Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, March 27, 2016

NAMTAFUTA MUNGU Ep: 3


Leo tunaendelea na safari yetu ya kumtafuta MUNGU, lakini kwanza tumetizama asili yetu ambayo mapak sasa bado hatujafahamu ni wapi, hivyo inakuwa vigumu hata kufahamu ni nani aliye nyuma ya vyote tunavyoviona ikiwemo sisi wenyewe. Sayansi imekosa lugha ya pamoja ya asili yetu ni wapi?

Leo tunaitazam roho, kitu kingine ambacho sayansi haikitambui, lakini tunaona athari ya uwepo wake katika maisha yetu ya kila siku, huenda huku kwenye roho tunaweza kutambua asili yetu na hatimaye kumtambua MUUMBA wetu ... tuendelee.



Tukiachana na wana NewAgers, na habari zao za zama mpya, ambazo malengo yake ni yaleyale ya kumkana MUNGU MMOJA, hebu tujitizame wenyewe, hasa, sisi ni akina nani?

Kila kona wapo, kwa sura tofauti, utawatambua kwa sauti yao moja, wanataka mabadiliko mapya katika kila kitu wakati tunapo ingia kwenye zama mpya, zama za Aqurius.

Eidha tunataka kuelezea ni nini maana ya mafanikio katika nyanja yeyote au nini maana ya kufeli katika lolote lile, au tunataka kutoa mtazamo wetu juu ya jambo lolote lile, hapana shaka maono hayo yata athiriwa moja kwa moja na mtazamo wetu juu ya asili ya binadamu.

Tunapo hitimisha asili ya binadamu ni ipi, moja kwa moja tunatoa majibu yanayo husu majukumu, malengo na njia ya binadamu ni ipi kwenye uso huu wa dunia. Lakini namna ambayo sayansi na dini zinavyo jibu swali hili, daima mgongano unakuwepo baina ya ‘wanasayansi’ na ‘wanadini’.

Sayansi inatazama asili ya mwanadamu kama mlolongo mrefu wa ukuaji na ubadilikaji wa maumbile, kutoka katika kiumbe duni, dhaifu, katika hali ambayo tofauti kati ya mtu na mnyama haionekani. Hatua ambayo sayansi inamtambua binadamu kama ni kulingana na maendeleo ya nje yanayo onekana kwa binadamu. Kama vile kutembea kwa miguu miwili, kutumia zana na kufanya mawasiliano kupitia maneno yanayo tengenezwa na ulimi. Hapa binadamu kwenye hii sayansi ni mtoto wa mazingira yake mwenyewe.[1]

Lakini dini na sanaa zina elezea uumbwaji wa binadamu. Siyo mlolongo wa evolution, bali ni kitendo cha Muumba mwenyewe. Siyo kitu kilicho pitia mabadiliko, bali kilicho tokea kwa mara moja kikiwa kikamilifu. Dini zote na kazi zote za sanaa zina mtambaulisha mwanadamu, siyo kama mtoto wa mazingira yake, bali mgeni wa mazingira haya.

 Ikiwa mwanadamu ni zao la mazingira yake ama au ameumbwa, swali linalo kuja, binadamu ni nani?[2]
Wana materialisim wao wameendelea kushikilia kwamba binadamu ni mnyama aliyekamilika. Ukuaji wa kutoka ‘mnyama’ na kwenda kuwa binadamu unatokana na mazingira yake. Kama mwana materilist Friedrich Angels aliavyo sema,

Mtu ni zao la mazingira yake na kazi zake.”

Ugunduzi wa zana zake na lugha ya kuwasiliana kwa maneno ndiko kuliko mvukisha daraja kutoka kwenye wanyama na kumfanya mtu mkamilifu.

Kwenye falsafa ya materilist mtu, ni zao la mahusiano yake ya kijamii, au kwa uwazi kabisa ni zao la zana ya uzalishaji inayo tumika. Mtu si chochote na hajatengeneza chochote, bali kinyume chake ni zao la mazingira anayo ishi.

Darwin akamchukua mtu huyu asiye na sifa ya ‘utu’ na akamjenga kupitia ‘natural selection’ mpaka akaweza kutengeneza zana, kuongea na kutembea kwa miguu miwili. Baiolojia ikaikamilisha hii picha ya Darwin kwa kutuonesha kuwa kila kitu kinarudi nyuma mpaka kwenye hatua ya kibubusa ya uhai ambapo ilikuwa ni mgongano wa kinasibu wa kemikali zilizo sababisha uhai. 

Hivyo hakukuwa na roho, na hivyo hakuna roho na hivyo hatuna ‘mtu’ bali tuna ‘binadamu’ aliye kuwa kupitia ‘natural selection.’

Lakini kile kilicho rekodiwa katika zama zote za historia kinacho fanywa na binadamu, kina tofautisha sana binadamu na ‘mtu’ wa Darwin na wana matirialisti wenzake. Picha ya wanamaterilist ni kuwa binadamu ni zao la mazingira yake, wakati kile kinacho fanywa na binadamu kinamchora kama mgeni kwenye mazingira yake. Mbali na kazi zinazo fanywa na binadamu kupitia ushawishi wa kidini.

Tukizitizama kazi za sanaa za mwanadamu ambazo kwa njia mbalimbali hazibebi ile dhana ya dini bado utamuona binadamu ni mgeni katika mazingira haya, na siku zote anajaribu kutafuta ni wapi aliko tokea.

Kulingana na sayansi mwanadamu si chochote zaidi ya mnyama aliye pewa akili. Lakini kwa mnajibu wa dini, mwanadamu ni mnyama aliye pewa utu.

Materilist siku zote wana yaelekeza macho yetu katika vitu vinavyo onekana, mkono siyo tu kwamba ni kiungo, bali ni zao la kazi zake. Maendeleo ya mwanadamu kwa upande wa materilist ni yale maendeleo ya kibaiolojia na siyo kiroho. 

Kwa vile materilist wameshaikana roho tangu mwanzo, basi eidha watajitia opofu pale wanapo ona matokeo na ‘ukuaji’ wa kiroho au hawaoni kabisa, na hivyo binadamu wanaye mwona ni ‘mnyama’ aliye pewa akili ambayo itamuwezesha kufanya ‘natural selection,’ na siyo binadamu aliye pewa ‘utu’ unao mtofautisha yeye na mnyama.

Lakini binadamu kumshusha na kuiweka thamani yake kwenye kazi anayoifanya, au hitimisho lake kuwa ni ‘maendeleo’ ya kibaiolojia, hapana shaka tu tutakuwa tumezifanyia dhulma nafsi zetu na kuzifanyia dhulma akili zetu pia. 

Kama ambavyo kazi ya sanaa haiwezi kushushwa thamani yake na kuwekwa kwenye rangi zilizo tumika kuichora kazi hiyo, au shairi thamani yake ikashushwa ikawa ni vina vyake.Vitu hivi viwili yaani uchoraji na shairi ni moja kati ya kazi za sanaa, kama ilivyo sanaa na ndivyo zilivyo kazi hizi thamani yake haipo kwenye ‘vitu’ vilivyo tumika kuitengeneza kazi hiyo, bali kwenye ‘moyo.’ kwenye ‘roho,’ ya kazi yenyewe ambayo inacho kieleza hakiwezi kamwe kikaeleweka kwenye ulimwengu wa ‘materialisim,’ roho ya kazi ya sanaa inazungumzia ulimwengu mwingine kabisa.

Kama ilivyo nyumba ya ibada, itakuwa imejengwa na idadi kadhaa ya matofali au mawe au chochote kile cha kuifanya nyumba hii isimame. Lakini ‘vitu’ vilivyo tumika kujenga msikiti siyo ukweli wa mwisho kuhusiana na msikiti. Hauwezi kuulinganisha msikiti na kambi ya jeshi, ingawa yote ni majengo. Materilist wanamuelezea binadamu kwa kumuangalia maumbile yake ya nje. Binadamu ni kama shairi, msikiti au kazi ya sanaa ambayo haiwezi kuelezewa na kuthaminishwa kwenye vitu vilivyo tumika kuitengeneza. Mtu ni zaidi ya kile ambacho sayansi zote kwa pamoja zitakavyo weza kumuelezea.[3]

Kutokana na nadharia ya Darwin ni kwamba, babu wa binadamu wa kale ndiye alikuwa mnyama aliye endelea zaidi. Lakini hata hivyo tunapo mlinganisha babu huyo wa kale na mnyama aliye endelea zaidi, tunakuta kuna tofauti kubwa baina yao. Kwa upande mmoja tunaona kundi la wanyama wanao tafuta chakula na wanao pambana na mazingira yanayo wazunguka ili waweze kuendelea kuishi;

Kwa upande mwingine tunamuona binadamu akishughulishwa na vitu vingine zaidi ya kutafuta chakula na kupambana na mazingira yake, tunamuona binadamu aliyezungukwa na ibada za ajabu ajabu, anaye changanywa na imani zisizo eleweka, anaye chora nembo za ajabu ajabu na kuzi thaminisha juu ya kila kitu. Utofauti huu hauwezi kuelezea kwenye hatua za maendeleo ya kimwili pekee ambazo Darwin kaziita, eveolution.[4]

Kanuni ya wanyama, au silka ya mnyama ni mfano mzuri kabisa katika usahihi wa utendaji na tija iliyo bora kulingana na aina ya kitendo au tabia ya mnyama. Wanyama wana utashi ulio bora sana kwenye muda, kumshinda binadamu mwenyewe. Mathalani wanyama huacha kula saa moja kabla ya jua kuzama, nyuki huzifanya kazi zao kwa kiwango cha juu mno cha usahihi. Maarifa na akili yana mashiko zaidi kwenye ulimwengu wa wanyama kushinda ule wa binadamu.

“Mbali na tabia nyingi ambazo tunaweza kusema wanyama waziigiza, au wanafanya bila hiari, lakini bado katika matendo hayo kuna mengi ambayo hatutosita kuyapa sifa ya kiintelejinsia. Katika hili kama pale mnyama anapo tumia zana duni kufanikisha jambo fulani au kutumia zana iliyo tengenezwa na binadamu mwenyewe...”[5]


Sokwe anatumia fimbo kuzifikia ndizi, dubu anatumia jiwe kushambulia windo lake. Kuna ushahidi wa kutosha wa namna sokwe, nyuki wanavyo kusanya taarifa baina yao na kuzisambaza katika kile ambacho binadamu anakiita mawasiliano.[6]

Kwa ujumla, hakuna ambacho kinapatikana kwa binadamu ambacho hatuwezi kukiona kwa wanyama na wadudu, kuna njia moja au zaidi ya mawasiliano, maarifa, ustaarabu, Paka kabla ya kujisaidia huchimba kishimo kadogo, na anapo maliza hufukia kinyesi chake, kisha hunusa kuhakikisha harufu haitoki au imekwisha, ndipo huondoka, kunguru ndiye aliye mfundisha binadamu namna ya kuzika maiti wake.[7] Kuna mipango ya kiuchumi kwa viumbe wengine, mipango ya kijamii na mengine mengi.

Lakini huwezi ukakuta katika ulimwengu wa wanyama, hata kwa kulazimisha au katika hali iliyo duni, kile kinacho itwa dini, maajabu, sanaa, imani, ibada na mengineyo mfano wa hayo, ambayo utayakuata kwa binadamu wa kale na wa sasa. Mnyama anapo kwenda kuwinda, hufanya kile ambacho kwenye jicho la mwanadamu litaonekana ni kitendo cha kutumia akili, au kitendo cha kufikiria, atanyata, atakwenda chinichini asionekane, atashika windo lake sehemu maalum. 

Lakini si binadamu, ambaye kwanza atafanya makafara kabla ya kwenda kuwinda, mke wake nyumbani naye kuna ambayo atatakiwa kuyafanya ili kubariki kazi yake, na asipo yafanya mumewe anaweza kuwa matatani. 

Nyuki ni mfano mzuri wa jamii na mfano mzuri wa jamii inayo fanya kazi kwa kushirikiana, lakini nyuki hawana huruma kwa mwana jamii mwenzao ambaye ni mdhaifu na hashiriki kazi na wenzake kutokana na udhaifu huo. 

Mdhaifu huyu hutolewa nje ya mzinga, akajifie huko. Hapa nyuki wanakosa kitu, hali au tabia tunayoiita ni ‘utu’; tabia ambayo inaambatana na kuwalinda madhaifu na wale wasio jiweza, tabia ya kuwapatia wengine haki ya kuishi na kuwatambua na mengineyo.

Kwa wanyama vitu ni vile vinavyo onekana, havina maana nyingine, kwa binadamu vitu vina maana elfu moja zaidi, na maana za ndani za vitu hivyo ambazo wanyama wengine hawatambui. kwa binadamu maana hizo zina uzito zaidi kushinda maumbile ya nje ya kitu chenyewe. Wakati wanyama wengine wataona pango au mti kubwa kama sehemu ya hifadhi, binadamu ataona ni sehemu ya kutolea makafara na nyumba ya ibada. 

Ni wapi binadamu anazitoa maana hizi. Kwa nini binadamu ambaye asili yake kama alivyoielezea Darwin kuwa ni moja sawa na viumbe wengine achukue njia tofauti sana na viumbe wengine katika masuala yake ya kijamii na yasiyo ya kijamii. Nadhari ya mungu binadamu kaitolea wapi, nadharia ya kafara kaitolea wapi, nadharia ya kujitolea kwa ajili ya mwingine na kuacha shida zake kukidhi haja za wengine anaitolea wapi, mbona hatuioni hii kwa wanyama wenzake? ... Darwin tusaidie tafadhali.

Mambo yake na tabia zake hizi, zinamfanya binadamu aonekane ni mgeni kwenye dunia hii kushinda wanyama wenzake. Kwanini anaamini juu ya nyota, ulimwengu ambao hata tembo wala bluu Whales baharini hautambui. Hisia zake kubwa ni zile za woga, lakini siyo ule waoga wa kibaiolojia ambao wanyama wengine huuhisi, ni woga wa kiroho. Woga wa kutokuridhika, woga wa maajabu yanayo mzunguka, woga wa ibada zake, woga wa matokeo ya vitendo vyake. Woga ulio zalisha majina ya vitu kama ‘kitukufu,’ ‘halali,’ ‘siyo halali,’ ‘haramu,’ ‘kibaya,’ ‘kizuri,’ nakadhalika. Lakini haya yote yanatoka wapi ikiwa hapa ni kwetu na ndiko asili yetu. Hapana binadamu ni kama mgeni kwenye uso huu wa dunia, ni kama anayo asili nyingine, asili ya kiroho.

Kwanini mwanadamu kisaikolojia haridhiki, pamoja na kuwa atamiliki kila kitu anacho kitaka. Kwanini pesa siyo kila kitu, atakuwa na nyumba, magari, viwanja, biashara kubwa, kubwa, familia kubwa, na mengine na mengine, lakini bado shimo lake la saikolojia halitotoshwa kujazwa na vitu hivyo? Kwa nini kujiua na magonjwa ya akili vimeongezeka kila pale, hali nzuri ya maisha ilipo ongezeka na elimu ilipo ongezeka? Kwanini maendeleo ya kivitu hayamaanishi maendeleo ya kiutu?



Tunapo mtazama binadamu wa Darwin ni kwamba, maendeleo yake ni maendeleo ya kibaiolojia ambayo yatatokana na juhudi zake za kupambana na mazingira yake, mkono wake utakuwa ni bora zaidi kadiri atakavyo itumia katika kazi zake. Misuli yake, akili na mengineyo kadiri yatakavyo tumika ndivyo ukuaji na nafasi ya kuyashinda mazingira yake itakavyo ongezeka.

Kwa njia hiyo basi matatizo ambayo   yana mwaandama binadamu wa leo tusinge tegemea kuyaona. Binadamu wa leo kapiga hatua kubwa sana ya kivitu na mali kutokana na kuutumia vyema mwili wake au viungo vya mwili wake, kutokana na Darwin huyu ndiye, ‘Perfect Man.’ Lakini mbona maendeleo hayo hayana sura ya utu, mbona matatizo yamezidi kila hatua moja ya maendeleo ya kivitu ilipofikiwa. Kwanini huu ulimwengu wa vitu unapingana na sehemu fulani ya mwanadamu huyu? Ni kipi kinacho kosekana katika hii picha kubwa iliyo pambwa kwa rangi za ‘kivitu’ za aina kwa aina?

Binadamu tunafanya mengi kufikia malengo yetu ya kivitu. Tunajinyima, tuna wanyima wengine, tunavunja udugu, tunauwa na kumwaga damu za wengine, tunafanya mambo kadha wa kadha ya hatari na yasiyo na utu ili kuweza kuzalisha mabilioni na mabilioni na mabilioni ya fedha. Kukusanya utajiri kwa binadamu wa Darwin hilo linaonekana kama lengo kuu la maisha yake, hilo ndiyo kila kitu, na binadamu inabidi ajitoe muhanga kwelikweli kufikia hatua hiyo, atauwa, atadhulumu, atafanya hiana, ilimradi atapitia katika kila aina ya uharibifu kukamilisha hilo. Lakini baada ya kukusanya matrilioni ya utajiri ghafla siku moja anakufa.
WHY DEATH, AFTER ALL THE SACRIFICE YOU HAVE MADE????

Kifo ni nini? Kwanini mtu huyu afe, kwa nini aache kila kile ambacho alitolea jasho lake kwa bidii zake zote, aliacha usingizi wake, godoro lake zuri, mke wake mzuri na kwenda kuuchuma huo utajiri, alidhulumu, aliuwa, alimwaga damu na mengine kama hayo alifanya kuupata huo utajiri, lakini ndani ya sekunde kadhaa, kama mshumaa ambao hautowashwa tena alitoweka na kuyaacha yote hayo.Thamani ya mali hizo iko wapi mbele ya kifo. Kwanini basi asiishi milele au walau mpaka mali aliyo yachuma yamalizike.

Kama kukusanya utajiri na mali ndiyo lengo kuu kama Darwin anavyo tuelekeza, na binadamu huyu kayapitia makubwa kuukusanya huo utajiri, mwishowe kafanikisha, iweje basi anakufa anauacha? Tayari kesha timiza lengo, inamaana malipo ya kutimiza lengo lake ni mauti? Au kuna ambacho Darwin hatuambii, au kuna ambacho Darwin katika nadharia yake amekiruka bila kutueleza. Huyu binadamu alistahiki abaki atumie mali yake ambayo ndiyo lilikuwa lengo kuu la maisha yake, lakini sasa anaiacha na anakwenda ambako hata hatupajui. 

Lakini hata yule ambaye ameshindwa kulifikia lengo hilo la Darwin, yaani masikini naye anakufa, sasa tofauti yao ni ipi kati ya yule alitekeleza lengo na kuwa tajiri na yule aliyeshindwa na kuwa ni masikini?

Hivi Darwin anatuambia ni kitu gani kinacho fuata baada ya binadamu kufa. Lakini kwanza kwa kuanzia kifo ni nini? Darwin hawezi kutuambia kifo ni nini kwa vile binadamu wa Darwini anacho kiwiliwili tu na hana roho. Ndiyo maana maendeleo ya binadamu huyu yanapimwa kivitu kama hatua ya maendeleo ya kiwiliwili hicho na siyo kiroho. 

Kama hana roho unadhani Darwin ataanzia wapi kuelezea maana ya kifo. Binadamu anakwenda wapi baada ya mauti. Ingawa Darwin anajaribu kutushawishi kuwa hatuna roho na bila kutoa ushahidi wowote, hatuwezi kuyachukua maneno yake kama ukweli wa msingi dhidi ya kile ambacho kiko wazi kama nuru ya jua katika uhakika wa kuwepo kwa roho.

Darwin anataka tukatae uwepo wa MUNGU, lakini kwanza anatufundisha kukata juu ya kuwepo kwa roho na juu ya kuwepo kwa kifo kwa sababu ni roho ndiyo inayo mtaambua MUNGU na siyo mwili wa Darwin, hivyo tukiweza kuikana roho kuwa haipo moja kwa moja kifo kitakuwa hakipo, na moja kwa moja maana ya uwajibikaji wa matendo yetu itafutika, na MUNGU naye atafutika pamoja na hayo katika maisha yetu.

Lakini ni vipi tunaweza kuikana roho/nafsi yetu. Mpaka leo sayansi haina tafsiri inayo eleweka juu ya kifo, na vipi wataipata tafsiri yake ikiwa kwenye kamusi zao hakuna ‘roho’ wala ‘kifo’ chenyewe.
Binadamu anayo roho, hayawani wengine na viumbe wengine wanayo roho pia, kwani hii ndiyo hasa sababu tunatumia neno ‘viumbe/kiumbe’ yaani kilicho umbwa na chenye uhai.

Lakini binadamu anayo, ‘uhuru’ ambao akiutumia vyema roho yake hiyo itakuwa na hadhi bora kushinda ile ya Malaika, na anapo utumia ambavyo sivyo atakuwa ni duni kuwashinda hayawani wengine. Roho/Nafsi ndiyo yenye silka ya kumtambua MUUMBA. Mbali na mwili roho/nafsi ndiyo yenye mamlaka juu ya mwili na yenye kuwajibika juu ya uhuru alio milikishwa mwanadamu na majini juu ya viumbe vyote.

Katika mafunzo ya Kiislamu tunajifunza kuwa siku ambayo MUUMBA atawasimamisha viumbe vyake na kutoa hukumu, siku hiyo viungo vya mwanadamu vitatoa ushahidi juu ya roho/nafsi yake kuwa ilifanya kadha wa kadha. Hii inatuthibitishia kuwa, roho/nafsi na mwili ni vitu viwili tofauti, na siyo mwili ambao Darwin kautilia msisitizo wenye jukumu la kumtambua MUUMBA, bali ni roho/nafsi ndiyo yenye jukumu hilo na mwili wake ni zana itakayo muwezesha kuutambua ukweli huo, ingawa roho/nafsi inayo wazo, dhana, silka juu ya kuwepo kwa MUUMBA, itautumia mwili wake na vile vinavyo mzunguka kuthibitisha hilo, au kutumia kiburi chake kulikataa hilo.

Kwani nafsi/roho yenyewe kuwepo ndani ya mwili, na kufikishwa hapa duniani, sehemu ngeni kwake, lakini inayo ‘fahamika’ zaidi na mwili wake ni dalili tosha kuwa yenyewe siyo ya hapa, na daima binadamu wa zama zote amekuwa akijiuliza swali moja, asili yake ni wapi, swali hili haliulizwi na ubongo, bali nafsi/roho, kinacho fanya ubongo kama sehemu ya mwili ni kuisaidia nafsi kuutambua au kuuthibitisha ukweli huo.

Mathalani imetokea mahala nyumba inaungua moto, pakasikika sauti ya kichanga ndani ya nyumba inayo waka moto, akatokea mtu mmoja akavua shati lake na kujitosa ndani ya nyumba inayo waka moto kwa nia ya kukaokoa kachanga hako. Baada ya muda ‘shujaa’ huyo anatoka akiwa na kachanga hako mkononi, lakini tayari kameshakufa. Hakufanikisha lengo la kuokoa maisha ya kachanga hako, je ni nini thamani ya kitendo hicho cha kishujaa ikiwa mtoto alikufa?

Kwanini tunakiita ni kitendo cha kishujaa, wakati kichanga kimetolewa kikiwa kimekufa? Kiungo cha mwili kinacho itwa ubongo kitachora picha ya kushindwa kwa mpango mzima, kuto kufanikiwa kwa mwokoaji ndiko kunako onekana kwenye kiungo kinacho itwa ubongo, lakini yule mwenye dhamana ya ubongo huo, yaani roho/nafsi kwake thamani haiko kwenye matokeo, kwake mwokoaji ni shujaa. 

Jina au sifa ya ushujaa haitafsiriwi na ubongo bali nafsi yenyewe, hii ndiyo maana pamoja na kwamba tendo halikufanikiwa, bado mtu huyu aliye jitolea maisha yake kuokoa maisha ya kichanga ataonekana ni shujaa.

Ubongo hauwezi kutafsiri maana ya ‘shujaa’ ila nafsi/roho ambako kitendo cha kuokoa maisha ya kitoto ndiko kilicho pewa jina la shujaa. Hata tunapo kataa juu ya kuwepo kwa roho/nafsi bado bila kujijua au kwa kushindwa na namna ni mengi ambayo tunashindwa kuyaelewa kwa kutumia ‘akili’ na kuyarudisha kwenye asili yake, nayo ni roho/nafsi. Kwa mnasaba wa roho/nafsi kitendo cha kuokoa maisha ya kichanga kilisha fanyika, hata kabla ya mwokoaji kuingia ndani ya nyumba inayo waka moto.

Kanuni hii muhimu inayo fahamika kwenye roho/nafsi zaidi kuliko kwenye ubongo imeelezewa vyama pia kwenye mafunzo ya Kiislamu, pale mtume Muhammad (s.a.w) aliposema kuwaambia wafuasi wake;
“Kila kitendo kinalipwa kutokana na nia ...” [8]

Kutokana na mafunzo ya hadithi hii ni kwamba, endapo mtu alinuia kwenda kumsaidia mtu mwingine kwa lolote lile jema, lakini akafika na kukuta muhusika shida yake ilishakwisha, hivyo hahitaji tema msaada wowote, MOLA wake mtu huyu anaandikiwa kuwa alishamsaidia muhusika na atandikiwa thawabu moja kama mtu aliyetekeleza wema huo kwa ukamilifu.

Katika mafunzo ya Kiislamu pale ambapo maji yame kosekana kwa ajili ya Mwisilamu achukue udhu, au anayo matatizo ambayo kwa yeye kushika maji kutamletea madhara zaidi, hana budi Mwisilamu huyo kufanya Tayamamu. Yaani Mwislamu atachukua mchanga, kisha atapiga viganja vya mikono yake juu ya mchanga huo na kisha kuikung’uta mikono yake, vumbi lililo bakia kwenye viganja vya mikono yake atalitumia kujipangusia uso wake na mikono yake miwili na hapo atakuwa amejitaaharisha (amejisafisha) tayari kwenda kuswali, tayari kusimama mbele ya MOLA wake. 

Lakini ni namna gani mchanga unaweza kumsafisha mtu, hata Waislamu wengi bado wanakuwa na wasiwasi juu ya tendo hili, lakini lazima wawe na wasiwasi, kwa vile amri ya kutumia mchanga kama njia ya kujisafishia na kama zilivyo amri zingine zote hazikutumwa au haziku amrishwa, akili/ubongo wa binadamu, bali nafsi/roho. Ni mengi kwenye masuala ya dini ambayo akili haiwezi kuyaelewa, kwa vile akili ni zana tu, na nafsi hasa ndiyo inayo lengwa.

Kwenye sheria zetu za kimahakama, mtuhumiwa wa mauwaji anasimama baina ya ‘vizimba’ viwili, eidha kauwa kwa bahati mbaya au kauwa kwa kukusudia. Adhabu ya kuua kwa kukusudia inakuwa ni kali na mara nyingi ni kifo, wakati ile ya kuuwa kwa bahati mbaya inakuwa ni kifungo maalum au faini na wakati mwingine vyote. Lakini tunajuaje kuwa alikusudia au ni bahati mbaya? 

Mara nyingi hakimu hutafuta namna yoyote ile au mazingira yoyote yale yatakayo wezesha kumfahamisha NIA ya muuaji ilikuwa ni ipi. Hapa hakimu hatizami mwili wa mtuhumiwa, bali roho yake. Je roho yake ilikuwa na dhamira ya kufanya kitendo hicho ama la. Kwa sababu kama roho/nafsi ya mtuhumiwa iliisha dhamiria kufanya kitendo hicho, kwa maneno mengine, kama ambavyo roho ya shujaa iliisha kiokoa kichanga kile kabla shujaa hajaingia ndani ya nyumba inayo waka moto, ingawa kichanga kilitoka kikiwa kimeshakufa kwenye mikono yake, ndivyo hivyo, hivyo kuwa roho ya mtuhumiwa iliisha muuwa mhanga wake hata kabla muuaji hajakamilisha tendo hilo. 

Sheria zetu wenyewe zina tuthibitishia kuwa kuna zaidi ya mwili wa binadamu, kuna roho, ambayo inawajibika, kuna roho iliyo pewa dhamana, kuna roho iliyo umbwa, nayo hiyo roho haina budi kumtafuta MUUMBA wake wa haki, na siyo mwili wake wenye jukumu hilo.

Ingekuwa hakuna roho, ni vipi hakimu angeweza kujua kwamba muuaji alikusudia au alifanya bahati mbaya? Ingekuwa hakuna roho ni vipi kitendo cha kutoka na kichanga kilicho kufa kwenye mikono ya mtu aliye weka rehani afya na hata uhai wake kuokoa maisha ya kichanga hicho, kitendo hicho kiitwe ni cha kishujaa? Wapigania uhuru wa nchi zetu, tunawahesabu ni mashujaa, ingawa wamelala chini wamekufa, ushujaa wao uko wapi? Ubongo unaweza kutupa tafsiri ya neno shujaa? Hapana, neno shujaa ni hali inayo jaribu kuelezwa na ubongo wetu kwa msaada wa mazingira yetu, lakini maana yake inafahamika zaidi kwenye nafsi/roho zetu kuliko bongo zetu.

Tofauti na dunia inayo tuzunguka, ambapo wamo matajiri na masikini, wajinga na wenye akili, wenye busara na wapumbavu, wenye elimu na wajinga, wenye nguvu na madhaifu. Hali zote hizi hazielezi maana ya kweli ya nafsi/roho zetu. Dunia yetu ya ndani au kwa maneno mengine nafsi/roho zetu zimejengwa kwa uhuru na usawa ambao hauna mipaka ya kivitu au kiasili.

Ulimwengu wetu wa ndani unajieleza wenyewe kupitia nia zetu na hamu. Kila binadamu anayo maono ya kuishi kwa furaha ndani ya nafsi yake. Mfano watu wengi hawawezi kuondoa uovu, lakini wana chukia uovu na wanaupinga ndani ya nafsi/roho zao na katika msingi huo ndipo inapo patikana maana ya toba. Utu haupo katika vitendo; bali kwenye hamu na nia ya kuishi kwa wema. Siyo ubinadamu kutokuwa mkosaji wala mtenda maovu. Bali kukosea na kutenda maovu, kisha ukatubia ndiyo kuwa binadamu. Mtume Muhamadi (s.a.w) amesema kila binadamu ni mkosaji na aliye M’bora wa wakosaji ni mwenye kutubia. Mwenyewe Mtume (s.a.w) alikuwa akitubia kwa siku mara mia moja ama zaidi, mbali na kuwa MOLA wake alisha muambia kuwa amemsamehe makosa yake yaliyo pita na yatakayo kuja katika maisha yake. Yeye alikuwa ni binadamu na mara kadhaa mwenyewe alilisisitiza hilo kwa wafuasi wake.

Ni vitu vingapi ambavyo tumevifanya na ambavyo hatukuwa tukitaka au penda kuvifanya? Na vipo vingapi ambavyo tuna nia na kutamani kuvifanya lakini bado hatujaweza kuvifanya? Zipo dunia mbili, ile ya kivitu na ile ya kiroho. Nia zetu, hamu zetu, ingawa hatuja zitimiliza katika dunia yetu ya kivitu, zilisha timilika katika dunia yetu ya kiroho, hivyo, hivyo kitendo cha bahati mbaya, kama muuaji aliyeua bila kukusudia, ingawa kitendo kile kimefanyika katika ulimwengu wa kivitu, hakikubaliki na hakija fanyika katika ulimwengu wa kiroho, na sheria zetu za kimahakama zinalitambua hili.

Mahusiano baina ya “hamu” na “kitendo” yana kinzana kama ambavyo mahusiano baina ya mwili na roho yanavyo kinzana. Katika maisha yako ya kila siku utakuwa unasikia watu wakisema na hata wakati mwingine wewe mwenyewe ukisema, “ningependa kufanya, lakini roho yangu inasita ...”

Nia na kitendo, roho na mwili ni dunia mbili tofauti. Moja thamani yake inaonekana kwa macho, nyingine thamani yake imehifadhiwa katika roho/nafsi za watu na ikihusishwa na ulimwengu mwingine kabisa; moto na pepo. Huko ndiko muuaji wa kukusudia ambaye sheria katika ulimwengu wa vitu, imekuwa ni ‘fupi’ mno kiasi haikuweza kumfikia, na shujaa ambaye ametaka kuokoa kichanga kwenye nyumba inayo waka moto hakufanikiwa kukiokoa na kwenye macho ya ubongo akaonekana kushindwa, katika dunia nyingine ya Moto na Pepo vitendo vya hao wawili vinayo malipo yake. 

Katika kila binadamu kuna sehemu ndani, inayo fahamika kama nafsi au roho. Neno hili lugha ya Kiswahili imelichukua kutoka kwenye lugha ya Kiarabu, na tafsiri yake inayo maana pana zaidi na kueleweka zaidi katika lugha hiyo kuliko Kiswahili, lakini juu ya yote neno hilo ndiyo ile nukta ya kati, au neno la mwisho au mstari wa mwisho katika kila kiumbe. Katika lugha yetu hakuna tofauti kati ya nafsi na roho. Nia inayo maana kwenye roho/nafsi, nia inamanisha maamuzi yaliyo kwisha fanywa ndani ya mtu binafsi, siyo kwenye ubongo wala kwenye kiungo chochote kile, bali ndani ya roho yake, ndani ya nafsi yake. Roho/nafsi siyo kiungo bali ... kiumbe. 

Hivyo kitendo ni uthibitisho au uhakikisho au utimilisho wa kile ambacho kilisha amuliwa na kupitishwa ndani ya nafsi/roho. Kitendo hicho kinaweza kwenye dunia ya kivitu, kufanyika au kutokufanyika, lakini katika ulimwengu wa roho, ndani kabisa kwenye nafsi yako kilisha kwisha kufanyika, tena mara moja na tena kitadumu hivyo milele.

Kitendo chochote cha binadamu ambacho hakijafanyika ndani yake kwanza, ni sawa na kitendo cha mashine yeyote ile unayo ifahamu. Mwenye ugonjwa wa akili akiuwa hapatwi na hatia ya kitendo hicho, bali atakwenda kutibiwa kwanza tatizo la akili, kwani kitendo alicho kifanya hakina tofauti na mashine, hakijafanyika ndani yake, bali katika ubongo wake.
Mtu siyo kile anacho kifanya, bali kile anacho tamani kukifanya.[9]

“Naapa kwa jua na mwangaza wake! Na kwa mwezi unapo lifuatia (jua)! Na kwa mchana unapo lidhihirisha! Na kwa usiku unapo lifunika! Na kwa mbingu na kwa Aliye ijenga! Na kwa ardhi na kwa Aliye itaandaza! Na kwa nafsi na kwa Aliye itengeneza! Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake. Hakika amefanikiwa aliye itakasa (hiyo nafsi).Na hakika amekhasirika aliye iviza (hiyo nafsi).(Quran 91:1-10)

Darwin alipo taka kumkataa MUUMBA, kwanza aliikataa nafsi/roho, na sisi tumejaribu kuitafuta nafsi/roho, ingawa kwa uchache, lakini tumeona uthibitisho juu ya kuwapo kwa nafsi/roho. Kukubali kuwepo kwa roho ni kukubali kuwepo au kupatikana kwa kitendo cha uumbaji nako ni kukubali kuwepo kwa  MUUMBA. Tabia na sifa za roho zinatuelekeza kule alipo MUUMBA.

Ikiwa roho zetu zinakiri juu ya kuwepo kwa MUNGU MMOJA WA HAKI. Je ni upi ushahidi ambao roho zetu zinajaribu kutuelekezea ambapo viungo vyetu hasa akili zetu zitusaidie katika kuthibitisha madai yanayo tolewa na roho zetu? Je MUUMBA amejitokeza kukiri dai linalo letwa na roho zetu kuwa yeye ndiye MUUMBA wa ulimwengu huu na vyote vinavyo tuzunguka zikiwemo roho na miili yetu?

HEY ... MTANANGE UNAENDELEA HAPA HAPA ... MPAKA TUFIKE TUNAPOKWENDA ...




[1]Άlija Άli Izetbegovic, Isalm Between Est and West, American Trust Publications.
[2]Ibid
[3]Ibid
[4]Ibid
[5]Henri Bergon:Creative evolution
[6]Konrad Lorenz, King Solomon’s Ring: New Light on animal ways
[7]Quran 5:31
[8]Bukhari kitabu cha kwanza, hadithi nambari 1.
[9]Ibid

1 comment: