Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Thursday, August 21, 2014

UKIMWI NA EBOLA NI SILAHA ZA MAANGAMIZI pt. 2


Tumejaribu kuangalia kwa kina ni namna gani virusi HIV vinaweza kusababisha ukimwi. Lakini si kwenye uchambuzi yakinifu wa kisayansi, wala si kwenye elimu ya matibabu na wala si kwenye sifa na tabia ya virusi hawa tuliko weza kupata uhusiano baina ya virusi wa HIV na ukimwi. Ukweli ni kuwa virusi hawa hawawezi kusababisha ukimwi katika kila hali kama tulivyo ona wenyewe kwenye maeneo ya msingi ambayo ndiyo yanayo shikiliwa na wale wanao beba nadharia hii ya HIV kusababisha ukimwi. Sasa kama HIV haisababishi ukimwi, je ni kipi hicho kinacho tupatia ukimwi?

Sababu zinazo msababishia mtu kuwa na ukimwi ni;




Sababu ya kwanza ni, kimazingira nayo inakutanisha vitu viwili, utapiamlo na ukosefu wa usingizi kwa muda mrefu. Mwaka 1985 mtafiti huru kwenye masuala ya ukimwi na mkurugenzi wa National Institute of Allergy and Infectious Diseases (NIAID) Dr. Anthony Fauci alitangaza kuwa utapiamlo ndiyo sababu kuu inayo sababisha upungufu wa kinga za mwili duniani kote, na hasa kwenye nchi zinazo endelea kama nchi za Afrika.

Utakumbuka takwimu zetu zilituonesha nchi zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara ndizo zinazo ongoza kwa wagonjwa, maambukizo mpaka vifo kwa wagonjwa wa ukimwi na ndizo nchi zilizo na tatizo kubwa la lishe. Umasikini, hali duni ya maisha, maji yasiyo salama yote haya yanapelekea kuwepo kwa maradhi ya kuambukiza sehemu nyingi za Afrika.

 Ukosefu wa usingizi kwa muda mrefu yote haya yanaudhoofisha mwili na kumpatia muhusika tatizo kubwa kwenye mfumo wa ulinzi wa mwili. Usingizi unasaidia mwili kujipumzisha, kuzalisha seli mpya zikiwemo za ulinzi, kuondoa seli zilizo kufa kama taka. Mtu anapo kosa usingizi kwa muda mrefu mfumo wa ulinzi lazima utadhoofu kwa vile hautakuwa na muda wa kujiboresha. (http://www.duesberg.com/articles/kmreason.html)

Tizama picha zote zinazo wekwa kwenye vyombo vya habari na mitandao kuhusu wagonjwa wa UKIMWI, utaona ni watu waliodhoofu kutokana na njaa, lishe duni na utapiamlo.


Sababu ya Pili ni ya Kikemikali.
Kemikali ambazo zinauathiri mfumo wa ulinzi wa mwili ni pamoja na dawa za AZT na tiba zingine za saratani, madawa ya protease inhibitors, dawa za maumivu, steroids, kokeni, heroini na methamphatamines kutaja kwa uchache. (http://aras.ab.ca/aidsquotes.htm)

Madawa ya saratani yanalenga kuharibu seli za bone-marrow ambazo kwazo seli zote za mfumo wa ulinzi ndiko zinako zalishwa. Pia zinaua seli za ulinzi zilizo kwisha tengenezwa na pia zinauwa B-Seli na seli nyekundu, maarufu kama red blood cells. Hii ndiyo sababu hakuna mgonjwa wa saratani anayetumia tiba ya aina hii na akapona au anayepigwa mionzi na akapona. Na hii ndiyo moja ya sababu zinatolewa kwa bei iliyo karibu na bure au bure kabisa sehemu mbalimbali duniani, kwa sababu lengo ni moja tu, kumuwa mtumiaji. (ibid)

Dawa za saratani zinauharibu mfumo wa usagaji wa chakula kwa kuuwa seli zilizopo sehemu ya ndani ya mfumo wa usagaji wa chakula na kuusababishia mfumo huo kupoteza uwezo wake wa kufyonza na kusaga virutubisho mbalimbali viingizwavyo na chakula, na hapo mgonjwa anapatwa na utapiamlo ambao nao utauwa mfumo wa ulinzi wa mwili. Hata pale zinapotumika kidogo dawa hizi za saratani zinauvunja nguvu kabisa mfumo wa ulinzi wa mwili, na kutengeneza mazingira ya mwili kupatwa na maradhi. AZT, ddl, ddC, C4T na 3TC yote haya ni madawa ya saratani na yanatumika  kama sehemu ya mchanganyiko wa kutengeneza madawa ya kuongeza kinga na madawa ya kurefusha maisha kwa wagonjwa wa ukimwi.(ibid)

 Mungu wangu umeona jina wanalo tumia, ‘madawa ya kurefusha maisha’, kisaikolojia wanakuambia maisha yako ni mafupi na madawa hayo ndiyo yatakayo refusha. Kwanini maisha yako ni mafupi? Kwa vile eti una virusi vya HIV. Virusi ambavyo vipimo inaweza kuonesha kwamba unavyo kumbe hauna, virusi ambavyo hata ukiwa navyo havina madhara kabisa na mwili wako. Lakini watakurubuni kwa matangazo mazuri na yale ya kutisha ili uanze kutumia madawa hayo, ambayo hasa ndiyo yatakayo kupatia ukimwi, kwani yatakwenda kuuvunja vunja na kuulia mbali mfumo wako wa ulinzi wa mwili.


Kuna madawa mengi yanayo tumika ambayo yanakwenda kuudhoofisha kama siyo kuuwa kabisa mfumo wa ulinzi wa mwili, hasa pale yanapo tumika kwa kipindi kirefu. Madawa kama Protease inhibitors yana madhara makubwa kwenye ini, na kulisababishia ini kushindwa kufanya kazi yake. Madawa ya kutuliza maumivu yanapo tumika mara kwa mara huleta matatizo kwenye mfumo wa ulinzi wa mwili.

Sababu za kibaiolojia.
Hapa kunajumuisha maambukizo ya mara kwa mara kwenye magonjwa ya zinaa kama kaswende, kisonono, na klamidia na pia magonjwa mengine ya hatari kama hepatitis, tuberculosis (T.B), Malaria, amoeba na vimelia kama giardia. Damu za kuchangia ambazo kutokana na hali ya uhitaji inapohitajiwa na mgonjwa na madhara yanayo kuwepo kwa mpokeaji damu katika mfumo wake ulinzi, mara nyingi mgonjwa anabaki katika mazingira ya kupata maambukizo ya magonjwa mengine. (ibid)



Sababu za kisaikolojia.
Wasiwasi wa muda mrefu, khofu, uchovu, woga na msongo wa mawazo vimekuwa vikionesha uwezo mkubwa wa kuharibu afya na kudhuru utendaji wa mfumo wa ulinzi, na kusababisha dalili zote za mtu mwenye HIV. Msongo wa mawazo kwenye ubongo unaipelekea kuzalishwa kwa homoni za cortisol, hizi cortisol zinapokuwa nyingi zinasababisha upungufu mkubwa katika uzalishwaji wa T-Seli. (ibid)

Hofu juu ya ukimwi inapokuwa ni kubwa husababisha hata mtu aliyepima na hakukutwa na virusi wa HIV, kuonekana ka mtu aliye athirika na ukimwi kwa kupoteza kiasi kikubwa cha uzito, upunguaji mkubwa wa uzalishaji wa T-Seli.(ibid)


Hivyo basi katika sababu hizi tulizo ziona zinasababisha ugonjwa wa ukimwi utaona kwa uwazi kabisa zote zimeonesha uharibifu wa kinga ya mwili ndiyo mwanzo wa mtu kupata ukimwi. Hakuna kesi yoyote ya mgonjwa wowote wa ukimwi katika kundi lolote lile la waathirika, kutoka kwa watoto mpaka watu wazima, kutoka kwa watumiaji wa dawa za kulevyea na watu wenye msongo wa mawazo au kundi lolote lile lenye kuathirika na gonjwa hili isipokuwa utakuta  upungufu mkubwa wa kinga za mwili au uharibifu mkubwa umeshafanyika katika mfumo wa ulinzi wa mwili. Hakuna kesi yoyote ya mgonjwa wa ukimwi iliyo rekodiwa ambayo sababu yake ni kuwa na HIV pekee, bali kila kesi naonesha kuwepo kwa mfumo duni wa ulinzi sababu inayo pelekea kwa mwili kupata magonjwa mengine ya hatari kwa haraka.
Kufahamu na hatimaye kulitatua janga hili kuna hitaji uchambuzi wa yakinifu wa taarifa huru za kisayansi. Hata kama taarifa hizo zinakingana na uelewa wetu wa sasa juu ya ukimwi. Haki na usawa bila mazingaombwe ya upotoshaji wa taarifa katika kulishughulikia suala la ukimwi, kuanzia kwenye tafiti, majaribio na ufikishaji wa taarifa ndiyo njia itakayo tufikisha katika ukweli wa mambo juu ya janga hili. Ukimya katika hili ni sawa na kifo cha mawazo na maendeleo kwa jamii. Maswali ya msingi yaulizwe na majibu yakinifu yaliyo egemea uchunguzi na tafiti huru yatolewe bila khofu.


Hadithi ya ukimwi ina mahusiano ya moja kwa moja na mpango ulio shindwa wa kutengeneza virusi wa saratani. Michael Verney-Elliot aliweka wazi zaidi pale aliposema: “Kutoka kwa watu walioshindwa kukuletea virusi wa saratani, wameleta virusi wa HIV ambao hawasababishi ukimwi”. ( Jad Adamsr, ‘The HIV Myth, 1989’)
“Ukimwi siyo ugonjwa mpya, bali ni ugonjwa wa kufikirika katika historia ya binaadam ulio pata kuwepo. Ugonjwa huu wa kufikirika unaonesha ushindi wa siasa dhidi ya sayansi” (Michael Fumento,  ‘The Myth of Heterosexual AIDS’, 1990)

“Huenda ningejihisi tofauti kuhusiana na hili kama ningefikiri kuwa watu wanakufa kwa ukimwi. Lakini sifikiri hivyo. Nafikiri watu wanakufa kutokana na madawa mabovu na mabaya, madawa haribifu, imani mbaya (saikolojia). Hakuna ninacho hitaji kutoka kwa ‘Big Daddy’, sihitaji madawa yake, sharia zake wala msimamo wake.” (Gavin Dillard, the Flesh, HIV positive since 1985, San Francisco Frontiers, May 20, 1999)

“Wala haiwezekani, achilia mbali utafiti wa kisayansi, kwamba HIV inasababisha ukimwi. Kama kuna ushahidi kuwa HIV inasababisha ukimwi, basi lazima kuna makabrasha ya kisayansi na maandishi yake ambayo kwa pamoja au hata limoja, limoja yanaelezea ukweli huo, japo hata kwa makadirio, lakini hakuna makabrasha wala maandishi hayo (ya kisayansi yanayo elezea kuwa HIV ndiyo  inasababisha ukimwi”.( Dr. Kary Mullis, ‘obel Laureate,’ HIV not Guilty’, October 5, 1996)



“Fikiria labda ni kweli (ingawa si kweli) kuna ushahidi kidogo wa kisayansi unao unganisha HIV na ukimwi, je lakini ni sawa kwenye taratibu za kimatibabu kumuandikia mgonjwa huyo dawa kama za AZT, ambazo ni sumu kali inayoweza kuharibu hata DNA, sumu iliyo tengenezwa miaka 30 iliyopita kwa ajili ya kutibu saratani, ni sahihi kuwapa dawa hii mama wajawazito na watoto, kama dawa ya kupambana na HIV (Ambao tumeona hawana madhara kabisa katika mwili wa binaadam)?” (Rep. Gil Gutknecht (R-MN), US House of Representatives, Letter to NIAID Director Dr. Anthony Fauci, March 14, 1995)

“Journal of American Medical Association na CDC wametangaza kuwa kumtambua mtu mwenye ukimwi hakuhitaji tena kupima kwa virusi vya ukimwi. Serikali kwa sasa inakutambua kuwa wewe una ukimwi endapo tu utakuwa una gonjwa moja au zaidi katika yale yaliyo orodheshwa na CDC ambayo yanachukuliwa kama ni dalili ya ukimwi kuwa nayo. Orodha hiyo ya CDC inajumuisha maradhi mengi ikiwemo T.B. Tafsiri hii mpya itapelekea kuwepo na vipimo visivyo isha dhidi ya ukimwi bila kujali kuwa mtu huyo anao au hana ukimwi.” (Los Angeles Weekly, Disemba 18, 1987)


Kwa nini kila mmoja wetu yupo tayari kukubaliana na taarifa zozote zile ambazo zitakazo tolewa na serikali kuwa ni za kweli. Daima serikali katika kipindi chote cha historia zimekuwa zikitoa taarifa za uwongo kabisa kwa wananchi wake ili kuweza kuendelea kuilinda ‘keki’ yao. Haijalishi taarifa hizo zitakuwa na madhara kiasi gani kwa wapiga kura, iwe ni kwa kisingizio cha amani, au vita daima serikali zinadanganya wananchi wake.
Huu ni ukweli usio pingika. Ikiwa hivyo ndivyo, tafadhali nakuomba wewe msomaji, anza kuzitizama kwa jicho la pili kila aina ya taarifa zinazo tolewa eidha na serikali au mashirika makubwa ya habari duniani, kwani wote lao ni moja. Haijalishi ni nani anaye toa taarifa hizo, tena kuwa makini zaidi pale ambapo taarifa hizo zinapo tolewa kupitia watu maarufu nchini au duniani kama vile wanasiasa, wanamichezo, waigizaji, wafanya biashara na watu wengine wenye ushawishi kwenye jamii.
Hivi sasa T.B inatibiwa bure nchi nzima, lakini sasa unaweza kupata picha ni kwa nini. Ni kwa sababu kuwa na T.B ni sawa na kuwa na HIV, nastaajbu ni kitu gani kilichomo ndani ya madawa haya ya T.B. Tena wanakuambia ukishaanza kutumia usiache.

Jiulize gharama za matangazo hayo nchi nzima kutoka kwenye luninga mpaka kwenye redio, kutoka kwenye magazeti na vijarida, kutoka kwenye mabango ya barabarani mpaka vichochoroni ni nani analipa? Ni gharama kiasi gani, unadhani serikali yako inaweza kujitolea gharama hizo, unadhani serikali yako inaweza kujinunulia madawa hayo na kuyagawa bure kwa wananchi wake nchi nzima.
Hapana. Je nani huyo asiyeoneka anayekuja nyuma ya kivuli cha serikali yetu kutupatia hizi huduma bure? Ana nini na sisi huyu, anatupenda kiasi gani huyu mpaka afanye hivyo, je ni kweli ana mapenzi ya kweli au anayo ajenda yake binafsi?
“ Watu wananiuliza, ‘unamaanisha kuwa huna imani na HIV kusababisha UKIMWI?’ Nami nawajibu

“ Asilimia hamsini ya waafrika hawana mifumo ya maji taka. Maji yao ya kunywa yanachnganyika na ya wanyama na vinyesi. Kila wakati wapo kwenye maambukizi ya ya T.B na Malaria ambazo dalili zake ni kuharisha na kupoteza uzito wa mwili, na ni salili hizo ambazo UNAIDS na WHO wanazitumia kupima UKIMWI Afrika. Hawa watu wanahitaji maji safi, neti na siyo kondomu, semina wala madawa yenye simu yanayo lazimishwa kwa wamama wajawazito. (Scheff, AIDS Debate, Boston Dig, 2003)
“Tumewekeza dola bilioni 118 kwa miaka 20 kwenye HIV. Hatujapata tiba, chanjo na wala hakuna manedneleo. Badala yake tunao malefu ya watu wanao kufa kwa madawa yenye sumu ya Ukimwi. Ukimwi ni sekta ya mabilioni na mabilioni ya dola ...” (Scheff)

“Kimberly Bergalis, kutokana na taarifa za vyombo vya habari, alikuwa ni msichana mdogo ambaye mwili wake ulikuwa na seli za kupambana na HIV ... akapatiwa dozi ya AZT ... madawa hayo yakamuuwa.”
“... Hata baada ya miaka mingi hakuna hata nyani mmoja (chimpanze) ambaye amekuja kukutikana na gonjwa la ukimwi.” — Dr. Charles Thomas, PhD, former Professor of Biochemistry, Harvard and Johns Hopkins Universities. Former chair of the Cell Biology Department, Scripps Research Institute


Wapendwa, wafuasi wa blogi hii, kesi hii ya HIV vs UKIMWI bado haijahitimishwa, naendelea kufanya uchunguzi na upelelezi utakamilika punde ... tukutane hapa tena kwa USHAHIDI MWINGINE  unaothibitisha kuwa mteja wangu (HIV) HAUSIKI HATA KIDOGO KATIKA KUMSAFIRISHA MLALAMIKAJI (UKIMWI) KUTOKA KWA SOKWE KWENDA KWA BINADAMU NA PIA HAUSIKI KUMPATIA BINADAMU UKIMWI

Till next time TCHAOOOOO …….

7 comments:

  1. duuh sasa inakuwaje m2 anapimwa anakutwa cd4 zake zipo chin then akitumia dawa anakutwa zimepanda cio cr ili somo limekuwa gumu mm kuelewa na inakuwaje mtu anapata HIV na mbona tunackia yule kafa kwa7bu hakutumia dawa apo napata wakati mgumu sana kaka

    ReplyDelete
    Replies
    1. HICHO UNACHO KISEMA NDUGU MSOMAJI UNAO USHAHIDI NACHO? UKITAZAMA POSTI HII NA ZINGINE KAMA HIZI KWENYE BLOGI HII UTAONA NIMEWEKA NA SOURCE AU CHANZO CHA TAARIFA HIZI, NI KIWA NA MAANA WEWE MSOMAJI UKIWA UNAPATA SHIDA KULIELEWA HILI BASI PITIA HIZO SOURCE, NA SOURCE MOJA ITAKUPELEKA KWENYE NYINGINE, NA NYINGINE NA NYINGINE MPAKA UTAELEWA SOMO LENYEWE.
      HATA MARA MOJA DAWA ZA KUREFUSHA MAISHA HAZIWEZI KATU KUONGEZA IDADI YA CD4 NDANI YA MWILI, INGEKUWA ZINAUWEZO WA KUFANYA HIVYO PASINGEKUWA NA MGONJWA WA UKIMWI LEO DUNIANI, ZINGEKUWA NA UWEZO WA KUFANYA HIVYO KILA MTU ANGESHAURIWA KUZITUMIA NA SI WAGONJWA WA UKIMWI PEKE YAKE, SABABU PIA ZINGEFANYA KAZI KAMA KINGA PIA. LAKINI HUO NI UWONGO, ZIKUWAPI TAKWIMU ZA WAGONJWA WA UKIMWI WALIO TUMIA DAWA HIZO NA CD4 ZIKAONGEZEKA? NI NINI BASI KIMEWAUWA IKIWA CD4 ZILIONGEZEKA?
      LAKINI KINYUME CHAKE NDIYO SAHIHI, KWAMBA HIV HAWANA MADHARA KWA KIAFYA HATA CHEMBE, NA KWA VILE HIV HAWAWEZI KUSABABISHA UPUNGUFU WA KINGA MWILINI, KAZI HIYO INABIDI KUFANYWA NA MADAWA YA 'KUREFUSHA MAISHA KAMA AZT NA MENGINE MFANO WAKE, MADAWA AMBAYO YALIPIGWA MARUFUKU KUTUMIKA KWA BINADAMU KUTOKANA NA KUWA NA SUMU KUBWA, MADAWA AMBAYO ASILI YAKE YALITENGENEZWA KUPAMBANA NA SARATANI NA YALISHINDWA SABABU SARATANI SI UGONJWA WA VIRUSI. SASA YAMEPEWA KIBALI YATUMIKE KAMA 'DAWA' KWA WAGONJWA WA UKIMWI KWA VILE TU WAMEPIMWA NA MIILI YAO IMEKUTWA INAYO KINGA DHIDI YA VIRUSI WA HIV. SASA IWEJE USEME KUWA DAWA ZENYE SUMU KIASI HICHO ZINAONGEZA UZALISHAJI WA CD4? HATA KIDOGO HAZIFANYI HIVYO, ISPOKUWA BAADA YA MGONJWA KUANZA KUTUMIA DAWA HIZO INAKUWA NI SAWA NA KUTIA SAHIHI SAINI YA KIFO CHAKE MWENYEWE, ATAPATWA NA KILA UGONJWA SABABU DAWA HIZO ZINAKWENDA KUSHAMBULIA 'WHITE BLOOD CELL' AMBAZO NI MUHIMU KATIKA KUZALISHA KINGA YA MWILI, HAWEZI KUPONA.
      AT THE END OF THE DAY AIDS IS JUST ANOTHER BUSINESS OF MULTMILLION DOLLARS, SO KUWA MAKINI NA CHOCHOTE UNACHO KISIKIA JUU YA UGONJWA HUU.

      Delete
  2. dad yangu kakutwa na ukimwi na kapewa dawa alivyoacha siku kama tano hv siku moja tulimkuta kaaanguka na hasemi wala haemi hospital wakasema alipewa dawa za kulefusha hakuzitumia kwa siku kazaa akatibiwa kidogo akaruusiwa hyo iko vp kwa upande wako

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kunayo namna nyingi ya kujibu swali lako, lakini cha kwanza kabisa cha kuzingatia katika blogi hii ni kwamba, 'NINACHO ANDIKA HUMU,MASWALI NINAYO JIBU SIYO USHAURI WA KIDAKTARI KWA NAMNA YEYOTE ILE, BALI NI TAFITI ZANGU BINAFSI, ZENYE LENGO MOJA TU, KUKUONESHA NJIA, KUPITA AU KUTOKUPITA KWENYE NJIA HIYO SIYO JUU YANGU,'

      Nirudi kwenye swali lako, kama tulivyoona kwenye mtiririko wa posti hizi, hakuna ugonjwa unaoitwa UKIMWI, sababu tafsiri ya UKIMWI ni tata, sasa ni kwanini mgonjwa alianguka baada ya kuacha kutumia dawa hizo nalo ni swali ambalo hatuwezi kulijibu kwa nadharia, lazima majibu ya vipimo ambayo yalipatikana baada kumrudisha hospitali yatizamwe, na mambo mengine kumhusu historia ya ugonjwa na mengine yatizamwe ndipo tutapata jibu ni kipi kilimsibu mpaka akaanguka.

      Delete
  3. Somo ni gumu kweli kaka, mi nawajua watu wana zaidi ya miaka 20 wanatumia dawa na wapo, alafu ni heri nyie mnaopingana mkaja na dawa but sio kupinga kwa maneno matupu, jaribun basi kutafuta tiba akapona mmoja tu muue hili janga, dawa unazopewa hazipandshi cd4 kweli.......zinakusaidia kupata cells ambazo zimeshambuliwa,kila dawa ina side effects zake

    ReplyDelete
  4. https://www.youtube.com/watch?v=3J7vHLXCphA

    ReplyDelete
  5. 10 scientific arguments why HIV can NOT cause AIDS (dr. Duesberg)
    https://www.youtube.com/watch?v=pB8g0b-FkW0

    ReplyDelete