Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, March 8, 2015

ISIS NA KHILAFAH YA OBAMA



IS (Islamic State) inatoa upenyo sawia kwa majeshi ya NATO na Marekani kuwepo na kuendelea kuafanya ‘kazi’ zao ndani ya Mashariki ya Kati.




Kila aina ya vita ya Ugaidi, inazalisha mamia kwa maelfu ya magaidi na kuwahakikishia majeshi ya nchi za Marekani za Ulaya kuendelea kuwepo katika eneo hilo. Nchi kama Iraq, Syria na Libya ambazo hazikuwa na watu wanao itwa Al Qaeda, lakini baada ya uvamzi wa wa majeshi ya US-NATO kumekuwa na kila aina ya Al Qaeda katika maeneo hayo na zaidi.


Sasa tunaiona IS kwenye uso wa dunia, kwa furaha, uhuru wanacheza ‘wimbo’ wowote wanao taka bila kuguswa na yeyote. Limekuwa ni jeshi kubwa kutoka kwenye mitandao ya kijamii, mpaka kwenye maisha halisi, wanamiliki silaha nzito na zile za kisasa. Wanapokea misaada ya kutosha kutoka baadhi ya nchi za Kiiarabu, Ulaya na Marekani.

Kukuwa kwa IS swali moja ni lazima tujiulize wenyewe, ‘Hivi inawezekana kweli kwa kikundi cha ugaidi kama IS kukuwa na kumiliki nguvu zote hizo za kifedha na kisilaha bila kuwa na msaada wowote kutoka nchi yeyote, shirika lolote?


Unapoitazama IS na vikundi mfano wake na maeneo ambayo shughuli zao za kusimamisha Khilafa zinalenga, utaona kuna maeneo manne mahususi ambayo yanalengwa.

Mwaka 2007 kiasi kukubwa cha gesi kiligundulika Mashariki mwa eneo la Mediterania ikihusisha Syria, Lebanon, Palestine, Israel na Cyrups, lakini pia Iran na Qatar.

Kisha vita vya kumiliki njia ya bomba la mafuta linalofahamika kama ‘Bomba la Iran-Iraq-Syria’ na ‘Bomba la Qatar’ ambayo kufika nchi za Ulaya ibidi yapitie Syria kwenye pwani ya Mediterani halafu Uturuki kisha Ulaya.

Kama Urusi na Ulaya watakuwa na umiliki wa gesi zao, watakazo safirisha kupitia kwenye mabomba yao, hiyo ni kusema kuwa Urusi na Irani watamiliki mpaka 50% ya mafuta yatakayo kwenda Ulaya. Kwa maneno mengine Urusi na Iran kwa pamoja zitakuwa zinatoa changamoto kwa Marekani ikiwa inastahiki kukalia kiti cha Super Power au La?

Upande mwingine wa habari ni kuwa si muda mrefu sana Marekani ataendelea kukalia kiti hicho, kama tunavyo jua kwa upande wa Biashara tayari Marekani imeshapitwa na China, lakini anayeandaliwa kuchukua kiti hicho baada ya Marekani si Mchina, wala Mrussi bali ‘Mwiisrael’.

Lakini Israel mwali mpya kwenye nyumba ya ‘Usuper Power’ hatoweza kupendaza na kukalia kiti hicho kwa imani ikiwa kuna nchi kama Iran, Iraq, Syria na washirika wao bado wako hai. Nchi hizi inabidi zivurugwe na kuchanwa chanwa kama makaratasi kwa kutumia aina yeyote ya mbinu, njia na mipango itakayo zalisha matokeo hayo, iwe ni Jihadi, iwe ni Khilafa, iwe ni Shia vs Sunni chochote kile, ilimradi mwali mpya akiingia akalie kiti chake kwa amani.


Qatari ilitoa dola milioni 2.5 kwa Abu Bakr al-Baghdad iliaweze kuitengeneza ISIS na yeye awe ni Khalifa wa eneo hilo.

Baada ya kugundulika kuwepo kwa kiasi kikubwa cha gesi 2007, Qatari ilianza kwa kumshawishi rais Assad kuachana na bomba la gesi la Iran-Iraq-Syria na ajiunge na Bomba la Qatar. Assad akajibu kuwa hawezi kumsaliti Mrussi ambaye ni rafiki na mshirika wake.

Aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa bwana Roland Dumas mwaka 2009, akasema kuwa Qatar ililipa dola bilioni 10 kwa waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Mr. Dovutoglu kwa ajili ya mpango wa kuivunja vunjia Syria kama siyo kuipindua kabisa.


Baada ya mpango wa Saudia wa kuiangusha Syria kushindikana, na wapiganaji wa kulipwa wapatao 20,000 kuchakazwa na jeshi la Syria, na propaganda za kuichafua serikali hiyo kwenye vyombo mbalimbali vya habari duniani kugonga mwamba, ndipo Saudia ilipongia kwenye kila mtaa wa dunia hii kuwasaka ‘magaidi’ ambao watakwenda kusimamisha Khilafa Syria chini ya Al-Baghdad, hata hapa kwetu Tanzania waliingia, na vijana wengi wanao fuata mkumbo tukawapoteza eidha kwenye magereza au kutaka kwenda kwenye nchi hizo zinazo taka kusimamisha Khilafa ya McCain na Obama. Mpaka sasa wengi wapo jela na wengine wameuwawa. 

Saudi na timu yake ya kusaka vijana walipita kwenye nchi zaidi ya 80 ikiwemo nchi za Ulaya na Marekani ambako huko walifanikiwa kwa kiasi kikubwa kupata vijana wa kwenda kupigana Syria kwa maslahi yao, lakini kwa kutumia jina la dini yetu tukufu; Uislam.


Jeshi la Iraq lililo pewa mafunzo kwa gharama kubwa na serikali ya Marekani, pamoja na kupatiwa silaha za kisasa kabisa, halikuweza kusimama mbele ya wanamgambo wa ‘kiislam’


wa Obama. Wakati mwingine wanajeshi hao walikimbia na kuziacha silaha zao, na vijana wa Obama wakaziokota.



 Nigeria nako tumeona mchezo kama huo, na sasa maafisa kadhaa wa jeshi la Nigeria wako ndani kujibu tuhuma za kwanini jeshi lao lilikimbia na kuwaachia Boko Haram silaha.

Ni kama mchezo wa kiigiza, hivi inakuingia akilini kabisa kuwa jeshi la nchi linazidiwa nguvu na kuacha silaha zao na kukimbia? Au ni njia za kuhakikisha kuwa magaidi wanamiliki silaha sawa na serikali wanayo pambana nayo?


Ghafla ISIS wanaonekana wako mtaani na vifaru, makombora ya kutungulia ndege, bunduki nzito, Helikopta nzito. Vyote wameteka kutoka kwenye jeshi la Iraq. Mara mji mmoja baada ya mwingine ukaanza kuanguka kwenye mikono yao. 



... ITAENDELEA ...

No comments:

Post a Comment