Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, July 13, 2014

TAIFA TEULE na URONGO WA ZAMA ZOTE.


“Sema uwongo kwa sauti kubwa sana na rudi rudia mara kwa mara kwa muda mrefu na watu watauamini huo uwongo.Adolf Hitler

“Ufuate ushahidi kokote unapoelekea”Socrates

“Ukweli inapaswa urudiwe mara kwa mara kwa sababu uwongo nao unahubiriwa muda wote, wala siyo na wachache lakini na wengi. Uwongo unahubiriwa kwenye magazeti na kwenye encyclopedia, kwenye mashule na kwenye vyuo, kila mahala unaonekana kuwa wenye nguvu, unajisikia huru, raha na furaha kwa vile unaaminiwa na wengi. Johann Wolfgang Von Goethe
 Mfumo tuliyo nao unatupotosha na kutujenga kukubali kuwa thamani yetu iko kwenye rangi ya ngozi zetu, ukoo au kabila fulani, na mmoja anaweza kuwa mtumwa na mwingine kuwa bwana.


 Kiuhakika hatuna tofauti, hakuna tofauti unapomtizama binaadam bila kutizama maumbile yake wala alicho nacho, na huyo ndiyo binaadam, lakini watu wengi wanatumia rangi zao, na au asili ya damu yao kuhalalisha matendo yao juu ya wengine. Tunapowatizama watu wanaojinadi kuwa na uhusiano na damu ya wa-Semetik watu walioishi katika Sumeri ya kale wakiwa wamelichukua jina la Sem na au Shem mmoja kati ya watoto wa Mtume Nuhu katika mafundisho ya Biblia na watu hao leo wanajiita Wayahudi.
Nembo hii si haihusiani chochote na dini ya 'uyahudi, ila zaidi ni ya kishetani, tizama posti ya 666 kwa maelezo zaidi.

Dini za Uyahudi, Ukristo na Uislamu zote tatu zina mizizi mikongwe ndani ya Palestina kupitia kwa mtume Ibrahim (a.s) Abraham alihamia kutoka Iraq eneo lililoitwa Ur nakuja katika mji wa Canaan ilipo Palestina hivi leo. Uhamiaji huu ulifanyika karibu miaka elfu nne iliyopita. Kupitia watoto wawili wa mtume Ibrahim (as), Isaac na Ismael zikaibuka dini hizi kuu tatu duniani, Uyahudi na Ukristo kwa Isaac na Uislamu kwa Ismail. Hata hivyo Palestina ni ya zamani mno hata kabla Ibrahim hajatia mguu hapo kulikuwa na mji uliopata kuishi miaka 8000 BC, mji huo uliitwa Jericho na upo maili moja kutoka eneo ilipo Jericho ya sasa, mji huu ni wakale mno na unawezwa kusemwa ni mji mkongwe kuliko yote duniani.

     Kama ilivyo desturi ya miji mingine mikubwa duniani na maeneo yake, eneo hili nalo halikuachwa nyuma na utaratibu wa uhamiaji, kwa karne nyingi makabila kadha wa kadha yalikuwa yakitafuta aridhi yenye rutuba na ahadi nzuri ya faida kwenye biashara yalihamia eneo hili, wahamiaji hawa walijulikana kama wa-Kanaan, na mwanzo eneo hilo likaitwa Canaan.

     Kundi jingine la wahamiaji ni lile lililokosa makazi Egypt na Mesopotamia na lilikuwa likikimbia utawala wa mflame wa Piramidi mfalme Rameses II (Firauni), watu hawa waliitwa Habiru, ama wakazi wa kuhama hama,[1] hawa ndiyo wana wa Israeli na wafuasi wa mafundisho ya dini ya Kiyahudi na mara nyingine wanaitwa Wayahudi kwa maana ya Imani yao na siyo taifa, kama vile Mkristo, Wakristo, na au Mwislamu, Waislamu zimaanishavyo imani na siyo utaifa ndivyo ilivyo Myahudi na au Wayahudi.

 Popote katika posti hii na mfano wake, ninapo taja Myahudi na au Wayahudi nina maanisha wafuasi wa imani hii ya Kiyahudi bila kujali rangi na wala utaifa, na nitajapo Israeli au Mwisraeli namaanisha mtu mwenye damu ya asili ya Isaack na ya Jacob bila kujali dini wala utaifa. Kundi hili halikuweza kuiteka Palestina ingawa lilifanikiwa kuishi kando, kando ya miji ya Palestina.


Wayahudi wakiokolewa na Farao akizamishwa baharini

     Wahabiru waliahidiwa aridhi hii ya ahadi kwa sharti moja, kusimamisha ufalme wa Mungu mmoja, wa Canaan hawakutakiwa tena humo kwa sababu ya machafu yao hivyo inabidi waondolewe na watu, wateule kwa maana ya kusimamisha ufalme wa Mungu Mmoja wachukue aridhi hiyo, kwa maneno mengine, Wahabiru walikuwa na haki na aridhi ile kwa muda mbao wataweza kusimamisha ufalme wa Mungu Mmoja, na watakaposhindwa kufanya hivyo hawatakuwa na tofauti na wa Canaan ambao wao wanaabudu mashetani.[2]
     ‘ … mimi ni bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa, usiwe na miungu mingine ila mimi. Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu chochote …’[3]
Musa (as) na watu wake, ingawa hawakuingia Caanan mpaka Musa alipofariki.

     Vitisho vya mara kwa mara na hata wakati mwingine vita kati ya Wahabiru na majirani zao ndiko kuliko pelekea haja ya kuwa na kiongozi wao mmoja, utaratibu huu ulianza na Sauli na kisha baadae akaja Daudi ambaye alichukua utawala mnamo mwaka 1000 BC . Baada ya Daudi kuwa shinda Wapalestina watu ambao walijulikana kuwa ni majitu makubwa, watu wenye sifa, watu waliochanganya damu zao na mashetani,  alichagua Jerusalem kuwa makao makuu ya Utawala wake. Jiji hili la Jerusalem lilikuwepo tangu mwanzo mwa milenia ya pili BC lakini halijawahi mpaka hii leo kuwa makao makuu ya wa Israeli.

     “Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamuendea Samweli huko Rama; wakamuambia, angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue mfano wa mataifa …”[4]

     Kundi hili la wa Habiru halikuwa na sanaa za kiutamaduni na ustaarabu wa kimiji walijifunza kutoka kwa wa Canaan. Hekalu lao la ibada lilijengwa na Wafonesia wakazi wa hapo ambao wana damu ya nyoka, michoro, mafundisho na mashairi yaliyopatikana ndani ya hekalu la Wahabiru yalikuwa na muundo na mitindo ile, ile ya wa Canaan na wa Syria. Mungu ndama, Tammuz na Ishtar wakalivamia hekalu, na mantiki ya dini ya Kiyahudi ya Mungu mmoja ikapotoshwa, na maana nzima ya kukaa kwenye aridhi ya hadi ikapoteza sifa na hadhi yake.

     Nikatika mazingira haya ya utata ndipo vitabu vitano maarufu vinavyotengeneza Taurati viliandikwa, vitabu hivyo vikiwemo vitabu vya ; Kitabu cha Kutoka, Mwanzo,  ..... kwa karibu milenia mbili Kitabu cha Kutoka kilifahamika kuwa ni kazi ya mtume Musa mwenyewe kwa mkono wake, mpaka kwenye karne ya 16 ambapo maswali yalianza kuhojiwa.
“ikiwa Mussa ndiye mwandishi wa kazi ile iweje aweze kuandika matukio ya kifo chake mpaka kuzikwa kwake?”
Lakini ni mpaka karne ya 18 ndipo ilipo bainika kuwa kazi ile ni mkusanyiko wa kazi za kimila mbazo kizazi hadi kizazi zilikuwa zikipitishwa kwa njia ya mdomo, kutoka kwa Wababiloni, Wasiria, Waigypti na watu kutoka Mesopotamia, mkusanyiko huo ulikamilika katika karne ya 10BC.



     Baada ya Daudi, akaja mwanae ambaye ni mtume Suleimani naye alifariki mnamo mwaka 926-5 baada ya hapo ufalme wa Waisraeli ukaanza kuporomoka, kwanza suala la kodi lilikuwa gumu kwao, pili mkanganyiko wa kidini nao uliwagawanya zaidi na tatu ni nani atakaye chukua nafasi ya mtume Suleiman. Mtu mmoja aliyejitwika sifa ya unabii ingawa haikuwa sifa yake akachukua kiti cha ufalme, mtu huyu aliitwa Jeroboam, na hapo jamii hii ikagawanyika makundi mawili, Judah ikawa upande wa kusini na Israeli upande wa kaskazini. Wakati wa mgawanyiko huo vita na majirani zao vikapamba moto na vita vibaya zaidi ni vile walivyopigana mnamo mwaka 722KK na wa Assyria, mfalme wa Assyria Tiglath –Pileser III alivamia Israeli na kuiteka na akalifanya eneo hilo kuwa chini ya himaya yake, Judah ilisalimika lakini ilibakia kama eneo dhaifu na tegemezi na halikuwa na nguvu za kiutawala.[5]




     Mwaka 612KK, historia ikaandikwa tena, Assyria iliporomoka na kuchukuliwa na wa Babilon wakati huo ikiongozwa na Nebuchadnezzar, ambaye aliivamia Jerusalem, akaiharibu yote, akalichoma moto hekalu la mfalme Suleiman na Judah nayo ikafutika kabisa.[6]

     Kidini Waisraeli walikumbana na machungu haya baada ya kuacha mafundisho ya Mungu Mmoja na hivyo hawakuwa tofauti na wa Canaan, katika vitabu vya Biblia tunaona onyo la kutokea kwa matukio haya endapo watakengeuka na kufuata mila za kishetani na ndivyo ilivyotokea.
Wanajeshi wa Nebuchadnezzar wakiondoka na agano baada ya kuwapiga waisrael na kulibomoa hekalu la bwana.

 Wakaanza kutawanyika katika uso wa aridhi tena, hawana mfalme, hawana nchi na mbaya kabisa hawana dini ya Mungu Mmoja. Kila mmoja alitawanyika kutafuta hifadhi anapo pafahamu na kichwani wakiota ndoto za kupewa tena aridhi ya ahadi.

     Mungu akawatumia tena mitume wake, lakini safari hii mitume hawakuja na maudhui ya aridhi ya hadi na ushindi wa kivita, bali na ujumbe wa kusimamisha dini ya Mungu Mmoja kwa amani na upendo. Zama hizi ziliwashuhudia mitume kama Ezra na Nehemiah na wengine waliofanya kazi ya kuihuisha imani ya Jehovah. Haikuwa kazi rahisi kwani fukuto la kisiasa lilizaa kuwagawanya Waisraeli. Kipindi cha utawala kutoka kwa wa Persia na kuja kwa Wagiriki mnamo mwaka 333BC vyote vilikuwa ni vipindi vya kubadilishana eneo hili kama bidhaa kutoka kwa huyu kwenda huyu, watawala waliowekwa na wa Roma walichunga maslahi yao zaidi kuliko ya watu wao, mfano wake ni Mfalme Herod, baba wa Mystery Force ambayo leo tunaiita Freemasons.
Mambo hayakuwa shwari kwa Waisrael wakati wa utawala wa Roma.

  Utawala wa Roma ndani ya Palestina uliwafukuzia ambali Wayahudi na kukiharibu hekalu lao ambalo ni alama kuu ya takatifu katika historia yao. Sababu za Wayahudi kufukuzwa zilikuwa ni zile za kisiasa na kijamii zaidi kuliko zile za kidini, hata hivyo muda ulivyopita masuala ya kidini nayo yakawa ni msumari wa moto juu ya kidonda kwa Wayahudi. Wayahudi waliruhusiwa kutafuta hifadhi sehemu zingine katika dola ya Roma lakini si ndani ya Palestina. Wa Roma wakaufanya Ukristo kuwa dini ya kitaifa dola lao, na hapo Wayahudi wakaonekana watu wabaya kuliko wote, makanisa ya Kiroma yakaanza kampeni za kuwahusisha Wayahudi na kifo cha Masiha, Yesu Kristo, Wayahudi wakaitwa ni wauaji wa Yesu na au wauaji wa mungu, walimsulubu mungu msalabani.

     Kuanzia karne ya sita na kuendelea hali ilizidi kuwa ni mbaya zaidi kwa wa Israeli, vipingamizi na vizuizi mbalimbali vikazidi kupamba moto, wakawa hawatakiwi katika ofisi za kiserikali, na masinagogi yao yakaanza kuharibiwa, imani yao ya Mungu mmoja ilionekana ni tusi dhidi ya imani ya Utatu Mtakatifu inayofutwa na dola ya Roma. Sharia ikaja ikiwakataza watu kula mkate wa kimila wa Kiyahudi, na wala wasioe kutoka kwenye familia za Kiyahudi wala kumuajiri daktari wa Kiyahudi, zama hizo Myahudi alichukuliwa kama najisi, na Mkristo aliyekuwa na mawasiliano na Myahudi alitengwa na kanisa.

     Katika nchi za Magharibi ambapo Wayahudi waliamua kutafuta hifadhi nako mambo hayakuwa shwari hata kidogo, Ujerumani, Uingereza na Ufaransa kote sheria kali dhidi ya Wayahudi zilipitishwa kuwaadhibu wauaji wa mungu. Sheria hizo ziliwabana katika masuala ya kibiashara na kijamii. Hawakuwa na utulivu kokote walipokwenda.

     Kipindi hichi ndicho kipindi ambacho kabila la wa Turk ambalo lilikuwa likifuata imani ya dini ya Kiislam lilikuwa likiisogelea Mashariki ya Kati na Antokia ya Asia ya Kati, walikuwa na jeshi kubwa na lenye nidhamu, wa Islamu hawa waliisukuma dola kubwa ya zama hizo iliyoitwa Byzantium kuelekea Constantintinople, maelfu ya Wayahudi waliokuwa wakiishi maeneo haya walishatoweka na walibaki wachache mno.


Dola ya Khazaria kama inavyo onekana mnamo karne ya 7
     Kundi jingine kubwa la wa Turk ambalo wao hawakuwa wa Islamu wala wa Kristo ila walikuwa wakifuata dini zao za kimila, kundi hili liliitwa Khazair, wa Khazairi walitawala sehemu kubwa ya Asia, hawa ni watu kutoka katika milima ya Caucasus na maeneo ya bahari ya Caspiani na baadae walihamia Asia ya Kusini, Katika kipindi hichi ambapo dini mbili kubwa yaani Uislamu na Ukristo zikikuwa kwa kasi, kiongozi wa dola hili aliona hatari inayoikabili dola lake la kuangukia katika mikono ya moja ya dini hizi, kisiasa hakuwa tayari kwa hilo, na hivyo akaamua kufuata imani ya Kiyahudi, ni katika kipindi ambacho Wayahudi wako katika hali ngumu sehemu mbalimbali duniani, na ni katika kipindi ambacho wameshapoteza ile nguvu yao ya kiubaguzi ya kujibagua kuwa wao ni kizazi teule, hawakuwa na taifa tena, lakini kiongozi wa Khazair kuamua kuingia katika dini ya Kiyahudi.[7]

     Wa Khazair wakaanza kuitwa Wayahudi, lakini hawa hawakuwa Wayahudi kwa maana ya taifa lenye damu ya Israeli iliyotiririka kutoka kwa Isaac, bali Wayahudi kwa njia ya imani, Wayahudi wachache waliobakia katika maeneo hayo nao wakapotolea ndani ya kundi kubwa la wa Khazair, ikiwa haijulikani nani Myahudi wa kweli na nani Mkhazairi. Kama ilivyokuwa katika nchi zingine za Ulaya waliko kimbilia, suala la kuingiliana na kuoana na wasiokuwa Wayahudi halikuweza kuepukika na hivyo wakapoteza ile damu yao ya asili kama watoto wa Jacob au Israeli mwenyewe.

     Mpaka hapo Wayahudi hawana nguvu ya kudai taifa huru kwa kutumia kitambulisho cha Uyahudi kama taifa, kwani kama tulivyoona, Uyahudi si Utaifa bali ni dini kama zile dini nyingine na mtu yoyote anaweza kuingia katika dini ya Kiyahudi kama tunavyoona leo, kuna Wayahudi weusi kutoka Uganda, kuna Wayahudi wakizungu na kadhalika, kama kungekuwa na uhalali wa kuomba utaifa basi wangetumia kitambulisho cha Israeli, ikiwa na maana wao ni kizazi cha Jacob, lakini kitambulisho hichi kimeshaharibiwa na mwingiliano na watu wengine wasio kuwa wa Israeli, kwa hiyo tukisema tumtafute Mwisraeli mwenye damu halisi ya Isaac na Jacob ni vigumu mno kuwapata, ingawa hili halifanyi wanyimwe utaifa wao, lakini hakuna uhalali wa kudai utaifa nje ya mahala ulipozaliwa. Kwa hiyo watu kutoka Milima ya Caucasua ndiyo waunda sehemu kubwa ya watu wanaojiita Wayahudi. Mfalme wa Khaizari kuchagua dini ya Kiyahudi kama dini ya kitaifa katika kipindi kigumu kama kile kwa Wayahudi inanipa wasi, wasi kuwa si jambo lililotokea kwa bahati mbaya bali ni sehemu ya mpango maalum ya kuwavisha watu wasio kuwa Wayahudi sura za Kiyahudi kwa ajili ya ajenda.
 ITAENDELEA HAPA HAPA ... INSHALLAH





[1] Sandmel, Samuel. "Hebrews (people)." Microsoft® Student 2009 [DVD].
[2] http://www.albalagh.net/kids/history/palestine.shtml
[3] The Holy Bilbe in Kiswahili union version published as Biblia Maandiko Matakatifu, 1997, ‘Kutoka 20, 1-5’
[4] The Holy Bilbe in Kiswahili union version published as Biblia Maandiko Matakatifu, 1997,  1 Samweli 8-7
[5] Robert Guisepi, ‘Civilization Of the Hebrews Along The Banks Of Rivers’ (Makala inapatikana kwenye ukurasa huu http://history-world.org/Hebrews.htm)
[6] Ibid
[7] Endrew Carrington Hitchcock ‘Synagogue of Satan’

3 comments:

  1. Nakuamin kaka mungu akupe uhai mrefu

    ReplyDelete
  2. Aminnnn, na wewe ubarikiwe hivyohivyo.

    ReplyDelete
  3. Hilo kundini la kutoka milimani ni milima gan lilitoka

    ReplyDelete