Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Thursday, February 26, 2015

HATUKWENDA MWEZINI PT 3

Kama tunavyojua mwezi haujazungukwa na blanketi la hewa kama hili la kwetu hivyo anga zima (Space) linaonekana jeusi tii hivyo hakuna kitu chochote kitakachoweza kurikodiwa nyuma ya weusi huo mpaka miale ya kamera iwe na nguvu ya kupenya weusi huo, lakini cha ajabu baadhi ya picha baada ya kuchunguzwa zimekutwa na duara kubwa nyuma wa weusi huo wa anga, duara mbalo kwenye picha zingine limetumika kama jua au chanzo cha mwanga wa jua. 


PICHA UNAZO ZIONA ZIMETUMIKA KAMA JUA KWENYE PICHA ZA APOLLO 11 NA APOLLO NYINGINE. LAKINI PICHA HIZO ZILIPONYAMBULIWA KWA KUTUMIA PROGRAMU NYINGINE KILICHO ONEKANA SI JUA BALI NI 'SPOT LIGHT' ZINAZOTUMIKA KURIKODIA MUVI.


Ni vipi duara hilo limeweza kurikodiwa nyuma ya kiza kinene cha kwenye anga?
PICHA HII INAJIELEZEA YENYEWE

Ingawa picha hizo zinaonesha anga likiwa safi na ndivyo lilivyo hatutegemei mawingu kwenye space lakini hakuna hata moja iliyonasa picha ya nyota za angani, ni ajabu sana katika weusi huo wa angani miongoni mwa vitu ambavyo vingeonekana kwa haraka na kwa wepesi zaidi ni nyota kwa sababu zinauwezo wa kuzalisha nuru mfano wa Jua lakini haikuonekana hata moja,

 cha ajabu zaidi kilichoonekana ni uso wa Dunia, kitu ambacho hakiwezi kuelezeka labda kwa nadharia za kibususa, Dunia haizalishi mwanga na katika mazingira hayo kuipata picha yake ni vigumu zaidi kuliko kuipata picha za nyota zilizoko angani, ni vipi katika umbali wa maili zote hizo waliweza kuipata picha ya dunia wakashindwa kuzipata picha za Nyota?


MAAJABU DUNIA INAONEKANA VIZURI KABISA, LAKINI NO STAR?

Katika picha ambayo Luna Module (LM) inaonekana ikikaribia kutua juu ya mwezi na kwa mbali dunia yetu na rangi yeka nzuri inaonekana kama jua linalozama, ni kitu gani kinachosababisha dunia isiyo zalisha mwanga wowote iweze kuonekana katika mazingira hayo na nyota yenye kuzalisha mwanga isionekane. 

MWISHO WA SIKU TUNAONA HATA HIYO INAYO ONEKANA NI 'DUNIA' NI KITU KILICHO ONGEZEWA KWENYE PICHA HIZI. KWAMBA HAKIKURIKODIWA MWEZINI BALI STUDIO.

Mazingira hayo ni magumu kwa mwanga kupenya kutokana na weusi mzito wa anga lililo izunguka dunia yetu kama picha inavyo onesha hivyo dunia yetu isingeweza kuonekana kutokana na kwamba haizalishi mwanga kama nyota wala haihakisi mwanga kama mwezi na hivyo ingekuwa ni sehemu ya weusi huo mzito wa anga na isingerikodiwa katika picha hii.

 Halafu ni kitu gani kilichozuia nyota ambazo zina uwezo wa kuzalisha mwanga zisirikodiwe katika picha hii. Hapana, tunaweza kuziona kwa jicho la kawaida wakati wa usiku iweje kwenye kamara hii zisirikodiwe. Picha hii ni maalum kwa kurubuni mawazo ya watu, lakini kiuhakika kitu kilicho rikodiwa kwenye picha hii hakiwezi kuelezeka na kuleta maana kwenye elimu ya mambo ya picha na wala kwa mtu mwenye mawazo na fikra huru, ni picha ya kughushi.


Picha zingine zimekuwa zikionesha mwanga wa Jua mahala ambapo wanaanga wamesimama juu ya mwezi na kwengine kote ni giza hii inakuwaje, ina maana huko angani jua linabagua kumulika baadhai ya sehemu na kuacha kwengine, baadhi ya picha utaona kuna mwanga mkali mahala waliposimama wanaanga na kama baada ya m 10 hivi kuna kiza totoro hili ni jua la aina gani jamani?  Nisaidieni labda mimi sizifahamu tabia za jua vizuri.



Mahala pengine utaona vivuli vinapishana, yaani kuna vyanzo vya mwanga zaidi ya kimoja hili unaweza kuelezea vipi, inamaana huko mwezini kuna majua mawili au matatu au manne? Jamani hivi ni kweli wametuona kuwa sisi ni wajinga kiasi hichi.
Picha za vidio zinazo daiwa kurikodiwa mwezini wanaanga wakitembea mwezini zikioneshwa kwa kasi ya mara mbili (fast forwad) basi wanaanga hao wanaonekana wakikimbia kama ambao wako duniani ambako nguvu yake ya mvutano inasababisha kukimbia au kutembea kwa namna hiyo na si kwenye mwezi.
Safari nzima ilijaa vituko, picha zingine imeonekana chupa ya Coca cola sasa hatujui kama na huko mwezini walienda kuziuza ama vipi, alama za matairi ya gari tofauti na kile kilichokwenda mwezini hatujui kama na yenyewe yalipelekwa na hizo Apollo ama vipi, alama za miguu yao na matairi ya chombo chao vinaonesha alama ambazo uzito wake ni sawa na ule wa mtu anayetembea juu ya uso wa dunia kitu ambacho hakiwezekani kabisa sababu kwenye mwezi uzito unapungua maradufu kutokana na kutokuwepo kwa nguvu kizani.


Mahala ambapo Apollo imetua hapa oneshi shimo lolote kutokana na kishindo cha kutua kwake, na inaponyanyuka utadhani inavutwa na uzi kwenda juu, mahala pengine tunakuta alama za matairi mawili wakati chombo kilichopita kina matairi manne hii inakuwaje.

Lakini baada ya mambo kuwekwa wazi na NASA kuonekana wamedanganya kwenye safari ya mwezini, shughuli nyingine ikaanza ya propaganda na vipindi maalum kwenye televisheni na filam vyikielezea safari hiyo ilikuendelea kuwalaza mamilioni katika usingizi wa ujinga na imani wasiyoijua uhakika wake, imani ya kuwa tulikwenda mwezini. Mfano wa filamu hizo ni ile iliyoitwa Apollo13, na ile ya Froma the Earth to the Moon.


MZIKI HAUJAISHA  ...... UNAENDELEA HAPA HAPA .....

4 comments:

  1. Kazin nzuri sana kaka! Bravoh.
    Ningependa tuwasiliane zaidi ili unifundishe mambo mengi, navutiwa sana na kazi yako.
    tupakule@gmail.com, robhinson.edson@gmail.com +255 756891212

    ReplyDelete
  2. Ñna mm ningeomba uwe unarusha kweny google +

    ReplyDelete
  3. ipo kwenye google+ unless kama kuna tatizo, na akama lipo just tuambie na litafanyiwa kazi ASAP

    ReplyDelete
  4. Uwongo huu ushaota mizizi kwenye jamii kwani tumeaminishwa tangu wadogo unazani jamii itatuelewa tukiwaambia n uwongo

    ReplyDelete