Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Wednesday, April 1, 2015

JE TUPO WENYEWE KWENYE ULIMWENGU?

“Wale ambao hawawezi kukumbuka historia, ndiyo ambao kimakosa wanarudia makosa ya kihistoria” - George Santayana



     Rais wa 40 wa taifa la Marekani, mwenye daraja la 33 kwenye asasi ya Freemasons na pia mwanachama wa asasi nyingine ya siri inayokwenda kwa jina la Knights of Malta na mwenye damu ya kifalme ya kishetani, Ronald Reagan mara kwa mara amekuwa akizungumzia ni namna gani dunia nzima itaweza kuungana endapo patakuwepo na kitisho cha uvamizi wa viumbe kutoka sayari nyingine.


Kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1987, Septemba 21 alisema;


“Katika hali yetu kubwa ya chuki na utengano tuliyo nayo hivi sasa, mara kwa mara tunasahau ni kiasi gani binaadam tumeungana. Huenda tunahitaji kitu kutoka nje, kitisho cha ulimwengu kitakacho tufanya sisi kuweza kutambua umoja huu tulio nao. Nimekuwa nikifikiria ni namna gani tofauti zetu zitatoweka pale ambapo tutakuwa tunapambana na kitisho cha viumbe kutoka nje ya sayari yetu”.( http://www.bibliotecapleyades.net/exopolitica/exopolitics_reagan03.htm)


Mwaka 1988 Mei 5, White House, kwenye chumba kilicho jaa waandishi wa habari, Reagan alisema,
 “Nimekuwa nikijiuliza mwenyewe kwamba itakuwaje kama sisi sote hapa duniani tukagundua ya kuwa kuna kitisho dhidi yetu kutoka nje ya dunia yetu … nguvu ya kutoka kwenye sayari nyingine. Je si mara moja tu tutaweza kutambua kuwa hatuna tofauti yoyote baina yetu, kwamba wote tu binadamu, wananchi wa dunia na je, hatutaungana kupambana na kitisho hicho?”( http://www.bibliotecapleyades.net/exopolitica/exopolitics_reagan03.htm)


Wazo hili la kuwa kuna au kutakuwa na kitisho kutoka nje ya dunia yetu, nje ya mfumo wetu wa jua, yaani nje ya galaxy ya Milk Way, raisi huyu amekuwa akilitaja mara kwa mara wakati na baada ya uongozi wake.

Henry Kissinger Kwenye mkutano wa Bilderberger, Evians, Ufaransa mwaka 1992 alisema,
“Leo hii Marekani itakasirishwa endapo Umoja wa Mataifa utaingia Los Angeles kutuliza amani. Lakini kesho watafurahia kitu hicho! Hii ni kweli hasa endapo wataambiwa kuna kitisho kutoka nje ya sayari yetu kinacho tishia uhai wetu.”( http://www.thirdworldtraveler.com/One_World_Government/Council_For_Relations_TBG.html)
“Itakuwa hivyo kwa watu wote wa dunia ambapo wataomba msaada wa kupambana na kitisho hicho. Kitu kimoja ambacho kila mtu anakiogopa ni kile ambacho hakifahamiki. Walimwengu watakapo letewa kitisho hicho, haki zao za msingi wataziachia na kuzikabidhi kwa serikali ya dunia ambayo itawahakikishia usalama wao.”( http://www.thirdworldtraveler.com/One_World_Government/Council_For_Relations_TBG.html)

Katika kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Marekani vyombo kadhaa vya habari na mitandao ya kijamii vimekuwa vikiripoti kuwa wananchi wa Marekani wangelipendelea kumpa Obama ushindi kwenye uchaguzi huo kama shujaa ambaye mwenye uwezo wa kuliokoa taifa hilo kwenye shambulizi la viumbe wasio julikana kutoka kwenye sayari nyingine. Asilimia 72 ya wananchi wataifa hilo wanaamini juu ya kuwepo kwa viumbe hao na uwezekano wa kutokea kitisho hicho.

Kwenye miaka ya karibuni neno ‘UFO’ (Unidentified flying object) limechukua kasi kwenye vyombo vya habari, hasa nchi za Magharibi, Asia, na Marekani. Vyombo hivi mwonekano wake ni duara lakini pia vinaweza kuwa na umbo jingine tofauti na hilo kama tutakavyo ona. Taarifa zisizo rasmi kutoka kwenye vyombo mbalimbali vya habari na maelezo ya watafiti mbalimbali kwenye suala hili ni kuwa UFO hutumika kama chombo cha anga cha kusafiria kwa viumbe hao wasio julikana kutoka sayari ya mbali. Lakini tabia yake ni tofauti sana na vyombo vyetu vya anga. 


UFO haionekani kuathiriwa na nguvu za mvutano, inakwenda kwa mwendo kasi mkubwa sana ambao hakuna vyombo vyetu vya kusafiria vilivyo pata kurikodiwa kuwa na mwendo kasi huo, huweza kubadili mwelekeo wake katika nukta yoyote ya safari yake, na inaweza kutoweka machoni pa mtazamaji ndani ya sekunde na asijue ameona nini.


Baadhi ya vyombo vikubwa vya habari, wanasiasa, wasomi, wanafunzi na viongozi wanauchukulia huu mtazamo mpya wa nafasi yetu na sayari yetu kwenye ulimwengu utatuletea amani ya kidunia ambayo haijapata kuwepo, umoja na udugu na maendeleo makubwa. Lakini kwa upande mwingine hasa watafiti huru na wasomi kadhalika wanaamini kuwa huu mtazamo mpya utatupeleka kwenye wakati mgumu na changamoto nzito tulizo pata kukutana nazo kwenye sayari yetu hii.

UFO kweli zipo au ni aina fulani ya udanganyifu?
Asilimia 72 ya wananchi wa Marekani wanaamini juu ya kuwepo kwa uhai nje ya sayari yetu na kwamba kuna viumbe wengine wanaishi huko. Asilimia 48 wanaamini juu ya kuwepo kwa UFO na asilimia 15 wanaamini kuwa wameona UFO. Asilimia 2-3 wanaamini kuwa wamewahi kutekwa na viumbe hao na kuingizwa kwenye UFO na baadaye kurejesha walipo kuwa.

Kuhusiana na UFO kumekuwepo na taarifa nyingi mno, kutoka kwenye magazeti mpaka majarida. Vijitabu na mavitabu. Kutoka kwenye taarifa za watu waliona UFO, walio waona viumbe hao, mpaka wale walio kamata na kupakiwa kwenye UFO. Wakati mwingine inakuwa ni vigumu kuzithibitisha taarifa hizo, wakati mwingine taarifa zinakuzwa kubwa kushinda tukio lenyewe, wakati mwingine kwa makusudi zinakuwa ni taarifa za kutengeneza au zenye upotoshaji. Lakini bado kuna wakati tukio moja linakuwa na mashahidi zaidi ya mmoja, linakuwa limeacha ushahidi wenye kuonekana, ushahidi unao weza kuugusa kwa mkono, ushahidi ambao ni zaidi ya maneno ya shuhuda.


UFO kwa wanahistoria zimerekodiwa kwenye majalada ya historia tangu enzi na enzi ya historia ya mwanadamu. Ingawa haipo kwenye mitaala ya somo la historia yenyewe, na hivyo ni kama hakuna kitu kama hicho.

Kuanzia mwaka 1991 mpaka 1993 jiji la Mexico lilifunikwa na taarifa za kuonekana kwa UFO. Julai 11, 1991. Watu 17 ambao hawana mahusiano yoyote katika maeneo tofauti ya jiji hilo wakiwa na kamera zao, waliweza kunasa picha ya diski kubwa la chuma karibu kabisa na usawa wa jua mbalo muda mfupi nyuma lilikuwa limepatwa na mwezi. Diski hilo lilikuwa limening’inia angani kwa muda bila kusogea upande wowote ule. Lakini watu hawa hawakujua kama wamepiga picha UFO mpaka watu wengine walipo ng’amua wakati wanaoneshwa video hizo.

Kutoka hapo watafiti wakaanza kupokea video na picha nyingi zinazo onesha umbo la duara kubwa la chuma, UFO zikiwa kwenye anga la Mexico ambazo picha zake zilipigwa na watu binafsi. Vyombo vya rada na hata marubani kadhaa wameripoti kuviona vyombo hivyo vikivinjari katika anga la Mexico. Kutoka kwenye uwanja wa Benito Juárez International Airport Machi 4-5, 1992 iliripotiwa marubani wawili na kuthibitishwa na rada ya uwanja huo juu ya kuionekana kwa UFO.  Mmoja wa rubani aliyehojiwa kuhusiana na tukio hilo alisema;
 ‘‘Ilikuwa ni siku nzuri. Mwanzo nilifikiri ni puto (balloon), lakini lilikuwa likisafiri haraka. Tuliliona vizuri na haikuwa ni ndege’’(http://www.bibliotecapleyades.net/ciencia/ufo_briefingdocument/1991.htm)


Tukiwa bado tupo hapo Mexico, ripoti nyingine inasema,
Jeshi la anga la Mexico limetoa kaseti ya video ambayo wataalam wa UFO wamedai ni UFO kumi na moja zilizo naswa na kamera zilipokuwa zikiizonga zonga ndege ya jeshi hilo iliyo kuwa ikifanya doria. Jaime Maussan ambaye anaamini juu ya kuwepo kwa vyombo vinavyo ruka vya viumbe wengine kwenye sayari yetu alisema alipokuwa kwenye mkutano na waandishi wa habari kuwa, vitu hivyo ni vya kweli na vinaonekana kusimamiwa na viumbe huru kutokana na tabia viliyo onesha. 

Vyombo hivyo vilikuwa vikifukuzwa na ndege ya doria baada ya kudhaniwa ni ndege za wabeba dawa za kulevyea, lakini ghafla zilitoweka na zilipo onekana tena zilikuwa zimeizunguka ndege ya doria ya jeshi la anga la Mexico.

Mexico imekuwa na historia ndefu ya kuonekana kwa UFO, nyingi kati ya hizo zimekuwa zikidharauliwa na wana sayansi kama ni vipande vya uchafu ama vumbi kutoka kwenye anga, roketi za kivita, Maputo ya hali ya hewa au uzushi.

Januari 2, 1993, kila gazeti kubwa ndani ya Mexico na taarifa za vyombo vingine vya habari viligubikwa na habari moja tu ya chombo kisicho fahamika na chenye tabia zisizo lingana na chombo chochote kinacho julikana na wakazi wa sayari hii. Chombo hicho kilibaki kwenye anga la Mexico kwa masaa matano. Gazeti moja kubwa la Mexico linalo kwenda kwa jina la, La Prensa lilikuwa na kichwa cha habari kilichosema, ‘Maajabu! UFO kwenye anga la Mji Mkuu’. Tukio hilo pia lilirekodiwa na rada kutoka kwenye uwanja wa kimataifa wa jiji la Mexico.( Gary Bates: UFOs and the Evolution Connection Uk 179)


Brit Elders mtafiti kwenye masuala ya UFO, alipokuwa akizungumzia tukio la UFO kunasa kwenye rada kwenye jiji la Mexico alisema,
 “… rada ya Mexico imefuatilia na kurekodi UFO sawa na yale yanayo semwa na watu waliyo ona kwa macho yao wenyewe kutoka aridhini na kutoka kwa marubani wa ndege wakiwa angani.”( Chuck Missler na Mark Eastman ‘ALIEN ENCOUNTERS’)

Serikali ya Mexico ilipo shinikizwa na wadau mbalimbali juu ya kulifanyia uchunguzi suala hili la UFO ilifanya mkutano na waandishi wa habari ambapo serikali ilitambua juu ya kuonekana kwa vyombo hivyo lakini ikasema – UFO hazina madhara yoyote kwa wananchi.


Tukitoka Mexico tunaelekea kwenye nchi inayo kaliwa kimabavu na utawala wa Kizayuni, Palestina. Septemba 17, 1996 kituo cha Polisi cha Tel Aviv kilipokea dazeni za simu toka kwa wakazi ambao wameona kitu chenye mwanga mkali kikifanya sarakasi kwenye anga lao kwa namna ambayo hakuna ndege wala helikopta ambayo ingeweza kufanya kitu kama hicho.
Mwaka 1997 kwenye mahojiano na jarida la British Journal UFO Reality, Rnen alisema yafuatayo kuhusiana na kile kinacho tokea kwenye aridhi hii inayo kaliwa kimabavu na Wazayuni, 

“Vyote kwa pamoja UFO zimeanza kuonekana kwenye maeneo ya Israel, na pia Iran na Australia kwa wakati mmoja. Agosti mwaka 1996 wimbi la mashahidi walio ona kwa macho UFO, na haikuwa watu wa kawaida peke yao, hata maofisa wa polisi na jeshi. Taarifa zilizo pokelewa ni nyingi na zilikuwa zikiongezeka siku hadi siku na hata kuwa ni vigumu kuweka taarifa ya mtu mmojammoja.”( Chuck Missler na Mark Eastman ‘ALIEN ENCOUNTERS’ uk 14-17)


Tukio hilo lilishuhudiwa na maelfu ya watu ambao waliona UFO ikisafiri taratibu mita 200 kutoka aridhini. Vituo vya polisi na vituo vingine vya dharura vilipokea simu za kutosha kutoka kwa watu ambao walitaka kujua kulikoni na wengine wakishuhudia kuyaona hayo. Ilikuwa ni usiku wa manane, saa nane na nusu usiku, watu walisimama na kutizama UFO kama kitu kubwa mno lilio na taa na muangaza wa kutosha kumulika anga la vitongoji viwili kwa mpigo. Tukio hili lilishuhudiwa kwa takribani dakika kumi, halafu ghafla, bila tahadhari yoyote chombo hicho kikatoweka kwenye macho ya watazamaji wake.( Chuck Missler na Mark Eastman ‘ALIEN ENCOUNTERS’ uk 14-17)

Machi 13, 1997 jimbo la Arizona kwa dakika 106 midaa ya saa mbili na robo usiku lilishuhudia kile ambacho baadaye kilijulikana kama ni UFO. Baada ya tukio hilo simu zilimiminika kwenye vituo vya dharura vya jimbo hilo kutoka kwa mashuhuda wa  maeneo kadhaa ikiwemo Prescott, Wickenburg, Glendale, Phoenix, Scottsdale na Tempe.

 Kutoka kwa mashuhuda ni kuwa chombo hicho kilikuwa karibu kabisa na kituo cha Luke Air Force, ndege aina ya F-16 tatu zilitoka kwenda kukifuatilia chombo hicho kujua kulikoni. Hata hivyo ndege hizo za kijeshi zilipo karibia chombo hicho kilitoweka ghafla kama kupepesa mboni ya jicho. Hata hivyo maafisa wa kituo hicho cha Luke kama ilivyo tegemewa walikataa kuwa hakuna ndege za kijeshi zilizo tolewa kwenda kukifuatilia chombo hicho na wala hawafanyi tafiti juu ya UFO.


Peter Davenport kutoka kwenye kituo cha taifa cha kutoa taarifa za UFO kilichopo Seattle, Washington alipokea mamia ya simu kuhusiana na tukio hilo na maoni yake binafsi ni kuwa,
 ‘Tukio la Arizona lilikuwa wazi kabisa kati ya matukio niliyo pata kuyaona … tulicho kiona pale ni kitu cha kweli kabisa. Tayari wako hapa (viumbe kutoka sayari nyingine)’(Chuck Missler na Mark Eastman ‘ALIEN ENCOUNTERS’ uk 14-17)


Miezi mitatu baada ya tukio, Juni 18, 1997 tukio hilo lilianza kuzungumziwa kwenye vyombo vikubwa vya habari duniani na kuanza kupata mvuto na kuvuta hisia za watu. Liliripotiwa kwenye NBC, MSNB,CNN na ABC.
Mike Fortsen, ambaye alishuhudia tukio hilo kwa jicho lake mwenyewe alipokuwa anahojiwa na CBS kuhusiana na tukio lenyewe la Arizona alisema hivi,
 ‘Ninayo uhakika kabisa na kushawishika kuwa kile kilikuwa ni chombo cha viumbe kutoka kwenye ulimwengu mwingine. Ni na hakika kabisa viumbe hawa si kwamba wametoka kwenye sayari nyingine, bali kutoka kwenye uwanda mwingine.( Chuck Missler na Mark Eastman ‘ALIEN ENCOUNTERS’ uk 14-17)

Kitu kidogo nikiweke sawa hapa kabla ya kuendelea mbele, ingawa na amini kitu hicho nitakizungumzia kwa mapana zaidi mbele, lakini ili nisikuache sana ngoja nikigusie kidogo. Fortsen amesema ‘kutoka kwenye uwanda mwingine’. Neno ‘uwanda’ ni neno ambalo utalikuta sana kwenye aina hii ya habari. Dunia tunayo ishi sasa ni maarufu kama ‘pande tatu’ au ‘miwanda mitatu’ miwanda ni wingi wa uwanda. Wanaita ‘Three Dimensional’ au 3D. Yaani kimo, urefu na upana. Hivyo kutoka uwanda mwingine ni kutoka nje ya mfumo wetu wa jua wa Milk Way, kwamba ni kutoka kwenye galaxy nyingine isiyokuwa na 3D!

Tukio hili la Arizona liliripotiwa pia na USA Today kwenye kurasa nzima iliyojaa mnamo  Juni 18, 1997. Kwenye makala hiyo mwandishi na mtafiti Richard Price ameliita tukio hilo,
“Tukio la ajabu na kushangaza la UFO tangu miaka 50 iliyopita.”( USA Today Juni 18, 1997)
Kitu kimetokea kwenye anga la Arizona usiku wa Machi 13. Hakuna mwenye uhakika wa kwamba kilikuwa ni kitu gani, lakini maelfu walikiona, dazeni kadhaa walikirekodi kwa njia ya video na watu kwenye jimbo zima bado fikra zao zimenaswa kwenye tukio hilo …. 
Mashuhuda hao wanakubaliana kwenye vitu vitatu juu ya tukio hilo. Kwanza jichombo lenyewe lilikuwa ni jikubwa mno. Makadirio ya karibu ni kuwa ukubwa wake ulikuwa ni sawa na urefu wa viwanja vitatu vya mpira wa miguu.
Uchambuzi wa kompyuta kupitia video zilizo rekodiwa wamekadiria ni sawa na futi 6000, au zaidi ya maili moja.

Pili chombo hicho hakikutoa ukulele wowote, kipo kimya kama hakipo.
 Tatu kilikwenda taratibu juu ya eneo la Phoenix, imekadiriwa kuwa na mwendo kasi wa 30 mph. Mara kadhaa kilikuwa kikinata kwenye anga.( Chuck Missler na Mark Eastman ‘ALIEN ENCOUNTERS’)
Venezuela, eneo la Maracaibo, Oktoba 24, 1886.Turkey eneo Istanbul, Mei 2008 – Septemba 2009.Portugal eneo la Fatima, Agosti 13, 1917, Septemba 13, 1917, Oktoba 13, 1917.Marekani, Aurora, Texas, Aprili 19, 1897.Urusi, Podkamennaya Tunguska River, Juni 30, 1908. Marekani, Stephenville, Texas, Dublin, Texas, Crawford, Texas, Januari 01, 2008 – Februari 09, 2008. Mexico, jiji la Mexico, Agosti 6, 1997. Brazil, Varginha, Minas Gerais, Januari 20, 1996. Australia, Victoria, Agosti 8, 1993. Uingereza, London, Aprili 21, 1991. Kanada, Montreal, Quebec, Novemba 7, 1990. Belgium, Ans, Wallonia, Machi 30, 1990. New Zealand, South Island, Disemba 21, 1978.

Kwa takribani miaka hamsini sasa tangu serikali mbalimbali duniani na watafiti walipoamua kulishughulikia suala la UFO na kutafuta majibu ya maswali kuhusiana na asili yake ni nini na tija au madhara yake kwa binadamu ni yapi hakuna kati ya hao walio kuja na majibu ya kuridhisha au majibu rasmi kuhusiana na suala hilo.


Kama UFO zitakuwa ni kweli zipo, na asili yake hasa ni kutoka nje eidha ya sayari yetu au galaxy yetu, ukweli huo hapana shaka utakuwa ni changamoto ya namna yake kwa binadamu wote. Kwa upande mwingine, ikiwa UFO si hivyo tunavyo ambiwa na si hivyo inavyo elezewa na wale walio shuhudia , basi vyombo hivyo vitakuwa ni ushahidi tosha wa mpango kamambe ambao mabilioni ya binadamu hawafahamu hatima na malengo yake ni nini na ambao athari yake huenda ikamuathiri kila binadamu aliyepo kwenye sayari hii.

NDIYO KWANZA TUNAANZA ..... NGOMA INAENDELEA HAPAHAPA ... CATCH YOU NEXT TIME ...

3 comments:

  1. Mmh sasa izi ufo mbona n za ajabu zimetengezwa na nani na zinahifadhiwa wapi

    ReplyDelete
    Replies
    1. Endelea kufuatilia hii blogi na utapata majibu yako na zaidi ...

      Delete
  2. UFO is man made so the eliens .... mengi yanaendelea ulimwengu huu elimu nyingi imefichwa ili kuamini wanachotaka kuamini... nimesoma mengi unajua vingi Bro Salim hongera, elimu yako itoe kwa jamii tafuta njia hii ya blog haitoshi. Reptilian r real ! Weka tofauti dunia inahitaji watu kama nyinyi. Mi niko nafanya kwa kadri yangu kuiokoa dunia yetu ...

    ReplyDelete