Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Thursday, March 12, 2015

ISIS NA KHILAFAH YA OBAMA PT 2


Ushirika wa US-NATO 2011 ulianza kuwagawia silaha vikundi vya kigaidi wakiwemo Al Qaeda kwa ajili ya kuangusha utawala wa Libya. 


Silaha hizo nzito zilisafirishwa kutoka Libya kupitia Kusini mwa Uturiki kisha zikavushwa mipaka na kuingia Syria mpaka kwenye mikono ya ‘FREE SYRIAN ARMY (FSA), JABHAT AL NUSRA (AL Qaeda wa Syria) na vikundi vingine vya ugaidi ambavyo Obama anaviita ‘Magaidi wenye Msimamo wa Wastani’ ambao wanastahiki kupewa silaha.  AJABU SANA YULE AMBAYE UMEKUWA KWA SIKU ZOTE UKIMUITA ADUI, NA AMBAYE IMEBIDI KUIITA DUNIA NZIMA WAKUSAIDIE JUMPIGA, LEO UNASEMA NI SAWA AKIPEWA SILAHA?!!! AMA KWELI UKISTAAJABU YA MUSA ...

Kwa upande mwingine FSA, NUSRA pamoja na ISIS wanafanya kazi pamoja na kushirikiana na June 2014 NUSRA na ISIS zilisimama pamoja kama kikundi kimoja.


Mtandao wa magaidi kwa makusudi makubwa kabisa, umeachiwa huru ukuwe na ukomae kiasi cha kuchinja mamia kwa maelfu ya watu na dunia nzima kunyamaza kimya.

Mtandao huu tangu ulipoanza kwenye miaka ya mwishoni mwa 70 wakati Mmarekani anapambana kumtoa Mrusi kwenye U-super Power, ulitumia jina la ‘HOLY WAR’ yaani ‘VITA VITAKATIFU’ au JIHAD, Kiongozi akiwa ni Osama Bin Laden, lakini nyuma yake wakiwemo, akina Abu Bush, Abu Kissinger, Abu Jimm Carter, Abu CIA na Abu Zbig mwenyewe,

Mtandao huo hivi sasa umetanuka na ukiwa na kisingizio cha ‘KHILAFA’ hivi sasa ni Jihadi ya kusimamisha KHILAFA, lakini sura za wafadhili zikibakia zile zile, Abu Obama, Abu Nato, Abu Zbig, Abu CIA, Abu Israel na wengine.


Kwa sasa mtandao huu umeweza kukusanya wanachama kutoka zaidi ya nchi 80, zikiwemo nchi za Ulaya na Marekani.

Marekani imekiri kupitia Retd. Lt.Gen. Ian Mclnerny kuwa ilishiriki vilivyo kuiyandaa, kuitengeneza na kuiacha ifikie hapo ilipo, ISIS.
Ukiacha taarifa hizo za kiongozi wa jeshi kukiri kuhusika katika kuitengeneza ISIS, taarifa zingine zinamuonesha Seneta John Mcain waziwazi akiwa amepiga picha na waasi wa Syria, ambao Marekani inakataa kuwaita magaidi. Kwenye Picha hiyo yupo mtu mashuhuri na maarufu ambaye Marekani inamtafuta, AL BAKR AL BAGHDADI aka ‘NEW OSAMA’

MCCAIN AKIWA NA AL BAGHDAD, BAADA YA KIKAO HICHI AL BAGHDAD AKAJITANGAZA KUWA KHALIFA NA MUDA SI MUDA ISIS IKAANZA KUPATA 'COVAREGE' KWENYE VYOMBO VYOTE VYA HABARI VYA MAGHARABI, NA HUKU KWETU IKAWA NI 'KU-COPY' N 'PASTE' HABARI HIZO NA GHAFLA ISIS IKIWA SI KITU KINACHO WEZEKANA KUSHINDWA TENA,

Lakini mbali na hili pia imefahamika kwamba Marekani imeshirikiana kwa karibu sana na Saudi Arabia, Jordan na Israel kuwasaidia waasi hao katika mipango yao ya kuivamia Syria.
Waasi hao wa Mr. Obama walipata mafunzo yao ya kijeshi katika kambi zilizopo Jordan, Uturuki na Qatar kabla hawajaingia Syria. Maeneo hayo yapo chini ya uangalizi wa NATO. Lakini zaidi waasi hao wa Obama, ISIS, FSA, JABHAT AL NUSRA walipopata majeraha walikwenda kutibiwa kwenye kambi za Israel zilizopo kwenye maeneo ya Golani yanayo milikiwa na Israel.
ALBAGHADAD ILIUNDA ISIS MWEZI MMOJA KABLA YA KIKAO HICHI CHA MCCAIN. NI KAMA KHALIFAH HUYO ALIKUWA AKIPOKEA MUONGOZO KUTOKA WASHINGTON KUWA KITU GANI AFANYE WAKATI GANI.

Msemo maarufu wa ‘Marekani hana adui/rafiki wa kudumu’ umedhihiri kwenye sera zake za mambo ya nje, hasa nafasi ambayo Seneta John Mcain aliyoitumia kuhakikisha ISIS na wenzake wanapata ‘Khilafa’ yao.

4 Februari 2011, NATO iliandaa mkutano kwa ajili ya kuanza mkakati wa kuishughulikia Syria na Libya. Mkutano huo mwenyekiti wake alikuwa ni John Mcain.

22 Februari 2011, McCain alikutana na Saad Harir Beirut na kumpatia jukumu la kuhakikisha waasi wa Obama wanapata silaha ambazo zitapelekwa Syria.
April 2013, Seneta McCain alitembelea kwa siri mji wa Idlib uliopo Kaskazini Magharibi mwa Syria na kufanya kikao na makamanda wa waasi na wanajeshi wao, ambao yeye McCain kupitia serikali ya Marekani anahakikisha kuwa wanapata silaha, fedha, matibabu na kila wanacho taka ilimradi eneo hilo la Mashariki ya kati liendelee kuwaka moto kwa jina la ‘Khilafa’.


Katika watu ambao McCain alikutana nao siku hiyo alikuwepo pia Abu Bakr al Baghdad, mtu aliye jitangaza mwenyewe kuwa ni Khalifa. Wakati McCain anakutana na AlBaghdad Marekani ilikuwa imeshatangaza zawadi ya dola milioni 10 kwa yeyote atakaye leta kichwa cha Albaghdad au atakaye pelekea kutoa taaria za kukamatwa kwake. McCain angeweza kushtakiwa kabisa kwa kushirikiana na Magaidi.

Lakini McCain si wa kwanza kufanya hivyo, wala hilo si jambo geni kwenye sera za mambo ya nje za Marekani. Bush alifanya hivyo kabla ya 9/11.

Ajabu ni kuwa ISIS baada ya ‘kuteka’ silaha hizo, walipita nazo mitaani waziwazi, wakijitapa na kuringa nazo. Lakini Marekani kinyume na sera zake za kivita, haikujaribu hata kuwashambulia ilikuharibu au kurudisha silaha zao, waliwaacha kama hawajui vile.


Muda huohuo Marekani ilikuwa ikiendesha mashambulizi ya drone Pakistan, lakini haikutumia drone zake kuwagusa ISIS katika mitaa ya Mosoul au kwengineko.


No comments:

Post a Comment