Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Monday, December 12, 2016

JE TUPO WENYEWE KWENYE ULIMWENGU? S02, Ep3 (Nyayo za Wageni Kutoka Sayari Ya Mbali)

Kwenye kile kinacho itwa 'elimu' kutoka awali mpaka vyuoni, huu ndiyo mtazamo wa namna binamu alivyo anza kujitambua (evolve), ni kwenye mafunzo ya kidini tu ndiyo tunapata piacha tofauti na hii, lakini kwenye mfululuzo wa posti hizi tutaona mazingira yanavyo mkataa huyu binadam wa Darwin.

“Kupotoshwa kwa historia kume mpotosha binaadam kuliko kingine chochote kinacho julikana kwa mwanaadam”
Jean   Jacques    Rousseau

“Kama utaweza kuwatenganisha watu mbali na historia yao, basi utaweza kuwaongoza unapotaka kwa urahisi”
Karl Max
“Wanao tawala historia yetu, ndiyo wanao tawala hatma yetu, na wanao tawala wakati wetu ulio kuwepo ndiyo wanao tawala wakati wetu uliopita”
George Orwell



Kauli maarufu ya Adolf Hitler akizungumzia nafasi ya uwongo kama njia ya kuwatawala watu.


Kwa mitazamo na maoni tofauti wageni hawa walifahamika kama kwa majina tofauti kwa zama tofauti, mojawapo ya majina hayo ni Atlantis.

Waliishi juu ya aridhi hii kabla ya kuja binaadam wa sasa. Wako wanao dai kuwa waliishi miaka 10000 BC, Wako wanao dai ni miaka baina ya 20000 na 50000 BC na wako wanao dai ni miaka milioni kadhaa kabla ya kufika kwa kizazi hichi cha binaadam.
Kwa wasomi mbalimbali, Atlantis imekuwa ni mada na somo jipya kwenye madarasa na vichwa vya wanahistoria. Kama tutakavyoona kuna ugunduzi wa kutosha wa kile kinacho itwa Pre-historic ambacho katu huwezi kukihusisha na binadam wa Darwin na kinahitaji ushawishi mkubwa wenye mashiko kukihusisha na binadam wa kwenye vitabu vitakatifu.

Yaani kabla ya binaadam wa kwanza, lakini waliishi. Wako wanao dai kuwa walikuwa ni binaadam hasa kama walivyo binaadam wa leo ispokuwa wao walikuwa na maumbo makubwa mno na wako wanao dai kuwa hapana hawakuwa binaadam ila majini. Mbali na tofauti hizi za kipindi gani waliishi na walikuwa na maumbile ya namna gani wote wanakubaliana kuwa walikuwa ni viumbe waliofanikiwa katika ustaarabu wa hali ya juu na katika teknolojia ambayo binaadam wa leo bado hajaweza kuigusa! Walikuwepo, waliishi, na wakatoweka, kama hawakupata kuwepo, Atlantis.
Mchoro huu unalenga kuonesha dola ya Atlantis, kabla haijatoweka.


Ni ukweli usiopingika kuwa kupata kuwepo kwa viumbe hao ni jambo lililo kuwa likijulikana muda mrefu, lakini huwezi kulikuta katika somo la historia. Ukiachilia mbali nadharia ya Alfred Wagener kuhusu kutanuka kwa tabaka la aridhi miaka milioni 240 iliyopita, si kweli kuwa wamekufundisha yote kuhusu nini kilitokea, kwa makusudi hawajaweka hilo katika mitaala, tangu dunia inaanza mpaka hapa tulipo sasa.
Moja ya somo muhimi kwenye Geographia, na hata Historia, halafu ghafla linakatizwa, tunaletewa binadam wa Darwin na majina yake magumu, ghafla naye anakatizwa, tunaletewa zama za mawe, kaaaazi kwelikweli.


 Mabadiliko mbalimbali yaliyoikumba sayari yetu yangetosha kutengeneza mabuku makubwa ya jiografia na historia na kutoa elimu sahihi ya wapi tunatoka na wapi tunakwenda na juu ya yote kwa nini tuko hapa tulipo sasa. Ila kinyume chake uwongo, uzushi vimekuwa ndiyo muhimili wa elimu yetu zama zote.


Chini ya bahari, Pyramid kubwa kama yale ya Gaza, nani aliyajenga, iweje

 yawe chini ya bahari na si juu ya aridhi. Miji mingi ya kale na masalio 

mbalimbali yamekutwa chini ya bahari, sehemu mbalimbali, imekuwaje?


Mtu wa kwanza kuweka katika maandishi maisha ya wa Atlantis ni mwana falsafa wa wa Kigiriki Plato, kabla yake ni wateule wachache ndiyo waliokuwa wakifahamu kuhusu Atlantis. Maelezo ya Plato kuhusu Atlantis yanatokana na maelezo aliyonakili kutoka kwa babu yake ambaye karne mbili kabla ya Plato alisafiri kuelekea Egypty na kukutana na mchungaji wa kiegypt aliyempa maelezo hayo, babu yake Plato alijulikana kama Solon . 
Plato na Ngano ya ATLANTIS

Maelezo hayo yalirithishwa kwa vizazi kadhaa mpaka yalipo mfikia Plato naye akawa mtu wa kwanza kuyaandika, ingawa vyanzo vingine vina onesha kuwa Solon aliyaandika maelezo yale kutoka kwa mchungaji yule, hivyo Plato ni mtu wa kwanza kuyatoa maelezo hayo kwa wasio kuwa wateule.



Kutoka kwenye maelezo hayo wa Atlantis waliishi kwenye bara la Antarctika na waliweza kusafiri kutoka kwenye bara hili kuja kwenye mabara mengine kama Egypt na Amerika zote mbili. Ni katika zama ambazo Antarctika ilikuwa na hali ya kimediterania. Hii itategemea ni mahala gani Polar Axis ilikuwepo kipindi hicho.

 Mnamo mwaka 9950 BC na wachunguzi wengine wakisema ni mwaka 10000BC, ndani ya mchana mmoja na usiku mmoja bara la viumbe hao, visiwa vyao, ustaarabu wao na juu ya yote teknolojia yao ya hali ya juu vilizamishwa chini ya bahari ya Atlantiki na huo ukawa mwisho wa hadithi yao.

Mengi yanasemwa kuhusu vilivyomo baharini, lakini moja wapo ni masalio ya

 miji yanayo patika kwenye maeneo fulani fulani ndani ya vina virefu vya bahati.

Kabla ya kuzama kwenye uchambuzi yakinifu juu ya Atlantis, tutizame uvumbuzi wa kijiografia wa kwenye miaka ya 1950, uchunguzi ambao ulipelekea kuipa nguvu ile nadharia ya Tectonic movement. Kutoka mwaka 1831 mpaka mwaka 1948 iligundulika kuwa North Magnetic Pole imesogea kiasi cha kilometa 250 kutoka sehemu ambayo ilikuwepo kabla ilipo pimwa mara ya kwanza.
Mgnetic Pole inahama eneo lake, tena kwa kasi ya ajabu, si mara ya kwanza kufanya hivyo, unajua nini kilitokea kipindi hicho, unajua nini kitatokea katika zama zetu inavyo endelea kuhama, unajua kwa nini hili haliripotiwi na chombo chochote cha habari? Stay tuned, maswali yote hayo yatajibika hapa.

 Wanasayansi wanakubaliana kuwa Magnetic Pole imekuwa ikihama hama kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa maelfu ya miaka, Uchunguzi huo pia umebainisha kuwa mabadiliko hayo hutokea kila mara baada ya miaka 300000 ambapo Magnetic Pole inakuwa inabadilisha mwelekeo wake kabisa na au inajirudia kufuata mwelekeo wake wa awali kama ilivyo kuwa kabla. Uchunguzi huo unaelezea kuwa kwa miaka milioni 330 iliyopita Magnetic Pole imebadilika mara 400.
Kinacho hama siyo North pole peke yake, hata south pole inahama ingawa siyo kwa kasi kubwa kama inavyo hama kwenye North Pole. Zote zinahama kuelekea muelekeo mmoja.


Kutokana na kuhama huko kwa North Pole na South Pole kunaathiri kiukamilifu kabisa hali ya hewa ya dunia yote. Wanajiolojia duniani kwa sasa wanakubali kuwa barafu inayopatikana Alaska, Marekani na kwenye maeneo mengine ya Pola yaani North Pole na South Pole kuwa maelfu ya miaka nyuma maeneo hayo yalikuwa katika ukanda wa kitropiki. 
Wanyama ambao wanayo asili ya kitropiki wamekutwa wameganda kwenye maeneo ambayo kwa sasa ni ya barafu tupu.

Mimea mingi, samaki na wanyama ambao asili zao ni mazingira ya kitropiki wamepatikana wakiwa wameganda chini ya barafu za maeneo hayo. Viumbe na mimea hiyo imepatikana katika barafu hizo vikiwa katika mazingira na hali mbalimbali zinazo ashiria maisha na uhai wa kitropiki katika vilele hivyo vya barafu nzito.
Masalio hayo yamekutwa hayana majeraha yoyote na matumbo yao yamejaa chakula na mazingira yakiashiria kuwa hapakuwa na barafu maeneo hayo hapo kabla.


 Hivyo North Pole na South Pole zimebadilisha maeneo yao kwa maelfu ya maili mara kadhaa katika vipindi vilivyo pita. Kwa maneno mengine maeneo ambayo awali yalikuwa ni ya kitropik leo yamekuwa ni vilele vya barafu kama vile Antarctica, na maeneo ambayo awali yalikuwa ni ya barafu leo yamekuwa ni ya kitropiki na mengine yamegeuka kuwa jangwa kabisa. Wataalam wanatuambia kuwa hali hii inaweza kutokea tena kwenye miaka 50 ijayo! Lakini ziko tafiti zinazo onesha kuwa hali hiyo huenda ikatokea mapema zaidi ya hivyo.


Siyo habari za kufikirika, kisayansi imethibiti kuwa tukio hilo limeshatokea hapo kabla. Maoni yanatofautiana ni namna gani linatokea, je ni ndani ya usiku mmoja, au ni uataratibu unao chukua muda mrefu, na je madhara yake ni wapi kwa wakakzi wa nyumba hii inayo itwa dunia.




 Picha za satelaiti za karibuni zimeonesha kuwa eneo la bara la Arabu ambalo hivi sasa ni jangwa awali lilikuwa na mazingira ya kitropiki. Ingawa hazikuonesha kuhusu kuwepo kwa barafu haimaanishi kuwa hiyo ndiyo kauli ya mwisho na kama wataendelea kuwa wazi katika uchunguzi wao basi punde tu watatuthibitishia kuwa palipata kuwa na barafu. 


Kwenye miaka ya karibuni, magnetic ya north pole imekuwa ikihama kwa kasi kubwa zaidi na kila mwaka kasi hiyo imekuwa ikiongezeka maradufu kama inavyo onekana kwenye mchoro huo hapo juu

Michoro ya awali iliyo patikana ndani ya mapiramidi ya Egypt ilikuwemo pia mimea na aina nyingine za uoto wa asili ambazo katu hazifikiriwi kuwa asili yake ni Egypt kutokana na kuwa na sifa za kitropiki zaidi kuliko ukame wa jangwa, kana kwamba wachoraji wake walikuwa wametokea India ambako ndiko mimea hiyo inapo patikana. Lakini huenda ni wakati ambao Egypt ilikuwa katika eneo la kitropiki zaidi.
Baadhi ya michoro ndani ya mapiramidi


Hii inaweza kuelezea ni kwa nini Tanzania kwenye mlima Kilimanjaro tuna barafu wakati tuko kwenye eneo la kitropiki. Kuwa na kilele kirefu kuliko vyote Afrika hakutoshi kufanya kuwepo kwa barafu hiyo, kwani tunaweza kuona barafu hiyo sasa inapungua kwa kasi mbali na kuwepo kwa urefu ule ule wa mlima huo, kupungua kwa barafu hiyo kunaelezeka na kueleweka zaidi kwa kuhama kwa Magnetic Pole na athari zake kuliko kutuambia mabadiliko ya hali ya hewa yanayosababishwa na uharibifu wa hali ya hewa kutoka kwenye nchi za viwanda. Kuna ushahidi kuwa Afrika ya Kusini na Hawaii hapo kabla zilikuwa zimefinikwa na barafu.


Mlima wetu wa Kilimanjaro na barafu yake, ulivyokuwa na ulivyo sasa na hapo ni baina ya 1921 -2002, nadhani 2016 habari ni nyingine kabisa. Unaweza kuniambia ni viwanda gani tulivyo navyo hapa Afrika Mashariki  vinavyo weza kutuletea athari ya kiasi hichi? Kama sababu ya barufu kuwepo ni urefu wa mlima hakuna takwimu zozote zinazo onesha kupungua kwa kimo cha mlima huo. Ikiwa ni athari ya gesi za viwanda mimi hainiingi akilini maelfu ya maili ya viwanda vilivyopo Ulaya vije kuathiri barafu ya mlima Kilimanjaro, nadhani barafu iliyopo Alaska ingemalizika kabla ya Kilimanjaro haijaanza kupungua, tunahitaji kulitazama hili kwa jicho jingine.


Mwandishi wa kitabu cha ‘Not By Fire But By Ice’ amekusanya ushahidi na vyanzo vya kisayansi kutoka katika sayari mbalimbali zilizopo kwenye mfumo wetu huu wa jua na kuonesha ni namna gani sayari hizo kama ilivyo dunia zinavyo athirika na ‘Global Warming’.  Kutoka kwenye sayari ya Jupiter mpaka kwenye Pluto, zote zipo kwenye ‘Glabal Warming’. 


Hawawezi kukuambia kuwa 'Global Warming' inaikumba solar systeam yote, sababu itabidi waje  na maelezo tofauti ambayo itawabidi wayaseme yale ambayo hayawapasi kusema, au huko kwenye Mars na Jupiter nako kuna viwanda.

Lakini tukumbuke kwenye sayari hizo hakuna hewa ya kabonidayoksaidi ambayo wana sayansi wetu na vyombo vya habari vya maadui zetu wanatuambia kuwa hewa hiyo ndiyo chanzo cha ‘Global Warming’. Ikiwa kwenye sayari hizo hakuna hewa ya CO² je nini kinacho sababisha hiyo ‘Global Warming’? Je si kitu hicho ndiyo chanzo cha ‘Global Warming’ kwenye sayari yetu pia ambayo inatumia jua moja na sayari nyingine zinazo athirika na ‘Glabla Warming?


Barafu inapungua kwa kasi kubwa kwenye bara la Antarctika

Hewa ya Co² inaathiri ndogo sana kwenye ‘Glabal Warming’ Lakini mabadiliko makubwa ambayo dunia yetu inajiandaa kuyaingia ndiyo hasa kiini na chanzo cha ‘Global Warming’ kinacho eleweka na kukubalika katika uwanja wa sayansi ya hali ya hewa.


Kwenye kitabu cha Atlantis Rising kilichoandikwa na Brad SteigerI mwaka 1973, tunakuta kuna maelezo yanayo elezea ugunduzi wa hekalu la Serapis katika jiji la la Italy kwenye mkondo bahari wa Adriatic, Venice, ugunduzi huo unaonesha kuwa hekalu hilo lilijengwa na viumbe walio ishi miaka 12000 mpaka 19000 iliyopita.

 Mwandishi huyo anadai kuwa hekalu hilo lilijengwa kipindi ambacho eneo hilo lilikuwa juu ya usawa wa bahari, ambapo kwa sasa eneo hilo liko chini ya bahari kwa kiasi cha futi 20. Kwa sasa eneo hilo liko kwenye nyuzi 46 za Latitude ya kaskazini na ambapo inakadiriwa kuwa wakati wa ujenzi wake ilikuwa  kwenye nyuzi 35 za Latitude. Ujenzi huo ulifanyika wakati North Pole ikiwa baina ya eneo inapo patikana Nigeria na Brazil ya leo.
Kwenye miaka ya 1900 mpaka 2000 kasi ya kuhama ni kubwa zaidi, unaweza kuona kwenye  grafu


Dr. Lturralde-Vinent yeye na timu yake waliamua kutembelea maeneo husika, kwenye visiwa vya Cuba chini ya bahari ilikupata ile hadithi ya ndani. Walikuta mengi ambayo ni kawaida kupatikana juu ya aridhi na siyo chini ya sakafu ya bahari, yakiwemo masalio ya wanyama na kazi za ufanisi zilizofanywa na mikono ya viumbe visivyo julikana, yote yalitoa hitimisho moja, kuwa hapo kabla vitu hivyo vilikuwa juu ya uso wa dunia vikiangaziwa na jua bila pingamizi. Mchunguzi huyu anathibitisha kuwa kuna mlolongo wa visiwa vilivyozama eneo hilo ambapo hapo kabla vilikuwa ni sehemu ya Cuba. 


Lakini cha ajabu zaidi ni kuwa sehemu ambayo kumezama pande kubwa la aridhi likiwa zima zima bila hata kuvunjika na ambapo kuna masalio ya ‘megalithic culture’eneo hilo liko tofauti zaidi na masalio mengine yaliyozama, kwa maana ya aina yake ya aridhi, haifanani hata kidogo na aridhi ya maeneo ya Cuba wala ya visiwa vilivyozama ni kama imetokea sehemu tofauti kabisa. Kwa kawaida mchanga wa maeneo ya Cuba, ni wa aina ya Limestone sawa na ile ya visiwa vilivyozama chini ya bahari ambavyo navyo vilikuwa ni sehemu ya Cuba, lakini siyo aridhi hii yenye masalio ya ‘megalithic’ aridhi hii mchanga wake ni wa aina ya granite ambao eneo la karibu na aina ya mchanga huu ni Mexico. 


Kuzama kwa Atlantis na visiwa vingine sehemu mbalimbali duniani kwa namna moja ama nyingine kunashindwa kutenganishwa na mabadiliko ya kimaumbile ya dunia, hasa yale ya kuhama kwa Axis yanayo ambatana na kuyeyuka kwa kiasi kikubwa cha barafu na kupelekea mafuriko makubwa na pia suala la tectonic movement, yaani kusogea kwa tabaka la juu la aridhi kunako ambatana na milipuko ya volkano.
Tctonic movement

 Kawaida mabadiliko hayo yanapo tokea madhara yake ni makubwa mno kama kuzama kwa maeneo ya aridhi baharini, mabadiliko ya hali ya hewa kwa kiasi kikubwa. Masalio mbalimbali ya viumbe na uoto wa asili ndiyo unao tosha kutueleza kuwa ni hali ya hewa ya namna gani ilikuwepo katika eneo husika.
Pande la aridhi ambalo ni sehemu ya kasri lililozama ndani ya maji, ni lini na kwasababu zipi lilizama baharini, bado ni kitendawili.


Mnamo mwaka 1940 Dr. Frank C.Hibben muhadhiri wa Archeology katika University of New Mexico aliamua kufanya safari ya utafiti kwenye eneo la Alaska kutizama kama atapata masalio ya binaadam aliyeishi maeneo hayo kipindi cha kabla haijafinikwa na barafu. Hakuna alicho pata kumuhusu binaadam zaidi ya dhahabu, na wanyama wa aina mbalimbali wa zama hizo wote wakiwa wamenaswa kwenye barafu.
Sanamu la mmoja wa wafalme wa Egypt likiopolewa kutoka baharini, eneo hilo palipatika mji mzima uliokuwa chini ya bahari.

 Muhadhiri huyu kutoka Mexico akahitimisha kuwa barafu kubwa iliyoyeyuka na kusababisha mafuriko makubwa ndiyo iliyo wasukuma wanyama hao ambao asili yao ni maeneo tofauti tofauti ya dunia, lakini hapakuwa na dalili ya binaadam. Viumbe wote hao kutokana na uchunguzi wake walikufa kwa wakati mmoja kwenye maeneo ya miaka ya 10000BC, sawa na kipindi ambacho wachunguzi wengi wanacho dai kuwa Atlantis ilizama kwenye bahari ya Atlantiki.
Masalio ya miji ya kale chini ya bahari.


Hivyo dunia tunayo ishi sasa ni dunia ambayo imepitia mabadiliko makubwa yaliyo sababisha athari mbalimbali ikiwemo kutoweka kwa wanyama na viumbe mbalimbali wakiwemo viumbe walio fahamika kama Atlantis na ustaarabu wao. Lakini hata hivyo dunia hii inakaribia kuingia kwenye mabadiliko hayo tena hivi punde, na hii ni sehemu ambayo nitaijadili kwa kina. Lakini kwanza nataka kuuthibitishia uma kwamba kabla ya kuja binaadam kwenye uso wa dunia, kuliwa na uma mwingine waliokwenda mbali kimaarifa na kiteknolojia kuliko teknolojia tuliyo nayo sasa, na uma huo ulitoweka , lini ulitoweka, vipi ulitoweka, still its a mystery.
Pande hili kubwa la aridhi limekuwaje likafika kwenye sakafu ya aridhi.

Kuna ramani ya zamani mno ya mwaka 1513, ambayo imeandaliwa na mtu aliyeitwa Piri Ibn  Haji Memumed, maarufu kama Piri Re’is. Jamaa huyu katika zama zake alikuwa ni maarufu na mwenye kuheshimika katika fani ya ubaharia ndani ya Uturuki. 

Piri Re’is amedai kuwa ramani hiyo inatokana na vyanzo vya ramani zaidi ya 20. Amedai pia kuwa sehemu ya magharibi ya ramani hiyo inatokana na Christopher Columbus. Amesema vyanzo vingine vya ramani vinarudi mpaka wakati wa Alexander the Great.
Moja ya ramani za Piri

Charles Hapgood aliamua kuifanyia uchunguzi yakinifu ramani hiyo akisaidiana na wanafunzi kutoka Keene State College na mtaalam wa michoro ya ramani kutoka US Air Force. Baada ya uchunguzi huo walihitimisha kuwa; ramani ya Piri Re’is inatokana na vyanzo vya ramani nyingine zaidi ya sita.


Katika ramani hii ya Oronteus Finaeus ya mwaka 1531 Antarctika inaonekana ikiwa haina barafu kabisa vilele vya milima na mito inaonekana kwa uwazi kabisa katika ramani hii.


Ramani hiyo inaonesha mistari ya kufikirika ya latitudo na longitudo kwa usahihi wake kwenye maeneo ya pwani ya Afrika, Amerika ya Kusini na Kaskazini na sehemu ya Antarktika. Kabla ya mwaka 1700 AD hakukuwa na maarifa wala elimu ya kuweza kupima longitudo kwa usahihi. Mwanzoni mwa karne ya 19 Urusi walichapisha ramani ya dunia na hakukuwa na bara la Antarktika, kwani mpaka kipindi hicho hapakufahamika kuwa kuna kitu kinachoitwa Antarktika.

Ramani ya dunia iliyo tolewa na urusi karne ya 19, haikuonesha bara la Antarctica.


Ramani ya kwanza ya Piri Re’is ya mwaka 1513 inaonesha rasi (peninsula) za Iberian, pwani ya Afrika Magharibi, visiwa vya Canary, Azore, bahari ya Atlantic, visiwa vya West Indies, pwani ya Mashariki ya Amerika ya Kusini. Afrika ya Kusini na pwani za Antarktika.

Kwenye karne ya 14 ramani za Piri Reis zinaonesha maeneo mbalimbali ya dunia, ikiwemo Antarktika tena bila barafu, sababu mito milima vinaonekana vizuri kabisa, wakati karne ya 19 urusi wanatoa ramani haina bara la Antarkitika. Ni wapi alizitolea ramani hizo.

Ramani ya pili ya Piri Re’is ya mwaka 1528 inaonesha Greenland, Labrodor, Amerika ya Kaskazini, Pwani za Mashariki za Canada, Pwani za Mashariki za Amerika ya Kaskazini mpaka Florida na Cuba. Inasemekana kuwa ramani ya tatu ipo na inaonesha Ulaya, Asia na bahari ya Hindi. Lakini kitu cha ajabu zaidi kwenye ramani za Re’is ni kiwango cha usahihi wa maelezo na vipimo vyake.
Wapi alizitoa ramani hizi?

Charles Hapgood katika kuzisoma ramani hizo aligundua pia kuwepo kwa milima ya Andean na mito iliyo kuwa ikitiririka kuelekea mashariki kutoka kwenye milima hiyo, maeneo ambayo hata Cristopher Culumbus na wenzake hawajapata kuitolea maelezo, kwa maneno mengine hawajawahi kufikia maeneo hayo. Lakini kilicho cha ajabu zaidi katika ramani za Re’is  ni topografia ya Antaktika, pamoja na visiwa vyake, mito na pwani zake, lakini ikumbukwe kuwa bara hili la Antaktika lilikuwa limefunikwa na barafu nzito yenye unene wa kadiri maili moja kwa maelfu ya miaka! Kimaandishi bara hili lilivumbuliwa mwaka 1820 na ni mwaka 1957 mpaka 1960 ndipo utafiti juu ya bara hilo ulianza kufanyika .


Kwenye kipande hichi cha ramani maeneo ya Afrika Magharibi na Amerika ya kusini yanaonekana vizuri sana. Kwenye karne hiyo ni wapi Piri Reis alizipata?


Mkufunzi wa michoro ya ramani kutoka US Navy Hydrographic Bureau baada ya kuzisoma ramani hizo na kuzilinganisha na ramani za kisasa kabisa aliandaa mkutano na  waandishi wa habari mwezi Agosti 28, 1958 na haya yalisemwa kwenye mkutano huo 

“… hatukuweza kudhania ni kwa namna gani waliweza kutengeneza ramani zilizo na vipimo sahihi kama hizi bila msaada wa ndege. Lakini ukweli ni kuwa walizitengeneza na zaidi ya hapo, waliweka digrii za longitudo sahihi kabisa, kitu ambacho hatukuweza kukifanya mpaka ilipofika miaka mia mbili iliyo pita”


Kwenye ramani hii ya mwaka 1563, iliyochorwa na Mercartor, imebeba taarifa nyingi na za kutosha kuhusiana na bara la Antarctica ambalo sisi tumekuja kugundua uwepo wake kwenye karne ya 18. Lakini kwenye ramani hiyo limechorwa likiwa halina barafu, kanakwamba mchoraji wake alilichora wakati wa kipindi ambacho halikuwa limefunikwa na barafu, mito, milima, visiwa na, pwani na mengine mengi. Je ni lini ramani hizi zilichorwa au kwa uwazi zaidi ni lini Antarctica haikuwa imefunikwa na barafu? 



Kivutio kikubwa na cha kushangaza kwenye ramani ya Re’is ni pande la aridhi lililo chini ya ramani hiyo, pande hilo linaonekana kama Antarktika ilivyo. Haya yalionekana kama maajabu kwa sababu Antarktika hakuwa ikijulikana mpaka mwaka 1820.

 Lakini cha ajabu zaidi ni kuwa ramani hiyo ilionesha kwa usahihi kabisa mwonekano wa pwani kwenye pande la Antaktika. Pwani kama ya Queen MudLand inayopatikana katika bara la Antarktika ilionekana kwa uzuri na kwa usahihi wake kwenye ramani hiyo . Maajabu ni kuwa pwani hiyo ya Queen Mud Land imekuwa imefunika na gamba zito, nene la barafu kwa karne nyingi na umbile lake limeweza kujulikana kwa watengeneza ramani wa kisasa kwa kutumia vyombo vya kisasa katika fani hiyo.


Wakati tunagundua uwepo wa bara hili kwenye karne ya 18, tayari lilikuwa limeshafinikwa na barafu yenye unene wa Kilometa 5! Tofauti na inavyo onekana kwenye ramani za karne ya 14 ambapo hazioneshi dalili yoyote ya bara hilo kufunika na barafu.


Ramani ya Piri Re’is inawaachia wachunguzi swali moja ni lini ramani hiyo imechorwa? Jibu lake ni kuwa ramani hiyo ilitengenezwa wakati ambao Antaktika bado haijafunikwa na barafu, na kwa namna inavyo onekana mchoraji wake alikuwa angani akifanya kazi hiyo kama zinavyo fanya satelaiti katika zama zetu hizi. Ramani hiyo pia inaonesha bara la Marekani ya Kusini ikiwa imeungana na Antarctica kitu ambacho kilitokea maelfu ya miaka kadhaa nyuma.  Sehemu kubwa inayo onekana katika ramani hiyo ni Pwani za magharibi za Afrika, pwani za mashariki za Amerika ya Kusini na pwani za kaskazini za Antarktika. Re’is, hakuwa na uwezo wowote wa kuchora ramani hii kwa kutumia uzoefu wake wa kusafiri baharini kwa sababu Antarctika yenyewe imegundulika miaka 300 baada ya yeye kukamilisha ramani yake hiyo. 


Antarctica inaonekana bila barafu, visiwa na pwani zake zikionekana vizuri, ikiwemo pwani ya Queen Maud Land, ni lini na ninani mchoraji wa ramani hizo.

Pwani ya Queen Maud Land ni utata mwingine kutokana na kuwa kumbukumbu zinaonesha wakati wa mwisho pwani hiyo kutokuwa na barafu ni miaka 9000BC iliyo pita kabla ya kumezwa na barafu iliyo ipoteza kabisa pwani hiyo . Ni akina nani walio fanya kazi hiyo katika kipindi ambacho katika historia hakukuwa na watu walio rekodiwa kuwa na ustaarabu na maarifa ya kufanya maajabu hayo?

Sanamu la Piri Rei's sambamba na ramani yake.

Ramani ya Piri Re’is ikafungua mlango wa kupatikana kwa ramani zingine za kale ambazo hapo kabla ziliruhusiwa kwa macho ya watu maalum tu. Ramani hizo kama ile ya Oronteus Finaeus aliyoichora mwaka 1531 nayo kutokana na vyanzo mbalimbali vya ramani za kale ikawa na hitimisho kama tulilolipata kwenye ramani ya Piri Re’is. Zaidi ramani ya Finaeus imeonesha milima, na mito inayo tiririka kuelekea baharini, ambavyo vyote kwa sasa vimefunikwa na barafu nzito, lakini kabla ya kufunikwa viumbe fulani waliishi hapo na waliweza kuichora ramani yake kwa usahihi kabisa kama ambavyo inavyo chorwa leo na wataalam wetu kwa kutumia vyombo vya kisasa katika fani.


Msimamo wa wanajiolojia ni kuwa maeneo hayo kama Antarctica mara ya mwisho kabisa kuwa kwenye hali ya kitropiki ni mamilioni ya miaka yaliyo pita. Kipindi ambacho kwenye historia ya vitabu vitakatifu au ile ya kisekula binadam alikuwa bado hajaikanyaga hii sayari, lakini zaidi si kipindi ambacho binadam huyo hasa kwa mtazamo wa Darwin angeweza kuwa na uwezo wa kutengeneza ramani hizo. Je ni nani katika zama hizo aliifanya kazi hiyo.



Ama katika ramani hizo maeneo ya kijiografia, kama vile mito, mabonde na milima imerekodiwa kwa usahihi wake kama ambavyo inavyo wezwa kuthibitishwa na teknolojia yetu ya sasa. Ni kazi ya kimahesabu na kiuchunguzi. Kuna mengi ya kusema kuhusu ramani hizi, lakini kubwa zaidi ya yote ni kujua hiyo ni kazi ya viumbe gani.



Ndiyo kwanza kumekucha, maswali haya hayahitaji majibu mapesi, umewahi kusikia kuhusu Mistari ya Nazca? Vipi habari ya Piramid na Sphinix? Unajua Peru kuna Piramidi kama zile za Gaza  lakini yote hayo yanakuja na swali moja ni kazi za akina nani, katika zama zipi... stay tuned... 

No comments:

Post a Comment