ni juu ya ulimwengu wa kivutu zaidi, ulimwengu wa materialisim.

Sasa ulimwengu huu wa materialisim unaboresha mwili na kuiacha roho imedhoofu, sasa watu wanarudi nyuma kutafuta ‘peace of mind’ ambayo wameikosa kwenye ‘materialisim’ na hapo wanakutana na new age movement ambayo inatoa ahadi ya kutatua matatizo ya leo ya ulimwengu kwa ujumla au kwa mtu mmoja mmoja, pao kwa hapo. Ndiyo utaona watu wanajazana kwenye aina hii ya mafunzo na dini bila kujali imani yake ni dini ipi, na sababu athari ya Darwin imekuwa kubwa sana kwenye maisha yetu ya kila siku, hata tukienda huko hatufati ‘peace of mind’ tunafuata sabuni ya roho, tunafuata pesa ambazo manabi wa dini hii wanahubiri kuwa watakupatia kwa wepesi, ili ukajitatulie shida zako kwenye ulimwengu wa kivitu zaidi kuliko roho.

Tunamtafuta Mungu, Muumba wa ulimwengu wote, Muumba wa tunavyo vijua na tusivyo vijua. Tulianzia na Sayansi yetu ya leo ya karne ya 21. Sayansi hii kwenye suala la uumbaji imejikita zaidi kwenye nadharia ya Darwin kama ndiyo msingi wa ukweli juu ya uumbaji, katika posti iliyo tangulia tumeichambua nadharia hii na kweli tumekutana na mapungufu ya kutosha na kiufupi tumeiyona haiwezi kutusaidia katika safari yetu hii yenye maana kubwa kuliko. Safari ya kujitambua na kutambua asili yetu.

Hata hivyo kwenye karne 21 sayansi yetu ikachukua njia nyingine isiyo rasmi kwa kasi zaidi. Njia hiyo ni uwezekano wa kuwepo viumbe wengine ambao huenda wakawa ndiyo waungu wenyewe, njia hii mpya imefuatana na ile ya kale kidogo lakini yenye jina jipya, New Age Movement, njia hii nayo tumeitazam kwa uchache lakini kama tulivyona katika misingi na taratibu zake ni kama muendelezo wa kazi za kina Darwin.

New Age inatuambia haina haja ya kumtafuta Mungu, kwani sisi wenyewe ndiyo waungu. Lakini tunapo itazama kwa undani tunaona kuwa madai hayo nayo hayana majibu sahihi juu ya kile tunacho kitafuta.

Kama sisi ni waungu, mbona ....? Kama sisi ni waungu mbona ...? Kama sisi ni waungu mbona ..,?
Maswali tutakayo jiuliza yanaweza kujaza majalada na majalada, mabuku na mavitabu makubwa makubwa na hayoto kuwa na majibu sahihi.

Hivyo kiukweli kabisa New Age imeshindwa kutuambia asili yetu ni wapi, imeshindwa kutuambia sisi ni akina nani. Ilichoweza kufanya ni kutuongezea dozi kwenye nadhari ya Darwin ambayo nayo ilisha shindwa kabisa. Hivyo hii nayo tuna achana nayo.

Bado tunaendelea kumtafuta Mungu na kwakuanzia tumetaka kufahamu sisi ni akina nani, ambapo tukiweza kujua asili yetu, tutaweza kumjua hata huyo aliyenyuma ya sisi kuwepo hapa ...

 Next post tutaendelea kuitafuta asili yetu, lakini safari hii tukitazama dunia zote mbili, dunia ya roho na dunia ya mwili


till next time ... 

1 comment:

  1. So ngoja nisema hivi mwenyezi mungu tuongezee imani tuwe na imani na uwepo wako

    ReplyDelete