Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Friday, December 4, 2015

SAFARI YA WWIII NA SHAMBULIZI LA PARIS

POST YA 'DOLA YA KISHETANI NA USHOGA' BADO INAENDELEA NIMEIKATIZA KIDOGO NI WAPE UP DATE ZA SHAMBULIZI LA PARIS ... 


NATO inagonga hodi Syria!
Wakati vilio na majonzi vikiendelea ufaransa na lawama zikirushwa kutoka kila kona ya Dunia kuelekea kwa ‘magaidi’, na mpenda amani ukibaki na kizingimkuti kutokujua kipi ni kipi katika zama hizi ngeni kihistoria, hatuna budi kulitizama tukio hilo kwa jicho jingine ili kuweza kupata ukweli wa mambo.


Marekani ilikuwa ni 9/11/01 ambapo karibu watu 3000 walipoteza uhai, Uingereza tulishuhudia tukio linalofanana na hilo 7/7/05 karibu watu 52 walipoteza uhai, Spain 3/11/04 watu 192 wakafa. Yote haya yakiwa na ujumbe mmoja, muuwaji au wauwaji ni waislam na lengo lao ni kusimamisha dola la kiislam na kuuwa wote wasiokuwa waislam kama inabidi iwe hivyo.


Tuanzie kwa kusema ikiwa mpaka sasa unakubali 9/11 ilitekelezwa na mtu mwenye ndevu nyingi, ambaye alikuwa kwenye mapango ya Torabora, akiwa kitandani anaugua ugonjwa figo, aliweza kuwaongoza wanafunzi 19 ambao wengi wao hawakuwa hata wamemaliza mafunzo ya Upailot, kuweza kuihadaa safu ya ulinzi wa taifa la Marekani na hatimaye kuteka ndege kwa visu vya plastiki na kuiteremsha minara miwili mirefu ndani ya NewYork na kuishambulia Pentagon, na Amerika ikitazama, ikiwa unaamini au unaelewa hivyo, basi ... tambua uwezo wako wa akili umefungwa.




Kilichofuata, ‘Ufaransa ipo vitani’ maneno ya Hollande, raisi wa Ufaransa. Maneno hayo hayo aliyasema Bush baada ya Minara miwili na pentagon kushambuliwa.

 Haikuchukua muda Hollande akasema washambuliaji wanatokea Syria, kama ambavyo haikumchukua muda Bush kumtaja Osama Bin Laden.

Haikuchukua muda hati ya kusafiria ya raia wa Syria (Mtuhumiwa) iliokotwa eneo la tukio, kama ambavyo haikuchukua muda hati ya kusafiria kuokotwa kwenye mavumbi ya minara ile ya Washngton ikimtaja mtuhumiwa ni mtu kutoka Mashariki ya kati.
ALWAYS MAGIC PASSPORT

Hollande akatangaza hali ya hatari, kama alivyo fanya Bush kwenye 9/11.

Kwenye hali hiyo ya hatari kama alivyo fanya Bush napo ufaransa watu walianza kukamatwa bila kibali cha polisi (warrants), fungwa pingu na kusekwa ndani bila haki yako ya kusikilizwa au kuwekewa dhamana, vizuizi vya barabarani kila kona, mipaka ikajazwa askari zaidi, hakuna kuandamana. Nchi iko kwenye hali ya hatari.

Kama ambavyo kauli ya Bush, ‘Marekani ipo vitani’ Ikawa ndiyo kibali rasmi cha Marekani kuingia Afighanistani kijeshi, kisha Iraq na baadae Mashariki ya kati yote kwa ujumla akiwatafuta ‘magaidi’ aliowatengeneza mwenyewe, ndivyo kauli ya Hollande inavyo ashiria, kwamba sasa Ulaya inaingia rasmi kwenye saga hilo ikiongozwa au ikisaidiwa na  NATO.
NATO WANAKARIBISHWA UWANJANI

Nafasi ya NATO ni muhimu kwenye hili hasa ukichukilia mwenendo wa Moscow kwenye hili sakata zima na namna Putin amekuwa akichezesha karata zake kulinda maslahi na urafiki wake wa muda mrefu na Syria.

Ni kama safu za WWIII zikijiweka na kufanya maandalizi ya mwisho kabla ya kipenga kulia.
Unakumbuka safu zilivyo pangwa kwenye WWI?
Unakumbuka zilivyopangwa kwenye WWII?
Huoni mchoraji yuleyule karudi mezani na mchoro WWIII utakavyo kuwa? Au bado unafikiri mtu mwenye mandevu mengi na kilemba jangwani ndiyo gaidi?



Kwa muda mrefu hii imekuwa ni mbinu chafu inayotumiwa na mataifa mbalimbali kote ulimwenguni kutengeneza mazingira ya kuishambulia nchi, taasisi au kikundi cha watu. Maarufu mbinu hii inajulikana kama False Flag, unabeba bendera ya nchi X halafu unaishambulia nchi yako ukiwa na bendera hiyo halafu unailaumu nchi X kuwa imekushambulia na hapo unapata kisingizio cha kuishambulia, tizama ukurasa huu utaona oradha ya mashambulizi ya False Flag yaliyo fanywa na nchi mbalimbali kote duniani, 

http://www.washingtonsblog.com/2015/02/41-admitted-false-flag-attacks.html



Shambulio la Paris Tarehe 13, siku ya ijumaa kwa kila namna lilikuwa limebeba alama za zote za False Flag.

Shambulio hili halikuwa na tija kwa yeyote ila kwa serikali a Ufaransa yenyewe na ajenda kuu ya NWO. Kinachotokea ni kuwa serikali zinazo tengeneza aina hii ya mashambulizi zinapata nguvu zaidi ya kupora uhuru na haki za wananchi wake na kushindikiza utawala wenye sheria kali na kuzima uhuru wa vyombo vya habari kwa pamoja na wakati huo huo ikiimarisha misingi na misimamo ya chuki baina ya wanachi wake, sababu itakuwa imewagawanya kwa misingi mbalimbali, kama vile Shia vs Sunni, Wananchi wa Ulaya dhidi ya Wahamiaji wa kigeni, Wakristo dhidi ya Waislam, Mweupe dhidi ya Mweusi, Mashariki dhidi ya Magharibi, kifupi inakuwa ni Divide and Rule na hakuna anayenufaika na mbinu hii zaidi ya mtawala.



Kama ilivyokuwa kwenye 9/11 ambapo mtangazaji wa BBC aliripoti kuanguka kwenye linalo fahamika kama Building 7. Jengo hilo halikugongwa na ndege wala kushambulia, na taarifa rasmi ya kuanguka kwake ilidai lilipata mlipuko kutokana na kurukiwa na moto kutoka kwenye Twin Towers. Lakini taarifa ya kuporomoka kwake ilikuja dakika 20 kabla halijaporomoka. Tunajiuliza BBC walijiaje juu ya kuporomoka kwa jengo hili ambalo halikushambuliwa? Baada ya hizo dakika 20 Building 7 liliporomoka kama yalivyo poromoka Twin Towers, utadhani nalo lilishambuliwa na ndege za magaidi.
 BBC Ikirusha LIVE kuporomoka kwa Building 7, wakati nyuma ya mtangazaji jengo hilo limesimama hata halitoi moshi, na siku hiyo haijaisha baada ya taarifa hiyo jengo hilo liliporomoka.

Paris nayo ikawa hivyo hivyo, siku mbili kabla ya tukio akaunti ya Twiter ilikuwa ikielezea kuwepo kwa tukio hilo.


 Hii ni twitter siku 2 kabla ya tukio, yaani 11/11/2015 inautangazia umma madhara ya tukio ambalo bado halijatokea.


Masaa mawili kabla ya tukio mtandao wa Wikipedia uliandika habari ya mwanzo kabisa kuhusu shambulio hilo, na ikitaja magaidi wanatokea Syria kutokana na mashahidi watano au sita waliohojiwa na kuthibitisha hivyo, lakini hapa ni masaa mawili kabla ya shambulizi lenyewe, na zaidi Wikipedia ikaweka na hadidi rejea kuonesha wapi imetolea taarifa hizo.

Dakika 52, yaani lisaa limoja kasoro dakika 2, tangu Wikepidia waweke taarifa hiyo, rais wa Ufaransa Hollande kwenye luninga akatangaza hali ya hatari na kufunga mipaka yake yote ya Ufaransa.

Lakini jingine linalo kwenda sambamba na matukio mengi ya False Flag ni kuwepo kwa mazoezi, siku na muda uleule, wakati mwingine mazoezi hayo yakilenga kushambulia eneo au kitu ambacho baadae kitatangazwa kuwa kimepigwa na magaidi.

Alfajiri ya 9/11 NORAD walikuwa wakifanya mazoezi ya anga, ambayo yalihusisha kushambulia Twin Towers. Wakati tukio rasmi la kigaidi linatokea maafisa wa usalama walikuwa hawajui kama ni mazoezi yanaendelea au ndiyo kazi imeanza. Kitu hicho hicho kilionekana kwenye mashambulizi ya Boston, Baltimore, London 7/7.

Madaktari wadharura na ambao waliwa wakwanza kuhudhuria eneo la tukio kwa ajili ya kutoa huduma ya kwanza wanakiri juu ya kuwepo kwa mazoezi ya ‘kigaidi’ yaliyofanywa na wanajeshi wa serikali muda mfupi kabla ya tukio. Washiriki wa zoezi hilo wakiwemo madaktari walikuwa wakifundishwa namna ya kufanya unapokuwa upo kwenye eneo lilipo tokea ugaidi, na mafunzo hayo yalilenga maeneo kama uwanja wa mpira na kwenye matamasha, maeneo ambayo masaa mawili baadae ‘ugaidi’ halisi ulitokea.



Sasa unajiuliza kwanini kila mazoezi yapofanywa yanaambatana na matukio halisi ya ugaidi?

Wiki mbili kabla ya tukio, Mkurugenzi wa CIA John Brennan alikutana na kiongoziwa ufaransa mwenye wadhifa kama wake, pamoja na aliyekuwa mkuu wa ushauri wa usalama wa Israel na kiongozi wa MI6 wa Uingereza, naa baada ya hapo Brennan akakiri juu ya kuwepo au kutokea kwa shambulizi la kigaidi Ulaya. Kauli ambayo iliwiana sawia kwa maneno na muda na zile zilizokuwa zikitolewa na wanaoitwa ‘magaidi.’



Utaona kauli za magadi na wanausalama zinawiana kila wakati, kabla na baada ya mashambulizi. Lakini hili linatiliwa nguvu zaidi na mwenendo usio rasmi wa taasisi za kiusalama kushiriki katika kutoa mafunzo, zana na hata watu wake kushiriki moja kwa moja kwenye matukio ya ugaidi.
Mathalani Mc mara kadhaa amekutana na viongozi IS.
Kiongozi anayeitwa El Baghdad upo ushahidi kwamba amepatiwa mafunzo na Mossad.

Bush kabla ya 9/11 yalikuwepo mazingira yanayo onesha likutana na Atta, mtuhumiwa nambari moja kwenye tukio la 9/11.
Lakini ipo wazi kwenye vyombo vyote vya habari na nyaraka mbalimbali na kauli za viongozi wa mataifa makubwa ambao wamewagawanya waasi wa Syria sehemu mbili, kunawaasi wenye msimamo wa wastani na wenye msimamo mkali, mara kadhaa Obama na Mc wamekiri kuwaunga mkono waasi wenye msimamo wa wastani dhidi ya Assad. Lakini ni kipi kinacho kuonesha huyu ni Gaidi wa msismo mkali na huyu wa msimamo wa kati. Kauli hizi hazifanyi chcochote zaidi ya kuziwezesha serikalui hizo kuwaunga mkono magaidi na kuwahadaa wanchi kuwa hawa wanamsimamo wa wastani.
Mc CAIN AKIWA NA AL - BAGHDADI

Tukio hili la kigaidi lililotokea Paris na mengine mfano wa hayo kokote ulimwenguni, ni matukio ya kulaaniwa na kupingwa kwa kila hali, na uchunguzi huru lazima ufanyike na wahalifu washughulikiwe kisheria. Bila ya hivyo matukio haya yataendelea kutagawanya na kuonesheana vidole kwa kutizama mwenye ndevu na asiye na ndevu wakati anatakiwa kuoneshewa kidole akitucheka.
WHO IS A TERRORIST???
OR 
YOU WAIT FOR CNN TO SHOW YOU ONE?
DONT BE SURPRISED WHEN THEY SHOW UR FACE ON TV THAT UR THE ONE.

Shambulio hili limefanywa na watu 8, kati yao 7 wameuwawa, mtu mmoja, anayesemekana ndiyo kinara wa mashambulizi, Salah Abdesslam ambaye alishikiliwa masaa kadha kwenye mpaka wa Belgian baada ya shambulio hilo, bila taarifa za kueleweka aliachiliwa huru na kuondoka, baadae zikaja taarifa natafuta, mpaka sasa anatafutwa!!!!!????????????


Wapo kwenye watch list lakini hakifanyiki chochote mpaka wakisha fanya tukio .

Hadithi hii inafanana na ile ya mwaka 2001, miezi miwili kabla ya 9/11, Ambapo mtuhumiwa nambari moja wa shambulizi hilo alikuwa akitibiwa kwenye Hospitali ya Marekani iliyopo Dubai kwa ajili ya matatizo yake ya Figo, akiwa hospitalini hapo alikutana na viongozi mbalimbali na waheshimiwa wengine, lakini zaidi, alikutana na afisa wa CIA ambaye naye walizungumza naye machache, halafu miezi miwili baadae walianza kumtafuta kwenye mapango ya Torabora.

Lakini kunahadithi ya Mohamed Atta na Bush. Siku tatu kabla ya 9/11 Bush alitembelea eneo la karibu kabisa na Hoteli aliyoishi Mohamed Atta na bodigadi wake.


Yupo kwenye watch list nyeneo zake zinafuatiliwa, tukio linatokea, ndiyo anatafutwa auwawe.

Hivyo utaona Salah Abdesslam hakuwa wa kwanza mtuhumiwa wa ugaidi ambaye yupo kwenye ‘watch list’ kwa miaka kadhaa kukamatwa na kuachiwa. Jibu la rahisi ni kuwa yeye ni sehemu ya mpango huo ambapo yeye anasimama kama mtu kati baina ya serikali ya ufaransa, maafisa wake wa usalama, na ‘magaidi’ ambao hawajui chochote. Ndiyo maana hawa 7 waliuwawa bila kupoteza muda wasije wakavujisha habari, na kinara wao kuachiwa huru.


Yupo kwenye watch list tukio linatokea, anakamatwa, anaachiwa, halafu anatafutwa!!!!!!???????????

Paul Craig Roberts, aliyekuwa Assistant Secretary of the Treasury for Economic Policy kwenye utawala wa Regan anasema alipokea taarifa kutoka usalama wa Ulaya kwamba palikuwa na shambulio kubwa la kwenye mifumo ya kimtandao ya Ufaransa masaa 48 kabla ya shambulizi la Paris. Shambulizi hilo linasemwa halikuwa la moja kwa moja, lakini lilikuwa likilenga miundo mbinu ya mawasiliano na mitandao na kuidhoofisha. Shambulizi kama hili huwezi hata nusu sekunde ukadhani limefanywa na vijana wenye ndevu, na wendawazimu wanao uwa na kuchinja watu ovyio.
WANAKUONA WEWE NI MJINGA KIASI HUWEZI KUIYONA MIKONO YAO KWENYE PICHA HII YA UGAIDI.

Shambulizi la namna hii limefanywa na watu wazito wanaijua miundo mbinu ya mitandao na mawasiliano ndani ya ufaransa na kwenye uslama wa taifa la ufaransa, na hapa utawakuta CIA, MI6, MOSSAD, na wale wa Ufaransa wenyewe, unakumbuka kikao cha maafisa hao wakubwa wa Usalama wiki moja kabla ya shambulizi? Unganisha doti na doti utapata picha ambayo si CNN wala Ajazeera watakao kuonesha.

Shambulizi limekuja wakati ambao Umoja wa Ulaya umegawanywa kwenye mstari wa wahamiaji wa kigeni. Ukiacha Ujerumani nchi nyingi za Ulaya hazikuwa tayari kuwapokea wakimbizi hao, na Ufaransa ilikuwa moja ya nchi hizo ambazo hazikuwa zikiwapokea kirahisi wahamiaji hao. Lisaa limoja kabla ya shambulizi Ufaransa ilishafunga mipaka yake, baada ya shambulizi nchi zingine za Ulaya zikafunga mipaka, na kwa muda tatizo la wakimbizi likawa linaufumbuzi.



Lakini shambulizi limekuja wakati ambao taifa la Urrusi linabadilisha mwenendo wa vita ndani ya Syria. Urusi imeweza kubadilisha mwenendo huo kiasi kwamba tangu mwaka 2011 kwa mara ya kwanza Bashir al Assad ameweza kuiacha Damaskasi na kwenda Moscow kumshukuru Putin ‘Personaly’ na kurudi Damaskasi.

Ni kwamba Putin amempa Assad ‘Confidence’ kiasi anaweza kukiacha kiti chake wazi katika wakati mgumu kama huo na kwenda kumshukuru Putin kwa kumsaidia kuwachapa ISIS.
THE PICTURE WHICH SURPRISE THE WEST.

Hii iliwa ni taarifa mbaya sana kwa Marekani, Ulaya, Uturuki na nchi za Kiarabu zilizo kwenye muungano huo wa kumng’oa Assad. Lakini zaidi ilikuwa ni tusi kubwa kwao na kwa taasisi zao za usalama na ujasusi, kwamba Putin na Assad wamekuwa na ngome imara na mfumo bora wa ‘ku-keep information’ kiasi Assad achomoke na kurudi bila wao kunusa chochote.

Lakini zaidi Urrusi anaelekea kumpa Assad ushindi kama ataendelea hivi bila kupata kipingamizi, Marekani peke yake na wanamgambo wake ‘wa msimamo wa wastani’ na baadhi ya nchi washirika wanaelekea kushindwa, na kama hakitafanyika chochote, Assad atabakia Damaskasi, na sisi tutaonekana vichekesho kwenye uso wa dunia. 
YES HAVE A SMILE

Hivyo umoja wa Ulaya, kwa maana ya Nato wanakiwa kwenye uwanja wa vita kumpa upinzani Mrusi na kuwapa nafasi Marekani na wenzake kumalizia kazi waliyo ianza.

Ufaransa anachotakiwa kufanya ni kugusa kifungu kimoja kwenye katiba ya Ulaya na NATO watakuwa uwanjani, na hata kabla Hollande hajafanya hivyo viongozi wa nchi hizo na wakuu wa NATO wako ‘standby’ wanasubiri mualiko wa Hollande waanza kazi.

Bado unafikiri mashambulizi haya yamefanywa na watu wendawazimu wenye ndevu nyingi na wanaongea lugha ya kiarabu? Fikiria tena …

Ukweli ni kuwa Washington wanaona uwezekano wa kupoteza nafasi ya ‘U-Super Power’, na kushindwa kwenye vita vyoa vya kutengeneza na washirika wao wakiwemo ISIS. Ujio wa Putin ni msiba kwao, lakini zaidi Putin ataonekana ni kiranja mpya kwenye uso huu wa dunia. Kwahiyo watu wazima wale Brennan na wenzake walipokutana wakaweka mazingira ya hii ‘False Flag’ ambayo itamkaribisha NATO uwanjani.


UPANDE MMOJA WA SAFU YA WWIII ...

NATO na washirika wake akiwemo kiongozi wao Marekani, hata kidogo mabomu na risasi zao hazita wagusa ISIS, na wala vituo vya mafuta ya magendo vinavyo shikiliwa na ISIS kwa ajili ya kuuza mafuta ya magendo kwa mwanachama wa NATO, Uturuki havita guswa. Wala bomba la mafuta linashikiliwa na ISIS kwenda Uturiki halitaguswa. Nguvu hiyo kubwa itaelekezwa kwenye kumshambulia Assad na vikosi vyake na kujaribu kumnyima pumzi Mrusi ambaye anashirikiana na Iran. Hili linanikumbusha hadithi ya WWI ilivyoanza.

Wakati WWIII itakapo andikwa kwenye historia, shambulizi la Paris halitaachwa kutajwa kama moja ya karata muhimu zilizo chezwa na wakubwa kabla ya zahama hilo kuanza.

Kaa vizuri historia inakaribia kujirudia, waandishi wa historia wakiwa ni walewale, amka sasa, acha kumnyoeshea kidole yule mwenye kanzu, au huyu mwenye ngozi ya rangi ile, wakati adui yetu akicheza muziki kwa raha zake. Vita dhidi ya Ugaidi havimlengi yeyoye ila WEWE na FAMILIA YAKO. Wewe ndiye gaidi, bila kujali rangi yako, dini yako, kabila lako, utaifa wako, wewe ndiye gaidi, ilimradi tu unayo uwezo wa kufikiri kwa akili huru, bila kutegemea CNN au Aljazeera, basi wewe ni gaidi na ni hatari kwa usalama wa dunia, na tizama kila sheria inayo kuja baada ya matukio haya kutokea inamkandamiza nani kama si wewe?

Sheria hizo hazitazami unayo kanzu ama la, una ndevu nyingi au huna kabisa, hapana Micrichip ikija kama njia ya kuzuia ugaidi mtapewa wote, sheria za uhamiaji zikija zitawabeba wote, kamera zikisambazwa mitaani zitatumulika wote, sheria ya kutembea mwisho saa 12 ikija itamhusu kila mtu. Halafu bado unasema Marekani na washirika wake waongeze msuli na nguvu dhidi ya magaidi, bila kujua gaidi hasa ni wewe.



Amka ndugu, soon your next ….

Catch You Next Time here here ……

7 comments:

  1. Mkuu nafuatilia habari zako kwa ukaribu mno endelea kunifungua ubongo

    ReplyDelete
  2. kila siiku akili yangu inapata kitu kipya kutoka kwako. naipenda sana hii kazi....
    blogger @ www.roryafinest.blogspot.com

    ReplyDelete
  3. Yaani nimekua nikisoma makala zako Bro na baada ya hapo ni kifanya INTEGRATION yaani uhalisia upo pale pale.......

    ReplyDelete
  4. mkuu napataje contact zko

    ReplyDelete
  5. daa nafikiria salim ana kichwa cha aina gani daah

    ReplyDelete