Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Wednesday, July 9, 2014

PICHA ZA UCHI NI SHIDA KWA JOGOO WAKO!!!



Porno kwenye mtandao si sawa na picha za Playboy. 
1. Picha za uchi kwenye mtandao zinasisimua kingono zaidi kuliko picha za kwenye majarida. Hii ni kwa sababu picha za uchi kwenye mtandao zinakila aina ya kile ambacho unaweza kufikiria kuhusiana na suala zima la ngono. Mtazamaji wa picha za uchi kwenye mtandao anazama katika kila aina ya uchafu wa kutisha na kugofua ambao anaufikiri.



2. Yeyote anaweza kuwa ni teja wa picha za uchi kwenye mtandao.
Wengi kati ya wale ambao ni waathirika wa picha za uchi kwenye mtandao hawana historia ya kuwa ni teja wa aina nyingine ya kilevi au mihadarati. Ni watu wa kawaida tu, na wengine wenye mafanikio kimaisha au hata kiroho, na walianza kutizama filamu za uchi na kila muda ulivyo zidi kwenda ndivyo walivyozidi kuzama kwenye shimo hilo. Na walipo acha kutizama filamu hizo hali zao zilirudi kawaida.

3. Kufahamu ni namna gani matumizi ya picha za uchi yanaathiri ubongo ni muhimu sana ilikuweza kujitoa kwenye janga hilo.
Unapofahamu ni namna gani ubongo wetu unafanya kazi ni muhimu na kukusaidia anapotaka kuchomoka kwenye uteja wa picha za uchi.
Kinachotokea kwenye ubongo wako nini pale unapokuwa ni teja wa picha za uchi mtandaoni?

Kwanza filamu hizo za uchi zina sisimua ubongo wako zaidi ya maumbile ya kawaida yanavyo weza kufanya na ubongo wako nao unabadilika kukubaliana na hali hiyo kama ndiyo njia sawasawa ya msisimko wa ngono. Kuwa teja kunafika pale ambapo ubongo wako umeshabadilishwa kiasi kikubwa na kutambua mazingira hayo kama ndiyo sahihi kwa ngono.

Mabadiliko hayo ya ubongo ndiyo yanayotengeneza mnyororo mgumu wa kuwa teja ambao unakuwa ni vigumu kuukata kila unapotaka kuacha, lakini mbaya zaidi unaimarika kila pale unapotizama filamu hizo.

Hivyo utaona basi kile ambacho unakiona kwenye picha za uchi ni msisimko wa ajabu kwenye ubongo wako ambao hauwezi kufikiwa kwa kutumia maumbile ya kawaida.

Maisha yako ni Ubongo wako.

Sheria # 1 – Lazima niishi, hivyo ubongo unafanya kazi na mbinu na mipango ya namna gani uishi, kusanya chakula, kula ina fulani ya chakula, kusanya kingi huwezi jua ya kesho.

Sheria # 2
Pata watoto, ongeza ukoo, acha alama yako duniani, kopi yako n.k.
Miaka 100 iliyopita nafasi ya mababu na mabibi zetu kukutana na watu wa jinsia nyingine ilikuwa ni ndogo sana, na pia kukutana kwa ajili ya tendo la ndoa nayo ilikuwa ni ndogo zaidi.

Lakini muathirika wa picha za uchi ndani ya muda wa saa moja anaweza kuwaona wanawake au wanaume wa sifa anazo taka, wakifanya aina ya ngono anayotaka zaidi ya 100.

Katika mazingira hayo ubongo wa muathirika wa picha za uchi nao unabadilika, unaona picha za uchi na yale yanayo fanyika ndiyo ukweli halisi wa maisha, LAKINI OLE WAKO, SIYO UKWELI HALISI HATA KWA NUKTA MOJA.

SHE IS HOT!!! BUT IS SHE REAL?

Sehemu ya ubongo inayohusika na kujamiiana inakuwa haiwezi kufanya kazi yake sawasawa bila picha za uchi ... shida inaanza ...

Ubongo unapoathirika, unakuwa hutosheki na kile unacho kiona, kila siku utataka kutizama mcheza picha za uchi mpya, mwenye staili tofauti n.k. Kadiri unavyozidi kuzama huko na mguso wa ngono kwenye maumbile halisi au kwa mwenza wako nao unatoweka, mwisho wa siku uume wako hauwezi kusimama mbele ya mke wako sababu UBONGO WAKO UNAYO PICHA ‘MATATA’ ZAIDI YA MWANAMKE WA KUFIKIRIKA KWENYE MTANDAO AMBAYE ANAFANYA MAMBO YA KISHENZI YA KUFIKIRIKA, NI KWA MWANAMKE HUYO TU NDIYO UBONGO WAKO UTAWEZA KUSIMAMISHA UUME WAKO!
HAPO NDOA INAINGIA UFA.

SOMEBODY HELP MEEEEEEEEE!!!!!!!

Hivyo basi utaona tatizo la kupoteza nguvu za kiume baada ya kutizama picha za uchi sana, si tatizo la viungo vyetu vya uzazi, bali ni tatizo la kwenye ubongo wetu. Ubongo umeathirika na picha za uchi.

Katika ubongo wetu kuna sehemu moja mahususi inafahamika na kazi za viungo vya mwili, maarufu kama ‘limbic system’ katika picha hiyo hapo chini sehemu hiyo imezungushiwa rangi ya chungwa. Wanyama wote aina ya ‘Mammal’ wanatumia au wanayo ‘limbic’ katika bongo zao.


Ubongo ni mmoja lakini, kila sehemu ya ubongo hiyo inayo kazi yake mahususi, na sehemu hiyo ya ‘Limbic’ ndiyo inayohusika na sheria # 1 ya ubongo. ‘survival’. Sehemu hii ndiyo inayo tawalia mambo ya hisia, kama vile woga, furaha, huzuni n.k. Lakini pia ni sehemu ambayo hamu na msisimko wa kitu fulani hutawaliwa hapo kama vile njaa, kuchagua mwenza na suala zima la ngono. Hamu yako ya ngono haitokei kwenye viungo vyako vya uzazi, bali kwenye ‘limbic system’ ndani ya ubongo wako. Sehemu hii ndiyo inayohusika na wewe kupata ashki na hatimaye uume wako kusimama, na hapo ndipo pahala ‘addiction’ zote zinapo tokea ikiwemo hii ya picha za uchi.

Mfumo wa utendaji wa ‘limbic systeam’ ni kukwepa maumivu au kuzia maumivu yasitokee na wakati huohuo kurudia lile lenye kuleta raha. Kuishi kunategemea na kukwepa majanga yatakayo kuletea maumivu kimwili na kisaikolojia, lakini na wakati huohuo, ni kupita kwenye njia ile ambayo itakuletea raha na furaha. “Moto, mbaya; aiskrimu tamu; Mama safi; nyoka mbaya; picha za uchi safiii.” Unanipata mpaka hapo?

Moyo wa limbic unafahamika kama ‘reward circuit’(rc), tizama picha hii hapo chini. Utaona kwenye picha hiyo RC inatoka kwenye limbic na kwenda kwenye sehemu ya ubongo inayofahamika kama cerebral, sehemu inayohusika na kufikiri na kufanya maamuzi mengine baada ya kupambanua vitu kadha.

Kwenye RC ndipo unapo pata ile raha ya kitu unacho fanya ikiwemo tendo la ngono na mwisho kupata ‘mshindo’. Pia ndipo pahala unapo amua ni kipi unakipenda na kipi hukipendi, ni sehemu ndogo sana ndani ya ubongo, lakini ndipo penye majibu ya mwisho, hakuna unacho fanya bila kuhusisha RC.

Kama wewe ni teja wa chochote kile, ikiwemo somo letu hili, picha za uchi, basi hali hiyo ya kuwa teja inatokea ndani ya RC.

RC inaamshwa au kupandishwa na vitu vingi, mathalani unahisi kiu, hamu ya kupata maji au kimiminika cha baridi inakuwa kubwa mno, unapofikiria aina fulani ya kinywaji kwa ajili ya kiu husika, basi hamu nayo inazidi zaidi, sehemu fulani ya ubongo wako ikikuambia pata kinywaji hicho, sehemu hiyo inafahamika kama ‘depamine’. Unapopata kinywaji husika na ukapiga fundo la kwanza, depamine’ inaanza kushuka, na RC nayo inakuwa imesharidhika, ukiendelea kupata fundo jingine na jingine, basi ile hali ya kiu inatoweka kabisa na unarudi kwenye hali ya kawaida.

Hali hiyo unaweza kuiona unapo fanya punyeto au unapofanya ngono.

Umepita mahala ambapo kuna mazingira ya wewe kutizama picha za uchi, RC inaamka, unapofikiria ni aina gani ya picha za uchi utizame depamine inapanda ikikuhimiza utizame picha husika nayo RC inakupa faida za kutizama picha hiyo, kama kupata raha n.k. Unapoanza kutazama kwa vile RC imerekodi starehe ya juu kabisa kwa wewe kutizama ni kupiga punyeto na hatimaye kupata mshindo, basi depamine itaendelea kupanda kadiri unapotizama picha moja hadi nyingine mpaka lengo litakapofikiwa.

Kutokana na tafiti za American Psychiatric, kama utasema ndiyo kwa maswali matatu au zaidi kati ya haya basi wewe ni teja, sahamani mwaswali yenyewe yataegemea kwenye suala la picha za uchi sababu ndiyo mada yetu.

1.          MUDA - Je matumizi yako ya picha za uchi kwenye mtandao yamekuwa yakiongezeka siku baada ya siku? Umekuwa kila unapotizama unapanda chati kwa kutumia muda mwingi zaidi au kwakuangalia mitindo na wachezaji wapya wa filamu hizo au kwa kutizama mambo ya ajabu na yenye kinyaa zaidi kwenye filamu hizo?
2.        MADHARA YA KUACHA – Je unapo acha kutazama filamu hizo kwa muda, huwa unajisikiaje. Wengi wa waathirika wanapoacha kutizama wanakuwa kama mazezeta, kila kitu kinasimama, na hamu ya kutizama inakuwa kubwa ikiwataka kurudi kutizama, wanajihisi wapo chini n.k.
3.        HUWEZI KUJITAWALA – Je wewe ashki ya kutazama picha hizo inapopanda unaweza kuahirisha na kuendelea na kitu tofauti?
4. KUACHA SHUGHULI ZINGINE – Je umekuwa ukiacha shughuli zingine zilizo za muhimu iliuwezea kutizama picha hizo za uchi?
5.        NATAKA KUACHA – Je umekuwa kwa muda mrefu unayo hamu na nia ya kuacha kutizama picha hizo, lakini kila siku unajikuta umenasa kwenye mtego huohuo? Umejaribu bila mafanikio kuacha lakini hutoki?
6.        MSAADA – Je umewahi kutafuta msaada juu ya tatizo lako, kwa ndugu, jamaa, rafiki au kwa yeyote unayemuamini?


Kama wewe ni muathirika (teja) wa picha za uchi ni kwamba ubongo wako, hasa sehemu ya limbic, imepata msisimko mkubwa kushinda uwezo wake kwa kutizama picha za uchi.

Hivyo, teja wa picha za uchi kwenye ubongo wao kunawa na mabadiliko yafuatayo.

Moja, RC inakuwa butu endapo itahitajika kufanya kazi yake kwa kitu chenye msisimko mdogo kushinda picha za uchi, na hapo ndipo utaona tunakuwa na tatizo kubwa la nguvu za kiume.
Pili, utaratibu wa ubongo kwenye tendo la ndoa unakuwa umetengeneza njia mpya ya kupata msisimko nayo ni kwakutizama picha za uchi badala ya maumbile halisi ya mwenza wako.
Hivyo basi tatizo linapokuwa kwenye hatua hiyo, ni kwamba ubongo wako hautahitaji kingine chochote zaidi ya kile kitakacho weza kuusisimua mpaka ufikie kileleni, nacho si kingine bali ni picha za uchi na wacheza filamu hao, na hapo taratibu utamuona muathirika anapunguza siku za kufanya tendo la ndoa na mwenza wake, na hamu ya kuwa naye kingono nayo inazidi kupungua siku hadi siku, mpaka wanakuwa kama KAKA na DADA ndani ya nyumba. Ndoa inakuwa hatarini.

NINI KIFANYIKE?
Ndoa zipo hatarini, wanaume wengi wamekuwa ni waathirika wa picha za uchi, na hivyo waathirika wa 'nguvu' za kiume. Waataala wa tiba za kienyeji wanauza kila kitu chenye lebo ya 'kuongeza' nguvu za kiume. Lakini tatizo bado lipo palepale, sababu hakuna ambaye anayetibu tatizo, wote wanatibu dalili au madhara ya tatizo, lakini tatizo kuu ambalo ni PICHA ZA UCHI KWENYE MTANDAO LIKO PALEPALE ...

TUKUTANE NEXT TIME INSHAALLAH KATIKA KUATAFU SULUHU YA KUDUMU YA TATIZO HILI.


REMEMBER SHE IS NOT REAL, BUT SHE MIGHT KILL YOU AND YOUR MARRIAGE!!!!




2 comments: