Bahati mbaya sana kwa wakazi wa dunia kila mpango wa uliofanywa na maadui zetu unakwenda kama wanavyo taka wao, New World Order iko wazi, lakini ni kwa wale walio huru kiakili ndiyo wanayo weza kuiyona, wengine tunasubiri itangazwe rasmi. Lakini nikipi hicho kilichoko kwenye New World Order?

Mpango mchafu, mweusi mbaya na hata usiofikirika kwa mtu wa kawaida ni KUPUNGUZA idadi ya watu duniani kwa asilimi 90! Iliasilimia 10 itakayo baki iwiane vizuri na mazingira yake. Kwa kutumia njia mbaya na kushinda mnyama. Hapo utakutana na Nyota ya Kijani, Mpango wa uzazi salama, elimu ya ngono mashuleni, vyakula na madawa yanayotiwa dawa na visababishi vya ugumba kwa siri, virusi na maradhi ya kutengeneza maabara kama ebola, ukimwi, chanjo za aina kwa aina, vita kila kona ya dunia na mapango wa WWIII, ukame na majanga mengine ya kutengeneza tunayo dhani ni ya asili.

Kisha idadi ya watu inayotakiwa ikisha fikiwa ajenda itawekwa hadharani ikiwa na Serikali Moja ya Dunia (Serikali ya Kishetani), Dini moja kwa watu wote (Dini ya Kumuabudu Shetani) Jeshi Moja la Dunia (Kwa ajili ya kupambana na wale watakao taka kuipindua serikali hiyo) Sarafu moja kwa dunia nzima, na wananchi wote wakuwa na Microchip kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila raia masaa 24/7.

Kifupi ni kuuwa asilimia 90 ya binadamu wote, na kutawala nyanja zote za maisha, na kumtawala kila mtu na kila kitu kutoka siku unazaliwa mpaka unaingia kaburini!

Wakati unafikiri hilo haliwezekani mpango huu umeshakamilika kwa zaidi ya asilimia 90%

NAIKUBALI HII

NJIA YA MATUMAINI KWA TEJA WA PORNOGRAPH

Hichi ndicho anachokisema Mwanasaikriatiki wetu Norman Doldge, “Ukurasa wa nyuma kwenye jarida la wanaume liitwalo Risque na kuras...

Sunday, November 27, 2016

JE TUPO WENYEWE KWENYE ULIMWENGU? S02, Ep1 (Ujio wa Wageni kutoka Sayari ya Mbali)

Bandiko la Queen Replaced, bado linaendelea, nadhani linaweza kuwa moja ya bandiko refu kupata kubandiko kwenye blogi hii. Muandishi anaendelea kukusanya ushahidi na taarifa zingine kuhusiana na kitimbi hichi cha Queen Replaced, na kadiri taarifa zenye mashiko zitakapo patikana basi nitaendelea kuririka hapa kwenye bandiko hilo, nadhani litaendelea na episode moja baada ya nyingine mpaka Mfalme Trump atakapo ondoka au kuthibitisha vinginevyo.

Leo nazungumzia kitu nilicho pata kukigusia hapoa nyuma kidogo kwenye bandiko hili ‘Je Tupo Wenyewe Kwenye Ulimwengu?’ unaweza kulipitia hapa http://salimmsangi.blogspot.com/2015/04/je-tupo-wenyewe-kwenye-ulimwengu.html
Leo nataka tuizungumzie mada hiyo kwa kina zaidi ...




“Historia ni mtazamo wa zama zilizopita ambapo watu wamekubaliana juu ya mtizamo huo”- Nepoleon Bonaparte

“Wanao tawala wakati wetu ulio kuwepo ndiyo wanao tawala wakati wetu uliopita, (na wanao tawala historia yetu, ndiyo wanao tawala hatma yetu) ” - George Orwell




Historia ya dunia inatazamwa katika mitazamo mikuu miwili, historia ya dunia kwa misingi ya kisekula, na historia ya dunia kwa misingi ya kidini. Lakini hiyo siyo yote, kuna kundi jingile lenye mtazamo tofauti wa historia ya dunia; tofauti na mtazamo wa kidini na kisekula ambayo mara zote inakinzana, kushindana na kila moja ikitafuta upenyo wa kumuangusha mwenzake.
Historia ya siri ya dunia, umeona Mapiramid  na alama ya jicho moja. 

Mtazamo wa kundi hili la tatu unajumuisha mitazamo yote miwili, ingawa inaifanyia marekebisho mitazamo hiyo katika baadhi ya sehemu kabla ya kuikubali, lakini zaidi kundi hili la tatu linaongezea na kingine zaidi kwenye mtazamo wao; wanaongeza kile ambacho hakikubaliki au hakiwafikiani na mtazamo wa kidini au kisekula. Kundi hili na la asasi za siri.
Mchoro wenye maana elfu moja kwenye asasi za siri. 

Asasi za siri al-maarufu secret societies kabla ya mapinduzi ya mawasiliano hasa kwa upande wa mitandao kilikuwa ni kitu kigeni masikioni pa wengi na bado hata sasa bado ni kitu kigeni mno kwa watu wa kawaida ambao wanaamini kuwa wanakwenda shule na wakifika huko watasoma na kujua kila kitu, lakini kinyume chake ni tofauti kabisa. 
Shuleni tunafundishwa kuwa wajinga na siyo waerevu.

Huwezi popote pale kwenye mtaala wa somo lolote, chuo chochote duniani ukakutana na somo linalo husiana na ‘secret societies’; ispokuwa kwa wale ambao si kwamba tunaamini juu ya kuwepo kwa secret societies, bali tunayo ushahidi wa kutosha kuthibitisha hilo.
Kitabu hichi kinaelezea historia ya asasi za siri. 

Tunakubaliana kuwa mwenendo wa dunia unayo iyona sasa, na dunia iliyo lala nyuma kwenye historia ya miaka 1,000 na Zaidi, na historia unayoisoma na utakayo endelea kuisoma, waandishi wake walikuwa, nab ado wataendelea kuwa ni ‘secrete societies’.
Jim Marrs akionganisha doti kuthibitisha uwepo wa njama za kuitawala dunia kupitia asasi za siri.

Asasi hizi za siri nazo zinayo mtazamo tofauti juu ya historia ya dunia. Ukitaka kupata dondoo za historia ya dunia kwa mujibu wa asasi za siri, tizama kazi iliyo fanywa na mtu anayeitwa, Jonathan Black, kwenye kitabu kinacho kwenda kwa jina la ‘The Secret History of the World.’ Halafu tazama kazi ya mwanafalsafa na mwanamasonia wa daraja la juu, bwana Mainly P Hall, kwenye kitabu chake alichokiita, ‘Secret Teaching of all Ages.
Kitabu hichi kinaelezea historia ya uumbwaji kwa mtazamo wa asasi za siri.

Historia ya dunia kwa upande wa kisekula haijawahi hata mara moja kukiri juu ya uwepo wa viumbe wengine wenye ‘uhuru’ kama binadam, lakini kinyume chake imekuwa ikikiri juu ya kuwepo kwa viumbe wa aina hiyo kupitia kazi mbalimbali za filamu, muziki na vitabu, lakini kazi hizo zimekuwa zikichukuliwa au kufahamika na watu wa kawaida kama ‘science fiction’.
Kiumbe kutoka sayari nyingine akiwa amejivikangozi ya binadam, kama inavyonekana kwenye series maarufu ya V. 

Maelfu na maelfu ya kazi zinazo zalishwa Hollywood na kwenye makampuni mengine ya filamu kote duniani, yamekuwa yakitumia elimu ya sekula kuthibitisha juu ya uwepo wa aina hiyo ya viumbe.
Kumekuwa na kazi nyingii za filamu na vitabu zikitahadharisha umma juu ya uwepo na ujio wa viumbe hao kwa mara nyingine tena. Picha hii ni mfano wa kazi hizo. 

Kwa upande wa dini, kumekuwa na hadithi nyingi zinazo zungumzia juu ya uwepo wa aina hiyo ya viumbe, hadithi kwa upande wa dini, mila na utamaduni wa jamii mbalimbali kote duniani, zimekuwepo na zimekuwa zikizunguka na kurithishwa kutoka vizazi hadi vizazi. 
Wa-Egypty wa kale ni moja ya jamii ambazo zilijikita sana na hadithi hizi za wageni kutoka sayari ya mbali. Mchoro huu ukionesha mashirikiano hayo baina ya wageni na binadam.

Ingawa zimetofautiana kwa namna mbalimbali, lakini dhana na maudhui ya hadithi hizo zimebaki kuwa moja; kwamba si binadam pekee yake mwenye ‘uhuru’ wa kuamua, wapo wengine wenye uhuru kama yeye.
Moja ya filamu zinazo zungumzia dhana ya binadam kuumbwa na viumbe kutoka sayari ya mbali.

Katika mfululuzo wa mabandiko haya ya ‘Je Tupo Wenyewe; Season 2, tutatizama kwa kina juu ya habari hizi, tutazitizama kote kwa upande wa dini, kisekula, na kwa uapnde wa asasi za siri, mpaka tutakapo maliza mabandiko haya, basi tutakuwa na majibu na msimamo sahihi juu dhana nzima ya kuwepo au kutokuwepo kwa viumbe hao, na kama wapo ni nafasi gani waliyonayo kwenye ulimwengu huu, je sote sisi na wao tunayo asili moja kwa maana ya Muumba Mmoja au wao wanao wakao na sisi tunao wa kwetu?
Wgeni kutoka sayari ya mbali kama wanavyo onekana kwenye filamu za leo na majarida mbalimbali. Juu yao ni meli yao ya angani maarufu kama UFO.
Kwa upande wa asasi za siri taarifa na mafunzo yao juu ya chochote kile siyo kitu unachoweza ukakibeba kama kilivyo, hii ni kutokana na kwamba, taarifa moja kwao inaweza kuwa na maana alrfu moja kwa watu tofauti wa madaraja tofauti. 
Kichwa cha shetani na alama mbalimbali za asasi za siri ikiwemo freemason.  

Mathalani kwenye freemason unapokuwa kwenye daraja la kwanza, au la pili au la tatu, ambayo ni maarufu kama Blue Degree, mambo utakayo fundishwa hapo ni tofauti nay ale utakayo fundishwa kwenye daraja la 28 na kuendelea ikiwa utabahatika kufika huko. Asilimia 80 ya freemason wote duniani wapo kwenye blue degree. 
Piramidi likionesha daraja mbalimbali za freemason. 

Wateule wa chache ndiyo wanao ruhusiwa kupanda na kufika madaraja ya juu. Kwenye Blue Degree Freemason anaambiwa kuwa anaye abudiwa ni Mungu Mmoja, lakini anapofika daraja la 28, anaambiwa kuwa yale yote aliyokuwa akifundishwa ni uwongo, na kwamba kuanzia hapo sasa ndiyo atakapo anza kufundishwa mambo ya kweli, na mojawapo ni kwamba freemason hawamuabudu Mungu Mmoja, bali Shetani.
Wakubwa wa kifreemason, lakini hawa ni visible freemason na wapo madaraja ya chini. 

 Kufika kwenye hizo daraja inaweza kumchukua mtu robo tatu ya Maisha yake, lakini unapokaribia na kudhani umefika, unambiwa kuwa ndiyo kwanza unaanza.

Hivyo tunapo itazama historia ya dunia kwa mujibu wa asasi za siri, hatutaweza kubeba kila kile wanacho tuambia, uchambuzi yakinifu unahitajika kuchambua almasi kwenye vipande vya vioo. 
Shaq O’nel naye ni mfuasi wa Freemason. 

Hivyo nitachukua machache kulingana na mada yetu. Asasi nyingi za siri zinaamini juu ya uwepo wa viumbe wenye nguvu, busara, elimu, maarifa na mapenzi makuu kushinda binadam. Viumbe hao kwenye asasi za siri kuna wanao tambulika kama waungu au wenye kusahiki kutawala na wengine wanao stahiki kutawaliwa.

Waunga wa kale wa Egypt, akiweno Osiris, alama ya jua ambayo ndiyo mungu mkuu anayeabudiwa tangu enzi na enzi mpaka leo. Waungu hao ni zao la mchanganyiko wa binadam na wageni kutoka sayari ya mbali. 

Kwenye asasi za siri dunia na ulimwengu haujatokea kwa nasibu kama anavyo dai Darwin, ambaye naye alikuwa ni mfuasi wa asasi ya siri iliyokwenda kwa jina la . Wala kwenye asasi za siri hawatambui juu ya kuumbwa kwa dunia na ulimwengu kama zinavyo tambua dini zenye Imani ya Mungu Mmoja; wao wanaamini kuwa nguvu iliyo umba hii dunia na ulimwengu wote ni nguvu mahususi na maalum ambayo ipo ndani ya kila mmoja wetu. Pia wanaamini kuwa binadam wa kwanza aliumbwa na wageni kutoka sayari ya mbali, wageni ambao waliwapatia binadam maarifa na ujuzi, wageni hao ndiyo walio muumba binadam wa kwanza wa kiume na mwanamke wa kwanza.
Buzz alipokuwa ana hojiwa na Luccry King kwenye CNN mnamo miaka ya 2000. Alisema kuwa walipkuwa huko mwezini waliona dalili ya uwepo wa viumbe wengine. Ingawa tunafaham hawakwenda mwezini, na hilo nimethibitisha hapa kwenye posti inayoitwa. HATUKWENDA MWEZINI. 

Wageni hao walipokuwa hapa duniani walianzisha asasi ya siri iliyo kwenda kwa jina la ‘Brotherhood of the Snake’ Haidithi hii imetajwa kwenye moja ya vitabu vinavyo tegemewa sana na asasi za siri, kitabu kutoka kwa jamii ya kale ya watu wa Sumeria. Hadithi ya nyoka nayo ni hadithi yenye maana elfu moja kwenye asasi za siri kama tutakavyo ona huko mbele.
Waungu, DNA, kwa juu inaonekana meli yao ya angani na kwa mbali ni nyota ya Draco wanaposema wametokea.

Wageni hao walikuwa na maumbile mfano wa nyoka au mijusi, nao walikuja kwenye sayari hii kwa ajili ya kutafuta malighafi, au walikimbia vita kutoka kwenye sayari yao, au walikuja kwa ridhaa yao kuwafundisha binadam maarifa mbalimbali, ambayo wao wamesha yafikia kwenye sayari zao. 
Vidio fupi ikielezea ikielezea ujio wa viumbe toka sayari ya mbali, kwanini walikuja na jinsi walivyo muumba binadam wa kwanza.


Dhana hii ya wageni kutoka sayari ya mbali unaweza kuiyona kama ukitazama series ya ‘The Event’, The V’ na nyinginezo pia filamu kama ‘Transformer 1, 2, na 3, They Lived, Men in Black na nyinginezo. Kuna maelfu na maelfu ya kazi za namna hiyo zinazo zungumzia ujio na uwepo wa aina hiyo ya viumbe.
Wageni wakimuumba binadam.

Binadam wa kwanza na kizazi chake walitengenezwa na wageni hao ili waweze kuwafanyia kazi za kukusanya hizo malighafi. Hivyo walitengenezwa kama aina Fulani ya watumwa. Baadae wakawaboresha Zaidi na kuwapa uwezo wa kuzaa. Kisha wakawapatia na maarifa ya juu Zaidi kuhusiana na asili ya waungu na hao binadam. 
Kitabu cha wasumeri kikionesha waungu wanao itwa Annunaki, wakiamuumba binadam kwa kutumia DNA yao na kile kinacho fahamika kama tree of life na zoezi hilo likisimamiwa na mungu anayeitwa ANU, au baba wa mbinguni.

Hili likaleta mvutano baina ya wageni wao kwa wao. Kwani usalama wao upo kadiri binadam anavyo baki kuwa mjinga wa kutokujua yeye ni nani na kwanini yupo hapa. Hili likapelekea baadhi ya wageni hao kuungana na binadam dhidi ya ndugu zao, ndipo asasi ya kwanza ya siri duniani ikatengeneza; The Brotherhood of the Snake, lengo la asasi hii likiwa ni kuwafundisha binadam na kuwafumbua macho juu ya asili yao, kwanini wapo hapa na mengine mfano wa hayo.


Asasi hiyo haikudumu sababu wageni waliokuwa kinyume na asasi hiyo walijipenyeza na kuisambaratisha; baadae zikazaliwa asasi nyingine za siri kama Freemasonry, the Rosicrucians, The Knight Templars, Ordo Templi Orientis, Knights of Malta, The Order of the Illuminati na nyingine nyingi.

Asasi za siri si tu kwamba zinatambua juu ya uwepo wa viumbe ‘huru’ mbali na binadam, lakini kwa milenia kadhaa kama tutakavyoona, asasi za sri zimekuwa zikiaandaa mazingira mahususi ya ujio wa wageni hao kwa mara nyingine kwa ajili ya kuwakomboa binadam na madhila wanayo pitia sasa.
Nembo hii maarufu sana kwenye ulimwengu wa afya na utabibu, lakini asili yake ni mbali zaidi ya hapo kama tutakavyoona.

Karatasi za kale za wasumeria zinaelezea kuwa Anunnaki waliokuja na vyombo vieleavyo angani vyenye umbo kama ya ungo, walikuwa ni kabila la mijusi au zaidi reptilia. Kwa wayahudi wametajwa kama ‘NEFILIM’ yaani watoto wa waungu au ‘AWWIM’ neno limaanishalo viumbe watambaao kwa tumbo , wafalme wa Egypt na utawala mzima wa kifarao mara zote wamekuwa wakihusishwa na nyoka, reptilia. 
Sina hakika juu ya pcha hii, lakini mengi yamesemwa juu ya uwepo wa binadam wenye maumbo makubwa

Mtafiti mmoja wa kimarekani, David Sielaff anasisitiza kwamba Nefilim siyo watoto wa waungu bali ni kizazi cha baina ya Binaadam na viumbe wasio kuwa binadam baada ya muingiliano wao.
Sisemi kuwa picha hizi ni za uwongo, lakini pia sisemi kuwa ni za kweli. Lakini katika dunia ambayo asasi za siri ndiyo watawala, ni vigumu kuwa na jibu la moja kwa moja kwenye mambo kama haya. Lakini ni nukta zinazo paswa kutizamwa kwa jicho la tatu.

Kwenye kitabu cha waumini wa dini ya kikristo, biblia agano la kale kwenye kitabu cha Mwanzo wavamizi hao wametajwa kama waungu.

“Ikawa wanaadam walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wakike walizaliwa kwao wana wa mungu waliwaona hao mabinti za wanaadam ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wao wowote walio wachagua. ... tena, baada ya hayo wana wa mungu walipoingia kwa binti za wanaadam, waka zaa nao wana, hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa”
Ni kweli? Sijui fanya uchunguzi wako binafsi.

Bibilia inawataja watu hawa kuwa walikuwa ni mijitu mikubwa mno. Katika Quran tunajifunza kabila jingine lenye sifa kama hizi kabila la Iram. Quran 8 9: 7 - 8, ambalo nalo limetajwa kama kabila lilikuwa na watu wakubwa mno ambao hawajapata kupatikana mfano wake katika uso wa dunia na ambalo lilijenga majumba yao kwa kuchonga na kukata majabali. Sina hakika kuwa ndilo kabila la kizazi cha wana wamungu kilichotajwa katika kitabu cha Mwanazo kwenye Bibilia ila uchunguzi zaidi unahitajika.

Wachunguzi wengine wanasema neno hili Nefilim lina maana ya “wale waliodondoka kutoka mbinguni” neno “watu wenye sifa” katika kitabu cha Mwanzo limefasiriwa kutoka kwenye neno la Kisumeria “shem” ambalo Sitchin anasema lina maana ya “gari la angani”. Anasema neno hilo linatokana na mzizi wa neno “shu-mu” ambalo lina maanisha kile ambacho ni “MU” na MU linamaana ya chombo cha kurukia, kwahiyo, anaendelea kusema “watu wenye sifa” iliyo tajwa katika kitabu cha Mwanzo inamaanisha sifa yao hiyo waliokuwa nayo ya kusafiri angani . Kwa hiyo hii ndiyo jamii iliyoingiliana na wanawake wa kibinaadam.
Bado tunao watu wenye maumbo makubwa katika zama zetu.

Wachunguzi wengi wa mambo kuhusiana na kabila hili la reptilia wanakubaliana kuwa wametokea katika Nyota ya Draco, iliyopo baina ya Nyota saba zing’arazo sana, ambazo kati ya majina mengi zijulikanazo kwayo moja wapo ni Great Bear na ile ilyopo kushotoni mwa nyota hizo yani Little Bear au Northen Star ijulikanayo kama Alfa. Majengo ya maelfu ya miaka nyuma kama mapiramid ya Egypt, sanamu la Simba lenye kichwa cha binaadam, Sphinx, lilloko Gaza ambalo nilazamani zaidi kuliko mapiramidi yenyewe, Angkor Wat lililoko Kambodia, na mengine huko Japan yaliyojengwa kwa vipindi tofauti kwa kutumia ustadi mkubwa wa elimu ya nyota, mahesabu, elimu ya maumbo na sayansi ya hali ya juu yamejengwa moja kwa moja kufuata muelekeo wa Draco.
Wanatoka wapi watu hawa?

Hata hivyo wachunguzi wengine wa mambo wanadai kuwa kabila hilo la reptilia liliishi katika mashimo na mapango na inawezekana ndipo walipo tokea. 

Gazeti la Horizona la  1909 mwezi wa nne liliandika habari kuhusu machimbo ya madini yaliyopatikana karibu na eneo la Grand Canyon lenye ukubwa wa kuchukua watu elfu hamsini pamoja na vitu vingine, vitu kadhaa vilipatikana vinavyohusiana na kabila hilo la reptilia. 

Mashimo mengine mengi yamepatikana sehemu mbali mbali duniani yanayo elezea hadithi ile ile kwamba yalikuwa ni nyumba na sehemu za uzalishaji za reptilia.
Sanamu maarufu kama Olmec, sanamu hizi zilipatikana Mexico. Ninani aliyachonga masanamu hayo makubwa hakuna anayefaham. Sura za masanamu hayo ni watu weusi, je mtu mweusi alifikaje Mexico kipindi hicho ambapo sanamu hizi zinasadikiwa kuwa ni za zamani hata kabla ya ustaarabu wa watu wa Mya, Inca na hata kabla ya Columbus kufika Amerika.

Wanakubaliana kuwa reptilia hawa moja wapo ya njia walizo zitumia kumtawala binaadam katika kila njia ni kujivaa katika mwili wa binaadam kama nguo au kifupi kama koti kubwa na kuanza kuutawala mwili huo au mtu huyo na pale muhusika anapo kufa basi reptilia huyo anahamia kwenye mwili wa binaadam mwingine ajenda ni kuichukua dunia na binaadam ndiyo gari la kufanikisha safari hiyo, likizimika moja anahamia kwenye gari lingine.
Mchoro huu unamuonesha binadam wa Mexico akipambana na mijitu mikubwa. Ni wapi wa Mexico walizitolea habari hizi?

Kwa sasa wachunguzi huru na wachambuzi wa dini pamoja na wanahistoria wanakubaliana kuwa kitabu cha Mwanzo kilichopo katika agano la kale kimechukuliwa kutoka vitabu na kwenye rikodi za vitabu vya Wasumeri wa kale, kama ambavyo Musa, Nuhu na Ibrahim walivyotajwa katika kumbukumbu hizo za Wasumeri na kuonekana kuwa ni kweli katika biblia ndivyo ambavyo walivyotajwa Anunnaki ambao nao kwa mtazamo wa rikodi za Wasumeri ni kweli walikuwepo na ndivyo ilivyo katika kitabu cha Mwanzo katika agano la kale. 
i hiLaurence ni mmoja wa wafuasi wa asasi za siri, na kazi zaki zimekuwa zikitia nuru kazi zilizokuwa zinafichwa na asasi za siri.


Mwandishi mmoja wa vitabu bwana Laurence Gardner, freemason na anaye jinadi kuwa anayo damu ‘tukufu’ ya waungu, anasema,

“Kila maandishi yaliyopatikana kuthibitisha kuwa Wasumeri waliishi na Anunnaki yamethibitisha kuwa jamii hiyo ya Anunnaki wakiwemo Enki, Enhil, Nin-khursag na Inanna walifanya kazi mbalimbali za kijamii hapa duniani. Walikuwa ni wasimamizi na viongozi, walimu na wanasheria, wataalam wa maarifa mbalimbali, teknolojia na wafalme... Kukubali kuwepo kwa Anunnaki ni jambo litakalo wachanganya wanahistoria, lugha yao itawakanganya wataalam wa lugha, na teknolojia yao ya hali ya juu itawachanganya na kuwaacha vinywa wazi wataalam na wanasayansi wetu, lakini endapo tutakataa kuwepo kwao huo utakuwa ni upuuzi. Wasemeriani wenyewe wameshatuambia kuwa Anunnaki ni akina nani na wapi walikuwepo na hakuna sayansi na au historia itakayo weza kutuambia vinginevyo.”

Rikodi za Wasumeria zimeelezea kwa mapana habari za Anunnaki pamoja na jamii yao wakiwemo Enki, Enlil, Ninki, Inanna, Utu, Ningishzida, Marduk na wengine wengi. Habari iliyotawala katika hadithi nzima ya watu hawa ni vita baina ya vizazi hivi na hasa Enki na Enhili, hadithi ambazo pia tunaweza kuzipata kutoka kwenye kitabu cha Mwanzo katika gano la kale.
                                                                                           
i hiWaungu wa kale wa Babiloni. Tizama maumbo yao ni kama mjusi.
                                                 
 Lakini hata hivyo jamii hiyo ilikuwa na zaidi ya vita baina yao, ilihusisha waungu wa kike na waungu wa kiume katika mabaraza yao ambayo kila wakati yalikutana kupanga na kutatua matatizo baina yao na pia kujadili hatma yao kwa wakati ujao na hatma ya binaadam kiumbe ambaye ana nguvu sawa na wao, kiumbe ambaye ni huru kama wao.
Inasemwa walipigana vita vya kinyuklia.

Miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia kuongezeka katika vyombo vya habari kazi mbalimbali zenye maudhui kuhusu Reptilia katika sura ya Dragon, Dinosaur na Reptilia wenyewe. 

Soko la vyombo vya habari, sanaa, michezo na burudani mbalimbali limetawaliwa kwa wingi na maudhi ya viumbe hawa na kulifanya soko lake kuwa ni kubwa mno kutoka kwenye midoli na vikaragosi vya watoto mpaka kwenye sinema zilizo pata mafanikio makubwa. Lakini kile ambacho wengi hawafamu ni kuwa binaadam tunaandaliwa taratibu kukubalina na kuwepo viumbe vya aina hii ifikie kiwango ambacho kila mtu anatamani kuwaona viumbe hao, hii itapunguza upinzani pale wakati utakapo fika ambapo waungu hao watakaporudi katika uso wa dunia na kuishi nasi kama awali.

Athari ya waungu hawa tunaipata zaidi katika umbile la nyoka. Katika jamii nyingi za kale na hata za sasa nyoka anahusishwa na hekima, maarifa, matibabu ambapo nembo nyingi za tiba duniani zinatumia alama ya nyoka, alama ambayo unaweza kuiyona pia kwenye noti ya shilingi mia tano ya Tanzania.
Alama ya asasi ya siri ya Brotherhood of the snake.

 lakini pia alama ya pesa kwa dola ya Marekani ni herufi ‘S’ na ‘I’ ambapo kwa pamoja zinatengeneza alama ya ‘$’ ambayo ni alama ya nyoka aliye jiviringisha kwenye mti. Nyoka amehusishwa na maajabu pamoja na mazingambwe rejea hadithi ya mtume Musa na wachawi wa Firauni, rejea hadithi za wahubiri waliobadilika na kuwa nyoka mbele ya waumini wao. Kutoka Babylon, Mexico,  Egypt na kwengineko duniani, hii ni alama tukufu na ya maajabu katika mambo mbalimbali.

Mabudha mmoja wa mwanafalsafa wao anayeitwa Nagarjuna wa India huoneshwa akiwa na miali ya mwanga inayowakilishwa na nyoka saba, ambayo hiyo ni alama ya daraja la juu katika utawa wa kibudha. Alama ya nyoka saba ambao mara nyingi huwa ni Kobra pia ni inapatikana kwa wamasonia mpaka kwa Mafarao wa Egypt.
Nagarjuna

 Afrika Magharibi tunakutana na hadithi ya mungu aliyeitwa Nana-Buluku na msaidizi wake ambaye ni mungu nyoka aliyeitwa Da. Hadithi kama hii utaikuta Afrika ya Kusini kwa jamii ya Wazulu, utaikuta Scandanavia, Mexico na kwa makabila mbalimbali hapa nyumbani Tanzania.
Medusa, mungu wa Babiloni ya kale.


Tuitizame India kidogo ambako hadithi kuhusu kile kinachoitwa mungu nyoka kina nafasi kubwa katika jamii hizo. Kwa jamii mbalimbali za wahindi mungu nyoka anajulikana kama Nagas. Waungu hawa wanaishi katika matabaka kadhaa yaliyoko chini ya aridhi, matabaka hayo yako saba na hivyo dunia saba, Mexico, Uturuki na England na baadhi ya sehemu zingine duniani pia wana hadithi hii ya matabaka saba na au dunia saba zilizo chini ya aridhi. Katika dunia hizo za chini ya aridhi waungu hao wanasadikiwa kuwa ndiyo walinzi wakubwa wa mali za dhahabu na vito vingine vyenye thamani katika macho ya mwanaadam na hii ndiyo sababu kuu ya makafara mbalimbali yafanywayo na wachimba madini katika sehemu mbalimbali duniani ili kuwaridhisha waungu hawa wa aridhi saba na au dunia saba waweze kutoa mali hizo.
mungu wa chini ya aridhi, au mungu wa kuzimu kwa watu wa Egypt ya kale.

Matabaka hayo saba kwa wahindi ni Atala, Vitala, Sutala, Talatala, Mahatala, Rasatala na Patala. Katika Dunia hizo saba zilizopo chini ya aridhi kutokana na mafundisho ya kihindi, Mexico na kwa Wagiriki wa kale kunapatikana nyumba nzuri mno, bustani na vitu vingine vya burudani kwa wakazi wa nchi hizo. Wakazi wengi wa nchi hizo za chini ya aridhi wanajulikana kama  Daityas, Danavas na Nagasi ingawa sehemu zingine duniani wanaweza kujulikana kwa majina tofauti, umewahi kusikia hadithi ya mji ulioko chini ya Ziwa Victoria? Ni mfano wa hadithi za miji saba katika matabaka saba chini ya aridhi katika jamii tofauti duniani.
Kumekuwepo na miradi mikubwa mikubwa ya kujenga makazi chini ya aridhi kama tutakavyoona kwenye mfululizo wa posti hizi.

Miji yao imejengwa na kurembwa kwa ustadi mkubwa na inahesabiwa kuwa na kila kinacho patikana katika miji yetu ya uso wa dunia, ispokuwa jua, na hivyo hawana mchana wala usiku ingawa miji hiyo imepambwa na mataa makubwa makubwa na inang’ara kama jumba la Taj Mahal, hizi ni ngano kutoka kwa jamii mbalimbali za kihindi, pia ni ngano unazoweza kuzipata katika jamii zingine tofauti duniani, lakini nashindwa kuendelea kuziita ngano pale ambapo hadithi hizo zinapothibitishwa na watu mbalimbali ambao wao binafsi wamepata kufika katika nchi hizo, na au athari na ushahidi wa nyoka hao wenye maarifa zinapo patikana katika uso wa dunia yetu na hata wakati mwingine kutembelewa na watu waliozaliwa na kuishi huko kama tutakavyoona. Hupaswi kuamini unapaswa kuelewa.


Imekuwaje binaadam akatawaliwa na hayawani? Nini hasa kilitokea mpaka binaadam akatawaliwa na mijusi? Kiumbe ambaye ni huru mwenye uhuru kamili atawaliwe na kiumbe asiye na uhuru anayeishi kwa kufuata silka yake inawezekana vipi? Binaadam alitawaliwa na bado anaendelea kutawaliwa na binaadam mwenzake katika hali mbalimbali lakini hii ni kwa sababu wote ni binaadam, wanatabia zinazo fanana, kibaiolojia, kikemia na kifizikia na juu ya yote hakuna kiumbe aliyepatikana na uwezo mkubwa wa kiakili kukabiliana na mazingira yake kama binaadam vipi atawaliwe na kilicho duni kishinda yeye?

Sayari ambayo viumbe hao wanadai wametokea kama ilivyoandikwa kwenye karatasi za kale za Wasumeria yaani sayari ya Neburu inamashaka kuwepo kwake, na pia katika sayari zingine ambazo waandishi na wachunguzi mbalimbali wanahisi wametokea huko hakuna ushahidi unao onesha athari kuwa viumbe hao walipata kuishi katika sayari hizo.
Viumbe hao ni akina nani?
Je kweli walipta kuwepo au ni ngano za kale tu?
Kwanini waliondoka, je watarudi tena?
Maswali ni mengi lakini yatajibiwa hapa hapa.

catch me here next time ....

2 comments:

  1. Mm binafsi napenda kulijua ilo mm mama mm naona niurongo mana majini niwaongo.

    ReplyDelete