NATO inagonga hodi Syria!
Wakati vilio na majonzi vikiendelea ufaransa na lawama zikirushwa kutoka
kila kona ya Dunia kuelekea kwa ‘magaidi’, na mpenda amani ukibaki na
kizingimkuti kutokujua kipi ni kipi katika zama hizi ngeni kihistoria, hatuna
budi kulitizama tukio hilo kwa jicho jingine ili kuweza kupata ukweli wa mambo.
Marekani ilikuwa ni 9/11/01 ambapo karibu watu 3000 walipoteza uhai,
Uingereza tulishuhudia tukio linalofanana na hilo 7/7/05 karibu watu 52
walipoteza uhai, Spain 3/11/04 watu 192 wakafa. Yote haya yakiwa na ujumbe
mmoja, muuwaji au wauwaji ni waislam na lengo lao ni kusimamisha dola la
kiislam na kuuwa wote wasiokuwa waislam kama inabidi iwe hivyo.
Tuanzie kwa kusema ikiwa mpaka sasa unakubali 9/11 ilitekelezwa na mtu
mwenye ndevu nyingi, ambaye alikuwa kwenye mapango ya Torabora, akiwa kitandani
anaugua ugonjwa figo, aliweza kuwaongoza wanafunzi 19 ambao wengi wao hawakuwa
hata wamemaliza mafunzo ya Upailot, kuweza kuihadaa safu ya ulinzi wa taifa la
Marekani na hatimaye kuteka ndege kwa visu vya plastiki na kuiteremsha minara
miwili mirefu ndani ya NewYork na kuishambulia Pentagon, na Amerika ikitazama,
ikiwa unaamini au unaelewa hivyo, basi ... tambua uwezo wako wa akili umefungwa.
Kilichofuata, ‘Ufaransa ipo vitani’ maneno ya Hollande, raisi wa Ufaransa.
Maneno hayo hayo aliyasema Bush baada ya Minara miwili na pentagon
kushambuliwa.
Haikuchukua muda Hollande akasema
washambuliaji wanatokea Syria, kama ambavyo haikumchukua muda Bush kumtaja
Osama Bin Laden.
Haikuchukua muda hati ya kusafiria ya raia wa Syria (Mtuhumiwa) iliokotwa
eneo la tukio, kama ambavyo haikuchukua muda hati ya kusafiria kuokotwa kwenye
mavumbi ya minara ile ya Washngton ikimtaja mtuhumiwa ni mtu kutoka Mashariki
ya kati.
ALWAYS MAGIC PASSPORT
Hollande akatangaza hali ya hatari, kama alivyo fanya Bush kwenye 9/11.
Kwenye hali hiyo ya hatari kama alivyo fanya Bush napo ufaransa watu
walianza kukamatwa bila kibali cha polisi (warrants), fungwa pingu na kusekwa
ndani bila haki yako ya kusikilizwa au kuwekewa dhamana, vizuizi vya barabarani
kila kona, mipaka ikajazwa askari zaidi, hakuna kuandamana. Nchi iko kwenye
hali ya hatari.
Kama ambavyo kauli ya Bush, ‘Marekani ipo vitani’ Ikawa ndiyo kibali rasmi
cha Marekani kuingia Afighanistani kijeshi, kisha Iraq na baadae Mashariki ya
kati yote kwa ujumla akiwatafuta ‘magaidi’ aliowatengeneza mwenyewe, ndivyo
kauli ya Hollande inavyo ashiria, kwamba sasa Ulaya inaingia rasmi kwenye saga
hilo ikiongozwa au ikisaidiwa na NATO.
NATO WANAKARIBISHWA UWANJANI
Nafasi ya NATO ni muhimu kwenye hili hasa ukichukilia mwenendo wa Moscow
kwenye hili sakata zima na namna Putin amekuwa akichezesha karata zake kulinda
maslahi na urafiki wake wa muda mrefu na Syria.
Ni kama safu za WWIII zikijiweka na kufanya maandalizi ya mwisho kabla ya
kipenga kulia.
Unakumbuka safu zilivyo pangwa kwenye WWI?
Unakumbuka zilivyopangwa kwenye WWII?
Huoni mchoraji yuleyule karudi mezani na mchoro WWIII utakavyo kuwa? Au
bado unafikiri mtu mwenye mandevu mengi na kilemba jangwani ndiyo gaidi?
Kwa muda mrefu hii imekuwa ni mbinu chafu inayotumiwa na mataifa mbalimbali
kote ulimwenguni kutengeneza mazingira ya kuishambulia nchi, taasisi au kikundi
cha watu. Maarufu mbinu hii inajulikana kama False Flag, unabeba bendera ya
nchi X halafu unaishambulia nchi yako ukiwa na bendera hiyo halafu unailaumu
nchi X kuwa imekushambulia na hapo unapata kisingizio cha kuishambulia, tizama
ukurasa huu utaona oradha ya mashambulizi ya False Flag yaliyo fanywa na nchi
mbalimbali kote duniani,
http://www.washingtonsblog.com/2015/02/41-admitted-false-flag-attacks.html
Shambulio la Paris Tarehe 13, siku ya ijumaa kwa kila namna lilikuwa
limebeba alama za zote za False Flag.
Shambulio hili halikuwa na tija kwa yeyote ila kwa serikali a Ufaransa
yenyewe na ajenda kuu ya NWO. Kinachotokea ni kuwa serikali zinazo tengeneza
aina hii ya mashambulizi zinapata nguvu zaidi ya kupora uhuru na haki za
wananchi wake na kushindikiza utawala wenye sheria kali na kuzima uhuru wa
vyombo vya habari kwa pamoja na wakati huo huo ikiimarisha misingi na misimamo
ya chuki baina ya wanachi wake, sababu itakuwa imewagawanya kwa misingi
mbalimbali, kama vile Shia vs Sunni, Wananchi wa Ulaya dhidi ya Wahamiaji wa
kigeni, Wakristo dhidi ya Waislam, Mweupe dhidi ya Mweusi, Mashariki dhidi ya
Magharibi, kifupi inakuwa ni Divide and Rule na hakuna anayenufaika na mbinu
hii zaidi ya mtawala.
Kama ilivyokuwa kwenye 9/11 ambapo mtangazaji wa BBC aliripoti kuanguka
kwenye linalo fahamika kama Building 7. Jengo hilo halikugongwa na ndege wala
kushambulia, na taarifa rasmi ya kuanguka kwake ilidai lilipata mlipuko
kutokana na kurukiwa na moto kutoka kwenye Twin Towers. Lakini taarifa ya
kuporomoka kwake ilikuja dakika 20 kabla halijaporomoka. Tunajiuliza BBC
walijiaje juu ya kuporomoka kwa jengo hili ambalo halikushambuliwa? Baada ya
hizo dakika 20 Building 7 liliporomoka kama yalivyo poromoka Twin Towers,
utadhani nalo lilishambuliwa na ndege za magaidi.
BBC Ikirusha LIVE kuporomoka kwa Building 7, wakati nyuma ya mtangazaji jengo hilo limesimama hata halitoi moshi, na siku hiyo haijaisha baada ya taarifa hiyo jengo hilo liliporomoka.
Paris nayo ikawa hivyo hivyo, siku mbili kabla ya tukio akaunti ya Twiter
ilikuwa ikielezea kuwepo kwa tukio hilo.
Hii ni twitter siku 2 kabla ya tukio, yaani 11/11/2015 inautangazia umma madhara ya tukio ambalo bado halijatokea.
Masaa mawili kabla ya tukio mtandao wa
Wikipedia uliandika habari ya mwanzo kabisa kuhusu shambulio hilo, na ikitaja
magaidi wanatokea Syria kutokana na mashahidi watano au sita waliohojiwa na
kuthibitisha hivyo, lakini hapa ni masaa mawili kabla ya shambulizi lenyewe, na
zaidi Wikipedia ikaweka na hadidi rejea kuonesha wapi imetolea taarifa hizo.
Dakika 52, yaani lisaa limoja kasoro dakika 2, tangu Wikepidia waweke
taarifa hiyo, rais wa Ufaransa Hollande kwenye luninga akatangaza hali ya
hatari na kufunga mipaka yake yote ya Ufaransa.
Lakini jingine linalo kwenda sambamba na matukio mengi ya False Flag ni
kuwepo kwa mazoezi, siku na muda uleule, wakati mwingine mazoezi hayo yakilenga
kushambulia eneo au kitu ambacho baadae kitatangazwa kuwa kimepigwa na magaidi.
Alfajiri ya 9/11 NORAD walikuwa wakifanya mazoezi ya anga, ambayo
yalihusisha kushambulia Twin Towers. Wakati tukio rasmi la kigaidi linatokea
maafisa wa usalama walikuwa hawajui kama ni mazoezi yanaendelea au ndiyo kazi
imeanza. Kitu hicho hicho kilionekana kwenye mashambulizi ya Boston, Baltimore,
London 7/7.
Madaktari wadharura na ambao waliwa wakwanza kuhudhuria eneo la tukio kwa
ajili ya kutoa huduma ya kwanza wanakiri juu ya kuwepo kwa mazoezi ya ‘kigaidi’
yaliyofanywa na wanajeshi wa serikali muda mfupi kabla ya tukio. Washiriki wa
zoezi hilo wakiwemo madaktari walikuwa wakifundishwa namna ya kufanya unapokuwa
upo kwenye eneo lilipo tokea ugaidi, na mafunzo hayo yalilenga maeneo kama
uwanja wa mpira na kwenye matamasha, maeneo ambayo masaa mawili baadae ‘ugaidi’
halisi ulitokea.
Sasa unajiuliza kwanini kila mazoezi yapofanywa yanaambatana na matukio
halisi ya ugaidi?
Wiki mbili kabla ya tukio, Mkurugenzi wa CIA John Brennan alikutana na kiongoziwa
ufaransa mwenye wadhifa kama wake, pamoja na aliyekuwa mkuu wa ushauri wa
usalama wa Israel na kiongozi wa MI6 wa Uingereza, naa baada ya hapo Brennan
akakiri juu ya kuwepo au kutokea kwa shambulizi la kigaidi Ulaya. Kauli ambayo
iliwiana sawia kwa maneno na muda na zile zilizokuwa zikitolewa na wanaoitwa
‘magaidi.’
Utaona kauli za magadi na wanausalama zinawiana kila wakati, kabla na baada
ya mashambulizi. Lakini hili linatiliwa nguvu zaidi na mwenendo usio rasmi wa
taasisi za kiusalama kushiriki katika kutoa mafunzo, zana na hata watu wake
kushiriki moja kwa moja kwenye matukio ya ugaidi.
Mathalani Mc mara kadhaa amekutana na viongozi IS.
Kiongozi anayeitwa El Baghdad upo ushahidi kwamba amepatiwa mafunzo na
Mossad.
Bush kabla ya 9/11 yalikuwepo mazingira yanayo onesha likutana na Atta,
mtuhumiwa nambari moja kwenye tukio la 9/11.
Lakini ipo wazi kwenye vyombo vyote vya habari na nyaraka mbalimbali na
kauli za viongozi wa mataifa makubwa ambao wamewagawanya waasi wa Syria sehemu
mbili, kunawaasi wenye msimamo wa wastani na wenye msimamo mkali, mara kadhaa
Obama na Mc wamekiri kuwaunga mkono waasi wenye msimamo wa wastani dhidi ya
Assad. Lakini ni kipi kinacho kuonesha huyu ni Gaidi wa msismo mkali na huyu wa
msimamo wa kati. Kauli hizi hazifanyi chcochote zaidi ya kuziwezesha serikalui
hizo kuwaunga mkono magaidi na kuwahadaa wanchi kuwa hawa wanamsimamo wa
wastani.
Mc CAIN AKIWA NA AL - BAGHDADI
Tukio hili la kigaidi lililotokea Paris na mengine mfano wa hayo kokote
ulimwenguni, ni matukio ya kulaaniwa na kupingwa kwa kila hali, na uchunguzi
huru lazima ufanyike na wahalifu washughulikiwe kisheria. Bila ya hivyo matukio
haya yataendelea kutagawanya na kuonesheana vidole kwa kutizama mwenye ndevu na
asiye na ndevu wakati anatakiwa kuoneshewa kidole akitucheka.
WHO IS A TERRORIST???
OR
YOU WAIT FOR CNN TO SHOW YOU ONE?
DONT BE SURPRISED WHEN THEY SHOW UR FACE ON TV THAT UR THE ONE.
Shambulio hili limefanywa na watu 8, kati yao 7 wameuwawa, mtu mmoja,
anayesemekana ndiyo kinara wa mashambulizi, Salah Abdesslam ambaye alishikiliwa
masaa kadha kwenye mpaka wa Belgian baada ya shambulio hilo, bila taarifa za
kueleweka aliachiliwa huru na kuondoka, baadae zikaja taarifa natafuta, mpaka
sasa anatafutwa!!!!!????????????
Wapo kwenye watch list lakini hakifanyiki chochote mpaka wakisha fanya tukio .
Hadithi hii inafanana na ile ya mwaka 2001, miezi miwili kabla ya 9/11, Ambapo
mtuhumiwa nambari moja wa shambulizi hilo alikuwa akitibiwa kwenye Hospitali ya
Marekani iliyopo Dubai kwa ajili ya matatizo yake ya Figo, akiwa hospitalini
hapo alikutana na viongozi mbalimbali na waheshimiwa wengine, lakini zaidi,
alikutana na afisa wa CIA ambaye naye walizungumza naye machache, halafu miezi
miwili baadae walianza kumtafuta kwenye mapango ya Torabora.
Lakini kunahadithi ya Mohamed Atta na Bush. Siku tatu kabla ya 9/11 Bush
alitembelea eneo la karibu kabisa na Hoteli aliyoishi Mohamed Atta na bodigadi
wake.
Yupo kwenye watch list nyeneo zake zinafuatiliwa, tukio linatokea, ndiyo anatafutwa auwawe.
Hivyo utaona Salah Abdesslam hakuwa wa kwanza mtuhumiwa wa ugaidi ambaye
yupo kwenye ‘watch list’ kwa miaka kadhaa kukamatwa na kuachiwa. Jibu la rahisi
ni kuwa yeye ni sehemu ya mpango huo ambapo yeye anasimama kama mtu kati baina
ya serikali ya ufaransa, maafisa wake wa usalama, na ‘magaidi’ ambao hawajui chochote.
Ndiyo maana hawa 7 waliuwawa bila kupoteza muda wasije wakavujisha habari, na
kinara wao kuachiwa huru.
Yupo kwenye watch list tukio linatokea, anakamatwa, anaachiwa, halafu anatafutwa!!!!!!???????????
Paul Craig Roberts, aliyekuwa Assistant Secretary of
the Treasury for Economic Policy kwenye utawala wa
Regan anasema alipokea taarifa kutoka usalama wa Ulaya kwamba palikuwa na
shambulio kubwa la kwenye mifumo ya kimtandao ya Ufaransa masaa 48 kabla ya
shambulizi la Paris. Shambulizi hilo linasemwa halikuwa la moja kwa moja, lakini
lilikuwa likilenga miundo mbinu ya mawasiliano na mitandao na kuidhoofisha.
Shambulizi kama hili huwezi hata nusu sekunde ukadhani limefanywa na vijana
wenye ndevu, na wendawazimu wanao uwa na kuchinja watu ovyio.
WANAKUONA WEWE NI MJINGA KIASI HUWEZI KUIYONA MIKONO YAO KWENYE PICHA HII YA UGAIDI.
Shambulizi la namna
hii limefanywa na watu wazito wanaijua miundo mbinu ya mitandao na mawasiliano
ndani ya ufaransa na kwenye uslama wa taifa la ufaransa, na hapa utawakuta CIA,
MI6, MOSSAD, na wale wa Ufaransa wenyewe, unakumbuka kikao cha maafisa hao
wakubwa wa Usalama wiki moja kabla ya shambulizi? Unganisha doti na doti
utapata picha ambayo si CNN wala Ajazeera watakao kuonesha.
Shambulizi limekuja
wakati ambao Umoja wa Ulaya umegawanywa kwenye mstari wa wahamiaji wa kigeni.
Ukiacha Ujerumani nchi nyingi za Ulaya hazikuwa tayari kuwapokea wakimbizi hao,
na Ufaransa ilikuwa moja ya nchi hizo ambazo hazikuwa zikiwapokea kirahisi
wahamiaji hao. Lisaa limoja kabla ya shambulizi Ufaransa ilishafunga mipaka
yake, baada ya shambulizi nchi zingine za Ulaya zikafunga mipaka, na kwa muda tatizo
la wakimbizi likawa linaufumbuzi.
Lakini shambulizi
limekuja wakati ambao taifa la Urrusi linabadilisha mwenendo wa vita ndani ya
Syria. Urusi imeweza kubadilisha mwenendo huo kiasi kwamba tangu mwaka 2011 kwa
mara ya kwanza Bashir al Assad ameweza kuiacha Damaskasi na kwenda Moscow
kumshukuru Putin ‘Personaly’ na kurudi Damaskasi.
Ni kwamba Putin
amempa Assad ‘Confidence’ kiasi anaweza kukiacha kiti chake wazi katika wakati
mgumu kama huo na kwenda kumshukuru Putin kwa kumsaidia kuwachapa ISIS.
THE PICTURE WHICH SURPRISE THE WEST.
Hii iliwa ni
taarifa mbaya sana kwa Marekani, Ulaya, Uturuki na nchi za Kiarabu zilizo
kwenye muungano huo wa kumng’oa Assad. Lakini zaidi ilikuwa ni tusi kubwa kwao
na kwa taasisi zao za usalama na ujasusi, kwamba Putin na Assad wamekuwa na
ngome imara na mfumo bora wa ‘ku-keep information’ kiasi Assad achomoke na
kurudi bila wao kunusa chochote.
Lakini zaidi Urrusi
anaelekea kumpa Assad ushindi kama ataendelea hivi bila kupata kipingamizi, Marekani
peke yake na wanamgambo wake ‘wa msimamo wa wastani’ na baadhi ya nchi
washirika wanaelekea kushindwa, na kama hakitafanyika chochote, Assad atabakia
Damaskasi, na sisi tutaonekana vichekesho kwenye uso wa dunia.
YES HAVE A SMILE
Hivyo umoja wa
Ulaya, kwa maana ya Nato wanakiwa kwenye uwanja wa vita kumpa upinzani Mrusi na
kuwapa nafasi Marekani na wenzake kumalizia kazi waliyo ianza.
Ufaransa
anachotakiwa kufanya ni kugusa kifungu kimoja kwenye katiba ya Ulaya na NATO
watakuwa uwanjani, na hata kabla Hollande hajafanya hivyo viongozi wa nchi hizo
na wakuu wa NATO wako ‘standby’ wanasubiri mualiko wa Hollande waanza kazi.
Bado unafikiri
mashambulizi haya yamefanywa na watu wendawazimu wenye ndevu nyingi na
wanaongea lugha ya kiarabu? Fikiria tena …
Ukweli ni kuwa
Washington wanaona uwezekano wa kupoteza nafasi ya ‘U-Super Power’, na
kushindwa kwenye vita vyoa vya kutengeneza na washirika wao wakiwemo ISIS. Ujio
wa Putin ni msiba kwao, lakini zaidi Putin ataonekana ni kiranja mpya kwenye
uso huu wa dunia. Kwahiyo watu wazima wale Brennan na wenzake walipokutana wakaweka
mazingira ya hii ‘False Flag’ ambayo itamkaribisha NATO uwanjani.
UPANDE MMOJA WA SAFU YA WWIII ...
NATO na washirika
wake akiwemo kiongozi wao Marekani, hata kidogo mabomu na risasi zao hazita
wagusa ISIS, na wala vituo vya mafuta ya magendo vinavyo shikiliwa na ISIS kwa
ajili ya kuuza mafuta ya magendo kwa mwanachama wa NATO, Uturuki havita guswa.
Wala bomba la mafuta linashikiliwa na ISIS kwenda Uturiki halitaguswa. Nguvu
hiyo kubwa itaelekezwa kwenye kumshambulia Assad na vikosi vyake na kujaribu
kumnyima pumzi Mrusi ambaye anashirikiana na Iran. Hili linanikumbusha hadithi
ya WWI ilivyoanza.
Wakati WWIII
itakapo andikwa kwenye historia, shambulizi la Paris halitaachwa kutajwa kama
moja ya karata muhimu zilizo chezwa na wakubwa kabla ya zahama hilo kuanza.
Kaa vizuri historia
inakaribia kujirudia, waandishi wa historia wakiwa ni walewale, amka sasa, acha
kumnyoeshea kidole yule mwenye kanzu, au huyu mwenye ngozi ya rangi ile, wakati
adui yetu akicheza muziki kwa raha zake. Vita dhidi ya Ugaidi havimlengi yeyoye
ila WEWE na FAMILIA YAKO. Wewe ndiye gaidi, bila kujali rangi yako, dini yako,
kabila lako, utaifa wako, wewe ndiye gaidi, ilimradi tu unayo uwezo wa kufikiri
kwa akili huru, bila kutegemea CNN au Aljazeera, basi wewe ni gaidi na ni
hatari kwa usalama wa dunia, na tizama kila sheria inayo kuja baada ya matukio haya
kutokea inamkandamiza nani kama si wewe?
Sheria hizo
hazitazami unayo kanzu ama la, una ndevu nyingi au huna kabisa, hapana
Micrichip ikija kama njia ya kuzuia ugaidi mtapewa wote, sheria za uhamiaji
zikija zitawabeba wote, kamera zikisambazwa mitaani zitatumulika wote, sheria
ya kutembea mwisho saa 12 ikija itamhusu kila mtu. Halafu bado unasema Marekani
na washirika wake waongeze msuli na nguvu dhidi ya magaidi, bila kujua gaidi
hasa ni wewe.
Amka ndugu, soon
your next ….
Catch You Next Time
here here ……
Mkuu nafuatilia habari zako kwa ukaribu mno endelea kunifungua ubongo
ReplyDeletekaribu sana na waalike wengine ...
Deletekila siiku akili yangu inapata kitu kipya kutoka kwako. naipenda sana hii kazi....
ReplyDeleteblogger @ www.roryafinest.blogspot.com
Yaani nimekua nikisoma makala zako Bro na baada ya hapo ni kifanya INTEGRATION yaani uhalisia upo pale pale.......
ReplyDeletemkuu napataje contact zko
ReplyDeletedaa nafikiria salim ana kichwa cha aina gani daah
ReplyDeleteYou make me smile
Delete