Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Tuesday, August 6, 2013

HAKI ZA WANAWAKE NA VITA DHIDI YA FAMILIA ...


Haki za wanawake, za watoto na zile za mashoga ni moja ya mfano mzuri wa namna ambayo Illuminanti wanatumia kuishika jamii yetu.

Kwa miaka michache hivyo, tkribani miaka 40 tangu kampeni hizi zilipoanza, wanawake wengi wamepoteza njia yao ya asili na lengo lao mahususi na muhimu katika jamii. Matokeo yake ni kwa familia kusambaratika, ngono holela kuongezeka, kuwa na idadi kubwa ya watoto wa zinaa na idadi ya watu kiujumla kupungua.



Kwa mwanamke yeyote mapenzi, huruma na kujitoa ni moja ya sifa za kipekee na adhimu katika maumbile ya mwanamke. Anajitoa kwa mume wake na watoto wako kwa mapenzi makuu na huruma na hamu yake kubwa ni kuona mafanikio ya familia yake. Kazi yake adhimu isiyo na mbadala ni kumleta duniani mwanafamilia, kumlea, kumkuza na kumfundisha mengi ikiwemo upendo na huruma. Kazi hii haina mbadala, hakuna anyeweza kuifanya kazi hii kwa ubora wake kumshinda mama mwenyewe, hakuna.


Haijalishi Daycare imepambwa kwa namna gani, inatoa huduma bora kiasi gani, kwa gharama gani, katu haiwezi kuvaa viatu vya mama. Wakati mama anamlea na kumkuza mwanafamilia, daycare inalea na kumkuza mwanajamii.

Mwanafamilia msingi wake mkuu ni MAPENZI mwanajamii msingi wake mkuu ni MASLAHI. Wakati mwanafamilia anaandaliwa kujitoa na kutumikia wengine kwa kutanguliza UTU, Mwanajamii anafanya hivyo kwa kutanguliza MASLAHI.
Mwanafamilia hawezi kumpeleka Mama yake mahakamani lakini mwanajamii anaweza kufanya hivyo. Anakuambia “What is it for me”
Hivyo mwanamke kama nguzo muhimu kwenye familia, anapofanya hayo yote, kwa upande mwingine, mwanamume naye silka yake inamuongoza moja kwa moja katika kumsaidia huyu mwanamke kwa kumuhakikishia ulinzi, ulinzi wa kiuchumi, ulinzi wa kimaamuzi na ulinzi wa kimazingira. Hapo ndipo tunapo pata maana halisi ya ndoa, ambapo sasa muhiri wa muungano huo ni tendo takatifu la ndoa linalo waunganisha wawili hawa na kila mmoja na majukumu yake na sehemu yake katika ndoa hiyo kuelekea kwenye kusimamisha serikali yao ndogo ya familia, yenye kiongozi ambaye ni baba na msaidizi ambaye ni mama, na watumishi ambao ni watoto, na anaye hudumiwa hapa kwenye serikali hii si mwingine, si chochote, bali ni malengo makuu ya kuletwa hapa duniani, MUNGU MMOJA, KUMUABUDU YEYE PAKE YAKE BILA KUMSHIRIKISHA NA YEYOTE.


Haki za wanawake zimewapika na zinaendelea kuwapika wanawake kulikataa jukumu hilo makhususi kwao, halikadhalika, haki za mashoga zikiwapika wanaume kulikimbia jukumu lao na haki za watoto zikimuandaa mtoto kuwa mwanajamii badala ya mwanafamilia. Harakati zote hizo zinaonekana kusimamia mambo ya msingi kwenye makundi hayo, lakini  kinyume chake ndiyo sahihi, na kundi la mashoga likiwa ni sumu mbaya sana kwenye familia.

Mwandishi mmoja wa Uingereza alipata kuwarekodi wanawake wawili wakisema hivi,
“Wanaume wote siku hizi ni bure kabisa,” alisema mmoja. “Ndiyoo,” akasema mwingine. “Shida ni kuwa hawajalelewa kupambana na changamoto za wanawake. Hawafahamu kuwa tunawahitaji wao kuonesha uanaume wao zaidi, lakini badala yake wamekimbia majukumu yao.”


Wanaume hawapo hapa kupambana au kushindana na wanawake, halikadhalika wanawake hivyohivyo, bali kusaidiana katika jukumu muhimu la kujenga familia. Ikiwa mwanamke analelewa kupambana au kushindana na mwanaume, kama wanavyo dai kinadada hao, na hayo ni maoni utakayo yapata kwenye majarida ya wanawake kama vile Jarida la TRUE LOVE, COSMOPOLITIAN na mengine mengi, matokeo yake ni kuwa mwanaume ataikimbia ndoa, sababu kwa nini mwanamume alale kitanda kimoja na mtu ambaye anayo mtizamo wa kumfanya yeye mwanamume awe kama yeye, yaani awe na mtizamo wa kike? Lazima ndoa itakuwa ngumu sababu badala ya kusaidiana, tunashindana.


Sababu thamani ya ndoa kwenye jamii imeondolewa na harakati za kinamama, wanawake sasa hawana cha kubadilishana kwa MAPENZI zaidi ya NGONO. Utakubaliana na mimi kuwa pamoja na yote mwanamke wa leo kafanywa ni chombo cha starehe, mwanamume hamtizami mwanamke kama mshirika wake, bali adui yake ambaye inabidi amtege, amlaghai, amdanganye, ili afanye naye NGONO na kisha kumuacha kwenye mataa, NOW RELATIONSHIP ITS A GAME, AND EVERYDAY PEOPLE A CHANGE COACHER LIKE A FOOTBAL TEAM.


Mtayarishaji wa filamu anayekwenda kwa jina la Aaron Russo, anathibitisha haya ninayo yasema,
Wakati maadui zetu walipokuwa wakimuandaa Russo iliwamuingize kwenye asasi ya siri inayo kwenda kwa jina la CFR, Nicholas Rockefeller alimuambia Russo kwamba, Rockefeller Foundation imetengeneza ‘HARAKATI ZA WANAWAKE’ kwa kutumia vyombo vya habari kama mpango wa muda mrefu wa kuutawala umma. Nenda ka Google, “Rockefeller Foundation” + “Women Studies” na utapata majibu yako.


Haki za akina mama zinafanya kazi ileile, kuivunja familia, kupunguza idadi ya watu, kumtoa mwanaume kwenye nafasi yake.
Mtazamo wa watu lazima ubadilishwe kutengeneza kile ambacho freemason na Illuminanti wanacho kihitaji. Rockefeller ni familia na ni moja wawachezaji hodari na mahiri kwenye New World Order, Rockefeller wanashikilia vyombo vingi vya habari vyenye kuaminika kwa jamii. Kwa kutumia nguvu hiyo ya vyombo vya habari wanaurubuni umma ili waweze kuutawala. Moja ya matukio ya kutengeneza wanayo tumia kuurubuni umma ni vita dhidi ya ugaidi na tukio la 9/11.

Rockefeller alimuambia Russo kuhusiana na mpango kamambe wa 9/11 mwaka mmoja kabla ya tukio lenyewe kutokea.

Illuminanti wanacho hitaji ni dhana au falsafa itakayo wapa kibali cha kuwatia walimwengu wote kwenye minyororo yao. Hivi sasa kila nchi duniani imeingia kwenye minyororo ya madeni kutoka kwenye mabenki ambayo yapo kwenye mikono yao, karibu kila mmoja wetu sasa analo deni katika benki fulani, kila kampuni au shirika, lipo kwenye mfuko wa suruali za wanao miliki mabenki.
Maadui wetu hawana dhana nyingine waliyo ona inayofaa ispokuwa dhana ya ushetani, wanautawala ulimwengu kwa kushirikiana na asasi zingine za kishetani kama vile, freemasonry, Ukomunisti, Demokrasia kutaja kwa uchache sana.


Utamaduni wa kimagharibi umeegemea kwenye dhana ya Ushetani, freemason inafundisha kuwa ni mtu na siyo mungu mwenye sauti juu ya dunia hii. Wanapindua dhana ya kiroho na imani ilikusimamisha dhana yao ya ushetani. Kupitia vyombo vyao vya habari, wanaharakati wao na propaganda, suala la kishetani la ushoga linafanywa kuwa ni suala la kijamii, la kiserikali, nchi lazima zikubali kuwatambua watu hawa.

Kwa ajili ya kuivunja serikali ya familia, Illuminanti na vyombo vyao vya habari vinawaambia kina mama lazima wasimame wenyewe wajitegee na wasimtegemee mwanaume, yaani wasitegemee mkataba wa ndoa kuwaokoa, ndoa haina maana, mahusiano baina ya mwanaume na mwanamke kama wanandoa ni suala la kupotezana muda.

Wanaharakati wa haki hizi za wanawake kwa kutumia vyombo vya habari, hichi ndicho wanacho waambia Mama, na Dada zetu kama njia ya ‘kuwapatia uhuru’ wao ambao kwa karne kadhaa umekuwa ukishikiliwa na wanaume visivyo halali.


i.         Wanaume hawaaminiki, wanaume ni mwaumbwa, walaghai, wezi, wanyonyaji, wakati mwanamke ndiye anaye fanya yote kwa mwanaume kuitwa mwanaume.
ii.        Wanawake ni wahanga wa jinsia zao, lazima waamke sasa wapambane na wachukue kilicho chao.
iii.       Wanawake lazima wawe ni wabinafsi sasa, muda waliokuwa wanautoa kwa waume zao, watoto hakuna tena muda huo, bora kutumia muda huo na ‘girl friend’ wako (lesbian au ushoga kwa wanawake) lakini bila kuwa na mume au mtoto.
iv.       Ngono si kwa ajili ya ndoa na mapenzi. Majarida kama Glamour na Cosmopolitan yanawaambia dada zetu wanapo toka ‘out’ na wanaume wawe wazi kuhusu ngono, na wawaoneshe umahiri wao kitandani hata kama ndiyo siku ya kwanza wamekutana. Hakuna kuzungumzia ambao ya ndoa au familia.
v.        Mafanikio ya kweli yapo kwenye kupata kazi nzuri na siyo kwenye kuolewa na kuwa na familia.


Kwa aina hizi za kampeni na harakati, hivi sasa wanawake wengi wapo njia panda baina ya kufuata silka yao na kufuata propaganda za wanaharakati wa haki za kinamama.


Wakati balaa hilo likiwakumba dada zetu na mama zetu, Majarida kama PlayBoy, mitandao ya porn na wenzake wanatengeneza ujumbe kama huohuo kwa ajili ya kina baba na kina kaka, kwamba huhitaji kuowa ili uweze kupata ngono, Ndoa na watoto ni pasua kichwa ... kwa kuna Girl Next Door changamka. Nakumbuka kwenye miaka ya 90 wakati nipo darasa la 4 kama siyo la 5, walitufundisha jinsi ya kuvalisha kondomu kwenye uume, sijui leo hii watoto wetu wanafundishwa nini huko mashuleni ...


Vyombo vya habari na harakati za haki za wanawake zimemgeuza mwanamke kuwa chombo cha jamii na kiburudisho cha ngono kwa yeyote anaye taka kwa bei inayofaa. Freemason wa daraja la chini huwa hawalioni hili kwa vile wao wanastahiki kudanganywa, lakini kuanzia daraja la 28 na kuendelea wanafahamu malengo ya harakati hizo dhidi ya umma, wamiliki wa vyombo vya habari pia wanalifahamu hilo vizuri sana, kwamba malengo yao ni kuharibu na siyo kujenga.
 THIS IS THE WAR, AND STILL YOU AND YOUR FAMILY ARE NUMBER ONE TARGET.

No comments:

Post a Comment