Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Thursday, July 21, 2016

NAMTAFUTA MUNGU Ep: 6 (Episode Finale)



Kuna somo la mahesabu katika Quran, ningependa nalo hili tulitupie macho kidogo.

Mahesabu ndiyo lugha ya sayansi, na mahesabu ndiyo lugha moja inayowezwa kuzungumzwa kote ulimwenguni, na ndiyo lugha ambayo haiwezi kuathiriwa na muda. 


Hata hivyo leo tunaufahamu ulimwengu na maajabu yake kwa kutumia kanuni mbalimbali za kimahesabu. Galileo ambaye ameyapa mahesabu haki yake katika tafiti zake, alisema kwamba, mahesabu ndiyo lugha ambayo MUNGU MMOJA ameitumia katika kuutengeneza ulimwengu.

Wanafalsafa kama Pythagoras, alikuwa akidhania kuwa, kanuni ya msingi ya ulimwengu imewekwa katika tarakimu, na wakuhusisha tarakimu na mambo ya kimaajabu na mazingaombwe. Na ni hivi karibuni tu, madai ya kisayansi yamethibitishwa kwa kutumia tarakimu au kwa uwazi zaidi kwa kutumia kanuni za kimahesabu.



Kutoka kwenye ugunduzi wa balbu wa Edson mpaka kwenye magari yaendayo kwa kasi, kutoka kwenye nadharia ya time relativity kutoka kwa Einstein, mpaka nadharia ya gravitationtoka kwa Newton, zote hizi asili yake ni deni walilokopa kutoka kwenye lugha ya ulimwengu, lugha ya kimahesabu. 




Quran nayo kitabu cha MUNGU MMOJA, hakikuacha kuelezea umuhimu wa lugha hii katika usawa na uyakinifu wa ulimwengu ndani ya mahesabu.

“Na kuisoma Qur’an. Na mwenye kuongoka, basi ameongoka kwa faida ya nafsi yake; na aliye potea - basi sema: Hakika mimi ni miongoni mwa waonyaji.”

“Na sema: Alhamdu Lillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Yeye atakuonyesheni Ishara zake, na mtazijua. Na Mola wako Mlezi si mwenye kughafilika na myatendayo.”(Quran 27:92-93)

Aya tuliyoisoma hapo juu, inaelezea kwamba, katika nyakati zijazo MUNGU MMOJA, atazionesha alama zake kwa watu, ili watu wale wenye akili, wenye kufikiri watambue juu ya kuwepo kwa MUNGU MMOJA, na wamuabudu kwa namna ile tu, anayoitaka yeye, kwa namna ile tu aliyo watuma mitume wake wafundishe, na siyo vinginevyo. 



Hili peke yake linatuthibitishia kuwa Muhammad yeye siyo mwandishi wa kitabu hichi, kwani ni namna gani angeweza kuandika vitu ambavyo baada ya milenia moja ndiyo viweze kujulikana? Hata kama angekuwa na maarifa na akili kiasi gani, Muhammad asingeweza hata kwa kujaribu kutabiri kwamba ataonesha miujiza siku zijazo, siku na miaka itakayo fuata baada ya kuondoka kwake. Yeye ni binadam kama binadam wengine, maono, fikra, mitazamo na mipango yake lazima yaathiriwe na nyakati kama ilivyo kwa binadamu mwingine, ni MUNGU MMOJA tu ndiye hawezi kuathiriwa na nyakati, sababu nyakati ni moja kati ya viumbe vyake, naye haathiriwi na viumbe vyake, naye ndiye mwenye nguvu, uwezo, mamlaka na maamuzi ya yasiyo athiriwa na nyakati kama ahadi aliyoitoa kwenye aya niliyo inukuu hapo juu.




Na vipi aweze kutabiri vitu vya baadaye ambavyo kuthibiti kwa vitu hivyo, hata kidogo kusingeweza kumnufaisha yeye kwa chochote, au kumpunguzia dhiki kutoka kwa maadui zake, au kuwanyamazisha maadui zake, kwa vile utimilifu wa utabiri huo ni kwa wakati ujao, ambo si yeye wala maadui zake watakao kuwepo kuthibitisha ukweli wa maneno yake. 


Mbali na hayo ulimwengu wa Kiislamu wenyewe, haukuwa ukifahamu vingi katika hii miujiza ya Quran mpaka hivi karibuni tu. Hivyo wakati mtume Muhammad Rehma na Amani ziwe juu yake alipokuwapo katika zama zake, maisha yake, na yale aliyo yafanya na hii Quran vyote vilikuwa ni miujiza kwa umma wake, baada ya kuondoka, harufu na ladha ya miujiza hakuondoka na yeye, zama hadi zama, kwa nyakati tofauti nuru ya Quran imekuwa ikiendelea kuwamulikia watu, kwa nuru ya kweli, kwenye matukio, maumbile, tabia na sifa za ulimwengu na vile vilivyomo na ikielekeza ni nani mfanyaji wa kazi hii, kwa lugha nyepesi sana, lakini iliyo ngumu mno kuiigiza. Quran ni muujiza na kama wanavyo sema, time will tell.



Tumeona kuwa Quran yenyewe imetoa changamoto kwa wale ambao wanaoipinga na kuikana, kwamba ikiwa wanadai kuwa hii ni kazi ya Muhammadi, yaani ni maneno yake, basi waandike japo sura kumi tu mfano wake na wailete kwa umma tuione. Lakini Quran ikapunguza makali ya changamoto, ikawataka wafanye basi japo sura moja tu, lakini hakuna aliyefanya, ikawaambia tena basi changanyikeni na majini musaidiane katika hili, na ikawathibitishia kuwa hata wakichanganyika juu ya hili hawato weza, na kweli mpaka leo binadamu wanashirikiana na majini kwenye mambo mbalimbali, lakini kwenye hili la kutengeneza japo sura moja tu, bado hawajaweza.



Hii changamoto peke yake inatosha kukifanya kitabu hiki kuwa ni muujiza. Kama ni maneno yake Muhammad ni wapi alipata hiyo nguvu na ujasiri wa kuipa changamoto dunia nzima, kwa zama zote, kwa watu wote na majini na mwishowe washindwe changamoto hiyo? Mbona hakuna aliyekuja na walau hiyo sura moja na sasa ni zaidi ya miaka 1400 tangu hiyo Quran ilipo sema hivyo.

Swali la kujiuliza kwa nini Quran, kitabu chenye sura 114, kilicho letwa kwa watu karne ya saba na mchunga mbuzi asiye fahamu kusoma wala kuandika, kiwe ni fumbo kwa ulimwengu na watu wa zama zote mpaka majini? Kina nini maalum kitabu hichi?

Kitu cha kwanza kabisa kwenye Quran ni mahesabu. Kila sura kwenye kitabu hichi imepangwa na kufungamanisha kimahesabu kwa namba maalum, na maneno yaliyo tumika nayo mpangilio na idadi yake umefungamanisha kimahesabu, kiasi kwamba ukiondoa neno moja au ukalizidisha au ukaondoa sura nzima, itakuwa ni sawa na kujaribu kutatua tatizo la kimahesabu kwa fomula isiyo kuwa yake. Kila aina ya hesabu inayo fomula/kanuni yake ya kuweza kuitatua, unapoingiza hesabu kwenye kanuni isiyo yake, hesabu hiyo inakataliwa na kanuni husika. 

Hivyo unapo toa herufi moja au kuizidisha kwenye kitabu hichi, moja kwa moja unauvuruga mfumo wote ulio tumika kuandikia kitabu hicho, mpangilio mzima unaporomoka na mkononi utajikuta unacho kitabu kingine, lakini siyo Quran. Katika lugha ya kigeni tunasema Quran imekuwa coded, ili uweze kupunguza au kuongeza chochote, kwanza uivunje code yake iliyo tumika, kitu ambacho kitapelekea kuivuruga Quran yote.



Hivyo unaweza kuongeza kitu au kupunguza kwenye kitabu hiki, lakini lazima ujue hicho utakachokiongeza au kukipunguza utabaki nacho wewe mwenyewe, na utakuwa unaidanganya nafsi yako na hao, walio kubali kurubunika, lakini Quran yenyewe itabakia vile, vile kwa vile utakuwa hujaweza kuivunja ile code yake. Utaweza kuandika msahafu wako kama walivyo fanya baadhi ya watu, utaweza kuongeza baadhi ya sura kama walivyo fanya baadhi ya watu, lakini vyote hivyo vitakapo zamishwa kwenye Quran vitakataliwa na Quran yenyewe. 

Yaani haihitaji watu, waumini au Waislam waseme kuwa hayo hayakuwepo yameongezwa, aihitaji hilo. Hata kama watu wote watakuja na Quran ya kughushi na kusema ndiyo ya ukweli, na majini wote wakaikubali, bado Quran yenyewe, itaikataa hiyo Quran ya kughushi kwa nafsi yake. Yaani Quran inajilinda yenyewe kwa kutumia code iliyo tumika kukiandika kitabu hichi, unapaswa kuivunja hiyo code, kabla ya kuivunja hiyo Quran, unapaswa kuivunja hiyo code, kabla ya kuighushi hiyo Quran, inakupasa ughushi hiyo code yake, na hicho ni kichekesho sababu hakuna code ya kughushi, na kwa code hiyo Quran inajilinda yenyewe hata kama dunia nzima, ikija na kitabu kingine na kusema ndiyo Quran.

Hivyo kughushi hii Quran kuko kwa namna mbili, eidha waandike kitabu kingine mbali kabisa na Quran, kisha wakiite Quran au waongeze na kupunguza chochote katika Quran.

Njia zote mbili ni ngumu na haziwezekani. Kuandika kitabu kingine mbali na kisha ukiite ni Quran, mwandishi atahitajiwa kati ya mengi asiwe mwenye kuathiriwa na kitu tunacho kiita muda, yaani wakati uliopita, wakati uliopo na wakati ujao visiwe na athari hiyo ya kinyakati kwa mwandishi, sifa ambayo tunajua hakuna kiumbe chochote chenye ujuzi huo, si majini wala binadamu. 



Hivyo basi hiyo kazi haitoweza kuhimili changamoto za muda kwa vile mwandishi wake, eidha hana ujuzi wa kutosha kwenye kile kinacho itwa wakati ujao, au uliopita au uliopo. Msomaji makini anaweza kuona ni aina gani nyingine ya ugumu ambao unawafanya mpaka leo washindwe kuja na walau sura moja tu. Njia ya pili ya kughushi ambayo ni kuongeza au kupunguza chochote kwenye Quran, inakumbana na kikwazo kimoja kikubwa sana, nacho ni code ya Quran.

Jinsi kilivyo kitabu hichi ni kuwa kila sura sehemu ilipo inafungamana kimahesabu na sura nyingine eidha iliyo mbele au nyuma yake, kila neno nalo linafungamana na neno jingine kama hilo na kila herufi inafungamana na herufi nyingine zilizomo humo, na vyote hivyo vinafungamana na code ya Quran ambayo ni nambari 19. Hii inamaanisha nini basi?



 Ni kwamba, endapo utaichomoa au kuiongeza herufi, neno, sura moja, itakubidi ubadilishe kila herufi au neno au sura ili hicho ulichokiweka au kukitoa kiweze kuingia kwenye code ya Quran. Kwa vile kila herufi, neno, sura inafungamana na nyingine, utakapoigusa moja, ni kwamba code haitakuwa sawa mpaka uiguse kila herufi katika Quran, hivyo ukigusa moja, nyingine iliyo fungamana nayo inadondoka, na hiyo iliyo dondoka itakuwa imefungamana na nyingine ambayo hata haukuwa na mpango wa kuigusa nayo itadondoka, na nyingine na nyingine, mwisho wa siku utajikuta inakubidi uiandike Quran yote upya, kwa vile lengo lako ni kutaka ikae ndani ya code nambari 19, nahofia utakacho kiandika kitakuwa hakisomeki, lakini kama utamaliza kukiandika kwani kunayo uwezekano mkubwa ukawa mwendawazimu, kwa sababu kila herufi, neno, sura unayoigusa inafyetuka, na inapo fyetuka inaifyatua nyingine na iliyo fyatuliwa nayo inaifyatua nyingine, na nyingine na nyingine, je ni muda gani utakuchukua kuzipanga hizi ili zikae kwenye code nambari 19 kabla haujawa mwendawazimu?



Wale wanao dai kuwa hii Quran tuliyo nayo imepunguzwa basi, waitizame kauli yao upya ama la, wailete hiyo sura wanao dai kuwa wanayo, au huo msahafu walio nao na kisha utumbukizwe kwenye code hii ya Quran na tuone ni majibu gani yatapatikana. Na ikiwa hawawezi kufanya hivyo, basi na tuache kibri, na tuache kumzushia MUNGU MMOJA na Mtume wake Rehma na Amani zimshukie, na tuogope adhabu zake kwani adhabu yake ni kali na wameandaliwa makafiri.



Katika Quran neno ‘siku’ kwa Kiarabu (yewm) limetumika mara 365. Idadi hiyo si kwamba tu inathibitisha idadi ya masiku katika kalenda, lakini pia inaonesha mahusiano baina ya kinyota baina ya dunia yetu na jua. Pale dunia yetu inapo maliza kulizunguka jua, inakuwa imefanya hivyo mara 365, yaani zimepita siku 365 tangu dunia ilipo anza kufanya hivyo kwenye nukta yake ya kwanza. Hivyo utaona neno ‘siku’ limetajwa mara 365, sawa na idadi ya siku ambazo dunia yetu inazitumia kulizunguka jua.




Neno
Idadi ambayo neno hilo limetumika ndani ya Quran
Siku
365
Idadi ya siku ambazo Dunia inatumia kulizunguka jua
365


     Quran hiyo, hiyo pia imetumia neno siku lakini kwa upande wa wingi, yaani masiku, katika lugha ya Kiarabu (eyyam,yewmeyn). Neno ‘masiku’ kwenye Quran limetumika mara 30. Nambari hii au idadi hii inawakilisha masiku 30 ya mwezi. Kwenye kalenda ya Jua mwezi huwa na masiku 30 au 31, wakati kwenye kalenda ya mwezi huwa na masiku 29 au 30. Hivyo idadi ya thelathini ni namba ya kati na kati baina ya kalenda hizi mbili. Unaichukua mwezi masiku 29.53 tangu kuandama mara ya kwanza mpaka kupotea na kuja kuandama tena, kama mwezi mpya, katika mahesabu kuna kitu tunacho kiita makadirio, hivyo tunapo ikadiria 29.53 tunapata 30, kama ambavyo ilivyo kwa jua ambapo dunia yetu hutumia siku 365.25 ambayo tukiikadiria, tunapata 365.


Neno
Idadi ambayo neno hilo limetumika ndani ya Quran
Masiku
30
Idadi ya Masiku katika mwezi
30


     Neno ‘mwezi’ (Qamar) pamoja na yale yanayo husiana na satelaiti hii, yametumika mara 27 kwenye Quran. Idadi hii ya 27 ni sawa na idadi ya masiku ambayo ‘mwezi’ kama satelaiti inayo yatumia kukamilisha mzunguko wake. Hapa ni kabla hauja onekana tena, yaani ndani ya siku 27, mwezi huwa umeshamaliza mzunguko wake, lakini mpaka tuje kuona kwa jicho itahitajika siku moja au mbili zaidi, hivyo basi, hapa Quran inazivuta fikra zetu kwenye masiku yale tu ambayo mwezi unakamilisha mzunguko wake kabla huja andama tena na kuwa mwezi mpya, nayo ni masiku 27. Hivyo hapa neno mwezi kama satelaiti limefungamana kimahesabu kwa idadi ya siku zake inazo zitumia kukamilisha mzunguko wake, hivyo huwezi kuliongeza, wala kulipunguza neno hili kama ambavyo huwezi kupunguza wala kuongeza neno siku au masiku kama tulivyo ona hapo juu, kwani nayo yamefungamana kimahesabu kwa idadi maalum.
Neno
Idadi ambayo neno hilo limetumika ndani ya Quran
Mwezi kama satelaiti
27
Muda ambao mwezi unatumia kukamilisha mzunguko wakekabla haujaonekana tena kwa macho.
27


     Mzunguko wa dunia kulizunguka jua ni siku 365, wakati mizunguko 12 ya mwezi kulizunguka jua ni miezi 12. Quran inasema kunayo miezi 12 kwenye mwaka, Quran 9:36. Kwa upande mwingine Quran imetumia neno ‘mwezi’ (shehr) mara 12 tu, kudhihirisha kuwa kunayo miezi 12 kwenye mwaka.

Neno
Idadi ambayo neno hilo limetumika ndani ya Quran
Mwezi
12
Idadi ya miezi au idadi ya miezi inayo patikana kwa kulizunguka jua kwa mwaka.
12

     Neno ‘bahari’ (al-bahr) limetumika mara 32 kwenye Quran, neno hili ‘al-bahr’ linatumika pia kumaanisha mito na maziwa. Na neno ‘aridhi’ (al-berr) limetumika mara 12 kwenye Quran. Uso wa dunia ni kilometa za mraba milioni 510. Inakadiriwa kuwa takribani kilometa za mraba milioni 360 ni mito, maziwa, bahari na kadhalika, halafu takribani kilometa za mraba milioni 15 ni barafu. Kama tukizitoa hizo kilometa za mraba milioni 15, aridhi itabakiwa na kilometa za mraba milioni 135. Tutakapo tafuta uwiano baina ya haya maneno mawili ‘aridhi’ na ‘bahari’ kwenye Quran ni 12/32 = 0.375. Na uwiano baina ya nchi kavu na sehemu za maji kwenye uso wetu wa dunia ni milioni 135/360 kilometa za mraba ambayo ni sawa na 0.375. Hapa maneno haya mawili yamefungamanishwa na mazingira halisi ya ulimwengu.

Neno
Idadi ambayo neno hilo limetumika ndani ya Quran
Uwiano wa maneno hayo kama yalivyo tumika kwenye Quran
Aridhi
12
12/23 = 0.375
Bahari
23




Neno
Idadi ya kilometa za mraba kwa maeneo hayo mawili katika uso wa dunia
Uwiano baina ya maeneo hayo mawili kwenye uso wa dunia
Aridhi ukitoa maeneo yenye barafu
Kilometa za mraba milioni 135
135/360 = 0.375
Bahari
Kilometa za mraba milioni 360



Hivyo utaona Quran, namna ilivyo fungamanisha, hapa tunaona maneno mawili tu yahusiayo bahari na nchi kavu yalivyo fungamanisha na mazingira halisi ya dunia, hivyo utakapo iondoa sura ambayo imetaja moja katika maneno hayo, moja kwa moja utaharibu uwiano huo, au ukazidisha kitu ambacho ndani yake yatakuwepo maneno hayo, moja kwa moja uwiano huo utatoweka., na kwa kupitia mazingira halisi, kitabu chako hicho kitaonekana ni kile cha kughushi.

     Sura ya 18, ambamo ndani yake kumeelezewa hadithi ya watu wa pangoni, hadithi ambayo Muhammad (s.a.w) alipo kuja kwa watu kuwapa ujumbe wa MUNGU MMOJA, katika moja ya majaribu waliyo mpa ni kutaka Muhammad awaelezee hadithi ya watu wa pangoni. 

Hadithi hii ilikuwa ikiwahusu vijana ambao walimuamini mtume  Issa, (Yesu) Rehma na Amani ziwe juu yake, lakini baada ya Issa (Yesu) Rehma na Amani ziwe juu yake, kupaishwa mbinguni na utawala wa Roma kuanza kuwanyanyasa wafuasi walio mfuata mtume Issa (Yesu) Rehma na Amani ziwe juu yake, ili waweze kuachana na dini yao na mafundisho ya MUNGU MMOJA, Vijana hawa katika kutafuta hifadhi walikimbilia katika pango kujinusuru na walipo kuwa huko pangoni MOLA wao akawajaalia kulala, na walilala kwa miaka 309. Vijana hawa walipo amka kutoka kwenye usingizi wao, hawakujua ni muda gani walilala, walidhani wamelala siku moja au sehemu ya siku. 

Iliwabidi kumtuma mmoja wao mjini kwenda kuwatafutia chochote wale kutokana na njaa waliyo kuwa wakisikia, aliyetumwa alipofika mjini alikuta mji umebadilika, dini ambayo mwanzo ilikuwa imepingwa na kuwafanya wao wakimbie waliikuta ndiyo dini ya serikali, lakini waliikuta dini hii tayari imeshabadilishwa vibaya sana, upagani umeingizwa ndani ya dini hiyo, sarafu yao nayo ilikuwa yakale mno, maneno aliyo kuwa akiyatamka, nguo alizo kuwa amevaa, ni vitu vya karne tatu nyuma na muongo mmoja kasoro mwaka mmoja, walikuwa kama kioja, lakini pia walikuwa ni watu wa ajabu, muda taarifa zilitapakaa kila kona ya mji…



     Hapana shaka hii ilikuwa ni hadithi ya kuvutia mno, basi Waarabu kupitia kwa wafuasi wa Ukristo na Uyahudi, walikuwa wakiambiwa vitu vya kumjaribu navyo Muhammad, Rehma na Amani ziwe juu yake, wakitegemea atashindwa kujibu vitu hivyo ili waweze kumpinga, ndipo wakataka kujua hadithi ya watu wa pangoni toka kwa Muhammad. 

Si kwamba Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake aliwaelezea hadithi yenyewe, lakini pia aliwaambia kuhusiana na vile ambavyo walikuwa wakitofautiana juu ya hadithi hiyo, lakini zaidi aliwapa na somo linalo patikana kwenye hadithi hiyo, tizama tafsiri ya Quran kutoka kwa Yusuph Ali, hapana shaka amekieleza vyema kisa hichi.



     Kwenye Quran kisa hichi kilipo tajwa, MUNGU MMOJA, hakutaja moja kwa moja miaka 309, bali, alisema miaka mia tatu jumlisha na tisa. Nambari zote zilizo tajwa kwenye Quran, jumla ya nambari hizo ni kigawanyo cha nambari 19, ambayo ndiyo code ya Quran. Hivyo basi endapo Quran ingesema moja kwa moja 309, jumla ya nambari hizo zisingeweza kugawanyika kwa 19.



 Hadithi ya vijana hawa 7, maarufu kwa ulimwengu wa Kikristo kama Seven Sleepers, imeanzwa kutajwa kwenye aya ya 9 mpaka aya ya 25. Aya zote hizo ni kuhusu vijana hawa saba, na aya ya 25 ikasema vijana hawa wamekaa kwenye pango kwa miaka 300+9. Kuanzia vijana hawa walipoanza harakati za kuinusuru imani yao, mpaka walipo ingia pangoni, Quran imetumia maneno 308 na neno la 309 ni neno la 300+9.

Ni muda gani vijana hawa walikaa pangoni
309
Ni maneno mangapi yametumika kuanzia mwanzo wa aya inayo waelezea vijana hawa mpaka muda walio kaa pangoni
309




     Ingawa sura hii, NAMTAFUTA MUNGU, ni moja ya sura muhimu sana kwenye Posti hiz, sura zilizo tangulia ni kama utangulizi wa kuitambulisha hii sura, nisingependa kuifanya ndefu kiasi cha kumchosha msomaji wangu, ningeshauri kwa ufafanuzi mpana, maarifa na elimu zaidi juu ya Quran, msomaji avipitie vitabu nitakavyo vitaja na ambavyo kwa njia moja ama nyingine, nimevitumia kwenye kazi hii, vitabu hivyo kwa sababu moja kwa moja vina zungumzia somo hilo kwa kina, hapana shaka vitawakilisha kazi yenye tija na matokeo mazuri kwa msomaji anaye taka kuufahamu ukweli, si dhani hata kidogo mpaka hapa ulipofika kwenye kukisoma kitabu hichi ni kwa ajili ya starehe, hapana, kuna ambacho unacho kitafuta, na kitabu hichi ni utangulizi tu wa kile unacho taka kukifahamu, basi pitia vitabu hivi na vingine ili uweze kuwa huru, na sehemu kubwa ya vitabu, makala, majarida yaliyo tumika humu yanapatikana bure kwenye wavuti, ni jukumu lako kuvitafuta. 

Kwa ajili ya undani kuhusu Quran tafadhali pitia kazi za Harun Yahya, tafsiri ya Quran ya Yusuph Ali na ile ya Ibn Katheer, The Bible, The Quran and The Science cha Dr. Maurice Bucaille na The Quran Unchallengeable Miracle cha Caner Taslaman, kuvitaja kwa uchache.



     Ulimwengu umeumbwa kwa kufuata taratibu na kanuni maalum, na viumbe vyote tunavyo vifahamu na vile tusivyo vifahamu navyo, vimeumbwa kwa malengo, taratibu na kanuni mahususi. Uhai wa ulimwengu huu na vyote vilivyomo umeegemea kwenye kanuni hizo, kitendo hicho cha ulimwengu na vyote vilivyomo kuwemo ndani ya kanuni hizo, kuziheshimu na kuzifuata vilivyo, ndicho kinacho itwa kujisalimisha, ulimwengu wote na vyote vilivyomo umejisalimisha katika sharia na kanuni hizo takatifu za maumbile, yaani ulimwengu wote ni Islam, umejisalimisha. 

Hali kadhalika mwanadamu naye, anawajibika juu ya kanuni na sharia hizo, tofauti na viumbe wengine, binadamu na majini wao wanayo hiari, ya kuzifuata au kutozifuata sharia hizo, lakini vyovyote watakavyo amua kutokana na uhuru walio pewa, malipo yake watayakuta mbele ya MOLA wao. 

Hivyo kwa mwanadamu, kukubali kuwa yeye ameumbwa, na amewekewa sharia na mipaka, ambamo anatakiwa kuishi kwa kufuata kanuni hizo, na anawajibika juu ya vitendo vyake, hilo ndilo lengo kuu la Uislamu kuanzia kwa mtume Adam (a.s) mpaka mtume wa mwisho Muhammad (s.a.w)



     Hivyo mwanadamu anayo HATMA ya kuwepo hapa, malengo mahususi. Binadamu analo jukumu zito zaidi kwa yeye kuwepo hapa, jukumu ambalo litaamua, hatma ya maisha yatakayo fuata baada ya haya. Kama tulivyo ona tabia ya roho ni tofauti sana na mwili wenyewe, imekuwa ikikitafuta kile ambacho mwili haukielewi, hatma yake. 

Tumeona na kujiuliza kwa nini mtu maarufu leo duniani mwenye utajiri unao tosha kulisha vizazi na vizazi kwa karne na karne, kwa nini afe na kuuacha nyuma huo utajiri, ikiwa hatma yake mwanadamu ni hapa duniani?



     Hebu tutizame maisha yetu wenyewe, ndoto zetu za utotoni, za ujana, mipango yetu, ni nini kimebakia katika hayo? Tumekuja duniani hali ya kuwa ni madhalili na baada ya hapo tukawa tegemezi juu ya mazingira yetu. 

Haijalishi tumezaliwa kwenye jumba la kifalme au kwenye kibanda, migombani au hospitalini, tukiwa na maarifa kidogo au hatuna kabisa, tukiwa na mwonekano ‘mzuri’ au ‘mbaya’, ukiwa nacho au huna, ni kiasi gani uwezo wa maumbile yetu unaweza kusimama dhidi ya mazingira yetu, ambayo roho zetu unayakana? Zaidi tunavyo yafahamu mazingira yetu, ndivyo tunavyo zidi kuyaogopa, ndivyo tunavyo zidi kuzikimbia ndoto zetu.


     Tunapo tambua kuwa tupo hapa duniani si kwasababu ya nasibu, wala hatuishi hapa na kuendelea kwa sababu ya natural selection, na yote yanayo tokea si kwasababu ya survive for the fittest, lakini kwa sababu na malengo mahususi ambayo hatma yake imelala kwenye dunia nyingine. 

Tunapo tambua kuwa hatma yetu ni juu ya namna tutakayo ishi hapa, na hatuwezi kuishi kama tutakavyo, bali kwa kufuata kanuni, taratibu na sharia za kimaumbile alizo ziweka MUUMBA mwenyewe, kanuni ambazo katufunza kupitia mitume wake mbalimbali, hapo tunautambua Uislamu, hapo tunautambua, ujumbe mmoja, toka kwa Mungu Mmoja, kwa watu wote wa zama zote, na tunapoufuata, basi tunakuwa Waislam, yaani wale waliojisalimisha, kwenye sharia na kanuni hizo za maumbile zilizo wekwa na MUNGU MMOJA.

No comments:

Post a Comment